Sunday, September 3, 2017

HABARI NJEMA KWA WALE AMBAO HAMKUWAHI KUIMALIZA SHUJAA







Habari za muda huu,

   Hii ni kwa wale wenye simu janja za androiid, riwaya ambayo haikuweza kumalizika kwenye blogu hii . Hivi sasa inapatikana huko hadi mwisho, ni wewe na maamuzi yako ndiyo kunaweza kukuzuia usiweze kuisoma riwaya hii ikiwa unayo simujanja.

Friday, August 18, 2017

TENDAGURU SEHEMU YA TANO






RIWAYA: TENDAGURU
NA: HASSAN O MAMBOSASA
MAHALI: TANZANIA NA MAREKANI





<><><>SEHEMU YA TANO<><><>

Hilo lilikuwa ni zao la kupigana mabusu mbele ya kumbe huyu mwenye miguu mwili asiyejua kuachia nyama yeyote, hapo ndipo wakajiweka huria zaidi hata alipokuja kuketi Mtu mwingine aliye na mwili mkubwa wala hawakujali lolote wao walitulia tu. Hakuna aliyempelekea jicho mtu huyo mwenye asili ya barani ulaya aliyevaa fulana iliyobana pamoja na suruali aina ya jeans


_

Thursday, August 17, 2017

TENDAGURU SEHEMU YA NNE





RIWAYA: TENDAGURU
NA: HASSAN O MAMBOSASA
MAHALI: TANZANIA NA MAREKANI




<><><>SEHEMU YA  NNE<><><>


"Huu ni mwanzo tu nyinyi, tena ninaanza na wewe jioni ya leo" Alisema huku  akiweka alama kwenye jina mojawapo ambalo lipo juu kabisa ya karatasi yake, alipomaliza kuiweka tu hilo jina barua pepe iliiingia kwenye tarakilishi yake na kutoa mlio kutokana na kuiweka proramu maalum ya baruapepe.

"Enheee!" Alijisemea

Monday, August 14, 2017

TENDAGURU SEHEMU YA TATU



RIWAYA: TENDAGURU
NA: HASSAN O MAMBOSASA
MAHALI: TANZANIA NA MAREKANI



<><><>SEHEMU YA TATU<><><>


"Nasa screenshot yake pamoja na ya gari lake hilo halafu play mwingine" Amri nyingine ilitoka na kijana alifanya kama alivyoagizwa, mkanda wa siku nyingine uliwekwa na mtu akiwa ni yuleyule anayemuona anakuja kupokea wageni uwanjani hapo.

"Piga screenshot kila mkanda wa siku ambazo anafika huyu mtu" Aliweka agizo jingine.

Sunday, August 13, 2017

TENDAGURU SEHEMU YA PILI




RIWAYA: TENDAGURU
NA: HASSAN O MAMBOSASA
MAHALI: TANZANIA NA MAREKANI




<><><>SEHEMU YA PILI<><><>


"Akili kuchekecha tu, hii inaonesha wazi hawa waliuawa ndiyo wakatupwa kwenye maji na si kingine. Haiwezekani wafe hivihivi tu, ninachokihitaji kutoka kwako kuanzia hivi sasa hakikisha kila picha unayoipiga kwenye miili hii zinafikia mezani kwangu"

"Afande" Amri yake iliitikiwa na Askari yule ambaye alikuwa na kamera pia mkononi mwake alisogea na  kuongeza walau picha zingine za upande tofauti kabisa kwenye miili ile.



Saturday, August 12, 2017

TENDAGURU SEHEMU YA KWANZA



RIWAYA: TENDAGURU
NA: HASSAN O MAMBOSASA
MAHALI: TANZANIA NA MAREKANI




<><><>SEHEMU YA KWANZA<><><>


               UWANJA WA NDEGE WA MWALIMU  NYERERE

      Wageni waliyokuwa na asili ya barani Ulaya walionekana wakitoka kwenye mlango maalum, huu ni mtokeo wa wale wote wanaowasili ndani ya uwanja huu. Lilikuwa ni kundi la wazungu waliyovalia mavazi marahisi haswa kwenye macho ya kadamnasi, ilionesha wazi hawa  ni watalii waliyokuwa wapo mapumzikoni na matembezini. Huu  ni mtazamo juu yao lakini hakuna aliyekuwa na uhakika na kile  kilichokuwa kikionekana, ujio wao ndani ya nchi hii ulibaki kuwa  ni habari yao iliyokaa mitimani kwa kila mmoja. kila mmoja alifunika kichwa chake kwa kofia kuhofia haswa jua la jiji  jinsi lilivyokuwa kali. Macho yao  yalistiriwa na miwani ya jua, ilionesha wazi hawakuwa wamezoea mmuliko huu   wa mchana.

Wednesday, August 2, 2017

WITO WA KUZIMU SEHEMU YA MWISHO






WITO WA KUZIMU

NA: HASSAN O MAMBOSASA

MAHALI:TANZANIA


SIMU:+255713776843
      +255762219759

WHATSAPP:+255713776843
         +255762 219759

BLOG: riwayamaridhawa.blogspot.com




SEHEMU YA MWISHO!!
Ndani ya chumba hicho alishuhudia wasichana watatu wakiwa wamekaa wanaongea huku wakicheza karata,alisimama mlangoni hapo akiyathaminisha mazingira ya humo. Kabla hata hajamaliza kuyathaminisha   alifunguliwa pingu zote alizofungwa na kisha alisukumwa ndani kwa nguvu.






______________TIRIRIKA NAYO

    Aligeuka kuwatazama mabinti watatu waliokuwa wamevaa sare kama zake wakiwa wanacheza karata, alibaki akishangaa wasichana hao ambao walimtazama kwa nyodo kila mmoja na kisha waliendelea kucheza karata kama kawaida. Josephine hakuwajali kabisa alienda hadi kwenye eneo ambalo kitanda kimojawapo kilikuwa kitupu kisha akajilaza akiwa anasikilizia maumivu. Alipojilaza tu kwenye kitanda hiko wale wasichna waliweka karata zao chini na kisha wakaenda hadi hapo walipo, bila kuuliza mmojawapo alimvuta mguu kamuangusha chini kisha akampiga teke la ubavu.

Friday, June 23, 2017

HANJAMU YA MSALITI



RIWAYA: HANJAMU YA MSALITI
NA: HASSAN O MAMBOSASA




 SURA YA KWANZA

    Mvumo  wa kutoka mashariki kuelekea magharibi ulirindima, minazi  pamoja na miti mingine mingine iliyopo  ndani ya mandhari hiyo. Ilipepesuka vibaya kwa mkumbo huo, hali hiyo ilidumu ikiwa na karaha kubwa kwa miti ambayo haikuisha kulalama ikitoa mivumo ya aina yake pale matawi au makuti yalipovamiwa. Karaha kwa viumbe hai waliyojichimbia ardhini, ikawa ni   burudani kwa viumbe hai watembeao juu ya mgongo wa ardhi. Mgeuko wa hali ya hewa kutoka ile ya joto  liletwalo na jua hadi kuwa mpulizo,  ndiyo ikawa hivyo kwa upande wao.

Tuesday, March 21, 2017

WITO WA KUZIMU SEHEMU YA ISHIRINI NA TISA


WITO WA KUZIMU

NA: HASSAN O MAMBOSASA

MAHALI:TANZANIA


SIMU:+255713776843
      +255762219759

WHATSAPP:+255713776843
         +255762 219759

BLOG: riwayamaridhawa.blogspot.com




SEHEMU YA ISHIRINI NA TISA!!
Ushahidi ambao ungeweza kumuweka huyo aliyekuwa akimkejeli nyuma ya nondo haukuwepo kabisa ndiyo maana alikuwa akitaabika yeye baada ya kukutwa na vidhibiti vyote vilivyokuwa  ni muhimu san kwa ajili ya kesi hiyo. Hakika alikuwa amepewa kesi ya kuiba Ng'ombe kwa kuwekewa mifupa ndani ya eneo lake, huo ulikuwa ni ushahidi tosha wa tuhuma hiyo ya kuiba Ng'ombe ambayo ilikua ikimkabili hakukuwa na ushahidi mwingine ambao ungeweza kumnusuru.


Monday, March 20, 2017

WITO WA KUZIMU SEHEMU YA ISHIRINI NA NANE



WITO WA KUZIMU

NA: HASSAN O MAMBOSASA

MAHALI:TANZANIA


SIMU:+255713776843
      +255762219759

WHATSAPP:+255713776843
         +255762 219759

BLOG: riwayamaridhawa.blogspot.com





SEHEMU YA ISHIRINI NA SABA!!
Kitendo hicho ilikuwa ni mpango kabambe uliokuwa umesukwa na ukasukika, wote walibaki wakitabasamu kwa kuweza kumtia nguvuni kwani tayari sifa zake walikuwa wameshazisikia kama alikuwa ni mjanja sana. Mwenyeji wake alinyanyuka pale kitini alipokuwa amekaa na alijongea hadi eneo ambalo Norbert alikuwa ameangukia, alimpiga teke la kumsukuma na kupelekea ageuke chali kwani alikuwa yupo kifudifudi.

"Simba hachezewi sharubu hata siku moja, sasa kakuparua na kucha"  ALiongea huku akimtazama mateka wake kwa dharau kuu.



Sunday, March 19, 2017

WITO WA KUZIMU SEHEMU YA ISHIRINI NA SITA

WITO WA KUZIMU

NA: HASSAN O MAMBOSASA

MAHALI:TANZANIA


SIMU:+255713776843
      +255762219759

WHATSAPP:+255713776843
         +255762 219759

BLOG: riwayamaridhawa.blogspot.com





SEHEMU YA ISHIRINI NA SITA!!
Alipotolewa gundi iliyokuwa imeweka mdomoni, bado Kamishna alikuwa amepigwa na bumbuwazi la mwaka.

"Shemeji wewe ndiyo wa kunifanyia hivi kweli?" Happy aliuliza akiwa haamini kabisa

"Haaa! Kamishna hongera kwa kutumia nguvu zako nyingi na kumteka shemeji yako, ninataka utambue kuwa mimi sipo njiani wala nini. Nipo kitandani nimepumzika kesho naendelea na kazi yangu ya kuwatia matumbo ya kuhara" Sauti ya Norbert iliyokuwa imejaa kejeli ilisikika.

Thursday, March 16, 2017

WITO WA KUZIMU SEHEMU YA ISHIRINI NA TANO

WITO WA KUZIMU

NA: HASSAN O MAMBOSASA

MAHALI:TANZANIA


SIMU:+255713776843
      +255762219759

WHATSAPP:+255713776843
         +255762 219759

BLOG: riwayamaridhawa.blogspot.com




SEHEMU YA ISHIRINI NA TANO!!
Kuwafuata wale ambao walikuwa wao mnyororo hatari ilikuwa ni kamari ya kifo lakini alikuwa akijiamini sana, pamoja na hayo alipokuwa kwenye eneo hilo alikumbuka kumshukuru Mungu kwa hatua hiyo aliyokuwa amefikia. Pamoja na kuwa ni mtu ambaye alikuwa  haishi kubadili wasichana bado alikuwa akimkumbuka Mumba kwani imani ilikuwa ipo ndani yake, ndiyo maana alimshukuru ingawa alikuwa akimuasi sana muda mwingine aliokuwa yupo kwenye kazi yake.

  Akiwa yupo kwenye kutoa shukrani hizo kwa aliyemjalia pumzi, simu yake ya mkononi iliita, alipoangalia jina la mpigaji alikuwa ni Kamishna ambaye alikuwa ametoka kumtia homa isiyohitaji  tiba muda mfupi uliopita.


Wednesday, March 15, 2017

WITO WA KUZIMU SEHEMU YA ISHIRINI NA NNE

WITO WA KUZIMU

NA: HASSAN O MAMBOSASA

MAHALI:TANZANIA


SIMU:+255713776843
      +255762219759

WHATSAPP:+255713776843
         +255762 219759

BLOG: riwayamaridhawa.blogspot.com





SEHEMU YA ISHIRINI NA NNE!!

"Kwahiyo unanipa hongo siyo"

"Hapana"


"Natoka mama maana ulishaniambia ila ukumbuke kabisa haya niliyokwambia kwani mwenzenu Khemiri ni marehemu sasa mzigo wake mtaubeba nyinyi" Norbert alingea na kisha alitoa Kirekodi sauti kingine ambacho klikuwa tofauti na kile cha awali, alikisitisha kurekodi na kisha akacheza sehemu ile ambayo alikuwa amerokodi . Sauti ya maongezi yao ndani ya ofisi hiyo yalisikika wazi ambapo Mwanamama huyo alizidi kuchanganyikiwa.

Tuesday, March 14, 2017

WITO WA KUZIMU SEHEMU YA ISHIRINI NA TATU




WITO WA KUZIMU

NA: HASSAN O MAMBOSASA

MAHALI:TANZANIA


SIMU:+255713776843
      +255762219759

WHATSAPP:+255713776843
         +255762 219759

BLOG: riwayamaridhawa.blogspot.com




SEHEMU YA ISHIRINI NA TATU!!
Aliipekua ndani ambako alitoka akiwa na kifa kidogo klichokuwa kikiwa taa ya rangi ya bluu na akamuonesha Norbert ambaye alisikitika tu.


"Huyu ndiye mchawi ndani ya ofisi hii ananasa mawasiliano na pia simu zinazoingia na eneo zinapotoka"  Norbert aliongea na kisha alimpa ishara Moses jun ya cha kufanya kwani walikuwa wametambua wazi kuwa walikuwa wakisilikizwa na msaliti huyo ambaye yupo humo ofisini.


Monday, March 13, 2017

WITO WA KUZIMU SEHEMU YA ISHIRINI NA MBILI




WITO WA KUZIMU

NA: HASSAN O MAMBOSASA

MAHALI:TANZANIA


SIMU:+255713776843
      +255762219759

WHATSAPP:+255713776843
         +255762 219759

BLOG: riwayamaridhawa.blogspot.com






SEHEMU YA ISHIRINI NA MBILI!!
Waandishi wa hxbari hao walibaki midomo wazi baada ndani ya eneo hilo kuingia waziri mbaye alikuwa ni chui na paka na Mheshimiwa Mahujuraja, huyu hakuwa mwingine ila ni Mheshimiwa Barnaba Liwale aliyekuwa waziri wa mambo ya ndani. Yeye alikutana na  maswali ya waandishi wa habari kuhusu ugomvi wao waliokuwa nao ingawa walikuwa ni wanachama wa chama kimoja, maswali hayo yalikuwa ni yenye kuudhi lakini Meshimiwa Liwale aliweka uvumilivu.



Saturday, February 25, 2017

WITO WA KUZIMU SEHEMU YA ISHIRINI NA MOJA


WITO WA KUZIMU

NA: HASSAN O MAMBOSASA

MAHALI:TANZANIA


SIMU:+255713776843
      +255762219759

WHATSAPP:+255713776843
         +255762 219759

BLOG: riwayamaridhawa.blogspot.com



SEHEMU YA ISHIRINI NA MOJA

"Yes! Leo hii tunamfuata hatusubiri  zaidi tukitoka hapa tu jioni hii" Josephine aiongea

"Mfuateni pia msiende kichwakichwa tena inabidi muwe wawili maana yule mtu naye ana akili kama mchawi"  Mheshimiwa aliwambia

"worry out Jack Shaw nipo kazini sasa hivi na tunaenda sasa hivi" Askofu alimtoa hofu

"Yaani tukiipata tu ile paltop yake tutamuachie huyo N001 hayo malaptop yote manne halafu ile tunaiharibu hakuna namna sitaki kwenda Segerea" Mheshimiwa aliongea.

Friday, February 24, 2017

WITO WA KUZIMU SEHEMU YA ISHIRINI



WITO WA KUZIMU

NA: HASSAN O MAMBOSASA

MAHALI:TANZANIA


SIMU:+255713776843
      +255762219759

WHATSAPP:+255713776843
         +255762 219759

BLOG: riwayamaridhawa.blogspot.com




SEHEMU YA ISHIRINI!!
Walikuwa wamecheza mchezo mmoja hatari sana ambao haukufahamika hata na Mhudumu mmoja wa ndani ya nyumba hiyo ya kulala wa geni ya kisasa zaidi, mchezo huo ndiyo maana walifanikiwa kutoka bila hata ya kubakisha maswali kwenye vichwa cha Wahudumu hao juu ya yule MZungu ambaye alikuwa ameingia na Eva mahala hapo. Muda huo hesabu ya haraka iliyokuwa imebaki upande wa maadui ulikuwa umebakia na watu wawili tu ambao ndiyo walikuwa na upinzani mkubwa sana, watu hao nao walikuwa wakihitajika kumalizwa ndani ya muda wowote  kwani mzee wa kazi alikuwa amedhamiria kumaliza kazi yake kabla ya muda aliokuwa amepewa.

Tuesday, February 21, 2017

WITO WA KUZIMU SEHEMU YA KUMI NA TISA

WITO WA KUZIMU

NA: HASSAN O MAMBOSASA

MAHALI:TANZANIA


SIMU:+255713776843
      +255762219759

WHATSAPP:+255713776843
         +255762 219759

BLOG: riwayamaridhawa.blogspot.com



SEHEMU YA KUMI NA TISA
Alipouona tu huo mwili alijikuta akiweka mkono kidevuni mwake na akaanza kukuna kidevu chake kilichokuwa hakina ndevu kutokana na kuzinyoa mara kwa mara, alipoacha kukuna aligeuza macho na kumtazama Askari ambaye alikuwa akikaribiana naye kicheo.

"Rangi hii ya ngozi ni dalili tosha ya kuwa aliuawa kwa sumu, sasa inabidi tuchunguze ili kuhakikisha hilo" Aliongea huku akivaa mipira ya mikono.


Monday, February 20, 2017

WITO WA KUZIMU SEHEMU YA KUMI NA NANE



WITO WA KUZIMU

NA: HASSAN O MAMBOSASA

MAHALI:TANZANIA


SIMU:+255713776843
      +255762219759

WHATSAPP:+255713776843
         +255762 219759

BLOG: riwayamaridhawa.blogspot.com



SEHEMU YA KUMI NA NANE!!
Muda aliokuwa akiendesha gari alipokuwa yupo kwenye barabara ya Mandela alitoa simu yake na kupiga mahali na kisha alizungumza kwa lughz ya kikabila na akakata, walipofika jirani na eneo la Tabata relini aliweka gari kando na watu watatu waliingia kwenye gari hiyo. Wawili kati yao walikaa nyuma katika kile upande na kumuweka Jama kati na mmoja alipanda mbele.



Sunday, February 19, 2017

WITO WA KUZIMU SEHEMU YA KUMI NA SABA



WITO WA KUZIMU

NA: HASSAN O MAMBOSASA

MAHALI:TANZANIA


SIMU:+255713776843
      +255762219759

WHATSAPP:+255713776843
         +255762 219759

BLOG: riwayamaridhawa.blogspot.com





SEHEMU YA KUMI NA SABA
Aliweza kuona nyendo zote ambazo alikuwa amezipitia Khemiri tangu alipotoka bandari  na hadi anafika kwenye nyumba yenye makao yao, eneo hilo alilikariri pamoja na kuchukua kifaa kingine ambacho alikitia faili hilo. Hicho kilikuwa kifaa ambacho kilikuwa kina uwezo kumuongoza hadi ndani ya eneo husika kwa kutumia rekodi iliyokuwa imechukuliwa hapo awali"

"Kazi kwao" Alisema na kisha akakichukua kifaa hicho na kunyanyuka kitini.

Saturday, February 18, 2017

WITO WA KUZIMU SEHEMU YA KUMI NA SITA



WITO WA KUZIMU

NA: HASSAN O MAMBOSASA

MAHALI:TANZANIA


SIMU:+255713776843
      +255762219759

WHATSAPP:+255713776843
         +255762 219759

BLOG: riwayamaridhawa.blogspot.com




SEHEMU YA KUMI NA SITA!!
Alimsogezea Josephine ambaye alishtuka sana akiwa haamini kwani walikuwa amehangaika sana, alimpatia Spider ambaye alijikuta akiinamisha uso wake na huku Tarakilishi hiyo akiiweka pembeni.

"Aaaargh! Norbert hii ni too much sasa, naingia mwenyewe kazini haiwezekani tuhangaike kote aje kufagia akaunti yote" Akosfu Valdermar aliongea

Friday, February 17, 2017

WITO WA KUZIMU SEHEMU YA 15




WITO WA KUZIMU

NA: HASSAN O MAMBOSASA

MAHALI:TANZANIA


SIMU:+255713776843
      +255762219759

WHATSAPP:+255713776843
         +255762 219759

BLOG: riwayamaridhawa.blogspot.com






SEHEMU YA KUMI NA TANO!!
Alikuwa akiendesha maisha hayo hapo kijiji akijifanya  ni mdogo wa babu yake mzaa mama, alikuwa yupo katika kuonekano wa kizee kabisa ambapo ingekuwa ngumu kabisa kwa mtu yeyote ambaye anamfahamu kuweza kumtambua. Huko kijini alikuwa akiishi kwa amani zaidi kuliko hata huko mjini ambapo kulikuwa na kila aina ya raha, alipaona ni mahali sahihi kwake kuweza kutulia kwa siku hizo akiwa huko hadi pale hali itakapokuwa shwari.


Thursday, February 16, 2017

NILE COROCODILE


                                    Nile crocodile





    Crocodile Nile crocodile is found communities in Africa, being the second largest in the world after the majichumvi Mamba. This category prefer to live in lakes, rivers and even dams. This

MAMBA WA NAILI

Mamba wa Naili wa Ethiopia


    Mamba wa Naili    ni jamii ya mamba inayopatikana barani Afrika, akiwa ni wa pili kwa ukubwa

WITO WA KUZIMU SEHEMU YA KUMI NA NNE



WITO WA KUZIMU

NA: HASSAN O MAMBOSASA

MAHALI:TANZANIA


SIMU:+255713776843
      +255762219759

WHATSAPP:+255713776843
         +255762 219759

BLOG: riwayamaridhawa.blogspot.com





SEHEMU YA KUMI NA NNE!!
Norbert alipoona hivyo  kuwa muonekano wa mwanamke huyo ulikuwa ni kama yupo akiendelea na shughuli zingine, ili kumshtua ilimbidi aachie mguno wa nguvu. Alipotoa mguno huo alihisi kunyemelewa, alisogea kando  kwa haraka sana baada ya kuhisi kitu kikija kwa nyuma yake.

Wednesday, February 15, 2017

WITO WA KUZIMU SEHEMU YA KUMI NA TATU



WITO WA KUZIMU

NA: HASSAN O MAMBOSASA

MAHALI:TANZANIA


SIMU:+255713776843
      +255762219759

WHATSAPP:+255713776843
         +255762 219759

BLOG: riwayamaridhawa.blogspot.com




SEHEMU YA KUMI NA TATU!!
Sehemu hiyo ilifunguka kama mfuniko ambapo ndani yake kulionekana kukiwa na mkoba unaofanana na mikoba ile miwili ambayo muda huo ilikuwa ipo mikononi mwa Norbert, alipouona mkoba huo alitoa tabasamu lake la kizee na kisha akafunika tena ambako hakukuonekana kama kulikuwa na mfuniko. Baada ya kuufunika mfuniko huo alijilaza kwenye kitanda cha kamba kilichokuwa humo ndani, alilala chali akawa anaangalia paa la nyumba hiyo.

"Ipo siku tu" Aliisemea mwenyewe huku macho yakiwa yapo juu

Tuesday, February 14, 2017

WITO WA KUZIMU SEHEMU YA KUMI NA MBILI


WITO WA KUZIMU

NA: HASSAN O MAMBOSASA

MAHALI:TANZANIA


SIMU:+255713776843
      +255762219759

WHATSAPP:+255713776843
         +255762 219759

BLOG: riwayamaridhawa.blogspot.com





SEHEMU YA KUMI NA MBILI!!
"Aaargh! Yaani huyu mlinzi badala apige simu kunipa taarifa anakuja kugonga mlango" Kaboneka alinyanyuka na akiwa anaenda kufungua mlango

"Mr Kaboneka wait" Norbert alimsimisha kisha akaongea kwa sauti ya chini, "Kama mlinzi alikuwa na utaraibu uliomuwekea nakuomba usifunue mlango na unisikilize mimi kwani huyo anayegonga mlango hakika siyo mlinzi"


Monday, February 13, 2017

WITO WA KUZIMU SEHEMU YA KUMI NA MOJA




WITO WA KUZIMU

NA: HASSAN O MAMBOSASA

MAHALI:TANZANIA


SIMU:+255713776843
      +255762219759

WHATSAPP:+255713776843
         +255762 219759

BLOG: riwayamaridhawa.blogspot.com




SEHEMU YA KUNI NA MOJA!!
  Hakujua kabisa kuwa huyo aliyekuwa naye alikuwa yupo hapo kwasababu maalum, yeye alichokuwa akiwaza ni penzi tu kutokana na kuchangamshwa sana na kilevi alichokuwa akikitumia. Hitaji ya kutengeneza nishati katika mwili nalo lilimfanya kijogoo aweze, yalikuwa ni majibizano ya kimapasho ya miili.

"Mamba na windo meno ndiyo huongea" Norbert alijisemea moyoni.

Sunday, February 12, 2017

WITO WA KUZIMU SEHEMU YA KUMI




WITO WA KUZIMU

NA: HASSAN O MAMBOSASA

MAHALI:TANZANIA


SIMU:+255713776843
      +255762219759

WHATSAPP:+255713776843
         +255762 219759

BLOG: riwayamaridhawa.blogspot.com




SEHEMU YA KUMI!!
Hakika walifanya kazi ya ziada nao lakini katu hawakuthubutu kuyatelekeza magari yao hata kulipotokea milipuko hiyo, waliendelea  na kazi ya kuzima moto na pia kuokoa baadhi waliokuwa wamejeruhiwa wakishirikiana na vikosi vya uokoaji ambao nao walikuwa wamejitoa mhanga wasikimbie kazi yao ili tu waokoe maisha ya majeruhi ambao walihitajika kupata msaada waweze kuendelea kuvuta pumzi ndani ya dunia hii.

Saturday, February 11, 2017

WITO WA KUZIMU SEHEMU YA TISA

WITO WA KUZIMU

NA: HASSAN O MAMBOSASA

MAHALI:TANZANIA


SIMU:+255713776843
      +255762219759

WHATSAPP:+255713776843
         +255762 219759

BLOG: riwayamaridhawa.blogspot.com






SEHEMU YA TISA
Norbert alinakili anuani za makazi ya mmiliki huyo akiwa amemuweka kwenye orodha ambaye alitakiwa kuipitia kwa ajili ya kazi yake hiyo iliyokuwa ikimkabili.

"Tandu ana miguu mingi sana na kila mguu hutoa mchango wake katika safari yake,nina imani yote nitaifikia" Aliongea mwenyewe huku akimkazia macho mmiliki wa kampuni hiyo ya usafirishaji.

Friday, February 10, 2017

WITO WA KUZIMU SEHEMU YA NANE


WITO WA KUZIMU

NA: HASSAN O MAMBOSASA

MAHALI:TANZANIA


SIMU:+255713776843
      +255762219759

WHATSAPP:+255713776843
         +255762 219759

BLOG: riwayamaridhawa.blogspot.com




 SEHEMU YA NANE!!
  Hadi kurejea kwake kazini alikuwa ameshaacha maafa mengi sana ikiwemo kupoteza maisha kwa Mutonga kule kwenye nyumba ya Mzee Mabina, sasa anaaamua kuungana na Scorpio katika kutafuta ukweli juu ya mwenzao ambaye hakuwa amerejea kabisa tofauti na kazi waliyompa muda iliyokuwa ikitaka ifanyike


Thursday, February 9, 2017

WITO WA KUZIMU SEHEMU YA SABA

WITO WA KUZIMU

NA: HASSAN O MAMBOSASA

MAHALI:TANZANIA


SIMU:+255713776843
      +255762219759

WHATSAPP:+255713776843
         +255762 219759

BLOG: riwayamaridhawa.blogspot.com





SEHEMU YA SABA!!

  Aligeuka kwa kasi ya ajabu  na kusimama pembeni akiwa ypo kujihami zaidi, alimuona yule mwanamke akiwa ameshika mkoba wa mabegani akiwa tayari amevaa  kwa ajili ya kuondoka. Hapo alishusha pumzi na kisha akaamua kuachana na bahasha hiyo, aliiweka bahasha hiyo chini na kisha akamshika mkono Mwanamke huyo na kutoka naye humo ndani ya nyumba hiyo kwa kutumia mlango wa nyuma wa nyumba  ambao ndiyo aliutumia kuingia humo ndani.

Wednesday, February 8, 2017

WITO WA KUZIMU SEHEMU YA SITA




WITO WA KUZIMU

NA: HASSAN O MAMBOSASA

MAHALI:TANZANIA


SIMU:+255713776843
      +255762219759

WHATSAPP:+255713776843
         +255762 219759

BLOG: riwayamaridhawa.blogspot.com





SEHEMU YA SITA!!

"Haya nyanyuka mwenyewe tena ukiguna maumivu tu kwa sekunde chache wakati nakupa amri hii nakuongeza tena, uongoze njia unipelke ilipo lapatop hiyo"

 Hakuwa na ujanja tena wa kuweza kuipinga amri hiyo kutokana na mapigo hayo mawili ya nguvu aliyokuwa amepewa ndani ya dakika zisizozidi mbili tu, mwenyewe aliongoza njia na kumpeleka huko kulipokuwa na kitu hicho alichokuwa akikitafuta Mgeni wake.

Tuesday, February 7, 2017

WITO WA KUZIMU SEHEMU YA TANO



WITO WA KUZIMU

NA: HASSAN O MAMBOSASA

MAHALI:TANZANIA


SIMU:+255713776843
      +255762219759

WHATSAPP:+255713776843
         +255762 219759

BLOG: riwayamaridhawa.blogspot.com




SEHEMU YA  TANO!!
"Naona wewe kijogoo umekuja leo,  mke wako umemkosa" Msichana huyo alimuambia

"Kwa akaliaye kiti hicho siku zote ni mke wangu sasa sijamkosa huyo hapo nimemkuta" Norbert aliongea na yeye

"Loh! Lione hivi ukijogoo utaacha lini wewe?"


"Simba akiacha kung'ata na mimi ndiyo nitaacha"

Monday, February 6, 2017

WITO WA KUZIMU SEHEMU YA NNE

WITO WA KUZIMU

NA: HASSAN O MAMBOSASA

MAHALI:TANZANIA


SIMU:+255713776843
      +255762219759

WHATSAPP:+255713776843
         +255762 219759

BLOG: riwayamaridhawa.blogspot.com





SEHEMU YA NNE!!
Huo ndiyo ulikuwa ni mwisho wa Mwanamama huyo aliyekuwa na wahka wa kufungua kile kilichokuwa hakimuhusu, mdharau mwiba  mguu huota tende na ndiyo hayo yaliyomkuta hapo mlangoni mwa nyumba yake umbali wa mita kadhaa kutoka mahali nyumba yake ilipo.

Saturday, February 4, 2017

WITO WA KUZIMU SEHEMU YA TATU










WITO WA KUZIMU

NA: HASSAN O MAMBOSASA

MAHALI:TANZANIA


SIMU:+255713776843
      +255762219759

WHATSAPP:+255713776843
         +255762 219759

BLOG: riwayamaridhawa.blogspot.com





SEHEMU YA TATU!!
Mlango wa sehemu ya maakuli  ulimvutia sana kuutazama na akajikuta kabisa akivutika kuusogelea pia ingawa kimuonekano ulikuwa hauvutii kabisa kwa jinsi ulivyoungua, alijikuta akipiga hatua kuelekea eneo hilo la jikoni ambapo kulikuwa kumemvutia sana.

Friday, February 3, 2017

WITO WA KUZIMU SEHEMU YA PILI



WITO WA KUZIMU

NA: HASSAN O MAMBOSASA

MAHALI:TANZANIA


SIMU:+255713776843
      +255762219759

WHATSAPP:+255713776843
         +255762 219759

BLOG: riwayamaridhawa.blogspot.com




SEHEMU YA PILI!!
Utulivu humuingia akipokea simu  kutokana na kupokea simu ambazo huwa na taarifa tofauti kwa kipindi tofauti cha muda hivyo umakini ulikuwa unahitajika sana zaidi hata ya atembeavyo eneno lenye vumbi kulinda macho yake yasiathiriwe, alitulia kabisa na sikio lake moja ndiyo likawa linafanya kazi zaidi kuliko jingine katika kusikiliza taarifa hiyo.

"Jambooo" Aliitikia baada ya kusikia salamu ya kiaskari kutoka upande wa pili wa simu .

"Unasemaa!" Aliongea kwa mshangao mkubwa baada ya kupokea taarifa  kutoka kwa mwanausalama aliyempigia simu.

Thursday, February 2, 2017

WITO WA KUZIMU SEHEMU YA KWANZA




WITO WA KUZIMU

NA: HASSAN O MAMBOSASA

MAHALI:TANZANIA


SIMU:+255713776843
      +255762219759

WHATSAPP:+255713776843
         +255762 219759

BLOG: riwayamaridhawa.blogspot.com






                  ******MWANZO********


   Akiwa ameketi ofisini kwake aliendelea kufanya kazi iliyokuwa ikimuhusu sana na ilitakiwa kufanywa ndani ya siku hiyo, kazi hiyo ilikuwa ni muhimu sana kuwasilishwa bungeni kwa siku

Wednesday, February 1, 2017

WAKALA WA GIZA SEHEMU YA MWISHO (KUMALIZIKA)


RIWAYA: WAKALA WA GIZA

MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU: +255713776843
          +255762219759


WHATSAPP: +255713776843

SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU MUUMBA WA ULIMWENGU WOTE KWA KUNIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA HII NIKIWA NA AFYA NJEMA




______________+18__________________



SEHEMU YA AROBAINI NA SITA(2)
   
              "Maluteni mimi si mkuu lakini shusheni silaha zenu chini" Alijipa ujasiri na kuongea kuangalia kama wangeweza kutii mari hiyo.

                "Hatukutambui kama mkuu wetu zaidi ya kuwatambua Amiri jeshi mkuu, Meja jenerali Belinda na Meja jenrali Mugiso  basi wewe si mmoja wetu na hapa tupo kwa ajili ya kukumata ufike kule unapostahiki kufika msaliti kama wewe. Afande mkamate huyo" Luteni yule wa kwanza kuongea alimpa amri mwenzake ambaye alinyanyuka na kwenda kumtia nguvuni L.J Ibrahim.
   

WAKALA WA GIZA SEHEMU YA MWISHO (KIPANDE CHA KWANZA)




RIWAYA: WAKALA WA GIZA

MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU: +255713776843
          +255762219759


WHATSAPP: +255713776843

SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU MUUMBA WA ULIMWENGU WOTE KWA KUNIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA HII NIKIWA NA AFYA NJEMA




______________+18__________________





SEHEMU YA AROBAINI NA SITA!!


>>>>>>SEHEMU YA MWISHO<<<<<<


    Josephine alikuwa amepigwa na mshngao sana aliposikia taarifa hiyo wala hakuwa amewaza juu ya kuwashwa kwa taa hizo ikiwa Wilson tayari kulikuwa na dalili tosha hakuwa amefika ndani ya nyumba hiyo. Alibaki akimtazama tu Mzee Ole ambaye uchungu ulikuwa umembana tayari ingawa machozi yalikuwa hayamtiririki kabisa, alikuwa ameinamisha kichwa chini. Ujasiri wake aliokuwa nao kipindi akiwa jeshini kabla hajaingia uwanja wa siasa ndiyo ulikuwa upo ndani ya moyo wake kwa muda huo ndiyo maana machozi hayakuwa yakimtoka kabisa, alikuwa asikitika kwa huzuni huku uso wake akiwa ameukunja kwa nguvu sana

                    "Aaaargh! Sasa naona ameamua kuikata furaha yangu, Aaaaargh!Norbert!" Mzee Ole aliongea kwa nguvu sana akiwa hajui kuwa huyo anayemuiita yupo hapo kwa umbali mita chache tu.

                    "My name(jina langu)" Norbert aliitika kidharaua na kusaabishwa wote kwa pamoja

Wednesday, January 25, 2017

WAKALA WA GIZA SEHEMU YA AROBAINI NA TANO



RIWAYA: WAKALA WA GIZA

MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU: +255713776843
          +255762219759


WHATSAPP: +255713776843

SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU MUUMBA WA ULIMWENGU WOTE KWA KUNIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA HII NIKIWA NA AFYA NJEMA




______________+18__________________




SEHEMU Y AROBAINI NA TANO!!



<<<<SEHEMU YA MWISHO TOLEO LA PILI>>>>>


               "Watakuwa hawanibomoi bali ndiyo kwanza wananijenga na watakuwa wanafanya kazi ya kufuatilia makala zangu online waweze kupata habariza kuuza, wanapata hela kwa maneno yangu huku wananuongezea wafuasi tu" Simon alimaliza kuongea maneno hayo na akafunika tarakilishi yake ya mapakato kisha akajitupa kitandani pamoja na mke wake, alikuwa akitumia akili ya kisiasa ambayo aliona kabisa ilkikuwa ikielekea kumpa mafanikio kwa muda huo huo hadi miaka kadhaa mbele kwenye uchaguzi mkuu wa Tanzania.

Monday, January 23, 2017

WAKALA WA GIZA SEHEMU YA AROBAINI NA NNE


RIWAYA: WAKALA WA GIZA

MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU: +255713776843
          +255762219759


WHATSAPP: +255713776843

SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU MUUMBA WA ULIMWENGU WOTE KWA KUNIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA HII NIKIWA NA AFYA NJEMA




______________+18__________________





 
****SEHEMU YA AROBAINI NA NNE****



<<<<SEHEMU YA MWISHO TOLEO LA KWANZA>>>>>    


      Yeye ndiye alikuwa akitoa amri kuu baada ya Rais Zuber muda huo ndani ya ikulu  hakukuwa na mwingine yeyote aliyekuwa akipinga amri zao, muda huo walikuwa wakiangalia mazingira ya hapo ndani ya ikulu kwa umakini sana kuhakikisha hakiharibiki kitu.

                 "Mheshimiwa usiwe na shaka kabisa ndani ya usiku huu, ikiwa kama operesheni fagio la chuma ndiyo ilikuleta wewe Rais mzalendo kabla hata haujafanyika uchaguzi mwingine ambao ulikupatia ushindi vilvile. Basi operesheni hii itahakikisha utaendelea kubaki madarakani kwa miaka mitano yako awali na hadi ukigombea tena ukipata ushindi" Moses aliongea huku akimshika Rais Zuber bega.

Sunday, January 22, 2017

WAKALA WA GIZA SEHEMU YA AROBAINI NA TATU





RIWAYA: WAKALA WA GIZA

MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU: +255713776843
          +255762219759


WHATSAPP: +255713776843

SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU MUUMBA WA ULIMWENGU WOTE KWA KUNIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA HII NIKIWA NA AFYA NJEMA




______________+18__________________





***SEHEMU YA AROBAINI NA TATU****


             "ama kweli umdhaniaye siye kumbe ndiye, sikutegemea kabisa kama mtu kama huyu ndiye atakuwa adui wa taifa hili hadi atumike kuja kujaribu kufanya mauaji" IGP Chulanga aliongea.

               "Mkuu unajua bado siamini lakini ule mkanda unaeleza kila kitu" DCP  John aliongea akijifanya kutoamini.

               "John ndiyo hivyo imeshatokea, na hapa hamna uchunguzi wa zaidi hata mchoro hauna haja kwa mtu kama huyu aliyeuawa na mwanausalama anayeijua kazi yake" IGP Chulanga aliongea kisha akawageukia Askari aliokuja nao akawaambia, "hakikisheni mnaangalia huko nyuma hadi muipate kamera yake aliyotumia kufanyia tukio"

          

Friday, January 20, 2017

WAKALA WA GIZA SEHEMU YA AROBAINI NA MBILI



RIWAYA: WAKALA WA GIZA

MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU: +255713776843
          +255762219759


WHATSAPP: +255713776843

SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU MUUMBA WA ULIMWENGU WOTE KWA KUNIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA HII NIKIWA NA AFYA NJEMA




______________+18__________________




SEHEMU YA AROBAINI NA MBILI!!
    Wilson alikuwa akitumia nguvu zaidi katika kukimbia huku akiwa amebana mdomo kwa nguvu sana  asiweze kuvuta pumzi kwa kutumia mdomo, akiwa bado yupo kwenye mbio na kasi yake hiyo Norbert aliupiga teke dhaifu mguu wake mmoja na kupelekea ugongane na mguu mwingine kisha aanguke vibaya na kubiringita kwenye mchanga.

Thursday, January 19, 2017

WAKALA WA GIZA SEHEMU YA AROBAINI NA MOJA



RIWAYA: WAKALA WA GIZA

MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU: +255713776843
          +255762219759


WHATSAPP: +255713776843

SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU MUUMBA WA ULIMWENGU WOTE KWA KUNIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA HII NIKIWA NA AFYA NJEMA




______________+18__________________




SEHEMU YA AROBBAINI NA MOJA!!

   Alipoiona kamera hiyo alitoka moja kwa moja ndani ya wodi hiyo kwa haraka sana akaeleka mapokezi katika hospitali hiyo, alitumia dakika mbili kutoka wodi aliyokuwa amelazwa Mufti hadi mapokezi akawa amefika kutokana na umbali uliopo.
 
   Alipofika hapo mapokezi DCP John akiwa yupo ndani ya mavazi ya kiraia alitoa kitambulisho cha kazi na akajitambulisha halafu akasema, "nahitaji kuonana na mhusika wa chumba cha kuongozea CCTV kamera sasa hivi"

Thursday, January 12, 2017

WAKALA WA GIZA SEHEMU YA AROBAINI

RIWAYA: WAKALA WA GIZA

MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU: +255713776843
          +255762219759


WHATSAPP: +255713776843

SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU MUUMBA WA ULIMWENGU WOTE KWA KUNIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA HII NIKIWA NA AFYA NJEMA




______________+18__________________





    SEHEMU YA AROBAINI!!
           "Niacheni mie nikamfuate huyu mshenzi!" Alifoka  kwa nguvu akiwa hafurukuti kwa jinsi alivyoshikiliwa kwa nguvu, Daktari na muuguzi huyo waliendelea kumshikilia Mufti kwa nguvu sana hadi alipotulia mwenyewe na kuacha kufanya fujo. Hapo walimuachia na wakabaki wakimtazama kwani machozi tayari yalikuwa yameshachukua nafasi yake machoni mwake, Mufti alianza kulia kwa muda mrefu kimyakimya na alipoacha kulia alimtazama Daktari aliyekuwa amekuja.

Wednesday, January 11, 2017

WAKALA WA GIZA SEHEMU YA THELATHINI NA TISA



RIWAYA: WAKALA WA GIZA

MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU: +255713776843
          +255762219759


WHATSAPP: +255713776843

SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU MUUMBA WA ULIMWENGU WOTE KWA KUNIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA HII NIKIWA NA AFYA NJEMA




______________+18__________________



SEHEMU YA THELATHINI NA TISA!!



             "Mufti amedondoka kwa mshtuko ofisini kwake na hivi sasa amelazwa Aga Khan"

              "Nilitarajia hilo suala litatokea maana udhaifu wake ndiyo upo mikononi mwetu, sasa mwambie Eva aje nimpe ujumbe aende kule akampe huo ujumbe  ataoukuta akiamka tu"

              "Sawa mkuu"


              "Mwambie aje ofisini sasa hivi leo hii siku ni hakuna kulala"

               " Sawa mkuu"

Tuesday, January 10, 2017

WAKALA WA GIZA SEHEMU YA THELATHINI NA NANE





RIWAYA: WAKALA WA GIZA

MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU: +255713776843
          +255762219759


WHATSAPP: +255713776843

SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU MUUMBA WA ULIMWENGU WOTE KWA KUNIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA HII NIKIWA NA AFYA NJEMA




______________+18__________________



SEHEMU YA THELATHINI NA NANE!!

             "Walaykum salaaam, nani mwenzangu....unasema nani" Aliposikia utambulisho wa mpigaji wa simu hiyo alianza kutetemeka huku mpigo ya yakimuenda mbio na alisema, "N001 nini unataka kwangu?.....Hapana Mama Ilham wangu na Ilham wamekusoea nini jamani.....no usifanye hivyo sikiliza kijana" Alipokuwa akijaribu kumuhimiza N001 ambaye  ndiye aliyempigi simu simu ilikatwa kwa ghafla.

Monday, January 9, 2017

WAKALA WA GIZA SEHEMU YA THELATINI NA SABA





RIWAYA: WAKALA WA GIZA

MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU: +255713776843
          +255762219759


WHATSAPP: +255713776843

SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU MUUMBA WA ULIMWENGU WOTE KWA KUNIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA HII NIKIWA NA AFYA NJEMA




______________+18__________________



SEHEMU YA THELATHINI NA SABA!!

                "Kiwewe cha namna gani kile ukumbuke kuvua viatu uvishike mkononi ukimbie vizuri na si kuvitupa, maigizo ya kibongo haya. Haya tuondokeni" Norbert aliongea huku akicheka na alitoa pia

Sunday, January 8, 2017

WAKALA WA GIZA SEHEMU YA THELATHINI NA SITA






MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU: +255713776843
          +255762219759


WHATSAPP: +255713776843

SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU MUUMBA WA ULIMWENGU WOTE KWA KUNIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA HII NIKIWA NA AFYA NJEMA




______________+18__________________



SEHEMU YA THELATHINI NA SITA!!
    Alijikakamua na akajaribu kujiinua sakafuni huku mikono yake ikiwa inamsaidia katika kuinuka huko ikiwa inatetemeka, alijitahidi aweze kufika hatua ya kusimama lakini mikono ilimsaliti na hatimaye akateleza mahali pasipokuwa na utelezi na akaangukia kidevu kwa mara nyingine.
             "Aaaaaaaaargh!" Alitoa ukelele dhaifu kwa viungo yake vya mwili kumsaliti katika kumkabili