Monday, March 13, 2017

WITO WA KUZIMU SEHEMU YA ISHIRINI NA MBILI




WITO WA KUZIMU

NA: HASSAN O MAMBOSASA

MAHALI:TANZANIA


SIMU:+255713776843
      +255762219759

WHATSAPP:+255713776843
         +255762 219759

BLOG: riwayamaridhawa.blogspot.com






SEHEMU YA ISHIRINI NA MBILI!!
Waandishi wa hxbari hao walibaki midomo wazi baada ndani ya eneo hilo kuingia waziri mbaye alikuwa ni chui na paka na Mheshimiwa Mahujuraja, huyu hakuwa mwingine ila ni Mheshimiwa Barnaba Liwale aliyekuwa waziri wa mambo ya ndani. Yeye alikutana na  maswali ya waandishi wa habari kuhusu ugomvi wao waliokuwa nao ingawa walikuwa ni wanachama wa chama kimoja, maswali hayo yalikuwa ni yenye kuudhi lakini Meshimiwa Liwale aliweka uvumilivu.






_________________TIRIRIKA NAYO

  Aliyajibu maswali yote kwanamna ya kistarabu sana huku akiwaumbua badhi ya waandishi waliokuwa wakiuliza maswali ambayo yalikuwa hayana maana, Mheshimiwa liwale aliutumia muda huo aliokuwa yupo hapo kujibu maswali yote ya  waandishi hadi pale waliporidhika ndipo akingia ndani ya jengo la hospitali akiwa ameongozana na kundi la watu. Hata yeye mmwenyewe hakuwa kwenye hali nzuri kabisa ila kutokana na kuwa mawenzake alikuwa amezidiwa kuliko yeye ilimbidi aje kumuona kwani ilikuwa ni muhimu. Muda huo alikuwa akiongea kwa kupooza sana ambako haikuwa kawaida yake kabisa. Ule uchangamfu wake aliokuwa nao ulikuwa umefifia ikiwa siku hiyo ni mara ya pili kumuona, mara ya kwanza kuonekana akiwa kwenye hali kama hiyo ilikuwa ni katika mwaka uliopita ambapo alifikia hatua ya kulazwa kwenye hospitali hali ilipokuwa mbaya.

  Alikuwa na tatizo moja kubwa kama alivyokuwa Mheshimiwa Mahujuraja, matatizo yao wote yalikuwa hayaponi kabisa katika hospitali yoyote jambo lililopelekea awe nimtumiaji wa dawa kwa ajili ya tulizo ya tatizo hilo. Sasa dalili za kuonekana kwa tatizo hilo lililokuwa nalo lilikuwa limeshamuanza lakini alivumilia na kuja kumuona huyo mwenzaekambaye alikuwa amezidiwa.

 Kitendo cha kuwaaacha wanahabari hapo nje ilikuwa ni kama amewapa habari , haikupita muda wale waliokuwa wana tovuti mitandaoni walianza kuiripoti habari hiyo huku wakimwagia sifa kedekede. Kitendo cha yeye kuja kumuona hasimu wake kwenye mambo mbalimbali wawapo kwenye Bunge ndiyo kilifanya apewe sifa hizo ambazo alikuwa amejichukulia muda huo aliokuwa ameingia humo ndani. Huko ndani alikutana na familia ya kiongozi mwenzake ambayo ilimpokea kwa ukarimu mkubwa sana. Wao kwa mara ya kwanza ndiyo walimpa kisa kizima cha kupatwa kwa hali hiyo, Mheeshimiwa Liwale alisikitishwa sana na hali hiyo ilikuwa imemkumba kiongozi mwenzake kisha akakaa na familia yake kwenye eneo la kusubiri wagonjwa.

  Akiwa amekaa eneo hilo alikuwa akifanya kazi kubwa ya kuifariji familia hiyo juu ya hali ya Mheshimiwa mwenzake, maneno yake anayoyatumia kwenye siasa aliyatumia hapo alipokuwa amekaa na familia hiyo. Haikuwa mara ya kwanza kwa familia hiyo kumuona Mheshimiwa Liwale hivyo walikuwa wamemzoea sana, walikuwa wameshazoea ukorofi wao waliokuwa wakiuweka ndani ya bunge na hata kwenye mitandao ya kijamii. Haikuwa kutokea ukorofi huo ukawa umewekwa uraiani, ndiyo maana walikuwa ano katika eneo hilo kwani walikuwa hawana ukorofi uliokuwa umewekwa sehemu kama hizo Hakika ya siasa ni mchezo wa kuigiza mtupu na wote waliokuwa wapo ndani yake ndiyo yalivyokuwa maisha yao, ndiyo maana hata hawa wenye kauli wawili walikuwa na maelewano geresha wakiwa wapo ndani ya ulingo wao mwingine ambao adhira ilikuwa ikiona kama walikuwa wakishindan kihoja.


****


 Joephine akiwa hana nguvu aliburuzwa hadi sehemu ya ndani ya nyumba ya Jama Wa Majama, alipelekwa hadi eneo ambalo kulikuwa na chumba kimoja kikiwa na bomba la chuma refu sana lililotokeza juu ya dari ya chumba hicho. Hapo alifungiwa kwenye bomba hilo imara kwa pingu kuanzi mikono hadi miguu. Ilikuwa ni mara ya kwanza kuanza kujuta kwenye maisha yake tangu ajiunge na upande huo haramu, sasa alikuwa ameishia kwenye eneo ambalo ilikuwa ni ngumu sana kupona au kutoka. Alikuwa ameingia kwa mara ya pili kwa mtu ambaye alinusurika kuuawa naye, aliona kupona ilikuwa ni ngumu sana kwani mtu huyo  alikuwa najuta sana kwa kuendelea kwake kuwa hai juu ya mgongo wa radhi.


  Mbele yake Jama Wa Majama ambaye tayari alikuwa ameshapatiwa huduma muhimu baada ya kupatwa na baala la kipigo, alikuwa yupo yupo kwnye kiti huku Norbert ambaye hakuwa na mzaha hata kidogo akiwa yupo amesimama. Wote wawili macho yao yalikuwa yapo kwa binti huyo aliyekuwa amefanya matukio mazito sana ndani ya nchi hii, matukio hayo ambayo yalikuwa ni muhimu sana kwa wakubwa zake ambao walikuwa wamempa ulaji ndani ya nchi hii.

"Haya sasa jiangalie upo wapi kwa huo ujinga wako" Norbert alimuambia huku akimtazama usoni, maneno hayo yalimfanya awe ni mwenye kujuta sana.

"sasa jiulize ni nani atakayekusaidia hapa zaidi ya sisi kukupa huruma hii tunayotaka kukupa, tunahitaji ukweli wako tujue ambao wapo nyuma ya masuala haya na kwa ajili gani wapo yake" mzee wa waotot warrembo wapendezesha macho aliongea.


"Nor please nipo tayari kukuambia ile niahidi kitu kimoja tu nitakuwa huru" Aliongea


"Yaani pamoja na kutuletea maafa yote hayo bado unatuletea masharti huna akili wewe" Norbeet aliongea na akamfuata kwa kasi hadi karibu yake na kuanza kumpiga kipigo kizito kama alikuwa akipigana na mwanaume mwenzake, kipigo hicho kilimchosha tu Josephine ndani ya muda mfupi na alikubali mwenyewe kuongea.

"Ukweli wako ndiyo utakaotufanya tukuonee huruma  haya ongea kwa sasa, ukichelewesha dakika  moja tu utakuwa upo kwenye kipigo kingine. Sitaki zaha na watu kama nyinyi kwenye kazi yangu kabisa" Alipewa kitisho kizito ambacho kilikuwa kikienda kumpata kweli ikiwa ataenndelea na ukaidi wake alikuwa ameuonesha, Josephine hakuwa na namna mwenyewe aliutapika ukweli ambao ulikuwa unashabihiana kila kitu na ukweli ambao alikuwa nao Jama. Mwenye ukweli huo mwenyewe aliafiki kuwa alikuwa akiongea ukweli mtupu na hakukuwa na uongo ndani yake.

"Baada ya kueleza ukweli una machaguo mawili tu kuanzia sasa, chaguo la kwanza ni kwenda kwenye gereza la magaidi lililokuwa lipo Iringa huko porini ukutane na wenzako waliokuwa wapo kwenye kazi kma hizi au uuawe hapo" Norbeert alimuambiwa pasipo kumjonea huruma yeyote kutokana na mabalaa aliyokuwa ameyaleta, Josephine alibaki akiwa ni mwenye kuumia sana kutokana machaguo hayo aliyokuwa amepewa. Mwenyewe alichagua kwenda kupelkewa huko gerezani,  lilikuwa ni gereza jipya lililokuwa mbali sana ambako hakukuwa na njia yoyote ya gari ingeweza kufika huko. Kamishna Wilfred na wale wote waliokamatwa kwa matukio ndani ya nchi ya Tanzania walitupwa huko ambako kulikuwa na mateso sana kuliko kawaida kwa wenye ujeuri.


  Wapo ambao gereza hilo walilifananisha na gereza la Guantanamo la ndani ya bara la Amerika, yote ilikuwa ni kutokana na jinsi lilivyo. Gereza hilo lililogharimu mabilioni ya shilingi katika kukamilika kwake na waliokuwa wamekamatwa kwenye kisa cha WAKALA WA GIZA na wale wote aliokuwa wamekamatwa kwenye matukio makubwa nchini walipelekwa huko kuanza maisha yao huku Magereza ya kawaida yakiendelea kuwa na wafungwa wa kawaida. Matukio ya kuawa  pamoja na kufanyiwa vitu vibaya baadhi ya wafungwa  wa kawaida waliokuwa wamechanganywa na wale wa matukio  ndiyo yalipelekea kujengwa kwa gereza hilo. Sasa Josephine alikuwa akitaka kupelekwa huko ambako kulikuwa na wanwake wajeuri zaidi yake, lililokuwa na utukutu zaidi yake.


"Mama eh! Huruma yako ni kwenda Nyumba ya giza huko na si vinginevyo hivyo jiandae tu  wewe ni wa kutupwa huko" Norbert alimuambia kisha akatoka kwenye eneo hilo akiwa ameongozana Jama Wa Majama  ambaye alikuwa akimtegema yeye kuweza kutembea vizuri.


****


   Baada ya kuweza kutoroka mkono wa kifo kutoka kwa Norbert alipoona amezidiwa nguvu, muda ambao Josephine alikuwa akimaliza kuutapika ukweli yeye alikuwa yupo ndani ya nyumba ya wageni kwani alikuwa yupo kwenye wakati mgumu sana kwenda kwenye makazi ambayo tayari yalikuwa yamegunduliwa na Norbert. Askofu muda huo alichukua simu na kumpigia Scorpio akijua bado yupo hai lakini simu yake iliita tu bia ya kupokelewa, aliipiga mara nyingi zaidi lakini jibu ilikuwa ni kazi bure kwani simu hiyo haikuwa ikipokelewa kabisa na huyo aliyekuwa akimpigia simu. Jambo hilo lilimuudhi sana akaona kuwa alikuwa akidharauliwa na huyo kijana wake, alijua kuwa alikuwa yupo kwenye umalaya kumbe hakuwa si miongoni mwa waliokuwa wakivuta pumzi ndani ya dunia hii. Hasira zilimpanda hasa na ziliongezewa na maumivu yaliyokuwa yakimsumbua, ubavu ulikuwa ukimsumbua sana na kuchnganya na kutojibiwa kwa simu yake ilikuwa ni hasira kabisa.

   Ubavu uliokuwa umechezea dhahama nao ulikuwa ukimjua kumtesa sana, alishindwa hata kuulalia na akajikuta akiuweka juu. Hakika ubavu huo ulijua kumpa masharti kama vile alikuwa yupo kwa Mganga wa kienyeji aliyekuwa akimtengezea dawa. Jeuri zote na ukaidi wote aliokuwa nao mbele ya ubavu huo , hakuwa mjanja kabisa kwani jinsi ulivyokuwa ukimuuma. Haukuwa umevunjika ila cha moto alikuwa amekionja na muda huo kinachoma ulimi wake, hakika maumivu yalijua kumkata hata uwezo wake wote wa kumudu kimapigano ukawa hauna msaada kwake. Alishikwa akashikika, alipatwa na akapatikanika kutokana namaumivu hayo yaliyokuwa yakimsumbua kwenye sehemu hiyo ya ubavu, kunnyanyuka ilikuwa ni mthili ya gari bovu kuupanda mlima kutokana na maumivu hayo aliyokuwa kiyasikia.  Yaliyokuwa yamezidi kabisa tofauti na muda ule almabo alikuwa amemkimbia adui yake, siku hiyo alikiri kabisa kuwa alikuwa amepigana na kiumbe mwenye uwezo kama yeye aliyekuwa amemzidi ujanja katika mapigano.

"Mara nyingine sitokubali, nishajua mbinu zake za kupigana sasa tutapambana vizuri sana" Aljisemea huku akiwa ameulalia ubavu usio a maumivu.


****

          [5]
    ASUBUHI ILIYOFUATA


  Hadi mwangaza wa siku mpya unaingia Norbert alikuwa yupo ndani ya nyumba ya Jama wa Majama ambaye alikuwa na nafuu muda huo hadi kuweza kutembea mwenyewe, ukweli wote uliokuwa ukiwahusu walikuwa wanao kwenye tarakilishi hizo na ilikuwa ikisubiriwa muda muafaka wa kuweza kuwasilishwa kwa Mheshimiwa ili kuweza kumuokoa yule ambaye alikuwa hana hatia kabisa. Yale manenosiri ambayo yalikuwa kwenye tarakilishi tofauti yalikuwa tayai yameshawekwa bayana , Jama alitumia muda huo kumuelekeza kila kitu Norbert juu ya uchambuzi wa maneno hayo. Siku hiyo Norbert alikiri kabisa wale waliokuwa wameanda utafiti huo walikuwa wametumia akili sana katika kuyaficha maneno hayo kwani pamoja na ujuzi kwa wote wa kujua maneno ya kimafumbo alishindwa kuyabaini maneno hayo yaliyokuwa yana maana kubwa.

  Alikubali kabisa kuwa Jama na kundi lote waliokuwa wamendaa utafiti huo walikuwa ni watu ambao walikuwa na akili ambazo waliziunda kwa pamoja wakapata kile ambacho kilikuwa kikihitsjika. Aliwapa pongezi kwa kazi hiyo nzuri waliyokuwa m
wameifanya na hawakukaa kabisa ndani ya nyumba hiyo, ilipofika majira ya saa nne asubuhi wote kwa pamoja walitoka na kuelekea zilipo ofisi za Moses ambaye alikuwa akimtafuta mfanyazi huyo aliyekuwa yupo chini yake kwa siku kadhaa alizokuwa ametoweka kwenye upeo wa macho yake.


  Safari yao ilifikia kwenye ofisi za za maabara ya Umoja wa mataifa huko hawakumkuta kabisa, hawakuwa na changuo jingine iliwabidi watoke na kwenda zilipo ofisi za  Idara ya usalama wa taifa kwani walijua kabisa takuwa yupo huko na alikuwa na kazi muhimu sana. Safari yao ilifikia kwenye ofisi hizo na waliingia hadi ndani, wote walisema shida ya kutaka kumuona Moses ambaye alipopewa taarifa ya uwepo wao eneo hilo aliridhia moja kwa moja waingie ndani. Norbert na Jama waliingia ndani ya ofisi ya Moses ambako alimkuta akiwa amekaa kwenye kiti chake akijizungusha, aliwakaribisha kwenye viti akiwa hajamjua kabisa huyo mwingine aliyekuwa na Norbert alikuwa ni nani.

"Mkuu nafikiri muda wako wa kuniona ndiyo huu umewadia" Jama aliongea kwa sauti yake ambayo ilikuwa imezoeleka na Moses na kupelekea mkuu wake huyo wa kazi ashangae sana kwani hakutarajia kabisa.

"Jama is tha you?" Moses aliuliza


"Ys its me, nimekuja kwa ajili ya kumkomboa yule asiye na hatia ambaye alikuwa yupo mbioni kutumikia hukumu isiyo yake" Jam aliongea.

"Aisee ni bora umeonekana yaani wewe ni mtu muhimu sana kuweza kuwasilisha ushahidi ulionao kwa Mheshimiwa kwani nao ulikuwa ukihitajika kwenye kesi ya Mheshimiwa Kabinuki. Huo ndiyo ungeweza kuamua kila kitu ila kwa ushahidi wa sasa umemuweka ndani" Moses aliongea, muda huohuo Jama alifungua tarakilishi yake ambayo alikuwa kaitunza kama mboni ya macho na kumpatia Moses hukua akiwa tayari ameshaingiza neno siri. Ilikuwa ni ndani ya siku ambayo Mkurugenzi huyu wa idara hii nyeti aliweza kabisa kukubaliana na maneno ya Norbert na kumjuona waziri huyo aliyekuwa amewekwa ndani hakuwa na hatia kabisa, alisoma ushahidi wote muhimu na kisha akairudisha Tarakilishi ile kwa mwenyewe kwani hakuwa na mamlaka ya kukaa nayo kutokana na masharti liyokuwa ameyatoa Rais Zuber wakati akitoa kazi hiyo kwa watu wake.


"Nikweli kabisa hapa Mheshimiwa ha  hatia na wale wawili ndiyo wenye hatia" Moses aliongea

"Ndiyo hivyo nilitaka ujue tu hilo kwani sikuona hatia aliyokuwa nayo hasa nikijiuliza jinsi alivyoshikwa kwa haraka sana na vidhibiti vilijulikana. Huu ushahidi unatakiwa ufike kwa Mheshimiwa mwenyewe ndiyo aamue" Norbert aliongea


"Kibaya zaidi Mheshimiwa kasafiri kikazi mara moja na anaingia nchini Alhamisi" Moses aliwaambia huku akiona taarifa hiyo ilikuwa  ikichelewa kabisa kufika kwani ndiyo kwanza ilikuwa ni jumapili

"Thats another issue, huyu jamaa inabidi alindwe kama mboni ya macho hadi inafika siku hiyo" Norbert aliongea kisha akamtazama Jama usoni halafu akamwambia, "Inabidi ukakae kwenye ofisi zetu hadi siku itakapofika kwa usalama wako yule Askofu ni mtu mmoja hatari sana"

"Hilo la muhimu awe chini ya uangalizi wako wakati unamalizia kazi yako" Moses alisisitiza


"Kingine kabisa dogo langu napenda nikuambie kuwa hapa ofisni kwako kuna msaliti ambaye ndiye anayeuza taarifa kwa maadui wa nchi hii. Mwanzo kabisa nilijua kabisa kuwa huyu jamaa kirudi jijini hatokutafuta kwa simu yako ya mkononi kamwe bali atatumia ya ofisini humu akijua ni salama zaidi kwani ya mkononi kunaswa mawasiliano ni kitu rahisi sana. Na kweli alitumia simu hiyo na hatimaye akakuambia yupo jijini, nilipokuwa nimesikia hicho ulichooongea kutokana na kukupa taarifa ya kufuatilia simu zako kuna mtu ambaye alikuwa tayari ameshanasa mawasiliano hayo sasa mjiulize vizuri alikuwa ni nani. Unasaji wa simu za humu mnaujua wenyewe hakuna wa nje anayeujua, jiuize ni nani huyo?" Norbert alieleza kwa kirefu, maelezo ambao yaliamsha kabisa akili ya Moses na kuwafikiria wafanyakazi ambao walikuwa wapo chini yake.

"Hii inaonesha hii simu ninayotumia imewekwa hardware inayofanya haya na sijui ni nani huyu" Moses aliongea na kisha aliichukua simu yake ya mezani na kuigeuza,aliifungua simu hiyo bila ya kifaa chochote kwani ilikuwa imefungwa kwa mtindo kama wa tarakilishi zisizo na nati. Aliipekua ndani ambako alitoka akiwa na kifa kidogo klichokuwa kikiwa taa ya rangi ya bluu na akamuonesha Norbert ambaye alisikitika tu.


"Huyu ndiye mchawi ndani ya ofisi hii ananasa mawasiliano na pia simu zinazoingia na eneo zinapotoka"  Norbert aliongea na kisha alimpa ishara Moses jun ya cha kufanya kwani walikuwa wametambua wazi kuwa walikuwa wakisilikizwa na msaliti huyo ambaye yupo humo ofisini.




ITAENDELEA!!

  

No comments:

Post a Comment