Tuesday, February 21, 2017

WITO WA KUZIMU SEHEMU YA KUMI NA TISA

WITO WA KUZIMU

NA: HASSAN O MAMBOSASA

MAHALI:TANZANIA


SIMU:+255713776843
      +255762219759

WHATSAPP:+255713776843
         +255762 219759

BLOG: riwayamaridhawa.blogspot.com



SEHEMU YA KUMI NA TISA
Alipouona tu huo mwili alijikuta akiweka mkono kidevuni mwake na akaanza kukuna kidevu chake kilichokuwa hakina ndevu kutokana na kuzinyoa mara kwa mara, alipoacha kukuna aligeuza macho na kumtazama Askari ambaye alikuwa akikaribiana naye kicheo.

"Rangi hii ya ngozi ni dalili tosha ya kuwa aliuawa kwa sumu, sasa inabidi tuchunguze ili kuhakikisha hilo" Aliongea huku akivaa mipira ya mikono.





________________TIRIRIKA NAYO
  Alipomalza kuvaa mipira yake ya mikononi alivaa mpira mwingine wa kufunika pua na mdomo na kisha aliusogelea mwili ule, aliutazama ule mwili kwa umakini sana katika kila sehemu na kisha akawageuka wale maaskari ambao walikuwa wamemuita hapo.

"Nahitaji huu mwili upelekwe kwenye eneo la uchunguzi ili niufanyie utafiti kuna zaidi ya jambo, huko ndiyo tutapata majibu yote jinsi sumu hii ilivyoingia mwilini ulikuwa ni muda gani na akatokwa na uhai muda gani" Maaskari wadogo walitii kiutiifu waliposikia kauli hiyo kisha wakajongea hadi ulipo ule mwili, walivaa mipira nao  kisha wakaubeba huo wili kwani gari la kuuchukua lilikuwa limeshafika tayari kuuchukua mwili huo.



****


  Wale majambazi waliokuwa wakijaribu bahati yao ya kufanya uhalifu mbele ya Jama Wa Majama walijikuta wakiwa hawana ujanja tena, dereva wagari hilo ndiyo tamaa kabisa illimfanya abaki na majuto muda huo. Ama kweli tamaa mbele mauti nyuma na hii ilikuwa imejidhihidrisha kwani hayo ndiyo yalikuwa matokeo ya tamaa yake aliyokuwa ameileta kwa kumuona Mzee tu akiwa amekumbatia Mzigo wake. Muda huo alikuwa ameishaingia kwenye eneo la Pugu sasa likakata kona kwenye njia iliyokuwa ikipita karibu  na kanisa la Pugu Kajiungeni, alifuata maelekezo ya Jamba ambaye alikuwa ameshika silaha mkononi mwake na kisha gari hiyo iliingia kwenye nyumba moja ya kifahari ambayo walipoisogelea tu lango lko lilifunguka mara moja. Gari hilo lilingia ndani ya nyumba hiyo ambayo ilikuwa na njia ya kuingiza magari iliyokuwa ikielekea hadi chini, walifika kenye eneo la chini ya ardhi kabisa ya nyumba hiyo na kisha aliamriwa kuegesha gari kwenye eneo ambalo kulikuwa na kijana mwenye mwili mkakamavu alikuwa amesimama akisubiria kwa hamu sana waweze kusimama. Baada ya wao kusimamisha gari tu yule kijana alifungua mlango na kuwatoa mmoja baada ya mmoja akiwa amewawekea silaha.


  Jama mwenyewe alishuka kwenye mlango akiwa mzigo wake na kisha aliwavuta wale waliokuwa wamepoteza fahamu hadi nje ya gari hiyo, dereva pamoja na yule jambazi ambaye alikuwa amebakia walikuwa  wakitetemeka sana  kwa uoga kutokana na kumvamia mtu ambaye walikuwa hawamjui. Waliwaku wakimuona ni Mzee aliyekuwa amechoka lakini aliposhuka ndani ya gari hilo alionekana yupo imara kabisa na hakuwa na dalili ya kuwa mtu aliyechoka. Walishngaa sana na hapo wakaona kuwa walikuwa wameingia kwenye anga ambazo hazikuwa zao kabisa, wote walibaki wakimtazama Mzee yule kwa huruma sana wakitamani hata awasamehe kutokana na jambo hilo walilokuwa wakitaka kumfanyia.

"Huruma yenu mimi haiwezi kunibadilisha niwaaachie, inaonekana mchezo huu mshauzoea nyinyi sasa nataka mkitoka hapa mkawasimulie wenzenu kilichowapata kutokana na kufanya ujambazi wenu. Nyote mna nguvu za kufanya kazi nyinyi lakini hamkuona njia za kufanya kazi zaidi ya kuchukua mali zisizo zenu siyo sasa ngoja muipate dawa mmeingia pabaya hapa"Jama aliwaambiwa kisha akampa ishara yule mtu ambaye alionekana yupo chini yake kwa utiifu aliokuwa akiuonesha, wote waliingizwa kwenye chumba kimojawapo ndani ya nyumba hiyo ambayo walikuwa wamejiiingiza wenyewe kwa kuendekeza tamaa zao.


****



  ALASIRI
 Ilikuwa ni kawaida yake kila akitoka kwenye ofisi zile kuja kupata kinywaji ili kuweka akili sawa, hakuna mtu ambaye alikuwa hamfahamu kabisa ndani klabu moja maeneo ya Ilala ambayo muda wa mchana huwa ni sehemu ya kunywea vinywaji na usiku huwa ni sehemu ya muziki. Siku hiyo aliingia ndani ya Klabu hiyo kama ilivyo kawaida yake akiwa ni mwenye mawazo tele kwani alikuwa ameshapewa taarifa ya kuuawa kwa rafiki yake kipenzi ndani ya nyumba yao huko Kibada. Scorpio aliagiza pombe akiwa kwenye meza kuu ndani ya Klabu  hiyo, alionekana kunywa pombe hiyo kwa pupa sana. Pombe ilipoisha aliongeza nyingine na kisha akaendelea kunywa kama kawaida huku akitikisa kichwa kuendana na mdundo wa muziki ambao ulikuwa ukiendelea humo ndani, haikupita muda mrefu kwenye eneo alilokaa alikuja kukaa Msichana mwenye urembo wa kuvutia  akiwa amevaaa kaptula fupi ambayo iliacha mapaja yake nje. Msichana huyo alipokaa tu hakujishughulisha kabisa kumuangalia Scorpio yeye alipaza sauti kuagiza kinywaji na kupelekea Scorpio amuone ambapo alibaki akimtazama kwa sekunde kadhaa huku akiutazama mwili wake ambao ulikuwa una mvuto kuliko kawaida, ALijikuta akipiga uruzi baada ya kuuona mwili wa mrembo huyo ukiwa na unavuti sana na kisha alimbania jicho baada ya Mlimbwende huyo   alipomtazama kwenye uso wake.

"Hellow" Alimsabahi

"Hi" Alijibiwa na kisha mrembo huyo akaweka umakini wake kwenye kinywaji hiko alichokuwa ameagiza, hilo halimkutia karaha kabisa aliona ilikuwa ni jambo la kawaida sana.

"My I Know your name(naweza kukujua jina lako)?"

"Hey   do not about the bush, say how much do you have(Hey usizunguke sana sema una kiasi gani)" Kauli hiyo ilimfanya Scorpio atabasamu kwani alikuwa ameingia mulemule alipokuwa akipataka, alikuwa amemtamani sana huyo mwanamke lakini alipotajiwa kuhusu hilo la bei alitambu wazi alikuwa ni kahaba hivyo halikuwa tatizo.

"Its Full time baby, are you ready?(Ni muda wote mpenzi upo tayari?)"

"Its you(ni wewe)" Alipopewa jibu hilo alimpa ishara huyo msichana ambaye alichukua kinywaji chake na kisha akaongozana naye, kwakuwa Makahaba wengi walikuwa wakijiandaa kwa kila kitu yeye alikuwa hana wasiwasi wowote kwani alijua kabisa huyo msichana alikuwa akielekea mahali ambapo alipazoea kwa ajili ya kufanyia kazi. Moyoni alijipa ushindi kwa kujifanya hajui kiswahili kwani hilo limemfanya aweze kuwapata wasichana wa namna hiyo wengi sana, huyo aliona ilikuwa ni kawaida kumpata ikiwa  ni Kahaba sasa alikuwa akielekea kutimiza hitaji lake la kimwili na huyo msichana huyo mrembo sana mwenye umbile la kibantu ambalo lilikuwa ni ugonjwa sana kwake.


 Walitoka kwenye eneo hilo hadi mtaa wa pili ambako kulikuwa na nyumba ya kulala wageni ya kisasa sana, hapo walikuta funguo ilikuwa tayari kabisa na ikamfanya ajue kabisa kuwa hiyo ndiyo ilikuwa eneo ambalo Mrembo huyo alikuwa akilitumia kujipatia kipato chake kwa kutegema viungo vyake alivyoumbwa navyo. Waliingia ndani ya chumba hiko ambacho kilikuwa na kila kitu ndani, Scorpio baada ya kuingia ndani ya chumba hiko alianza papara yake ya kuuparamia mwili wa msichana huyo kwani ulikuwa ni ugonjwa wake mkubwa sana tangu alipoingia ndani ya nchi hii.

  Alitokea kuvutika sana na wasichana wa kibantu tangu alipoonja ladha zao ndiyo maana hakung'atuka kabisa, ilikuwa ni kawaida sana kila msichana aliyekuwa kinavutia kumfuata na kisha kumtongoza akiwa namna hiyo ilikuwa ni kawaida yake kujitolea pesa yoyote ilimradi aonje asali iliyopo. Hakika alikuwa ni Simba ambaye alikuwa ameonja nyama ya binadamu hivyo kuiacha kula nyama hiyo ilikuwa ni ngumu sana, alikutana na ladha mpya kabisa tofauti ya ladha ya mawindo yale aliyokuwa ameyazoea huko alipotoka. Kitu kipya na mazoea yake kulimfanya awe namna hii na si kama alivyokuwa akivila huko alipotoka, hakika alikuwa mgonjwa wa hicho kitu kuliko kawaida.

  Alianza kuutomasa mwili wa binti huyo akakutana na laini ambayo ilikuwa ikimpa hamasa ya kutaka kuendelea kufanya kile ambacho alikuwa akikifanya, alipotaka kupunguza vizuizi vya mrembo huyo alikutana pingamizi ambalo hakuwahi kukutana nalo kutoka kwa warembo wote ambao aliwahi kukutana nao tangu aanze kuonja asali mpya mali ya bara adimu sana.

"What?!" Aliuliza kwa mshangao akionekna alikuwa hajapenda kabisa kuzuiwa huko kwani alikuwa akilipia kila kitu.

"The door please close it(Mlango tafadhali ufunge" Hakubisha kabisa aliuachi mwili wa Msichana huyo na kisha alienda kuufunga, muda huo msichana huyo alichukua taulo lililokuwa limetundikwa humo ndani na kisha akawa anaingia mahali ilipo choo na bafu ndani ya chumba hiko. Hiyo ilimfanya Scorpio akereke lakini alipewa tulizo muhimu na akaombwa asubiri kwani alikuwa yupo naye kwa siku nzima, Msichana huyo alizama bafuni muda huo akimuacha Scorpio akitoa mavazi yake na kisha akabakiwa na kaptula tu ambayo ilikuwa imeishia mapajani. Alifika hapo kitandani akiwa na hamu sana na muda huo tayari 'Ali haji bin Kofia' alikuwa ameamka kutoka kwenye usingizi wake lakini amekaa mguu sawa, alikuwa akizidi kumsumbua Scorpio katika muda huo ambao alikuwa akimsburia huyo mrembo aliyekuwa amezama ndani ya maliwato kwa ajili ya kubadili nguo.

 Hakuchukua muda mrefu sauti ya hatua zilisikika ambazo hazikumfanya ashtuke hata kidogo, kutawaliwa na mawazo ya jimai yalikuwa yamemsahaulisha kabisa Mrembo aliyekuwa ameingia huko ndani alikuwa amevua viatu kabisa na alichukua viatu vya wazi viliwekwa maalum kwa ajili ya kuuingia huko. Alizidi kutabasamu aliposikia mlio wa viatu ivyo kutokana na tamaa kuizidi akili yake ya kufikiri, alipokuja kutahamaki aliona bastola yenye kiwambo cha kuzuia sauti ikitokea kwenye mlango wa huko Maliwatoni. Mshongo wote uliokuwa umekuja ndani ya mwili wake ulimtoka muda huohuo akiwa ameitazama Bastola hiyo akijua tayari alikuwa amekwisha, alinyanyuka hapo  ktandani lakini bastola ile ilichezeshwa kumpa ishara akae hapohapo.  Mwenye bastola hiyo alipojitokeza alimuona hakuwa mwingine ila ni Norbert ambaye walitaka kuyatoa maisha yake siku chache zilizopita, alishtuka sana kwani alikuwa amekuja kwenye muda ambao hakutaraji kabisa. Sasa alianza kuulaumu mshongo wake ambao alikuwa akiuendekeza kila akiona msichana mrembo wa kibantu ambaye alikuwa ana umbo tata, alijilaumu katika muda ambao alikuwa ameshachelewa kabisa kwani kila kitu kilikuwa kimeharibika. Norbert alipiga hatua kuingia ndani ya chumba hicho akiwa anatabasamu tu huku akimtazama adui yake ambaye alikuwa ameingiwa na uoga ingawa bado alikuwa akijifanya yupo sawa.

"Scorpio hatimaye tumeonana ten kwa mara ya pili tangu siku ile tulivyokuwa pamoja kule Singita na bosi wenu shoga pamoja na mume wake" Norbert aliongea maneno ambayo yalimshtua sana adui yake ambaye hakujua kabisa kuwa alikuwa akifuatilia hivyo.

"Unashangaa nini? Kutana na yule Mtumishi wa Mungu mliyefikiri mlimuua kule Mbugani na bomu sasa nimerejea tena sifi kijinga namna ile" Norbert alizidi kumuandama Scorpio kwa maneno ambayo yalikuwa yakimfanya azidi kuchanganyikiwa na hakujua ndani ya nchi hii kulikuwa na watu wajanja zaidi hadi kufikia hatua hiyo aliyokuwa ameifanya.

   Muda huohuo yule Kahaba ambaye alikuwa amemchukua kule Klabu alijitokeza akiwa amebadili mavazi, alikuwa amebadili pia mtindo wa nywele ambao ulikuwa umemfanya aonekane ni mtu tofauti kabisa. Alisogea hadi akaja kusimama kwenye eneo ambalo lilikuwa lipo jirani kabisa na eneo alilokuwa yupo Norbert,yule naye aliachia tabasamu huku akimtazama Scorpio ambaye alionekana kutoamini.

"Huyu ndiye ulikuwa ukidhania kuwa ni Kahaba, muite NORMAL SERVICE TZ 97 au jina halisi ni Eva" Alimtambulisha hapo, Msichana huyu alikuwa ni mpelelezi wa EASA liyekuwa yupo chini ya Norbert. Huyu ndiye alshiriki katika kumuwekea mtego Thomas hotelini katika siku ile ambayo aliuawa kwa bomu, amerudi tena baada ya kuitwa na mkuu wake wa kazi ambaye alimpa kazi ya kumnasa huyo Mzungu mpenda wasichana.

"We mzungu koko karibu sana kwenye anga ya EASA nafikiri ulikuwa hujui kama ukanda huu sasa hivi unatisha kwa ujasusi sasa jionee mwenyewe" Eva aliogea huku akimuegemea Norbert began

"Eti jana walikuwa wamekaa wanapanga kabisa kuwa waninase kupitia mwanamke akiwa hajafikiria kabisa nilikuwa nimeshamjua kuwa yeye ana udhaifu uleule, sasa bwana Scorpio eleza mwenyewe  mkuu wake ni kina nani la hivyo nakuua taratibu na si kistarabu kama nilivyomuua Spider" Aliambiwa lakini kutokana na jeuri yake aligoma kueleza na alikaa kimya tu huku akitazama suruali  yake ambayo ilikuwa ipo mbali na  hapo, kutazama huko Norbert alikuwa ameshamuona muda mrefu sana na alimpa ishara Eva akaenda kuichukua suruali hiyo. Scorpio aligoma kueleza na hapo risasi ile yenye kiwambo cha zuia sauti ikatoa kikohozi hafifu sana, bastola hiyo ilitua kwenye mfupa wa paja na kumfanya ashikilie eneo hilo ndani ya sekunde chache tu baada ya maumivu kusambaa. Norbert alimtolea tabasamu tu na kisha alimuongeza risasi nyingine kwenye paja la upande mwingine.

"Yaani mpaka uongee leo ndiyo nitaacha kuvifyatua hivyo viungo vyako" Aliongea na kisha akikoholesha tena bastola na safari hii ilienda kuvua kwenye kifuniko cha goti, maumivu yalimzidia na hata alitamani kupiga kelele lakini alijizuia kutokana na uwepo wa mwanamke humo ndani. Alibaki akigaragara hapo kitandani huku damu ikimvuja, bado hakutaka kusema kuonesha ni jinsi gani alivyokuwa jeuri. Alipoongezewa risasi nyingine aliona kabisa kuwa angeweza kuongea hilo suala hakutaka kabisa, kwa kasi ya ajabu akichoamua kukifanya iikuwa ni kuuweka mkufu ambao alikuwa amevaa shingoni ambao ulikuwa na msalaba wenye mapambo ya ajabu. Alifumba mdomo wake kwa nguvu alipouweka mkufu huo kwa muda wa dakika kadhaa, alipokuja kufungua mdomo alikuwa hana uhai tena. Hapo wanausalama hao wa EASA wakajua kabisa kuwa huyo alikuwa amejiua kwa kutumia sumu na  hawakutaka kuendelea kubaki humo kwani walikuwa wakipoteza muda.


  Norbert alitoka hadi zilipo nguo za Scorpio na akazipekua, hakuona cha maana kabisa kwenye nguo hizo na aliamua kuziacha na kisha akafuta kwenye sehemu zote alizokuwa amegusa na kiganja cha mkono wake na kisha wote kwa pamoja walitoka hadi nje ya chumba hicho na wakaufunga mlango kwa ufunguo na kisha funguo hiyo  wakitua ndani ya chumba hicho kwa kupitia uwazi wa chini ya mlango, Baada ya hapo Norbert aliuzungusha mkono kwenye kiuno ch Eva na kisha akaanza kupiga hatua kuelekea naye nje kupitia eneo la mapokezi. Walipofika eneo la mapokezi Norbert aliingiza mkono mfukoni na akatoa funguo nyingine kabisa ambayo alimpatia Mhuhumu huyo, baada ya hapo waliaga na kisha wakatoka nje yNyumba hiyo hadi kwenye gari na kisha wakatokomea kwenye eneo hilo baada ya kuwa walikuwa wameshawapunguza nguvu maadui zao kwa mara nyingine ndani ya siku moja. Walikuwa wamecheza mchezo mmoja hatari sana ambao haukufahamika hata na Mhudumu mmoja wa ndani ya nyumba hiyo ya kulala wa geni ya kisasa zaidi, mchezo huo ndiyo maana walifanikiwa kutoka bila hata ya kubakisha maswali kwenye vichwa cha Wahudumu hao juu ya yule MZungu ambaye alikuwa ameingia na Eva mahala hapo. Muda huo hesabu ya haraka iliyokuwa imebaki upande wa maadui ulikuwa umebakia na watu wawili tu ambao ndiyo walikuwa na upinzani mkubwa sana, watu hao nao walikuwa wakihitajika kumalizwa ndani ya muda wowote  kwani mzee wa kazi alikuwa amedhamiria kumaliza kazi yake kabla ya muda aliokuwa amepewa.



*SCORPIO AMEKWENDA NA  MAJI

*JAMA WA MAJAMA JIJINI

ITAENDELEA!!





UKIHITAJI RIWAYA HII KUANZIA ILIPO HADI MWISHO, BEI NI  SHILINGI 2200. WASILIANA NASI KWA NJIA YA UJUMBE MFUPI WA  MANENO(SMS) KWENDA NAMBA +255762219759 AU WHATSAPP +255713776843

No comments:

Post a Comment