Showing posts with label Riwaya za kichawi. Show all posts
Showing posts with label Riwaya za kichawi. Show all posts

Sunday, November 27, 2016

MPYA! MPYA!




KIONJO KWA WALE WAPENZI WA RIWAYA ZA KICHAWI



DAR MPAKA SONGEA

“Shenzi kabisa nyinyi si wabishi sasa tune kama mtafika” Bibi yake Nyoni alisema huku akiweka macho yake kwenye maji yaliyopo ndani ya chungu.
Ndege iliyokuwa ikitumiwa na kina Nyoni ilionekana ikiyumba kila upande. Huku maji yaliyopo

Wednesday, November 16, 2016

WAKALA WA GIZA SEHEMU YA TATU



     

 RIWAYA: WAKALA WA GIZA

MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU: +255713776843
          +255762219759


WHATSAPP: +255713776843

       SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU MUUMBA WA ULIMWENGU WOTE KWA KUNIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA HII NIKIWA NA AFYA NJEMA




     SEHEMU YA TATU!!

           "nafikiri tu..." Moses aliongea lakini alishindwa kumalizia kauli yake baada ya simu ya Norbert kuita, Norbert alizuia Moses asiongee kisha akapokea simu akasikiliza bila kusema kitu hadi ikakatwa.

     Aliirudisha aliweka simu yake kisha katikitisa kichwa chake  halafu akavuta pumzi kwa nguvu akaiachia akmtazma Moses.

Friday, December 4, 2015

DHAHAMA SEHEMU YA MWISHO





     DHAHAMA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE



SEHEMU YA MWISHO!!
 Vijana hao walifaniliwa kuwateka Ally na Jamadin na kuondoka nao ambapo njiani Ally alipigwa kisogoni akazirai akatupwa kando ya reli mita chache kutoka katika mzunguko wa Kwa Minchi majira ya usiku, kupotea kwa Jamadin na Ally nyumbani kwangu ilikuwa ni huzuni sana kwa mke wangu lakini kwangu mimi ilikuwa ni kawaida kwani nilikuwa najua kila kitu. Tulikusanyika nyumbani wanaume wote huku mimi nikionekana kulia sana na nilibembelezwa hadi nikanyamza ndipo tulipoanza kujadiliana kimaigizo nini cha kufanya, baada ya mjadala wanaume wote sita tulikubaliana tuongie mtaani kumtafuta Jamadin na Ally na wake wote wakakaa nyumbani kwangu wakimbembeleza Farida.


****

Thursday, December 3, 2015

DHAHAMA SEHEMU YA KUMI NA SITA





 DHAHAMA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE


SEHEMU YA KUMI NA SITA!!
Mara ya kwanza nilianza kwa Faimu nikawa najipitisha sana kwao ili anuone nikijua nitamnasa tu kama nilivyonasa vijana wa hapo kijijini kumbe Faimu hakuwa kijana wa hivyo, uvumilivu uliponishinda niliamua kumuambia ukweli  lakini pia nilimkosa baada ya kukataliwa na akanitishia kumuambia Hamis.  Mara ya pili niliirudia tabia yangu kwa kumtaka Ally baada ua uzuri wake  kuonekana alipofikia kwenye balehe  lakini pia alinikataa nikajikuta nazidi kumsumbua nikijua nitampata tu kwani ni mtoto yule bado akili haijapevuka zaidi ya kupevuka mwili tu, nilipoona nakataliwa sikuchoka na niliamua kuanzisha mazoea ya kawaida naye.  Siku nilipokuja kuwafuma Farida na Faimu na wote wakakiri kuwa wana uhusiano ndiyo siku niliyoona ya kutumia sababu hiyo kwa njia mbili, kwanza ni kulipa kisasi cha kukataliwa na Faimu na pili ni kumteka Ally kiakili. Nilijua Ally ni bado ana akili za kitoto hivyo nilipanga nimuambie hii habari ili ajue ni jinsi gani nampenda hadi nikaamua kumuambia hiyo habari ili aamini moyo wangu upo kwake, pia nilitaka nimuambie mpenzi wangu juu ya usaliti wa rafiki yao kwao waweze kumfanyia kitu kibaya ili nimcheke na hata amkose Farida.

Wednesday, December 2, 2015

DHAHAMA SEHEMU YA KUMI NA TANO

RIWAYA: DHAHAMA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE




SEHEMU YA KUMI NA TANO!!
Niliendelea kujipa moyo nikijua ipo siku nitampata na sikutambua kama mawazo yangu ni sawa na kuchemsha mawe nikitegemea yatachemke kutokana na upendo mzito nilionao kwake, sikutambua kama najipa matumaini hayawezekani kutokea hivihivi kama kubadilika kwa majira ya mwaka kutoka kiangazi hadi vuli. Nilichojali ni kupata jibu sikujali itachukua muda gani hadi niwe naye, niliendelea kusumbuka katika kumueleza kila siku lakini niliambulia patupu na nikawa natembea na matumaini ya kumpata tu kichwani mwangu. Matumaini yangu yaliishi katika moyo wangu lakini baadaye yalikufa baada ya muda wa miezi kadhaa tu na nikajikuta nikiumia moyoni, kufa  kwa matumaini yangu kulikuwa ni baada ya kuingia kikwazo katika kumpata Farida...


****


Nakumbuka vizuri kijijini kwetu waliingia wageni ambao walipatiwa eneo ambalo baadaye  walilinunua wakajenga makazi yao ya kudumu, wageni hao walikuwa ni wenye asili ya tofauti na watu walioko kijijini

Tuesday, December 1, 2015

DHAHAMA SEHEMU YA KUMI NA NNE

 DHAHAMA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE



SEHEMU YA KUMI NA NNE!!
"Lakini Ally mpenzi wangu nimefanyaje?" Salma aliuliza kwa masikitiko makubwa huku akionekana kuumia baada ya kusukumwa.
"Unajifanya hujui siyo tena usiniite mpenzi wako kuanzia hivi sasa, we wa kunifanya mimi mtumwa wa ngono hadi umesababisha nisioe wakati natakiwa kuwa na familia sasa hivi" Ally alifoka.
"Ally nakupenda ndiyo maana nimefanya hivyo hadi nikazaa na wewe" Salma akaongea huku akilia.
"Weee tena ishia hapo hapo" Ally alimkaripia huku akimuongeza teke la mguu Salma.
"Ally nikatae ila ukae ukijua Hamida siyo mtoto wa mume wangu bali ni damu yako, ndiyo maana hata alipozaliwa kaka yako alikutania umefanana naye miguu ila ukweli ile ni damu yako kabisa" Salma aliongea huku akilia, Ally alipuuza maneno ya Salma akaondoka eneo akimuacha akilia ingawa kuna jambo lilikuwa likiisumbua akili baada ya kusikia maneno hayo.



****


"  "Ally huyu mtoto kafanana na wewe hiyo miguu balaa ingawa ana sura ya mama yake na baba yake" Shafii aliongea huku akicheka.
"Haaaa! Shemeji nawe waanza kwahiyo waataka sema kafanana na babaye na Ally pamoja nami" Salma alisema huku akimtazama Shafii.
"Ndiyo hivyo ahemeji" Shafii alisema.
"Wewe Chumbio waleta zako sasa huoni kama hiyo miguu ni ya mama yake kabisa, wamefanana tazama kucha hizo uache msifia mdogo wako" Hamis aliongea na kusababisha wati wote wacheke humo ndani.
"Bonoeza usichukie basi masihara ni jadi yetu tangu twacheza michezo ya kitoto, hongera bwana kwa kupata binti mrembo huyo na urembo wake unaonekana tangu akiwa mtoto" Shafiu aliongea huku akimpa mkono wa pongezi rafiki yake kipenzi.
"shukrani Chumbio rafiki wa tangu utotoni" Hamis aliitikia huku akicheka
"sasa Bonoeza hapo inabidi ufuge mbwa na bunduki ununue mapema maana wajanja wataanza kuja kutoa salamu sana kumbe wataka wampate malkia hapa" Shafii alisema na wote waliopo nyumbani kwa Hamisi wakacheka " Maneno aliyoambiwa na Salma ndiyo yalivuta kumbukumbu yakamkumbusha siku hiyo ambayo Hamida alikuwa ndiyo kaletwa nyumbani baada ya kuzaliwa katika hospitali ya Ngamiani, alizidi kukumbuka zaidi na hapo akakumbuka tukio jingine kabisa baada ya kumuona Hamida akiwa na miaka mitano tu tangu azaliwe na siku hiyo alikuwa akibadilishwa nguo na mama yake Salma, siku hiyo alimuona Hamida akiwa ana mwili unaofanana wake sana. Ally alikumbuka zaidi juu ya siku hiyo na akawa anajifikiria kwa umakini haswa ndipo akajikuta anaamini lakini siyo kwa asilimiia zote yale maneno aliyoambiwa na Salma.
"Dah nimefanyishwa dhambi mbaya ya kuzini na mke wa mtu bila kujijua" Alky aliongea huku akikata mitaa na alionekana ni mwenye majuto makuu juu ya jambo hilo ingawa hakutegemea kama atalifanya, alitembea huku uelekeo wake maalum ukiwa haujulikani kwani alikuwa anazurura mitaani tu.
"ni bora nilale nje kuliko kulala kwenye mali haramu niliyokuwa nimekabidhiwa na nikajikuta nimeipokea bila kujijua, ni bora nisifanye kazi niwe masikini kuliko kuitumia hii elimu niliyosomeshwa kwa kutumia fedha haramu zilizosababisha mwanadamu mwenzangu amwage damu kwa manufaa ya wengine. Shahada nimeipata kwa pesa zilizotokana na damu ya mwenzangu kumwagika, nawachukia Shafii, Hamid, Hassan, Hussein, Falzal, Hamisi pamoja  mke wako Salma aliyetoa kitu kichafu ili aangamizwe kiumbe asiye na hatia. Hisan Shelukindo pia mwanaharamu mkubwa wewe umekuwa na maisha mazuri kwa ukatili wenu  huo" Ally aliongea kwa hasira akiwa tayari ameshafika Sahare kwa kutembea tu bila hata mpangilio; alihisi uchovu kwa kutembea siku hiyo nzima na akakaa katika baraza la maduka ambayo yalikuwa ndiyo yamekamilika ujenzi wake lakini bado hayajafunguliwa. Alijiona ni mmoja wa wenye makosa kwa kutumia sehemu ya mali iliyotokana na  njia haramu ingawa hakujijua, alijikuta hata akilengwa na machozi na hatimaye alianza kulia kimya kimya hadi pale alipochoka akainuka kwenye baraza hiyo.
"Bora uwe masikini utaabike kuliko uwe tajiri kwa njia isiyo ya halali bila kujijua, inauma sana" Ally alisema kwa uchungu huku akinyanyuka tena barazani hapo na kuanza kutembea kama ilivyokuwa awali, alitembea akawa anafuata uelekeo wa nyumbani kwa baba yake hadi alipofika akaingia ndani na moja kwa moja akaenda kujitupa sebuleni akalala usingizi mzito bila hata kuwa amekula kitu chochote siku hiyo.

   Asubuhi ya siku iliyofuata aliamka akajisafisha mwili wake akatoka hadi nje, akamuona dereva wa gari za baba yake akiwa yupo barazani akipata kifungua kinywa akamsabahi kisha akawa anaelekea getini.
"Kaka unaelekea wapi nikutoe maana gari zipo hapa" Dereva wa baba yake alimuambia.
"unaweza ukapumzika kaka mkubwa" Ally alimuambia dereva wa gari ya baba yake kisha akatoka nje akawa anaelekea ilipo barabara ya Mombasa, alitembea hadi akipoifikia hiyo barabara akamuita dereva wa pikipiki akaja mara moja.
"Mpirani kaka" Ally alimuambia dereva wa pikipiki ambaye alimchangamkia akamuambia apande tu bila hata kutaja bei, Ally alipanda hiyo pikipiki na safari ikaanza ambapo ilichukua dakika kumi na tano kwa mwendo wa pikipiki akawa ameshafika Mpirani akampa dereva yule pesa yake kisha akaingia mtaani na akatembea hadi mahali ambapo nyumba zipo moja moja na hatimaye akaifikia nyumba kubwa ambayo ipo kama gofu tu ikiwa ipo katikati ya shamba kubwa  ikionekana  kuwa ipo peke yake mbali na makazi ya watu wengine. Nyumba hiyo ilionekana kutolewa milango na baadhi ya madirisha baada ya kukaa siku nyingi bila kutumiwa kama makazi ya watu na eneo zima lenye kuizunguka nyumba hiyo lilikuwa  na majani mengi yaliyoonekana hayaku punguzwa kwa muda mrefu.
Ally aliingia ndani ya nyumba hiyo iliyoezekwa kwa bati  lililochakaa na sakafu ya chini ilionesha kuwa ni ya udongo mwekundu  ambao hutumiwa kukandika kuta za nyumba za udongo, ilikuwa ni nyumba kubwa yenye  vyumba takribani vinne na sebule ambayo ndani ina kuta za udongo zilizowekwa plasta kwa nje. Sebule kubwa ya nyumba hiyo ilikuwa na usafi mkubwa kupitiliza ambao ulimshangaza sana Ally na vyumbani kulikuwa kuna nyuzi nyingi za buibui kiasi kwamba haiwezekani hata kidogo mtu wa kawaida kuingia humo ndani bila hata kusafisha hizo nyuzi za buibui, Ally aliangalia kila chumba akawa anakumbuka matukio tofauti ambayo yalikuwa yakifanyika hasa kipindi ambacho anaishi katika nyumba hiyo ambayo kwa sasa imetekelezwa na mwenyewe.
"Ni historia nisiyoweza kuisahau na ni mazingira yasiyoweza kusahaulikavkwa mtu kama mimi na natamani niyarudie niishi kama nilivyokuwa awali huenda amani ya moyo wangu itarejea kama ilivyokuwa awali" Ally aliongea akiwa amesimama katika mlango wa chumba ambacho ndiyo alikuwa akikitumia kipindi akiishi katika nyumba hiyo.
Akiwa amesimama hapo alisikia sauti ya mtu akipiga uruzi kutoka nje ya nyumba hiyo na ikamlazimu atoke aende kutazama ni nani huyo, alipokuwa akikaribia mlango wa kutokea mlango wa nyumba hiyo alikutana na kijana wa kisomali aliyekuwa akifanana sana na mtu ambaye alikuwa anamjua ila jina lilikuwa limemshamtoka kichwani mwake. Kijana huyo alikuwa amevaa kanzu nyekundu  iliyomka vyema na kofia ya rangi ya kahawia, Ally alipomuona huyo kijana alizidi kuvuta kumbukumbu juu ya alipomuona lakini hakukumbuka chochote.
"habari yako kijana" Ally alimsabahi yule kijana.
"salama tu, shikamoo" Yule kijana aliitikia.
"Marhaba sijui ni nani mwenzangu" Alky aliitikia kisha akamuiliza swali yule kijana.
"naitwa Fahmi ni mjukuu wa mzee mmoja maarufu wa kiarabu anayeitwa  Muburaka" Yule kijana alieleza.
"Mzee Mubaraka huyuhuyu baba yake Faimu waliyehamia kijiji cha Bwagamacho" Ally alisema.
"Ndiyo huyo huyo na mimi ni mtoto wa Faimu" Fahmi alieleza.
"ok ok karibu bwana leo nimekuja kuzuru makazi yetu ya zamani" Ally alieleza.
"Asante sana, mimi huwa ni sehemu yangu ambayo napenda kukaa huwa inanikumbusha mengi sana hii na nikiwa na huzuni basi huwa nakuja kukaa hapa ndiyo maana unapaona pasafi sana hasa upande wa sebule hii" Fahmi alieleza.
"Ok kijana ndiyo maana nilitaka nishangae imekuwaje mpaka pawe  hivi, karibu tukae sote na mimi leo nimependelea sana kukaa humu" Ally alimuambia huku akimpa mkono Fahmi ambaye aliupokea akiwa na tabasamu pana usoni.
"umefanana sana na baba yako hadi mkitabamu mpo hivyohivyo, hakika mungu kawajalia tabasamu pana kijana" Ally alimwambia Fahmy na kusababisha Fahmy atabasamu.
"asante anko, napenda nikuite anko kama hutajali" Fahmi alimuambia  Ally.
"si vibaya waweza kuniita hivyo tu kwani umeonesha heshima kubwa sana kwangu kijana" Ally alisema.
"asante sana nafurahi kuongea na wewe" Fahmi alisema.
"hata mimi pia, vipi baba yako hajambo?" Ally aliongea huku akitabasamu kisha akamuuliza juu ya hali ya baba yake, swali hilo lilimfanya Fahmi aondokwe na uso wa tabasamu usoni mwake ingawa alilazimisha tabasamu hilo lirudi katika uso wake.
"Baba yupo uarabuni kwa sasa na huko ndipo alipojenga maisha yake" Fahmi alijibu huku akilazimisha tabasamu usoni mwake.
"ohoooo! Mpe hongera sana rafiki yangu aliyenijali sana yule" Ally aliongea huku akitabasamu.
Maongezi yao yaliendelea hadi ilipotimu adhuhuri Fahmi akaaga akaondoka na akamuahidi Ally angerejea akiwa na ugeni mkubwa sana kama angekuwepo hapo. Alky alimpa ahadi ya kuwepo eneo kwa siku nzima hivyo angemkuta, hakuutambua ugeni huo ulikuwa ni ugeni gani na laiti angeutambua angetamani hata auone muda huo lakini haikuwezekana. Ally aliendea kukaa hapo hadi ilipofika muda wa alasiri akaja kijana mwingine akiwa na chombo cha chakula akampatia, yule kijana alimuambia chakula hicho kilikuwa kimeagizwa aletewe na Fahmi.  Ally alishukuru sana akakila chakula chote kutokana na njaa  ambayo tayari ilishaanza kushambulia tumbo lake, baada ya kumaliza kula alitoa shukrani kwa ubinadamu aliofanyiwa na yule kijana
aliyetumwa pia akamwambia apeleke shukrani za dhati kwa Fahmi kwa kumjali namna hiyo.
Baada ya kijana yule kuondoka Ally aliendelea kukaa hapo akikumbuka mambo mbalimbali kipindi akiishi  ndani ya nyumba hiyo kabla hajahama, mambo mengine ya furaha na upendo na alivyokuwa akiishi na shemeji yake ambaye alimjali yalimpa tabasamu kila akiyakumbuka ila alipokumbuka wema aliofanyiwa na kaka yake alijikuta anasonya tu kwani hakuupenda hata kidogo huo wema wake na wala hadi muda hakuona umuhimu wake.
"Shetani katumia ushetani kunifanikishia malengo yangu, hadi sasa sioni umuhimu wa mimi kufikia haya malengo ikiwa kuna mwenzangu kateseka kwasababu ya huyo shetani. Kakimbia kwao kwasababu ya huyo shetani. Shetani huyu kanisaidia ili na mimi anitumbukize katika ushetani"Ally aliongea kwa hasira  kisha akanyanyuka akasema, "namchukia maana bila yeye mimi nisingetumiwa kama mtumwa wa ngono na yule malaya aliyekubuhu kwa umalaya tangu yupo kigori. aaargh! Nawachukiaaa!" Ally aliongea kwa hasira kisha akapiga ngumi ukutani na kupelekea sehemu ya plasta iliyowekwa juu ya ukuta wa udongo wa nyumba hiyo uanguke.
Chuki za waziwazi kwa  kaka yake ndiyo zilikuwa zimeutawala moyo wake na hakumpenda kama ilivyokuwa akimpenda hapo awali, hakuona umuhimu wa yeye kumuita kaka wakati kafanya mambo yasiyopendeza kwa mwanadamu yoyote mwenye moyo wa kibinadamu na siyo wa  kama aliokuwa nao kaka yake. Alitokea kuwachukia ndugu zake wote walioshiriki mpango ule hakuona faida ya kuwa na ndugu kama wao katika dunia hii, aliona ni bora angekuwa na undugu na jiwe kuliko kuwa na undugu na hao aliowaheshu kama kaka zake lakini hakuona ustahiki wao wa heshima hiyo aliyowapa.






               SURA YA NANE.
   Majira ya magharibi katika eneo hilo alilokuwepo Ally paliiingia ugeni mwingine ambao haukutia mguu katika eneo hilo kwa miaka kadhaa tangu walipoondoka, ugeni huo ulikuwa ni msafara wa magari mawili ya kifahari yenye thamani kubwa sana nchini Tanzania kwa kipindi chote. Magari hayo yalikatisha katika majani baada ya barabara ya kuingia eneo hilo kuwa imeota majani kila sehemu.  Ally aliposikia mingurumo ya gari hiyo wala hakujishughulisha kwenda kuangalia zaidi ya kutulia vilevile sehemu ya dirishani ya sebule hiyo alipokaa katika eneo ambalo  dirisha limetolewa, aliposikia hatua za mtu akiingia hapo ndani yeye alielekeza machp mlangoni tu na hadi mtu huyo anaingia tayari alikuwa ameshamuona na ni mtu kati ya watu anaowaheshimu akiwa amebeba mikeka inayotengenezwa kwa ukindu maarufu kama majamvi kwa wakazi wa jiji la Tanga
"Ally kumbe huku" Sauti ya mtu huyo ilimsemesha na hapo Ally akainuka akamfuata.
"ndiyo baba nipo huku, shikamoo" Ally alimuamkia baba yake baada tu ya kumjibu swali alilouliza.
"marhaba tumekutafuta sana mchana wa leo ili uje huku maana kuna jambo muhimu sana" Mzee Buruhan alisema.
"sawa baba nipo tayari hakuna kilichoharibika" Ally aliongea huku akimpokea  baba yake majamvi.
"yatandike hapo chini kwa ajili ya wageni watakaokuja maana mzee Mahmud kasema kuna ugeni utafika hapa kwa ajili ya jambo hili tuliloitiwa hapa.
"sawa baba" Ally alitii amri akaanza kuyatandika majamvi chini kama alivyoambiwa na baada ya muda akawa amemaliza.
"vizuri sasa tumsubiri mzee mwenzangu anakuja sasa hivi na nimeambiwa nisiwaruhusu ndugu zako kuingia mpaka yeye afike" Msee Buruhan  aliongea huku akienda kuketi dirishani alipokuwa ameketi Ally awali, Ally naye aliungana naye kwenda kukaa alipokuwa  awali.
Baada ya dakika tano mlio wa pikipiki ulisikika nje ya nyumba hiyo ikija na kisha baada ya dakika moja ikaondoka, muda huo huo mzee Mahmud alionekana akiingia mlangoni akiwa amebeba taa nne kubwa za kuchaji baada ya pikipiki hiyo kuondoka.
"vipi kila kitu tayari?" Mzee Mahmud aliuliza.
"ndiyo kila kitu tayari mzee mwenzangu" Mzee Mahmud alijibu.
"vizuri basi, Ally hujambo mwanangu" Mzee Buruhan alipongeza kisha akamjulia hali Ally.
"Sijambo baba shikamoo" Ally alijibu kisha akamsalimia.
"Marhaba mwanangu vizuri kwa kuwepo hapa, ngoja nianze kazi" Mzee Buruhan aliongea kisha akaanza kutamka maneno yasiyoeleweka akawa anazunguka eneo zima lenye mikeka halafu akafanya hivyo kwenye kila pembe ya ukuta hadi akamaliza sehemu zote na alipomaliza kufanya hivyo aliwasha taa alizokuja nazo akazitundika ukutani kwenye kila kona.
"Sasa hao wanaweza kuingia wakae upande wa kushoto na uwaambie wasiongee mpaka niwaambie mimi, Ally kaa pembeni yangu"  Mzee Mahmud aliongea kisha akakaa chini, mzee Buruhan alitoka nje na baada ya muda akarejea akiwa pamoja na Shafii,Salma, Hamida na Jamal.
Shafii aliongozwa na Jamal hadi eneo wanalotakiwa wakae na alishushwa kwenye kiti akakalishwa kitako, baada ya wote kukaa chini kwenye jamvi waligeuka wakawa wanamtazama mzee Mahmud kujua kinachofuata.
"Bado ugeni mmoja uingie, wageni karibuni" Mzee Mahmud aliongea huku akitazama mlangoni na kupelekea watu wote watazame mlangoni, ugeni ulioingia hapo ulikuwa ni watu  wanaowajua ambapo wengine walishtuka baada ya kuuona ugeni huo ambao haukueleweka umefika hapo kwa usafiri gani kwani walionekana tu wapo mlangoni.
Wa kwanza kuonekana mbele ya macho yao alikuwa ni Zalabain akiwa amevaa joho jeusi  na kofia nyupe ambaye alitambulika kwa Ally na Shafii pamoja na mzee Mahmud, Ally alimtambua Zalabain  kama Fahmi aliyekuwa naye hapo hadi muda wa adhuhuri na hakumfahamu kwa vingine kabisa. Shafii alimtambua huyo mtu kama mbaya wake baada ya kuiona sura yake siku aliyokufa mganga Sauti ya radi na alimkimbia, alipomuona alishtuka sana alitamani hata ardhi ipasuke atumbukie asionekane eneo hilo kwani alishuhudia ukatili wa Zalabain hivyo alimuogopa. Wageni wengine walioingia eneo hilo walikuwa ni Bi Farida na Zayina wakiwa wamevaa nguo za thamani kubwa walizopata wakiwa katika ulimwengu wa majini, Shafii alipowaona alijikuta akijawa na furaha akataka kutamka neno ila ishara ya baba yake ikimkataza kutozungumza ikamfanya atulie.
"Karibu Zalabain mwana Zaif mjukuu wa Zulain mfalme wa himaya ya majini ya  Majichungu, karibu uketi upande ule wa pili ukiwa na wageni wenzako" Mzee Mahmud alisema huku akitabasamu na kusababisha Zalabain atabasamu pia, Zalabain na mama yake pamoja na dada yake walienda kukaa mwingine kabisa pembeni ya upande aliopo Shafii.
"Sasa basi nimewaita hapa ili tuweze kutatua tatizo ambalo lingemsababishia mzee mwenzangu hapa asibakiwe na hata muhomili mmoja ndani ya dunia hii, utatuzi wa tatizo hilo utaanza kuonekana tu ikiwa ukweli wote utakuwa utakuwa hadharani" Mzee Mahmud alisema kisha akamwangalia Shafii akamwambia, "Shafii napenda uanze kuongea ukweli kuanzia unaanza kumpenda Bi Farida na ulivyompata hadi ukamuoa, tafadhali narudia tena tafadhali ukweli ni muhimu katika kila kitu".
Baada ya mzee Mahmud kumaliza kuongea alimpisha Shafii ili aeleze ukweli wake wote, Shafii naye hakuwa na jinsi zaidi ya kueleza ukweli wote juu ya suala hilo ili apate  nafuu ya matatizo yake kwa jinsi anavyoamini na kwa jinsi alivyoambiwa na mzee Mahmud. Shafii alianza kwa kusafisha koo lake kisha akasimulia, "Kwanza napenda nitangulize msamaha kwa hichi nitakachokusimulia ikiwa kitakuwa kimemkwaza yoyote kwani si kizuri, nilikuwa ni mtoto mtiifu sana kwa wazazi wangu kwa kipindi ambacho bado sikuwa nimepevuka kutokana na malezi ya kimaadili aliyonilea baba yangu kwa  kipindi hicho. Ndiyo muda huo huo mke wangu mama Zayina alikuwa angali binti mdogo hata kuvunja ungo bado ingawa alikuwa akitajwa ni mmoja kati ya mabinti wenye uzuri ambao haukuwahi kutokea katika kijiji chetu cha Bwagamacho Baada ya Farida kuanza kupevuka ndipo uzuri huo wa umbo na kila kitu ulianza kuonekana na kipindi hicho na ndiyo wavulana wa rika langu wakaanza kumfuata lakini waliambulia kukataliwa na binti huyo na hata wengine walishtakiwa kwa wazazi wao baada kumtongoza, jambo hilo lilinitisha na kunifanya nishindwe kwenda kumuambia kwa kuhofia ukali wa baba yangu kama akijua. Nilimpenda sana tena sana lakini nilihofia kupigwa sana na baba yangu kama nilivyoshuhudia wenzangu wakifanyiwa hivyo na baba zao baada tu ya mashtaka kuletwa nyumbani juu ya kumtongoza Farida. Baada ya miaka miwili kupita ndipo nilipoanza kupata ujasiri wa kumtongoza ingawa nilikuwa nina uoga kwa mbali, kutongoza kwangu kuligonga mwamba na hata nilipomueleza rafiki yangu kipenzi Hamis ambaye ni kaka yake juu ya suala hilo aliniambia yupo tayari kumsaidia ikiwa tu na yeye nitamsaidia kufanikisha jambo analolitaka.
"Jambo gani wataka nikusaidie  Bonoeza" Nilimuuliza Hamis.kwa kutia jina la utani ambalo hakuwa analipenda kabisa kwa kipindi hicho.
"Shafii waanza sasa nimesema hilo jina silitaki nitaacha kusaidia nikamjaze sumu dada yangu umkose" Hamis alinijia juu baada ya kumtajia hilo jina.
"Hamis nisamehe rafiki yangu niambie shida yako sasa" Nilimuomba radhi na nikawa tayari kuisikiliza hiyo shida yake kwani ndiye rafiki yangu wa shida na raha.
"rafiki yangu hii ni aibu sana hasa kwa vijana wa rika langu na nimeificha ila kwakuwa wewe ni rafiki yangu wa muda mrefu nimeamua nikueleze ili unisaidie na wewe  nikusaidie, kiufupi nampenda sana Salma yule mtoto mzee Rajabu ila mdomo wangu ni mzito kutamka neno hili kwake na ninabaki nikiungua ndani kwa ndani tu" Hamis alinieleza tatizo lake ambalo nilikuwa nipo tayari kumsaidia tu ili nipate moyo wa dada yake  kipenzi, tatizo lake lilikuwa ni dogo tu kwani  hata Salma alikuwa akimpenda vilevile na ishara zote niliziona ila tu wote hawakuwa na ujasiri huo. Nilimsaidia hadi akampata Salma na mimi akaanza harakati za kunisaidia lakini hazikuzaa matunda kabisa kwani msimamo wa Farida bado ulikuwa ni uleule na hata alipomtumia Salma katika suala hilo ilikuwa vilevile na yeye alizidi kunipa moyo kuwa nitampata ingawa nilianza kukata tamaa juu ya suala hilo.  Niliendelea kumbembeleza Farida lakini sikuchoka kwani niliamini yeye alikuwa akinipenda mimi pia na kama angekuwa hanipendi basi angelikuwa amenishitaki siku nyingi nyumbani kwetu juu ya kumsumbua kwangu lakini hakufanya hivyo, hakika sikutambua kama kaanza kukomaa kiakili na jambo kama hilo hakuwa na haja tena kulisema kwani ingeonekana ni akili za kitoto. Niliendelea kujipa moyo nikijua ipo siku nitampata na sikutambua kama mawazo yangu ni sawa na kuchemsha mawe nikitegemea yatachemke kutokana na upendo mzito nilionao kwake, sikutambua kama najipa matumaini hayawezekani kutokea hivihivi kama kubadilika kwa majira ya mwaka kutoka kiangazi hadi vuli. Nilichojali ni kupata jibu sikujali itachukua muda gani hadi niwe naye, niliendelea kusumbuka katika kumueleza kila siku lakini niliambulia patupu na nikawa natembea na matumaini ya kumpata tu kichwani mwangu. Matumaini yangu yaliishi katika moyo wangu lakini baadaye yalikufa baada ya muda wa miezi kadhaa tu na nikajikuta nikiumia moyoni, kufa  kwa matumaini yangu kulikuwa ni baada ya kuingia kikwazo katika kumpata Farida...



*Hatimaye akubali kufunguka

*usikose kujua alichofunguka.

Monday, November 30, 2015

DHAHAMA SEHEMU YA KUMI NA TATU




TEMBELEA: www.facebook.com/riwayamaridhawa 



 DHAHAMA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE



SEHEMU YA KUMI NA TATU!!
"Faridaaa!" Shafii aliita jina la mke wake  kwa nguvu huku akijaribu kuinuka kitandani
"Shafii hebu tulia kwanza utasababisha  matatizo mengine tu" Mzee Buruhan alimuambia huku akimzuia asifanye fujo.
"Mama Zayina, Zayina mpo wapi?" Shafii alipiga kelele zaidi na ikabidi daktari aitwe mara moja ili kumtuliza, Mzee Buruhan na Mzee Mahmuf walimshikilia  Shafii hadi daktari alipokuja akamchoma sindano ya usingizi ndiyo ikawa ahueni.
Baada ya Shafii kulala mzee Buruhan na mzee Mahmud  walitoka pamoja na mke wa Hamis wakaenda kuka kwenye madawati ya kusubiria wagonjwa, baada ya muda mke wa Hamis aliondoka kwenda kufuata chakula kwa ajili ya mgonjwa akawaacha wazee hao peke yako.
"Kama nilivyokuambia mzee mwenzangu kuhusu huyu mwanao, awe mkweli ujue tatizo alilonalo ndiyo nitakubali kumsaidia" Mzee Mahmud aliongea.


****


"Mzee mwenzangu tatizo kila kukicha una misemo ambayo imejaa vitendawili vitupu hebu niweke wazi walau kidogo nipate fununu ya jambo linalomsumbua mwanangu" Mzee Buruhan alimlalamikia rafiki yake kutokana na kauli zake zilizo jaa mafumbo.
"mzee mwenzangu hiyo kinyume na utaratibu wa taaluma yangu siwezi kusema hata kama nalitambua tatizo hili, huwa sina tabia ya kukuficha kitu ila kwa hili wacha nikuambie ukweli tu nitakuwa nimekiuka masharti ya utalaamu wangu wa uganga ikiwa nitalisema suala hili pasipo muhusika mwenyewe kufungua kinywa chake na kuliongelea. Utanisamehe kwa hilo" Mzee Mahmud aliongea huku akimshika bega mzee Buruhan ambaye alionekana kuwa njia panda kutokana na matatizo yaliyomkumba mwanae
"mzee mwenzangu hakuna hata njia nyingine ya kunisaidia niweze pata fununu kidogo ya hili suala?" Mzee Buruhan aliuliza huku akiwa ameinamisha uso wake chini akionekana amekata tamaa kabisa ya suala hilo.
"Siku zote mwanamke atakaye mtoto lazima akubali kuvua nguo ya ndani ili alichokificha kionekane na hawezi kupata mtoto ikiwa atakataa kuivua hiyo nguo. Ndiyo hivyo hivyo mwanao akubali alilolificha moyoni mwake lifumbuke la si hivyo hataweza kupata msaada katika hilo, cha kukusaidia akiamka muambie umebaki peke yako ukitaka usipoteze vyote awe muwazi kwangu na kwako. Naenda msalani mara moja mzee mwenzangu" Mzee Mahmud aliongea kisha akajiinua kivivu  kwenye dawati la kusubiri wagonjwa akawa anaelekea chooni, mzee Buruhan alimtazama tu akiwa anatamani sana ajue jambo lililopo ndani ya kichwa chake lakini hakuwa na uwezo wa kufanya hivyo. Mzee Mahmud  aliipopotea katika upeo wa macho yake aliinua kichwa juu akiweka ishara ya kuomba dua halafu akatikisa kichwa kuonesha anasikitishwa, hakuwa na jambo jingine alilomuomba Mungu zaidi ya kumshtakia tu  juu ya balaa lililomkuta mwanae na kumfanya awe na matatizo tu katika mwaka huo ambapo miaka mingine yote aliishi kwa amani na furaha pamoja na familia yake lakini sasa furaha hiyo imetoweka  katika maisha yake. Laiti angelijua kwamba alikuwa anashtaki mtuhumiwa kuwa ameonewa wala asingelifanya hivyo lakini kwakuwa hakujaliwa uwezo wa kulibaini kwani alikuwa ni mwanadamu wa kawaida tu, hakutambua kama jereha la mwanae ni  la kujitakia hivyo halihitaji pole hata kidogo.
   
Mzee Mahmud alipofika kwenye mlango wa msalani baada ya kuondoka pale kwenye dawati alihisi hali isiyokuwa ya kawaida katika mwili wake lakini aliipuzia na kuingia humo msalani, alipoingia ndani alipitiliza sehemu za kujisaidia haja ndogo akawa anaelekea sehemu maalum ya yenye vyoo ndani ambayo hutumiwa na wale wanaohitaji kumaliza haja zao kwa siri tu. Alipofika hilo eneo  alifuata mlango wa moja wa vyoo akashika kitasa ili aufungue lakini alisita baada ya  kusikia upepo mzito ukivuma kwa ghafla ambao ulitaka hata kuupeperusha msuli aliojifunga kiunoni lakini aliuzuia, upepo huo ulipotulia Mzee Mahmud alionekana kukerwa nao kwa kitendo cha kutaka kumuadhiri ambapo aligeuka nyuma akionekana kuwa na hasira za waziwazi juui ya tukio hilo.
"Adabu gani hizo ewe mwanajini wataka kuniadhiri kwa hizo nguvu zako ulizojaliwa?" Mzee Buruhan alilalamika baada ya kumuona yule aliyetaka kumuadhiri kwa kutaka kuupeperusha msuli aliojifunga kiunoni alikuwa yupo mbele yake baada ya kugeuka nyuma, alikutana uso kwa uso na Zalabain akiwa amefumbata mikono kifuani mwake.
"Samahani mzee wangu kwa hilo" Zalabain aliomba radhi.
"sema una shida gani" Mzee Buruhan aliongea huku akiuweka msuli aliojifunga kiunoni vizuri.
"nimekuja kukuambia tu mimi ndiye ninayemtesa Shafii na huwezi kuharibu kazi yangu kwa kujaribu kumsaidia" Zalabain aliongea kwa msisitizo.
"Ndiyo nimeshakutambua tangu unajitokeza pia sipo kwa ajili ya kumsaidia dhalim kama yule bali nipo kwa ajili ya kumsaidia Buruhan ili asiondokewe na nguzo zake zote, kiufupi ni hivi nazuia usimuue yule mziwanda wake asiye na hatia" Mzee Mahmud alimuambia huku akijiamini halafu akameza mate kidogo kisha akaendelea, "Shafii ni haki yake kwa alichokifanya ila Ally hana hatia yoyote na usimuingize katika orodha hiyo, pia ningependa mumponyeshe sikio lske na taya lake ambayo mumjeruhi kutokana na kujaribu kuleta kile kitakachoyafanya majini ya marehemu Hamis yafanye kazi. Ukumbuke pia  yeye anachukia ulilofanyiwa ila mali yako anayoimiliki Shafii ndiyo inamfanya ashindwe kufanya jambo lolote, usihukumu yule asiye na hatia kama ni ufalme utapewa pasipo yeye kupoteza uhai wake".
"unasema nini wewe?" Zalabain alimuuliza Mzee Mahmud
"kama ulivyosikia ewe mwana wa jini, ukumbuke mimi nilikataa kutengeneza uchawi kama uliomtapisha mama yako jana kwasababu najua siyo haki kufanya hivyo, pia niligoma kufanya dawa ya kumuua baba yako ili mama yako awe chini ya mwingine kwasababu najua haikuwa haki. Pia utambue nakuambia usimuue Ally kwasababu najua utakuwa hutendi haki ewe mwanajini kamuuulize ibin Zultash atakueleza, mwisho kabisa nakuambia hivi upotee sasa hivi kuna mtu anaingia humu msalani sasa hivi asije akaniona naongea peke yangu kama kichaa wakati nina akili  zangu timamu" Mzee Buruhan aliongea kisha akageuka nyuma akaingia chooni bila kujali kama Zalabain ameondoka au yupo, baada ya kumaliza haja zake  alitoka hakumkuta Zalabain na akarudi kule alipokuwa yupo awali. Alimkuta mzee Buruhan yupo na Ally wakiongea na iilonekana Ally alikuwa kapona kabisa tatizo la kuvunjika taya na sikio kwani hakuwa mwenye kuweza kuzungumza wala kusikia, lakini hapo alikuwa akizungumza na kusikia vizuri kabisa.
Mzee Mahmud alimuonesha ishara ya kumsalimia Ally kama ilivyokuwa akifanyiwa kwa kutoweza kusikia vizuri lakini.
"Mzee mwenzangu anaongea huyu na kusikia sasa hivi usimsabahi kama vile unamsabahi bubu" Mzee Buruhan alimuambia rafiki yake.
"Yapaswa  tumshukuru Mungu basi mzee wangu maana huu muujiza tosha" Mzee Mahmud aliongea akionekana kufurahishwa na suala hilo.
"Alhamdililah" Ally na baba yake waliitikia kwa pamoja.
Mzee Mahmud alibaki kutabasamu tu kila alipomuangalia Ally kwa kufurahishwa na usikivu alionao Zalabain baada ya kufanya kile alichomuambia, tabasamu lake lilifanya Mzee Buruhan na Ally nao watabasamu  wakijua kafurahishwa na hali ya Ally kutengemaa.
"Ally hebu sogea karibu" Mzee Mahmud alimuambia Ally  huku akimtazama kwa umakini, Ally alimsogelea Mzee Mahmud pasipo kujua ni kipi alichokuwa anataka kufanyiwa kwani alimzoea sana mzee Mahmud na alimchukulia kama baba yake tu. Alipomsogelea Mzee Mahmud aliambiwa achuchumae mbele yake naye akatii amri kama alivyoambiwa, mzee Mahmud alimshika kichwani na akamtamka maneno yasiyoeleweka na kusababisha Ally ashtuke halafu aangalie mazingira ya hapo yalivyo halafu akaenda kukaa kwenye dawati pembeni ya baba yake alipokaa awali.
"Baba hivi hapa tupo kwa ajili gani?" Ally aliuliza tu baada ya kukaa pembeni ya baba yake akionekana kutotambua yupo hapo kwa ajili gani.
"Kha! We Ally maswali gani hayo hutambui kama tupo hapa kumuangalia kaka yako kalazwa tangu jana" Mzee Buruhan alimuambia Ally akionekana kutoelewa kitu alichofanyiwa na  mzee Mahmud hadi akasahau  yupo pale kwa lengo gani wakati alipoingia tu aliulizia hali ya kaka yake.
"Khaa! Kumbe tupo hapa kwa ajili ya kumuangalia firauni huyo, sina muda huo muache afe  maana huyo ni zaidi ya shetani" Ally aliongea maneno ambayo yalizidi kumshangaza sana Mzee Buruhan na akajikuta  akimtazama  mzee Mahmud akionekana kutoelewa kafanya nini, Ally alinyanyuka ili aondoke lakini mzee Mahmud alimuita akamuomba aketi akakaa chini.
"Ally tambua undugu ni kovu na halifutiki usifanye hivyo, najua unaumia kwa kile alichokifanya kaka yako lakini kumbuka ndugu ni ndugu tu" Mzee Mahmud aliongea kwa ustarabu wa hali ya juu akitegemea ataeleweka na Ally lakini haikuwa hivyo.
"Baba zangu mngejua alichokifanya huyo firauni mnayekuja kumuangalua wala msingethubutu kukaa hapa, na sijui hata ni kwasababu gani nilikuwa nikimpenda kwa kipindi chote hicho nahisi aliniroga yule maana miale ya mkufu wake sielewi hata imemifanyaje wakati nilikuwa nikimchukia" Ally aliongea  huku akionesha kumchukia  kaka yake.
"Ally unaongea nini wewe?" Mzee Buruhan aliuliza akionekana kushangaza na maneno anayoyaongea mwanae.
"Mzee mwenzangu kama nilivyokuambia hili tatizo linajulikana ila huyu hatakiwi kulisema na akilisema atakuwa kiziwi kama mwanzo muache huyo Shafii aeleze kila kitu. Unajua..." Mzee Mahmud aliongea maneno yaliyomfanya Mzee Mahmud atulie kimya na alishindwa kumalizia kauli yake baada ya mke wa Hamis kurudi akiwa amebeba chombo cha chakula kwenye mfuko wake.
"Vipi mgonjwa jamani tayari ameshaamka?" Mke wa Hamis aliongea baada tu ya kuwasili na alimuonesha Ally tabasamu kisha akampa mkono akampa mkono ili amsalimie akijua kuwa Ally hawezi kuongea.
Ally hakuupokea mkono wa Mke wa Hamis zaidi ya kusonya kwa nguvu kisha akanyanyuka akasema, "shetani jike mkubwa wewe".
Ally alinyanyuka kwenye dawati la kusubiri wagonjwa akaelekea mahali akimuacha wazee wake na mke wa Hamis wakimshangaa sana, mke wa Hamis alipotaka kumfuata nje Mzee Buruhan alimshika akamzuia.
"Salma mama naomba unisikilize kwa umakini, achana na Ally kwa sasa kaa hapo usubiri muda wa kumuona mgoniwa akizinduka tukamuone" Mzew Buruhan alimuambia Salma mke wa Hamis.
"Lakini Ally kapatwa na nini wazee wangu kwani alikuwa hawezi kuongea na kusikia ila sasa hivi anaongea na kusikia  ila amekuwa kama akili haziko sawa hadi ananisonya mimi" Salma aliongea huku akishangazwa na hali ya Ally yule aliyekuwa anamsikiliza na kumtii na kumuheshimu ameamua kuonesha dharau.
"Hebu mama kuwa muelewa achana na habari za Ally sasa hivi, tufikirie kuhusu mgonjwa tu" Mzee Mahmud aliongea kwa msisitizo huku  akionekana kutopendezwa na maneno ya Salma.
"Sawa baba zangu nimewaelewa" Salma alijibu kwa shingo upande ili tu asiwaudhi  wazee ambao anawaheshimu.


****

 Wakati Ally akifunguliwa na kuanza kumuoneshea dharau upande wa himaya ya Majichungu Zalabain ndiyo alikuwa amerejea muda huo na aliamua kupitia chumbani walipo mama yake na dada yake ili awaone kutokana na upendo alionao kwao, alibisha hodi kwa adabu ingawa alitambua hata akiingia muda huo asingewakuta wakiwa bila stara. Alipokaribishwa aliingia kwa adabu  na akaenda hadi walipokuwa wamekaa kitandani na akawasalimia, halafu naye  akaketi kitandani jirani yao.
"Mwanangu kila nikikutazama namuona baba yako kwa jinsi wote mlivyokuwa na sura zilizofanana, haya niambie unatoka wapi?" Bi Farida aliongea kisha akamuuliza Zalabain.
"Nilikuwa Tanga kwenye  hospitali ya SBN nilienda kuongea na mzee Mahmud" Zalabain alimuambia mama yake.
"Mh! Huyo mzee huko hospitalini anafanya nini?" Bi Farida aliuliza.
"Amekuja kumuangalia mumeo amelazwa" Zalabain alimuambia mama yake.
"Jamadin sina mume kama huyo mimi tena sitaki kumsikia ukimtaja, mume aliyetakiwa kunioa mimi ni Faimu tu na sijui ilitokea nini mpaka nikamkana na nikamsababishia matatizo makubwa sana akahama kijijini akiwaacha jamaa zake. Nampenda Faimu na natamani nimuone hata leo ili nimuombe msamaha maana yeye ndiyo kila kitu kwangu" Bibi Farida aliongea na  mwishowe akalia kutokana na kujutia aliyoyafanya ya hapa zamani, Zalabain ilimbidi amkumbatie mama yake ambembeleze kutokana na upendo alionao kwake.
"Samahani mama kwa kukupa taarifa smbayo hutaki kuisikia,  sipendi uhuzunike nakupenda sana" Zalabain alimuambia mama yake baada ya kunyamaza.
"Nakupenda pia mwanangu" Bi Farida alisema huku akitabasamu kwa mbali, waliendelea kuongea maongezi mengine kwa furaha wakiachana na suala ambalo lilionekana kutomfurahisha kabisa Bi Farida.


****


 Baada ya masaa mawili Shafii aliamka kutoka usingizini akiwa yupo vizuri kiafya kuliko awali, hali yake iliendelea kutengemaa na ilipofika muda wa alasiri aliruhusiwa na daktari na alirudi nyumbani akiwa ameongozana ns wote waliokuja  kumuona hospitali kasoro Ally tu ambaye hakurudi tangu aondoke pale hospitali. Shafii alipelekwa moja kwa moja chumbani kwake na akaachwa apumzike na kisha wazee wake wakakaa sebuleni hadi ilipoingia jioni ndiyo mzee Buruhan na mzee Mahmud waliingia chumbani kwa Shafii wakamkuta akiwa ameamka ameegemea mito kitandani kwake,  Shafii alipoona ujio wa wazee wale alihisi kuna jambo ila alikaa kimya ili apate uhakika wa wasiwasi wake.
"Shafii" Mzee Buruhan alimuita
"Naam Baba" Shafii aliitikia
"unajua kama wewe ndiyo nguzo kuu kati ya nguzo zangu nne zilizobakia?" Mzee Buruhan alimuuliza
"nafahamu hilo baba" Shafii alijibu.
"Hussein hatunaye, Hamid hatunaye, Hassan ni mdogo kwako, Falzal ni mdogo kwako na Ally pia ni mdogo kwako. Wewe pekee ndiyo mkubwa ndiyo kiongozi wao ingawa wote wana maisha yao na hata wanajisomesha wakitaka kujiendeleza kielimu. Nadhani unatambua hilo" Mzee Buruhan alisema.
"Ndiyo baba natambua hilo" Shafii alijibu.
"Sasa basi inapotokea tatizo lenye kuhitaji kuelezewa ili lisizidi zaidi inabidi lielezewe mwanangu ikiwa utakaa kimya haitasaidia chochote" Mzee Buruhan aliongea.
"Baba sijakuelewa unachomaanisha" Shafii aliongea.
"Shafii najua unatambua suala la upotevu wa mke wako na hata mwanao linalokufanya uwe na matatizo kila kukicha, sasa mwanangu ukilificha itakusaidia nini ikiwa unalifahamu chanzo chake. Kumbuka mficha maradhi kifo humuumbua mwanangu, mwanangu ni bora uitoe aibu mbele ya daktari ili utibiwe kuliko kuficha tatizo halafu ufe na ugonjwa. Ongea chanzo cha  haya ni nini?" Mzee Buruhan alimsihi mwanae.
"Baba kusema ukweli sijui wala sitambui suala hili linasababishwa na nini?" Shafii alikataa.
"Shafii vuta kumbukumbu zako vizuri umefanya nini mpaka yote haya yatokee au hutaki  familia yako uione tena ikiwa na upendo" Mzee Buruhan alizidi kumsihi.
"Baba napenda sana familia niione tena ikiwa ina upendo lakini sikukumbuki chochote kilichosababisha haya ninayofanyiwa"  Shafii alikana kabisa juu ya suala hilo.
"Jirani na mashine ya kusaga unga kule Mpirani miaka ishirini na moja iliyopita unakumbuka kilitokea nini pale kwenye  nyumba yako uliyokuwa unaishi  baada ya wewe kuhama tena ilikuwa majira ya saa sita usiku?" Mzee Mahmud aliongea kwa mara ya kwanza na kumfanya Shafii ashtuke kwa jambo alilotajiwa, lilikuwa ni jambo ambalo alishalisahau kabisa katika ubongo wake na sasa alikumbushwa na mzee huyu ambaye ni mganga mtaalam.
"Shafiii unakumbuka nini hiyo siku" Mzee Buruhan naye aliunganisha maelezo ya rafiki yake ingawa hakuyaelewa kabisa, maneno ya mzee  Mahmud  yalimfanya anyamaze ghafla huku akiwa ameinamisha kichwa chake chini.
"Shafii si nakuuliza" Mzes Buruhan aliongea huku akimtikisa bega baada ya kuona yupo kimya, Shafii alikurupuka baada ya  kutikiswa bega kama alikuwa yupo  katika usingizi mzito.
"Ha..hapana  si....sikumbuki chochote" Shafii aliongea kwa kubabaika baada ya kuhisi moja ya jambo baya alilolifanya linakaribia kugundulika.
"Una uhakika?" Mzee Mahmud aliuliza.
"ndiyo baba zangu nina uhakika wa kile ninachokiongea" Shafii alijikaza akajibu kwa kujiamini.
"mzee mwenzangu sisi twende tukanywe kahawa si unaona muda huu na kiubaridi cha kipupwe kimeanza, Shafii kama hujui juu  ya hilo basi inakupasa utambue kuwa maisha ya mkeo  na binti yako yapo kwenye kinywa chako kueleza unachojua na ukikaa kimya jua kinachofuata ni kama kilichowapata wadogo zako ia utambue umebaki peke yako" Mzee  Mahmud huku akiwa tayari amesimama na Mzee Buruhan naye akasimama, wote kwa pamoja walianza kutembea kuelekea ulipo  mlango ili waondoke lakini sauti ya Shafii ikiwaita iliwafanya wasimame na kugeuka wakamtazama.
"Nipo tayari kuwaambia kilichotokea wazee wangu naomba mnisaidie" Shafii aliongea baada ya kuona maji yamemfika shingoni na maneno ya mzee Mahmud ndiyo kabisa yalimfanya akubali. Mzee Mahmud alimtazama Shafii kwa tabasamu hafifu halafu akamuambia, "kesho muda kama huu pale ulipokuwa unaishi kule mpirani ndiyo kutakupa ahueni ya  tatizo lakokwa familia yako"
Mzee Mahmud aliposema maneno hayo alitoka humo ndani bila hata kumuangalia Shafii kwa mara nyingine, Mzee Buruhan naye alifuata akiwa nyuma yake.


****


Maneno ya Ally baada tu ya kupewa mkono na Salma yalimfanya Salma karibia siku nzima akiwa anajifikiria kwani Ally alikuwa amepatwa na nini mpaka awe vile, ilipofika jioni aliamua kutoka na kwenda kumtafuta Ally bila ya kumueleza mtu ili aongee naye tu kwani Ally alikuwa ni mmoja kati ya wanaume aliokuwa anawapenda na kipindi cha nyuma alipokuwa msichana alishajaribu kujivika ujasiri na kumueleza Ally yaliyo moyoni mwake lakini aliishia kukataliwa baada ya Ally kuwa anamuheshimu sana Hamis ambaye alikuwa na mahusiano na Salma kabla hajamuoa. Baada ya mpango ambao ndiyo chanzo cha balaa lote lililowakumba watoto wa  mzee Buruhan, Ally alifungwa akili na akawa anasikiliza wote waliofanya mpango ule bila hata kuwapinga na alifungwa akili baada ya kuujua mpango huo akawa  amekasirishwa nao. Baada ya kufungwa akili ndipo Salma alipompata Ally kutokana na yeye pia ni mmoja kati ya watu walioshiriki huo mpango, alimtumia Ally vyovyote atakavyo baada ya Ally kutopinga kauli yake. Sasa akili ya Ally ilipofunguliwa na Mzee Mahmud na Salma kujibiwa vile alijikuta roho ikimuuma akijua Ally amepatwa na tatizo hivyo  aliamua kumtafuta.  Hakukujua kama Ally wa leo siyo wa jana alichokuwa anakijali yeye ni penzi lake  haramu alilolianzisha kwa Ally hata alipokuwa yupo ndani ya ndoa.
Tamaa za kutamani kingine wakati akiwa tayari ana kingine mkononi ndiyo zilimfanya Salma afanye jambo hilo ambalo lilipelekea afiche siri nzito sana ambayo laiti ingaligundulika mapema basi angekuwa ameleta matatizo makubwa sana kwa Hamis na Ally.
Juhudi za Salma kumtafuta Ally ziliendelea kwa usiku huo akiwa yupo ndani ya gari yake na hatimaye alimkuta akiwa amekaa kwenye matairi yaliyochimbiwa katika uwanja wa mpira  uliopo mkabala na shule ya sekondari ya Usagara, Salma alimfuata hadi hapo akaegesha gari pembeni kisha akashuka akaenda kumkumbatia Ally akitegemea atapokelewa lakini alijikuta akisukumwa hadi akaanguka chini akaumia.
"Kaa mbali na mimi malaya wewe!" Ally alimuambia kwa ukali.
"Lakini Ally mpenzi wangu nimefanyaje?" Salma aliuliza kwa masikitiko makubwa huku akionekana kuumia baada ya kusukumwa.
"Unajifanya hujui siyo tena usiniite mpenzi wako kuanzia hivi sasa, we wa kunifanya mimi mtumwa wa ngono hadi umesababisha nisioe wakati natakiwa kuwa na familia sasa hivi" Ally alifoka.
"Ally nakupenda ndiyo maana nimefanya hivyo hadi nikazaa na wewe" Salma akaongea huku akilia.
"Weee tena ishia hapo hapo" Ally alimkaripia huku akimuongeza teke la mguu Salma.
"Ally nikatae ila ukae ukijua Hamida siyo mtoto wa mume wangu bali ni damu yako, ndiyo maana hata alipozaliwa kaka yako alikutania umefanana naye miguu ila ukweli ile ni damu yako kabisa" Salma aliongea huku akilia, Ally alipuuza maneno ya Salma akaondoka eneo akimuacha akilia ingawa kuna jambo lilikuwa likiisumbua akili baada ya kusikia maneno hayo.




ITAENDELEA!1

Sunday, November 29, 2015

DHAHAMA SEHEMU YA KUMI NA MBILI

RIWAYA: DHAHAMA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE


SEHEMU YA KUMI NA MBILI!!
"Asante  kiongozi wetu, mimi hapa
naungana na wazo alilolitoa mkuu wa majeshi la kwenda kuharibu utengenezwaji wa hao wadudu kwani sote tunatambua kwamba Dainun mpya imeibiwa na mpaka ije kupatikana hatujui

Saturday, November 28, 2015

DHAHAMA SEHEMU YA KUMI NA MOJA


 DHAHAMA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE



SEHEMU YA KUMI NA MOJA!!
"haina haja ya kuhuzunika mzee mwenzangu bali inabidi uwalaumu wanao na janga hili mzee mwenzangu limeanzwa na wao na sasa mwenzao wanalimaliza" Mzee Mahmud aliongea kisha akanywa kahawa funda moja bila hata kumtilia maanani Mzee Burhan aliyeonekana kutoielewa kauli hiyo.

Friday, November 27, 2015

DHAHAMA SEHEMU YA KUMI

DHAHAMA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE





SEHEMU YA KUMI!!
Laiti kama wanadamu tungalipewa uwezo wa kuona yaliyojificha katika mioyo ya wenzetu basi Bi

Thursday, November 26, 2015

DHAHAMA SEHEMU YA TISA

 DHAHAMA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE


SEHEMU YA TISA!!
Kilikuwa kimetawaliwa na jazba miongoni mwa watu waliomo humo ndani, kiongozi wa watu

Wednesday, November 25, 2015

DHAHAMA SEHEMU YA NANE

TANGAZO! TANGAZO!

Bado nawathamini wasomaji wangu popoote mlipo, kuonesha kuwathamini kwangu nimeamua kuingiza kitabu cha kielektroniki cha Dhahama katika mtandao wa kimataifa wa Amazon. Wale waliopo mbali na nchi ya Tanzania na wanakihitaji kitabu hiki waweze kukisoma wanaweza kukinunua huko kwa gharama nafuu kabisa iliyoorodheshwa hapo. Kitu cha kufanya ni kuingia amazon.com halafu search Dhahama utakipata hapo, kukisoma ni vizuri ukawa na app ya kufungua ebook kwa wale watumiaji wa smartphone utaipata ndani ya playstore.

NI HAYO TU

Tuesday, November 24, 2015

KOSA SEHEMU YA SABA




 KOSA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA

SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE

DHAHAMA SEHEMU YA SABA

DHAHAMA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGIN

Monday, November 23, 2015

DHAHAMA SEHEMU YA SITA




 DHAHAMA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGIN



SEHEMU YA SITA!!
Alikiweka kile chombo  mbele ya Shafii kisha akamwaga dawa zake kwenye moto uliomo kwenye chombo hicho, moshi mzito ulitanda humo ndani na mzee Sauti ya radi akawa anaimba nyimbo zisizoeleweka huku akimzunguka Shafii akicheza kama anacheza ngoma ya kikabila. Moshi huo ulipokuja kupungua Mganga akiendelea kucheza alihisi anashikwa kiuno wakati akicheza, moshi ulipoisha alihisi anashikwa makalio kwa kutomaswa. Alipogeula nyuma kumuangalia anayemshika alikutana uso kwa uso na Zalabain akiwa anatabasamu.

Sunday, November 22, 2015

DHAHAMA SEHEMU YA TANO

 DHAHAMA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGIN

Saturday, November 21, 2015

DHAHAMA SEHEMU YA NNE




                             DHAHAMA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGIN



SEHEMU YA NNE!!
"Afande tumefanya juhudi za kuuzima huu moto kwa kutumia  kila njia ila imeshindikana hadi maji yanaisha hatukuweza kuuzima na ikatubidi tutumie gesi lakini bado tumeshindwa kuuzima na inasadikika Mkuu wa idara ya sheria makao makuu ya kampuni hizi yupo ndani ya nyumba ya tatu na hajatoka hadi muda huu na hata tulipofika tulikuwa tukisikia kelele za mtu akiomba msaada lakini sasa hazisikiki" Mmoja wa maaskari wa zimamoto aliongea kwa ufupi juu ya tukio hilo la kuungua kwa nyumba hizo, James aliposikia maelezo hayo alipiga kelele huku akiita, "Babaa!". Aliwapita askari wa kikosi cha zimamoto akakimbia kuelekea ulipo moto katika nyumba ya tatu ya kampuni, maaskari wote walianza kumkimbiza ili wamuwahi asiingie ndani ya moto huo kutokana na ukali wake.

DHAHAMA SEHEMU YA TATU

MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE



SEHEMU YA TATU!!
Asp John aliyanakili maelezo ya James kisha akajiandaa kuuliza swali jingine lakini king'ora cha gari la zima moto kilimkatisha na akajikuta akiangalia lilipo gari la zima moto. Wale vijana nao waliliona lile gari la zimamoto likipita pembezoni mwa eneo la tukio kwa tabu kisha likaingia barabarani kisha likaingia barabarani likawa linaelekea Duga Maforoni kwa mwendo wa kasi sana huku milio ya ving'ora vyake ikiwa imetawala njia nzima. Asp John alipoona hali hiyo alihisi kuna jambo na akawa anataka kujua kuna nini kilichotokea, alinyanyua simu ya upepo akaongea kwa muda kisha akatulia akasikiliza upande wa pili na akajikuta amegwaya.
"nyumba za kampuni yenu zilizokuwa zinazinduliwa zote zimeungua kwa moto  wa hitilafu ya umeme" Asp John aliwaambia wale vijana.
"eti nini?" James alisema kwa mshangao.

Thursday, November 19, 2015

DHAHAMA SEHEMU YA PILI









DHAHAMA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE



 SEHEMU YA PILI!!
"we mwanaharamu wewe simamisha gari nishuke sio kuongeza mwendo" Yule mwanamke alizidi kufoka baada ya kuona mwendo wa gari unazidi kuwa mkali, dereva hakumjibu yule yeye alitoka kwenye usukani akasimama kisha akawaangalia wafanyakazi wa idara nzima akiwa na hofu.
"si mimi ninayeendesha jamani gari linaenda lenyewe hili hebu oneni" Dereva aliongea huku akiwaonesha wafanyakazi wote jinsi usukani ulivyokuwa unajiongoza wenyewe, wafanyakazi wote walipoona hicho kioja walijikuta wakijaribu kutoka nje lakini walishindwa kwani milango haikufunguka na vioo vyote vilijifunga ghafla hata vile vilivyokuwa wazi vyote vilijifunga. Wafanyakazi wote walijaribu kupiga vioo ili wavunje lakini walishindwa kwani vioo vilikuwa vigumu sana, gari nayo ilizidi kuongezeka mwendo hadi ikawa kama ipo kwenye mashindano.