Tuesday, December 1, 2015

KOSA SEHEMU YA KUMI NA NNE

   KOSA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA

SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE



 ILIPOISHIA

Furaha ilidhihirika machoni mwetu kwa kufanikiwa kukivuka kikwazo kile lakini furaha hii haikudumu kwani dosari kubwa iliingilia furaha hii, tukiwa tupo katikati ya pori usiku majira ya saa sita milio ya risasi ilianza kusikika na vioo vya  gari letu vikaanza  kupasuka.Yule askari ambaye ndiye aliyekuwa dereva wetu alitoa ukelele wa maumivu akiachia usukani wa  gari
 na gari likaingia pembeni ya barabara nusura ligonge mti baada ya  yeye kuwahi kukanyaga breki ya gari.




ENDELEA NA MKASA HUU WENYE KUELIMISHA NA KUSISIMUA




SEHEMU YA KUMI NA NNE!!
Milio ya risasi iliendelea kurindima mithili ya ngoma kwenye sherehe ya kikabila, vioo vya gari letu vilitobolewa na matundu ya risasi ambazo zilikuwa zinatokea upande wa pili wa barabara. Muda huo mimi nilikuwa nimesharuka nje ya gari baada ya kuona kuwa ni hatari ndiyo ipo mbele yetu, Nurulayt naye alikuwa amesharuka nje ya gari kisha akajilaza chini kwenye miti mita kadhaa  kutoka barabarani. Hali ilikuwa ngumu kwa yule askari wa uhamiaji aliyekodiwa na Nurulayt atuvushe mpakani kwani alipojaribu kutoka kupitia mlango wa kushoto ambao alikuwepo Nurulayt kutokana na mlango wa kwake kutokuwa salama kuutumia risasi ilitua mgongoni mwake na kumfanya ageuke nyuma ili aweze kumshambulia aliyemtupia risasi, yule askari alipogeuka aliinua kichwa  ili aone vizuri kwani alikuwa amelala kifudifudi kutokana na risasi iliyompata mgongoni. Nikiwa nimejibanza kwenye mti mnene uliopo mita kadhaa kutoka barabarani, nilimshuhudia yule askari akitobolewa kichwa chake na risasi baada ya kuinua kichwa ili atazame upande anaotokea adui yake. Askari yule hakutoa hata neno la mwisho baada ya risasi hiyo ya masafa marefu  kutoboa kichwa kisha kuendelea na safari hadi kwenye shina mti nililosimama ikapita juu kidogo ya kichwa changu kisha ikaendeleana safari.
"Abdul lala chini haraka utakufa huoni risasi imekukosa hiyo"  Nurulayt aliniambia kwa sauti huku akiweka sawa bunduki aina ya short gun  aliyopewa na yule askari, nililala chini kwa haraka sana na macho nikawa nayaelekeza kwenye gari  letu ambalo bado lilikuwa linanguruma hadi muda huo kutokana na kutozimwa na taa bado zilikuwa zinawaka kuanzia ya ndani hadi za nje. Mlango mbele wa gari letu upande wa kiti cha kushoto cha dereva ulikuwa wazi baada ya yule askari kuufungua akijaribu kutoka nje hivyo ikawa njia  rahisi sana kwa mlengaji  kumuua kwani gari hii mlango mmoja ukiwa wazi basi taa ya ndani inawaka hivyo mtu wa nje anakuona kirahisi. Tukio hili ni tukio jingine linalonifanya nimshukuru Mungu katika maisha yangu kwani nafsi yangu ilinisihi nifungue kioo cha dirisha nililokaa baada tu ya kuvuka mpakani, Nurulayt naye alifanya hivyohivyo na dereva wa gari ambaye ndiye yule askari wa uhamiaji nchini Botswana wala hakufanya hivyo yeye aliendelea kuacha kioo kimepandishwa. Ndiyo maana hata kioo kilipovunjwa ni risasi iliyolengwa na ikampata begani kisha nyingine zikafuata
Tukiwa bado tumelala chini huku bunduki zetu tukiziweka tayari kwa lolote tuliwaona watu wasiopungua kumi wakiwa na bunduki aina ya AK47 karibia wote kasoro mmoa alikuwa ana bunduki aina ya sniper rifle, walikuwa wakitokea katika pori lililopo upande wa pili wa barabara.
"huyu mwenye bunduki ya wadunguaji ndiye aliyempiga dereva wetu risasi ya mgongo na ya kichwa, hivyo tunahitajika kuwamaliza wote ili tuendelee na safari la si  hivyo tutakwamia hapa" Nurulayt aliongea kwa sauti ya chini huku akiweka bunduki yake sawa.
"Hatuhitaji shambulizi la risasi wapo wengi wale tunahitajika tufanye kitu cha ziada" Nilimwambia Nurulayt huku nikiishusha bunduki yake chini kwani alionekana anataka kuitumia.
"come on Abdul kitu kipi hicho zaidi ya risasi kuwamaliza" Nurulayt aliniambia akionekana hajanielewa.
"una visu hapo?" Nilimuuliza
"ndiyo ninavyo hivi hapa" Nurulayt alijibu huku akifungua sare ya askari wa uhamiaji aliyoivaa akatoa visu vinne akanipatia.
"kuwa mtazamaji mama wa mtoto wangu" Nilimuambia huku nikichukua visu, Nurulayt  aliishia kutabasamu tu kisha akanikonyeza halafu akasema, " good luck ingawa sitaweza kukuona ili niwe mtazamaji". Nilitabasamu kisha nikaviweka visu mafichoni halafu nikaanza kujiburuta kama nilivyofundishwa na jeshi la jeshi la kujenga taifa kipindi namaliza kidato cha sita kwa mafunzo miezi mitatu, nilitambaa kwa umbali mrefu kidogo bila hata kujulikana na wale watu waliopo barabarani. Nilipokaribia eneo lenye nyasi ndefu niliokota kipande cha jiwe nikakirusha mbele yangu kiasi cha mita kadhaa huku nikiwatazama wale watu waliopo barabarani. Risasi zilimiminika kuelekwa upande niliorusha jiwe bila hata kuangalia kama kuna adui wanayemlenga, walipoacha kupiga risasi  nilimuona yule mwenye bunduki aina ya Sniper rifle akiwalaumu waliokuwa wanapiga  risasi kisha akawaamrisha waende kuangalia kuna nini. Amri hiyo waliyopewa ilinifanya nitabasamu tu kisha nikachukua majani mengi nikavijivisha mwilini mwangu kuanzia kwenye viatu hadi kwenye kofia ya sare niliyoivaa,  wale watu walikuja sita upande niliokuwepo kwa kasi bila umakini na walikuwa wanapita sehemu niliyopo mimi kwani ni sehemu yenye njia ya kuelekea upande niliorusha jiwe. Walikuwa wakitembea wawili wawili kwa haraka kuwahi eneo lenye majani mengi bila hata kuonekana kama wanafuata tahadhari yoyote, walipofika usawa wangu ndipo walipojuta kuja mbio bila uangalifu kwani wawili wa nyuma niliwazoa mtama na walipoanguka nilikuwa tayari nimesharukia nikawapiga magoti ya kwenye koo kila mmojs wakatulia kama maji mtungini. Wawili wa kati niliwarushia visu vya kwenye shingo kwa haraka walipotaka kugeuka nyuma kuangalia kilichowapata wenzao, nilipomaliza hayo nilijitupa pembeni kwenye vichaka haraka sana na hata wale wawili waliokuwa mbele walipogeuka waliona miili ya wenzao isiyo na uhai ikiwa ipo njiani.
" Oooh! Shit!" Aliongea mmoja kwa sauti huku akihangaika kuchomoa simu ya upepo iliyopo kiunoni mwake bila hata kuangalia usalama wa eneo hilo kutokana na kuchanganyika na vifo vya wenzao vilivyotokea ndani ya muda usiozidi dakika moja, hakutambua kama kufanya hivyo ni uzembe mkubwa katika eneo lisilo na usalama kama hilo. Vichwa vyao tayari vilikuwa vimevurugwa na tukio la kufa wenzao na hapo ndipo nilipopata nafasi ya kufanya shambulizi jingine la kimya kimya na la ghafla, niliachia visu viwili vilivyobakia ambavyo vilitua katika shingo zao nikilenga sehemu ya shingo ambayo ni mwanzo wa koromeo. Walidondoka kama mizigo kutokana shambulizi hilo kisha wakatulia bila hata kuonekana kufurukuta wakati roho zao zikiachana na mwili, hapo ndipo nilipojiuliza kwanini hawa watu wanakufa hivi bila hata kuonesha purukushani zozote kipindi wanaiaga dunia. Maswali yangu niliona hayana mtu wa kunipa  majibu hivyo sikutaka kupoteza muda eneo hilo hata kidogo, nilichukua bunduki nne zenye mikanda nikafunga usalama wa bunduki zote kisha nikazivaa mgongoni  na nilichukua vibebea visasi vilivyojaa kisha nikaanza kusogea upande wa barabarani kwa kujivuta taratibu mithili ya chatu aliyemmeza mnyama ambaye hajamshibisha kisawasawa. Nilipokaribia nililitazama eneo kwa umakini kisha nikachukua bunduki moja aina ya AK47 niliyoichukua kutoka kwa wale watu niliowaua, niliiangalia nikatoa uaalama wake nikaiweka tayari kuanza shambulizi huku nikiwatazama wale watu ambao sasa hivi wamebaki wanne tu. Sikutaka kusubiri tena nilianza kuwalenga kwa mfululizo wawili wakasalimiana na ardhi wakiwa wameshaacha roho za mikononi mwa malaika mtoa roho, waliobaki ni yule mwenye bunduki ya Sniper rifle na wengine wawili wenye AK47 kila mmoja.Walikuwa wamegusana migongo yao huku bunduki zao wakiwa wamezielekeza mithili ya pembe mshabaha, kila mmoja alikuwa akilinda usalama wa wenzake kwa nyuma yake. Walikuwa wakizunguka kula upande  ili wajihami kwani bunduki ile iliyowaua wenzao hawakujua imetokea wapi, walikuwa wakizunguka kuangalia pande tofauti wakionekana wamechanganywa na vifo vya wenzao. Yule mwenye sniper rifle alipoelekea upande aliopo Nurulayt wakati mwenzake akiwa nyuma yake akimlinda nilisikia mlio uliokaribiana na mzinga na wote wawili wakatupwa umbali wa mita moja toka pale waliposimama na damu ilikuwa imeanza kutoka katika vichwa vyao. Mlio huo ulipotoka na wale walipoanguka sikuona dalili za mtu yoyote kuja barabarani ingawa sauti hiyo ilikuwa ni ya bunduki aina ya shortgun, niliamua kutamba hadi nilipomuacha Nurulayt ili kuhakikisha kama ni yeye aliyepiga kwani bunduki kama iliyowapiga wale watu anayo mikononi mwake. Nilimshukuru Mungu nilipomkuta wa mama mtoto wangu salama akiwa amelala kifudifudi akiwa ameelekeza bunduki barabarani, nilimsogelea  Nurulayt karibu na nilipomfikia alishtuka  akanielekezea bunduki usoni kwa haraka sana akiwa amejigeuza akalala chali kwa haraka sana.
"hey ni mimi" Nilimwambia huku nikishtuka kutokana na uso wangu kutazamana na midomo miwili ya bunduki.
"muda mwingine uwe makini unapokuja kwani hiyo mijani uliyoivaa ningekutambua vipi, utakufa wewe mwanaume" Nurulayt aliniambia
"ok nimekuelewa, ile kazi ni ya mkono wako?" Nilimuuliza kuhusu wale watu wawili waliouawa na risasi moja niliyoisikia ikitokea upande aliopo.
"ndiyo, na wale watatu ni kazi ya mkono wako?" Alikiri ndiye aliyepiga ile risasi kisha akaniuliza swali.
"ndiyo, tena nina nyongeza mama" Nilimjibu huku nikiushuaha ule  mzigo wa risasi mgongoni.
"vizuri nadhani wale wengine umewazima" Nurulayt aliongea
"kabisa nimetumia vile visu hata sauti hawajatoa" Nilimpa uhakika wa kumalizika kwa kazi.
"kwa sumu iliyokuwa kwenye vile visu hata maji hawaombi kama vimetua shingoni mwao, twende zetu" Nurulayt huku akijiinua kutoka pale chini alipokuwepo  kisha akaanza kutembea huku akiwa ameinama na amakunja magoti kidogo. Nilimfuata kwa mwendo huo huo aliokuwa anatembea yeye hadi kwenye gari  letu, Nurulayt aliuvuta mwili wa yule askari wa uhamiaji aliyekusaidia kutuvusha hadi nje ya gari kisha akaokota silaha zote za wale watu waliotuvamia akazitia ndani ya gari. Tulilikagua gari letu.kwenye matairi tukakuta ni zima halina tatizo lolote, baada ya kuona tuna uwezo wa  kuendelea na safari hatukuwa na muda wa kusubiri zaidi ya kuingia ndani ya gari na safari ikaendelea kama kawaida ili  tulivuke pori hilo. Hadi tunalipita pori hilo tayari ilikuwa ni saa nane usiku na sasa tulikuwa tumeingia katika mji mdogo ambao sikuujua jina lake unaitwaje, mji ulitawaliwa na ukimya kutokana na wakazi wake kuwa wamepumzika muda huo wa usiku.  Nurulayt naye alizidi kubadili gia za gari akilipita eneo hilo ambalo  hakunitajia  linaitwaje hadi leo hii, alizidi kuwa makini na barabara huku akiwa kimya kabisa na alionekana hakutaka kuongea kabisa. Nilimuacha aendelee kuchezea usukani na mimi nikanyoosha kiti nikajilaza taratibu na usingizi ukachukua nafasi yake, nilikuja kushtuka usingizini baada ya kusikia napigwa kibao . Nilipofumbua macho nilimuona Nutulayt akiniashiria niinuke na mimi nikainuka, nilipotazama pembeni nje niliona giza bado lipo.
"vipi mbona umesimamisha gari hapa?" Nilimuuliza huku nikiangalia njia na nikagundua tupo sehemu yenye miti mingi.
"hebu vua hayo magwanda ya askariwa uhamiaji wa Botswana ni hatari kwetu" Nurulayt aliniambia huku akivua  magwanda yake pamoja na viatu, nami nilivua  magwanda yangu nikavaa nguo za kawaida nilizokuwa nimezivaa hapo awali. Nurulayt naye alivaa nguo zake za mwanzo na safari ikaendelea huku nikiuchapa usingizi kama kawaida. Niliamshwa kwa mara ya pili na Nurulayt tukiwa tupo katika eneo lenye mji mdogo uliochangamka ambao sikuutambua unaitwaje, kwa makadirio ilikuwa ni saa nne asubuhi kutokana na kuangalia upande ambao jua lipo tangu lilipoanza kuchomoza.
"hapa ni wapi?"Nilimuuliza huku nikipiga miayo kutokana na uchovu niliokuwa nao.
"hebu kwanza funga mdomo huo usije ukanimeza bure, hapa ni Runde hebu shuka tukapate stafustahi" Nurulayt aliniongea huku akinifunga mdomo  nilipokuwa napiga miayo, nilishuka kwenye gari na Nurulayt naye alishuka kisha tukaingia kwenye  mgahawa  uliopo pembezoni mwa barabara. Tulipata stafustahi tukarudi kwenye gari tukaendelea na safari kama kawaida, muda huo mimi ndiye niliyekuwa dereva wa gari na ikawa zamu yake Nurulayt kulala. Hadi inatimu saa tisa alasiri tayari nilikuwa nimeshafika katika kijiji ambacho sikukijua kinaitwaje kilichopakana na msitu mkubwa sana, nilipofika hapo nilimuamsha Nurulayt ambaye alishtuka kisha akaanza kutazama mazingira ya eneo tulilopo kisha akanitazama kwa mshangao sana.
"vipi mbona hivyo?" Nilimuliza baada ya kumuona ananishangaa sana.
"Abdul naona sasa tunataka kuuana" Nurulayt aliongea kwa kulalamika.
"kivipi?"Nilimuuliza.
"mwendo gani umeutumia hadi sasa hivi uwe umefika hapa kwenye hichi kijiji jirani na msitu huu wa Chirinda" Nurulayt aliongea akionekana ameshangazwa na mwendo nilioutumua hadi nimefika hapo.
" wa kifo" Nilimjibu
"sikupi uendeshe tena utaniua we mwanaume unafikiri hii formula one" Nurulayt aliongea.
"wewe ulivyokuwa unaendesha kule Kalahari ulikuwa huoni kama utaua mtu, tema unabahati ulilala yaani ungekuwa hujalala ungekufa kwa uoga" Nilimwambia huku nikishuka ndani ya gari, Nurulayt naye alishuka kwenye kisha akaniambia, " funga milango ya gari na unifuate". Nilifunga milango nikamfuata kuelekea katikati ya kijiji ambacho pia sikukitambua kinaitwaje hadi leo hii, Nurulayt aliniongoza hadi katika mlango wa nyumba ambayo inaonekana ni ya siku nyingi ingawa ina kila dalili za kufanyiwa marekebisho. Aligonga mlango  mara moja kisha akatulia kumya, mlango wa nyumba hiyo ulifunguliwa na mwanamke aliyejitanda vitenge vya kizaire ambaye hakuongea chochote zaidi ya kutuashiria tuingie ndani tu ndiye aliyefungua mlango. Sote wawili tuliingia ndani na mwanamke huyo akafunga mlango kwa makomeo kisha akatuuliza, " za safari?".
"Salama lakini sio salama sana" Nurulayt alijibu huku akimfuata yule mwanamke ambaye alikuwa anaingia katika chumba kimojawapo katika nyumba hiyo, nami niliwafuata bila hata kuambiwa niwafuate hadi ndani ya chumba hicho. Mandhari pana ya chumba chenye mitambo mbalimbali ya tarakilishi ndiyo ilionekana ipo ndani ya chumba hicho, upande mmoja kulikuwa kuna kitanda kipana cha kulala.
"jamani karibuni tena" Alituambia tena yule mwanamke.
"tushakaribia nadhani ni muda  muafaka wa kujua tusichokijua Madam Rhoda" Nurulayt alimwambia yule mwanamke kisha akanigeukia mimi akaniambia "Abdul huyu anaitwa Madam Rhoda kama ulivyosikia nikimuita, alikuwa ni msaidizi wa kaka yangu Sabir ambaye aliuliwa na Faiz kama nilivyokueleza hapo awali na ndiyo yeye aliyenipa mwongozo wa kazi hii ya kumtafuta mwanangu kwa kunipatia vifaa vya  kazi vya kusnzia".
Nilitabasamu baada ya kupokea utambupisho huo wa mwanamke aliyetupokea, yule mwanamke naye alitabasamu baada ya mimi kutabasamu.
"Madam huyu ni Abdul baba yake Ilham na nipo naye  kwenye kazi hii" Nurulayt alimpa utambulisho wangu yule mwanamke.
"ok, sasa tuanze kueleweshana" Yule mwanamke aliongea huku akibonyeza vitufe vya tarakilishi ya mapakato iliyopo humo ndani. Kwenye tarakilishi zilikuja picha mbalimbali za kambi ambayo ilionekana ilikuwa ipo katikati ya msitu, kambi hii ilikuwa imezungukwa na minara mbalimbali yenye vibanda kwa juu ambavyo hutumiwa na walinzi wa kambi hiyo.
"jamani hii ndiyo kambi ya kundi la Gorilla katika msitu wa chirinda, ipo kilomita mbili kusini mashariki mwa barabara ipitayo  katikati ya msitu huo, kambi hii ipo ni mali ya Scorpio nadhani Nuru unamfahamu" Yule meanamke alitoa maelezo halafu akamuuliza Nurulayt.
"Scorpio?! Hapana simfahamu" Nurulayt aliongea huku akivuta kumbukumbu katika halmshauri kuu ya mwili wake kama anaweza kumkumbuka lakini halmashauri kuu ambayo ni ubongo ilionesha kutolikumbuka jina hilo, hivyo yeye pia alikataa  kutolikumbuka jina hilo.
"ngoja nikuoneshe picha yake labda unaweza kumkumbuka maana sikuwahi kulijua jina lake halisi zaidi ya hilo la Scorpio" Madam Rhoda aliongea kisha akafungua faili moja lililopo kwenye tarakilishi  yake lililokuwa na picha ambayo sote tuliitambua kwa jina jingine kabisa.
"Faiz!" Nilisema kwa mshangao sana.
"sasa huyu ndiye mmliki wa hilo kundi ingawa kwa sasa hayupo nchi hii na hajulikani wapi alipo, Nurulayt nadhani unamfahamu." Madam Rhoda aliongea.
"muuaji aliyeutoa uhai wa kaka yangu nitamsahsu vipi? Kumbe bado yupo hai wale waasi  wa Kongo tumewalipa hela nyingi wamuue wamemuacha" Nurulayt aliongea kwa uchungu sana.
"haya jamani tuendeleeni na kilichowaleta" Madam Rhoda alisema huku akifungua picha za msitu wa Chirinda  sehemu ya kambi ya Gorilla boys halafu akasema, "kambi hii ina tower zisizopungua ishirini ambazo zina masniper zote sasa ukiingia bila tahadhari umeisha. Kushoto kwake ndani kuna majengo makubwa mawili ya ghorofa yenye makao makuu  ya kambi hiyo, upande wa kusini mwa makao makuu hiyo ndipo kwenye  ghala lenye vito vya thamani na madini mbalimbali waliyowahi kuyateka hawa watu".
ramani hii hapa itawasaidia kupata mwongozo mzuri tena inabidi muwe na bunduki aina sniper rifle kila mmoja kama mnataka muingie bila kugunduliwa kwani wale walinzi wa juu kwenye zile tower mnatakiwa muwaue mkiwa mbali ili wasiwaone wakawatungua, kumbuka wao ni sniper na ndiyo wenye kibarua kikuu cha kuilinda hiyo kambi. Je mna sniper rifle katika silaha zenu?" Madam Rhoda alieleza mwisho akatuuliza juu ya bunduki hiyo kama tunayo.
"ndiyo tunayo moja tuliyoipata kama ngawira" Nurulayt alijibu
"mnatakiwa muwe na ya pili kwani kutungua masniper ishirini sio mchezo hivyo kila mmoja anatakiwa awe na yake" Madam Rhoda alitusisitiza,  kusikia suala hilo wote tuliinama chini kutokana na kutokuwa na namna ya kuipata hiyo silaha.
"hilo msijali nitawasaidia mtimize wajibu wenu, Nuru hebu lete briefscafe mbili zipo chumba ninacholala" Madam Rhoda alimuamuru Nurulayt ambaye alitoka haraka aliposikia amri hiyo kisha akarejea akiwa mikoba miwili ya kufunga kwa namba akampatia Madam Rhoda.


*kesho kutwa nayo siku uhai na afya vinahitajika kulijua KOSA.

DHAHAMA SEHEMU YA KUMI NA NNE

 DHAHAMA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE



SEHEMU YA KUMI NA NNE!!
"Lakini Ally mpenzi wangu nimefanyaje?" Salma aliuliza kwa masikitiko makubwa huku akionekana kuumia baada ya kusukumwa.
"Unajifanya hujui siyo tena usiniite mpenzi wako kuanzia hivi sasa, we wa kunifanya mimi mtumwa wa ngono hadi umesababisha nisioe wakati natakiwa kuwa na familia sasa hivi" Ally alifoka.
"Ally nakupenda ndiyo maana nimefanya hivyo hadi nikazaa na wewe" Salma akaongea huku akilia.
"Weee tena ishia hapo hapo" Ally alimkaripia huku akimuongeza teke la mguu Salma.
"Ally nikatae ila ukae ukijua Hamida siyo mtoto wa mume wangu bali ni damu yako, ndiyo maana hata alipozaliwa kaka yako alikutania umefanana naye miguu ila ukweli ile ni damu yako kabisa" Salma aliongea huku akilia, Ally alipuuza maneno ya Salma akaondoka eneo akimuacha akilia ingawa kuna jambo lilikuwa likiisumbua akili baada ya kusikia maneno hayo.



****


"  "Ally huyu mtoto kafanana na wewe hiyo miguu balaa ingawa ana sura ya mama yake na baba yake" Shafii aliongea huku akicheka.
"Haaaa! Shemeji nawe waanza kwahiyo waataka sema kafanana na babaye na Ally pamoja nami" Salma alisema huku akimtazama Shafii.
"Ndiyo hivyo ahemeji" Shafii alisema.
"Wewe Chumbio waleta zako sasa huoni kama hiyo miguu ni ya mama yake kabisa, wamefanana tazama kucha hizo uache msifia mdogo wako" Hamis aliongea na kusababisha wati wote wacheke humo ndani.
"Bonoeza usichukie basi masihara ni jadi yetu tangu twacheza michezo ya kitoto, hongera bwana kwa kupata binti mrembo huyo na urembo wake unaonekana tangu akiwa mtoto" Shafiu aliongea huku akimpa mkono wa pongezi rafiki yake kipenzi.
"shukrani Chumbio rafiki wa tangu utotoni" Hamis aliitikia huku akicheka
"sasa Bonoeza hapo inabidi ufuge mbwa na bunduki ununue mapema maana wajanja wataanza kuja kutoa salamu sana kumbe wataka wampate malkia hapa" Shafii alisema na wote waliopo nyumbani kwa Hamisi wakacheka " Maneno aliyoambiwa na Salma ndiyo yalivuta kumbukumbu yakamkumbusha siku hiyo ambayo Hamida alikuwa ndiyo kaletwa nyumbani baada ya kuzaliwa katika hospitali ya Ngamiani, alizidi kukumbuka zaidi na hapo akakumbuka tukio jingine kabisa baada ya kumuona Hamida akiwa na miaka mitano tu tangu azaliwe na siku hiyo alikuwa akibadilishwa nguo na mama yake Salma, siku hiyo alimuona Hamida akiwa ana mwili unaofanana wake sana. Ally alikumbuka zaidi juu ya siku hiyo na akawa anajifikiria kwa umakini haswa ndipo akajikuta anaamini lakini siyo kwa asilimiia zote yale maneno aliyoambiwa na Salma.
"Dah nimefanyishwa dhambi mbaya ya kuzini na mke wa mtu bila kujijua" Alky aliongea huku akikata mitaa na alionekana ni mwenye majuto makuu juu ya jambo hilo ingawa hakutegemea kama atalifanya, alitembea huku uelekeo wake maalum ukiwa haujulikani kwani alikuwa anazurura mitaani tu.
"ni bora nilale nje kuliko kulala kwenye mali haramu niliyokuwa nimekabidhiwa na nikajikuta nimeipokea bila kujijua, ni bora nisifanye kazi niwe masikini kuliko kuitumia hii elimu niliyosomeshwa kwa kutumia fedha haramu zilizosababisha mwanadamu mwenzangu amwage damu kwa manufaa ya wengine. Shahada nimeipata kwa pesa zilizotokana na damu ya mwenzangu kumwagika, nawachukia Shafii, Hamid, Hassan, Hussein, Falzal, Hamisi pamoja  mke wako Salma aliyetoa kitu kichafu ili aangamizwe kiumbe asiye na hatia. Hisan Shelukindo pia mwanaharamu mkubwa wewe umekuwa na maisha mazuri kwa ukatili wenu  huo" Ally aliongea kwa hasira akiwa tayari ameshafika Sahare kwa kutembea tu bila hata mpangilio; alihisi uchovu kwa kutembea siku hiyo nzima na akakaa katika baraza la maduka ambayo yalikuwa ndiyo yamekamilika ujenzi wake lakini bado hayajafunguliwa. Alijiona ni mmoja wa wenye makosa kwa kutumia sehemu ya mali iliyotokana na  njia haramu ingawa hakujijua, alijikuta hata akilengwa na machozi na hatimaye alianza kulia kimya kimya hadi pale alipochoka akainuka kwenye baraza hiyo.
"Bora uwe masikini utaabike kuliko uwe tajiri kwa njia isiyo ya halali bila kujijua, inauma sana" Ally alisema kwa uchungu huku akinyanyuka tena barazani hapo na kuanza kutembea kama ilivyokuwa awali, alitembea akawa anafuata uelekeo wa nyumbani kwa baba yake hadi alipofika akaingia ndani na moja kwa moja akaenda kujitupa sebuleni akalala usingizi mzito bila hata kuwa amekula kitu chochote siku hiyo.

   Asubuhi ya siku iliyofuata aliamka akajisafisha mwili wake akatoka hadi nje, akamuona dereva wa gari za baba yake akiwa yupo barazani akipata kifungua kinywa akamsabahi kisha akawa anaelekea getini.
"Kaka unaelekea wapi nikutoe maana gari zipo hapa" Dereva wa baba yake alimuambia.
"unaweza ukapumzika kaka mkubwa" Ally alimuambia dereva wa gari ya baba yake kisha akatoka nje akawa anaelekea ilipo barabara ya Mombasa, alitembea hadi akipoifikia hiyo barabara akamuita dereva wa pikipiki akaja mara moja.
"Mpirani kaka" Ally alimuambia dereva wa pikipiki ambaye alimchangamkia akamuambia apande tu bila hata kutaja bei, Ally alipanda hiyo pikipiki na safari ikaanza ambapo ilichukua dakika kumi na tano kwa mwendo wa pikipiki akawa ameshafika Mpirani akampa dereva yule pesa yake kisha akaingia mtaani na akatembea hadi mahali ambapo nyumba zipo moja moja na hatimaye akaifikia nyumba kubwa ambayo ipo kama gofu tu ikiwa ipo katikati ya shamba kubwa  ikionekana  kuwa ipo peke yake mbali na makazi ya watu wengine. Nyumba hiyo ilionekana kutolewa milango na baadhi ya madirisha baada ya kukaa siku nyingi bila kutumiwa kama makazi ya watu na eneo zima lenye kuizunguka nyumba hiyo lilikuwa  na majani mengi yaliyoonekana hayaku punguzwa kwa muda mrefu.
Ally aliingia ndani ya nyumba hiyo iliyoezekwa kwa bati  lililochakaa na sakafu ya chini ilionesha kuwa ni ya udongo mwekundu  ambao hutumiwa kukandika kuta za nyumba za udongo, ilikuwa ni nyumba kubwa yenye  vyumba takribani vinne na sebule ambayo ndani ina kuta za udongo zilizowekwa plasta kwa nje. Sebule kubwa ya nyumba hiyo ilikuwa na usafi mkubwa kupitiliza ambao ulimshangaza sana Ally na vyumbani kulikuwa kuna nyuzi nyingi za buibui kiasi kwamba haiwezekani hata kidogo mtu wa kawaida kuingia humo ndani bila hata kusafisha hizo nyuzi za buibui, Ally aliangalia kila chumba akawa anakumbuka matukio tofauti ambayo yalikuwa yakifanyika hasa kipindi ambacho anaishi katika nyumba hiyo ambayo kwa sasa imetekelezwa na mwenyewe.
"Ni historia nisiyoweza kuisahau na ni mazingira yasiyoweza kusahaulikavkwa mtu kama mimi na natamani niyarudie niishi kama nilivyokuwa awali huenda amani ya moyo wangu itarejea kama ilivyokuwa awali" Ally aliongea akiwa amesimama katika mlango wa chumba ambacho ndiyo alikuwa akikitumia kipindi akiishi katika nyumba hiyo.
Akiwa amesimama hapo alisikia sauti ya mtu akipiga uruzi kutoka nje ya nyumba hiyo na ikamlazimu atoke aende kutazama ni nani huyo, alipokuwa akikaribia mlango wa kutokea mlango wa nyumba hiyo alikutana na kijana wa kisomali aliyekuwa akifanana sana na mtu ambaye alikuwa anamjua ila jina lilikuwa limemshamtoka kichwani mwake. Kijana huyo alikuwa amevaa kanzu nyekundu  iliyomka vyema na kofia ya rangi ya kahawia, Ally alipomuona huyo kijana alizidi kuvuta kumbukumbu juu ya alipomuona lakini hakukumbuka chochote.
"habari yako kijana" Ally alimsabahi yule kijana.
"salama tu, shikamoo" Yule kijana aliitikia.
"Marhaba sijui ni nani mwenzangu" Alky aliitikia kisha akamuiliza swali yule kijana.
"naitwa Fahmi ni mjukuu wa mzee mmoja maarufu wa kiarabu anayeitwa  Muburaka" Yule kijana alieleza.
"Mzee Mubaraka huyuhuyu baba yake Faimu waliyehamia kijiji cha Bwagamacho" Ally alisema.
"Ndiyo huyo huyo na mimi ni mtoto wa Faimu" Fahmi alieleza.
"ok ok karibu bwana leo nimekuja kuzuru makazi yetu ya zamani" Ally alieleza.
"Asante sana, mimi huwa ni sehemu yangu ambayo napenda kukaa huwa inanikumbusha mengi sana hii na nikiwa na huzuni basi huwa nakuja kukaa hapa ndiyo maana unapaona pasafi sana hasa upande wa sebule hii" Fahmi alieleza.
"Ok kijana ndiyo maana nilitaka nishangae imekuwaje mpaka pawe  hivi, karibu tukae sote na mimi leo nimependelea sana kukaa humu" Ally alimuambia huku akimpa mkono Fahmi ambaye aliupokea akiwa na tabasamu pana usoni.
"umefanana sana na baba yako hadi mkitabamu mpo hivyohivyo, hakika mungu kawajalia tabasamu pana kijana" Ally alimwambia Fahmy na kusababisha Fahmy atabasamu.
"asante anko, napenda nikuite anko kama hutajali" Fahmi alimuambia  Ally.
"si vibaya waweza kuniita hivyo tu kwani umeonesha heshima kubwa sana kwangu kijana" Ally alisema.
"asante sana nafurahi kuongea na wewe" Fahmi alisema.
"hata mimi pia, vipi baba yako hajambo?" Ally aliongea huku akitabasamu kisha akamuuliza juu ya hali ya baba yake, swali hilo lilimfanya Fahmi aondokwe na uso wa tabasamu usoni mwake ingawa alilazimisha tabasamu hilo lirudi katika uso wake.
"Baba yupo uarabuni kwa sasa na huko ndipo alipojenga maisha yake" Fahmi alijibu huku akilazimisha tabasamu usoni mwake.
"ohoooo! Mpe hongera sana rafiki yangu aliyenijali sana yule" Ally aliongea huku akitabasamu.
Maongezi yao yaliendelea hadi ilipotimu adhuhuri Fahmi akaaga akaondoka na akamuahidi Ally angerejea akiwa na ugeni mkubwa sana kama angekuwepo hapo. Alky alimpa ahadi ya kuwepo eneo kwa siku nzima hivyo angemkuta, hakuutambua ugeni huo ulikuwa ni ugeni gani na laiti angeutambua angetamani hata auone muda huo lakini haikuwezekana. Ally aliendea kukaa hapo hadi ilipofika muda wa alasiri akaja kijana mwingine akiwa na chombo cha chakula akampatia, yule kijana alimuambia chakula hicho kilikuwa kimeagizwa aletewe na Fahmi.  Ally alishukuru sana akakila chakula chote kutokana na njaa  ambayo tayari ilishaanza kushambulia tumbo lake, baada ya kumaliza kula alitoa shukrani kwa ubinadamu aliofanyiwa na yule kijana
aliyetumwa pia akamwambia apeleke shukrani za dhati kwa Fahmi kwa kumjali namna hiyo.
Baada ya kijana yule kuondoka Ally aliendelea kukaa hapo akikumbuka mambo mbalimbali kipindi akiishi  ndani ya nyumba hiyo kabla hajahama, mambo mengine ya furaha na upendo na alivyokuwa akiishi na shemeji yake ambaye alimjali yalimpa tabasamu kila akiyakumbuka ila alipokumbuka wema aliofanyiwa na kaka yake alijikuta anasonya tu kwani hakuupenda hata kidogo huo wema wake na wala hadi muda hakuona umuhimu wake.
"Shetani katumia ushetani kunifanikishia malengo yangu, hadi sasa sioni umuhimu wa mimi kufikia haya malengo ikiwa kuna mwenzangu kateseka kwasababu ya huyo shetani. Kakimbia kwao kwasababu ya huyo shetani. Shetani huyu kanisaidia ili na mimi anitumbukize katika ushetani"Ally aliongea kwa hasira  kisha akanyanyuka akasema, "namchukia maana bila yeye mimi nisingetumiwa kama mtumwa wa ngono na yule malaya aliyekubuhu kwa umalaya tangu yupo kigori. aaargh! Nawachukiaaa!" Ally aliongea kwa hasira kisha akapiga ngumi ukutani na kupelekea sehemu ya plasta iliyowekwa juu ya ukuta wa udongo wa nyumba hiyo uanguke.
Chuki za waziwazi kwa  kaka yake ndiyo zilikuwa zimeutawala moyo wake na hakumpenda kama ilivyokuwa akimpenda hapo awali, hakuona umuhimu wa yeye kumuita kaka wakati kafanya mambo yasiyopendeza kwa mwanadamu yoyote mwenye moyo wa kibinadamu na siyo wa  kama aliokuwa nao kaka yake. Alitokea kuwachukia ndugu zake wote walioshiriki mpango ule hakuona faida ya kuwa na ndugu kama wao katika dunia hii, aliona ni bora angekuwa na undugu na jiwe kuliko kuwa na undugu na hao aliowaheshu kama kaka zake lakini hakuona ustahiki wao wa heshima hiyo aliyowapa.






               SURA YA NANE.
   Majira ya magharibi katika eneo hilo alilokuwepo Ally paliiingia ugeni mwingine ambao haukutia mguu katika eneo hilo kwa miaka kadhaa tangu walipoondoka, ugeni huo ulikuwa ni msafara wa magari mawili ya kifahari yenye thamani kubwa sana nchini Tanzania kwa kipindi chote. Magari hayo yalikatisha katika majani baada ya barabara ya kuingia eneo hilo kuwa imeota majani kila sehemu.  Ally aliposikia mingurumo ya gari hiyo wala hakujishughulisha kwenda kuangalia zaidi ya kutulia vilevile sehemu ya dirishani ya sebule hiyo alipokaa katika eneo ambalo  dirisha limetolewa, aliposikia hatua za mtu akiingia hapo ndani yeye alielekeza machp mlangoni tu na hadi mtu huyo anaingia tayari alikuwa ameshamuona na ni mtu kati ya watu anaowaheshimu akiwa amebeba mikeka inayotengenezwa kwa ukindu maarufu kama majamvi kwa wakazi wa jiji la Tanga
"Ally kumbe huku" Sauti ya mtu huyo ilimsemesha na hapo Ally akainuka akamfuata.
"ndiyo baba nipo huku, shikamoo" Ally alimuamkia baba yake baada tu ya kumjibu swali alilouliza.
"marhaba tumekutafuta sana mchana wa leo ili uje huku maana kuna jambo muhimu sana" Mzee Buruhan alisema.
"sawa baba nipo tayari hakuna kilichoharibika" Ally aliongea huku akimpokea  baba yake majamvi.
"yatandike hapo chini kwa ajili ya wageni watakaokuja maana mzee Mahmud kasema kuna ugeni utafika hapa kwa ajili ya jambo hili tuliloitiwa hapa.
"sawa baba" Ally alitii amri akaanza kuyatandika majamvi chini kama alivyoambiwa na baada ya muda akawa amemaliza.
"vizuri sasa tumsubiri mzee mwenzangu anakuja sasa hivi na nimeambiwa nisiwaruhusu ndugu zako kuingia mpaka yeye afike" Msee Buruhan  aliongea huku akienda kuketi dirishani alipokuwa ameketi Ally awali, Ally naye aliungana naye kwenda kukaa alipokuwa  awali.
Baada ya dakika tano mlio wa pikipiki ulisikika nje ya nyumba hiyo ikija na kisha baada ya dakika moja ikaondoka, muda huo huo mzee Mahmud alionekana akiingia mlangoni akiwa amebeba taa nne kubwa za kuchaji baada ya pikipiki hiyo kuondoka.
"vipi kila kitu tayari?" Mzee Mahmud aliuliza.
"ndiyo kila kitu tayari mzee mwenzangu" Mzee Mahmud alijibu.
"vizuri basi, Ally hujambo mwanangu" Mzee Buruhan alipongeza kisha akamjulia hali Ally.
"Sijambo baba shikamoo" Ally alijibu kisha akamsalimia.
"Marhaba mwanangu vizuri kwa kuwepo hapa, ngoja nianze kazi" Mzee Buruhan aliongea kisha akaanza kutamka maneno yasiyoeleweka akawa anazunguka eneo zima lenye mikeka halafu akafanya hivyo kwenye kila pembe ya ukuta hadi akamaliza sehemu zote na alipomaliza kufanya hivyo aliwasha taa alizokuja nazo akazitundika ukutani kwenye kila kona.
"Sasa hao wanaweza kuingia wakae upande wa kushoto na uwaambie wasiongee mpaka niwaambie mimi, Ally kaa pembeni yangu"  Mzee Mahmud aliongea kisha akakaa chini, mzee Buruhan alitoka nje na baada ya muda akarejea akiwa pamoja na Shafii,Salma, Hamida na Jamal.
Shafii aliongozwa na Jamal hadi eneo wanalotakiwa wakae na alishushwa kwenye kiti akakalishwa kitako, baada ya wote kukaa chini kwenye jamvi waligeuka wakawa wanamtazama mzee Mahmud kujua kinachofuata.
"Bado ugeni mmoja uingie, wageni karibuni" Mzee Mahmud aliongea huku akitazama mlangoni na kupelekea watu wote watazame mlangoni, ugeni ulioingia hapo ulikuwa ni watu  wanaowajua ambapo wengine walishtuka baada ya kuuona ugeni huo ambao haukueleweka umefika hapo kwa usafiri gani kwani walionekana tu wapo mlangoni.
Wa kwanza kuonekana mbele ya macho yao alikuwa ni Zalabain akiwa amevaa joho jeusi  na kofia nyupe ambaye alitambulika kwa Ally na Shafii pamoja na mzee Mahmud, Ally alimtambua Zalabain  kama Fahmi aliyekuwa naye hapo hadi muda wa adhuhuri na hakumfahamu kwa vingine kabisa. Shafii alimtambua huyo mtu kama mbaya wake baada ya kuiona sura yake siku aliyokufa mganga Sauti ya radi na alimkimbia, alipomuona alishtuka sana alitamani hata ardhi ipasuke atumbukie asionekane eneo hilo kwani alishuhudia ukatili wa Zalabain hivyo alimuogopa. Wageni wengine walioingia eneo hilo walikuwa ni Bi Farida na Zayina wakiwa wamevaa nguo za thamani kubwa walizopata wakiwa katika ulimwengu wa majini, Shafii alipowaona alijikuta akijawa na furaha akataka kutamka neno ila ishara ya baba yake ikimkataza kutozungumza ikamfanya atulie.
"Karibu Zalabain mwana Zaif mjukuu wa Zulain mfalme wa himaya ya majini ya  Majichungu, karibu uketi upande ule wa pili ukiwa na wageni wenzako" Mzee Mahmud alisema huku akitabasamu na kusababisha Zalabain atabasamu pia, Zalabain na mama yake pamoja na dada yake walienda kukaa mwingine kabisa pembeni ya upande aliopo Shafii.
"Sasa basi nimewaita hapa ili tuweze kutatua tatizo ambalo lingemsababishia mzee mwenzangu hapa asibakiwe na hata muhomili mmoja ndani ya dunia hii, utatuzi wa tatizo hilo utaanza kuonekana tu ikiwa ukweli wote utakuwa utakuwa hadharani" Mzee Mahmud alisema kisha akamwangalia Shafii akamwambia, "Shafii napenda uanze kuongea ukweli kuanzia unaanza kumpenda Bi Farida na ulivyompata hadi ukamuoa, tafadhali narudia tena tafadhali ukweli ni muhimu katika kila kitu".
Baada ya mzee Mahmud kumaliza kuongea alimpisha Shafii ili aeleze ukweli wake wote, Shafii naye hakuwa na jinsi zaidi ya kueleza ukweli wote juu ya suala hilo ili apate  nafuu ya matatizo yake kwa jinsi anavyoamini na kwa jinsi alivyoambiwa na mzee Mahmud. Shafii alianza kwa kusafisha koo lake kisha akasimulia, "Kwanza napenda nitangulize msamaha kwa hichi nitakachokusimulia ikiwa kitakuwa kimemkwaza yoyote kwani si kizuri, nilikuwa ni mtoto mtiifu sana kwa wazazi wangu kwa kipindi ambacho bado sikuwa nimepevuka kutokana na malezi ya kimaadili aliyonilea baba yangu kwa  kipindi hicho. Ndiyo muda huo huo mke wangu mama Zayina alikuwa angali binti mdogo hata kuvunja ungo bado ingawa alikuwa akitajwa ni mmoja kati ya mabinti wenye uzuri ambao haukuwahi kutokea katika kijiji chetu cha Bwagamacho Baada ya Farida kuanza kupevuka ndipo uzuri huo wa umbo na kila kitu ulianza kuonekana na kipindi hicho na ndiyo wavulana wa rika langu wakaanza kumfuata lakini waliambulia kukataliwa na binti huyo na hata wengine walishtakiwa kwa wazazi wao baada kumtongoza, jambo hilo lilinitisha na kunifanya nishindwe kwenda kumuambia kwa kuhofia ukali wa baba yangu kama akijua. Nilimpenda sana tena sana lakini nilihofia kupigwa sana na baba yangu kama nilivyoshuhudia wenzangu wakifanyiwa hivyo na baba zao baada tu ya mashtaka kuletwa nyumbani juu ya kumtongoza Farida. Baada ya miaka miwili kupita ndipo nilipoanza kupata ujasiri wa kumtongoza ingawa nilikuwa nina uoga kwa mbali, kutongoza kwangu kuligonga mwamba na hata nilipomueleza rafiki yangu kipenzi Hamis ambaye ni kaka yake juu ya suala hilo aliniambia yupo tayari kumsaidia ikiwa tu na yeye nitamsaidia kufanikisha jambo analolitaka.
"Jambo gani wataka nikusaidie  Bonoeza" Nilimuuliza Hamis.kwa kutia jina la utani ambalo hakuwa analipenda kabisa kwa kipindi hicho.
"Shafii waanza sasa nimesema hilo jina silitaki nitaacha kusaidia nikamjaze sumu dada yangu umkose" Hamis alinijia juu baada ya kumtajia hilo jina.
"Hamis nisamehe rafiki yangu niambie shida yako sasa" Nilimuomba radhi na nikawa tayari kuisikiliza hiyo shida yake kwani ndiye rafiki yangu wa shida na raha.
"rafiki yangu hii ni aibu sana hasa kwa vijana wa rika langu na nimeificha ila kwakuwa wewe ni rafiki yangu wa muda mrefu nimeamua nikueleze ili unisaidie na wewe  nikusaidie, kiufupi nampenda sana Salma yule mtoto mzee Rajabu ila mdomo wangu ni mzito kutamka neno hili kwake na ninabaki nikiungua ndani kwa ndani tu" Hamis alinieleza tatizo lake ambalo nilikuwa nipo tayari kumsaidia tu ili nipate moyo wa dada yake  kipenzi, tatizo lake lilikuwa ni dogo tu kwani  hata Salma alikuwa akimpenda vilevile na ishara zote niliziona ila tu wote hawakuwa na ujasiri huo. Nilimsaidia hadi akampata Salma na mimi akaanza harakati za kunisaidia lakini hazikuzaa matunda kabisa kwani msimamo wa Farida bado ulikuwa ni uleule na hata alipomtumia Salma katika suala hilo ilikuwa vilevile na yeye alizidi kunipa moyo kuwa nitampata ingawa nilianza kukata tamaa juu ya suala hilo.  Niliendelea kumbembeleza Farida lakini sikuchoka kwani niliamini yeye alikuwa akinipenda mimi pia na kama angekuwa hanipendi basi angelikuwa amenishitaki siku nyingi nyumbani kwetu juu ya kumsumbua kwangu lakini hakufanya hivyo, hakika sikutambua kama kaanza kukomaa kiakili na jambo kama hilo hakuwa na haja tena kulisema kwani ingeonekana ni akili za kitoto. Niliendelea kujipa moyo nikijua ipo siku nitampata na sikutambua kama mawazo yangu ni sawa na kuchemsha mawe nikitegemea yatachemke kutokana na upendo mzito nilionao kwake, sikutambua kama najipa matumaini hayawezekani kutokea hivihivi kama kubadilika kwa majira ya mwaka kutoka kiangazi hadi vuli. Nilichojali ni kupata jibu sikujali itachukua muda gani hadi niwe naye, niliendelea kusumbuka katika kumueleza kila siku lakini niliambulia patupu na nikawa natembea na matumaini ya kumpata tu kichwani mwangu. Matumaini yangu yaliishi katika moyo wangu lakini baadaye yalikufa baada ya muda wa miezi kadhaa tu na nikajikuta nikiumia moyoni, kufa  kwa matumaini yangu kulikuwa ni baada ya kuingia kikwazo katika kumpata Farida...



*Hatimaye akubali kufunguka

*usikose kujua alichofunguka.

Monday, November 30, 2015

KOSA SEHEMU YA KUMI NA TATU


TEMBELEA:http://www.facebook.com/riwayamaridhawa




  KOSA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA

SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE



 ILIPOISHIA

Nilienda sehemu yenye silaha nikachagua bastola za aina mbili pamoja na maboksi kadhaa ya risasi, kwa bunduki kubwa nilichukua bunduki aina ya UZI ya nchini Israel ambayo imeundwa na mwanajeshi wa kiyahudi anayeitwa Uziel Gal mwaka 1948. Bunduki hii ni moja  kati ya bunduki hatari duniani yenye uwezo kupiga risasi mfululizo kama ilivyo AK47, MP5 na nyinginezo, nilibeba risasi za kutosha na viwambo vya kuzuia sauti nikaenda kuviweka pale nilipoelekezwa.
"vipi visu hubebi?" Nurulayt aliniulixa huku anipatia visu sita vikubwa, nilivipokea visu hivyo bila ya kusema chochote nikaviweka kwenye gari kisha nikamtazama kama anaweza kuniambia la ziada.
"panda tuondoke" Nurulayt aliniambia nami nikazunguka mbele kwenye mlango wa pembeni ya dereva nikapanda.



ENDELEA NA MKASA HUU WENYE KUELIMISHA NA KUSISIMUA


SEHEMU YA KUMI NA TATU!!

Usukani wa gari hili ulikamatwa na Nurulayt na safari ya kuelekea pori la Chirinda ikaanza mara moja baada ya geti lililokuwa lipo humo ndani kufunguliwa na kifaa maalum, baada ya gari kutoka geti lile lilijifunga tena kama ilivyokuwa awali na tukawa tupo nie ya nyumba hiyo kwa upande mwingine kabisa. Ilikuwa ni majira ya saa tano kasoro za usiku barabara ilikuwa tulivu sana kuliko kawaida, tulikuwa tukipishana na magari machache tu njiani yaliyokuwa yanaitumia barabara kwa muda huo. Tulirudi hadi katikati ya jiji la Widhoek kuifuata barabara ambayp sikuijua inaitwaje hadi muda huo, Nurulayt aliifuata barabara hiyo kuelekea mashariki ya jiji la Widhoek kwa mwendo wa kasi sana. Alikuwa akiweka gia na kutoa gia nyingine huku akicheza na usukani kwa umakini sana na kusababisha gari hii iende mwendo mkali hadi ikawa inatoa mlio kama wa kulalamika kwa kuendeshwa  mwendo huo, gia tano za gari hii zilitumiwa ipasavyo na Nurulayt kama anaendesha gari ya mashindano hali iliyonisababisha nifunge mkanda mwenyewe kwani mwanzo sikuwa nimefunga mkanda. Baada ya muda mfupi tulikuwa tumeingia kwenye eneo la jangwa lisilo na majani wala nyumba za watu, tulipongia katila jagwa hilo ambalo nalijua kwa jina la Kalahari ndiyo mwendo wa gari  ulizidi . Nurulayt hakuonekana kujali sana kwa mwendo aliokuwa anautumia yeye ndiyo alizidi kukanyaga mafuta hadi mshale wa mngurumo  wa gari ukafika sehemu yenye alama nyekundu huku kengele ya hatari ikigonga kwa fujo.
"we mwanamke sikuwezi hata kidogo" Nilimuambia huku nikisikitika kwa mwendo aliokuwa anautumia Nurulayt
"kwanini unasema hivyo?" Nurulayt aliniuliza huku macho yake yakiwa makini kuangalia mbele.
"huu mwendo sijui upo mashindano ya formula 1" Nilimwambia kuhusu mwendo anaoutumia tena niliufananisha mashindano maarufu ya magari ya formula 1 yenye magari yanayooenda kwa kasi sana, maneno yangu yalimfanya Nurulayt atabasamu kisha akasema "we unataka tutembee mwendo wa harusini unafikiri tutafika leo Abdul yaani hapa hatujafika Botswana halafu tunaelekea Zimbabwe".
"Mh! Haya suka twende kazi" Nilimwambia kukatisha mazungumzo yetu kisha nikakaa kimya na sikuongea hadi Nurulayt alipopunguza mwendo akaingia kwenye sheli iliyopo pembezoni mwa barabara.
"vipi mafuta yamepungua?" Nilimuuliza.
"hayajapungua ila yanahitajika yaongezwe" Nurulayt alijibu huku akishuka kwenye gari baada ya gari kuliegesha gari jirani na mashine ya kujazia mafuta, Nurulayt alilipa pesa na gari ikajazwa mafuta hadi tenki lote likajaa kisha akarudi kwenye gari lakini hakukaa kwenye kiti cha dereva bali alikaa kwenye viti vya nyuma na kiti cha dereva kikabaki kitupu kama kilivyo.
"Nuru mbona unakaa huko mbona sikuelewi ?" Nilimuuliza huku nikigeuka nyuma nikamtazama.
"Abdul huelewi nini au mimi kuachia usukani kuja kukaa huku?" Nurulayt aliniuliza.
"ndiyo maana yake hicho ndicho nisichokielewa" Nilimwambia.
"Abdul hapa tupo karibu na West gate na West gate camp katika jangwa hili la Kalahari, mbele kidogo kiasi cha mita 500 kuna mpaka wa Trans Kalahari ambao unatenganisha nchi hii na Botswana na una ulinzi mkali. Sasa basi hatuwezi kuuvuka mpaka huo bila ya kuwa na mtu ambaye ni askari wa pale, nimetoka kwenye kiti cha dereva ili kumpisha askari niliyemkodi kwa ajili ya kutuvusha atuvushe" Nurulayt aliongea kunielewesha juu ya mpango wake ambao nilikuwa siujui kabisa.
"hapo sawa nimekuelewa" Nilimwambia kukubali kuuelewa mpango wake mzima alioupanga, maelezo yake yaliniridhisha na nikatazama mbele.
" sasa sikiliza" Nurulayt aliniambia huku akinivuta bega, niligeuka kumtazama ili  kumsikiliza nini anachotaka kuniambia.
"katika kazi kama hizi usipende kuwa muongeaji na muulizaji wa maswali sana, unatakiwa uwe kimya Abdul ingekuwa mwingine tayari ameshakupiga risasi" Nurulayt aliniambia huku akinitazama kwa umakini usoni, nilimsikiliza maneno yake kisha nikashusha  pumzi halafu nikasema "poa" nikageuka mbele. Baada ya muda takribani dakika kumi kupita mlango wa dereva ulifunguliwa na mtu mwenye mavazi ya kiaskari aliingia ndani ya gari  kisha akatutazama akasema, "samahani kwa kuchelewa".
Askari huyu aliwasha akaliingiza barabarani na safari ikaendelea wote tukiwa kimya bila ya kuongea chochote, baada ya dakika tano tulikuwa tumefika sehemu hiyo ya mpaka ambayo ilkuwa na ukaguzi wa magari yanayotoka na kuingia nchini Namibia. Mpaka huo ulikuwa na njia mbili ambayo moja yanapita magari yanayokwenda nje ya nchi na nyingine yanapita magari yanayoingia ndani ya nchi, tulipokaribia  eneo hilo yule askari aliwela gari kando akatuomba tumsubiri anarejea sasa hivi. Alishuka ndani ya gari akaenda kwenye ofisi zilizopo hapo mpakani, tulibaki tukiwa tunamsubiri na alirejea baada ya dakika takribani tatu kisha akaingia ndani ya gari safari ikaendelea tukawa tunaelekea kwenye mpaka kuvuka. Alipofika eneo la ukaguzi alitoa kadi na makaratasi akawaonesha askari ambao walimruhusu kupita bila hata kumuuliza  lolote, tuliendelea na safari tukivuka bango kubwa linalo  tukaribisha  nchini Botswana. Yule askari aliendesha gari kwa mwendo wa mita takribani 400 kisha akashuka akatuaga akikutakia safari njema, baada ya askari kuondoka Nurulayt alirudi  kwenye usukani kama kawaida na safari ikaendelea kwa mwendo ule ule wa kilevi. Baada ya saa moja tangu tuvuke pale mpakani tulitokea kwenye mji mdogo uliokuwa umechangamka sana, ilikuwa yapata saa saba za usiku na ilitubidi tuegeshe gari kando ya barabara ili tupumzike humo humo ndani ya gari kwa ajili ya usalama wa
vitu vyetu, tulilala usingizi wa mang'amng'am hadi kunakucha tukaendelea na safari yetu. Usukani wa gari kama kawaida ulikamatwa na Nurulayt na mwendo wa gari aliupunguza kwa sababu tulikuwa tumeingia katika makazi ya watu. Tulitembea kwa umbali wa kilomita kadhaa tukawa tumefika sehemu yemmnye barabara mbili ambayo moja inaelekea kushoto na nyingine inaelekea kulia, Nurulayt alipokaribia njia hizo aliweka gari pembeni na jirani na mgahawa aliweka breki ya mkononi huku akiliacha gari likiwa linawaka.
"twende tukanywe chai saa tatu hii" Aliniambia huku akiteremka garini nami nikamfuata bilab kuongea jambo lolote, tuliingia ndani ya mgahawa. Tulipata kifungua kinywa kwa pamoja na tulipomaliza  tulirudi garini na safari ikaendelea huku macho yangu yakiwa dirishani kuangalia mandhari ya nchi hii kwa upande wa sehemu wanazoishi watu wenye hali ya chini. Baina ya zile njia zilizokuwa zimegawanyika sisi tulifuata njia ya upande wa kushoto, tulienda kwa mwendo wa masaa kadhaa tukawa tumefika sehemu yenye mji mdogo uliochangamka sana.
"hapa panaitwa Maun ni sehemu iliyo karibu na hifadhi ya wanyama kwa upande wa kushoto na delta ya mto Okavango kwa upande huo huo" Nurulayt alinielezea  juu ya sehemu iliyokuwa ipo mbele yetu.
"ok" nilimuitikia kwa ufupi tu kisha nikakaa kimya nikimuacha Nurulayt acheze na usukani wa gari, Nurulayt naye hakuwa muongeaji sana  baada ya kunielezea hivyo alikaa kimya akaelekeza umakini  wake barabarani. Haikupita hata nusu saa tangu alivyonieleza hivyo usingizi mzito ulinichukua kutokana na uchovu nilionao uliotokana na kutolala usinfizi wa kutosha, nilikuja kuamka baada ya kusikia napigwa kibao huku jina langu likiitwa.
"Amka wewe tukale jioni hii"Nurulayt aliniambia nilipofumbua macho kumtazama, hapo nilibaini giza llishaanza  kuingia na tulikuwa tunaonana kupitia taa ndogo iliyopo ndani ya gari.
Nilipiga muayo mrefu kisha nikamtazama Nurulayt ambaye alionekana kuchoka sana.
"shuka bwana twende au wewe huhisi njaa?" Nurulayt aliniuliza baada ya kuona namtazama bila ya kushuka kwenye gari.
"hapa ni wapi?" Nilimuuliza bila hata  kujali maneno aliyoniambia.
"bwana hebu shuka huko  mwanaume una maswali kama mwanao, nahisi  kachukua tabia yako" Nurulayt aliongea huku akinisukuma nishuke. Muda huo  yeye alikuwa tayari ameshafungua mlango wa upande wake alikuwa anasubiri mimi tu nishuke, nilifungua mlango nikashuka chini kisha nikaenda hadi upande aliopo Nurulayt ili aniongoze kuelekea hiyo sehemu ya kwenda kula kwakuwa nilikuwa mgeni ndani ya eneo hilo.
"yaani wewe na mwanao mkikaa na mimi nahisi mtaniua maana mna maswali mengi kama polisi" Nurulayt aliendelea kuongea huku akinishika mkono kuelekea ndani ya nyumba moja yenye milango mikubwa ambayo ilikuwa ipo mbele yetu.
"huyo mtoto kachukua tabia zako mimi unanipakazia tu" Nilijitetea kimasihara na kusababisha Nurulayt anisukume begani kimasihara.
"Loh! Lione yaani mwanao nimekaa naye kwa miaka mitano tu lakini alipoanza kuongea kazi nilikuwa nayo ya kujibu maswali tu, na sasa nakutana na baba mtu habari ni hiyohiyo tu yaani kama mnanihoji vile" Nurulayr aliongea akiingia ndani nami nikamfuata, tulikuwa tumeingia kwenye mgahawa mdogo wenye watu wachache jioni hiyo. Nurulayt aliagiza chakula kama ilivyo kawaida yake halafu akaja kuketi meza moja nami, chakula kililetwa na kila mtu akawa anashughulika katika kulijaza tumbo lake. Hatukuongea hadi tulipotoka tularudi ndani ya gari, Nurulayt alienda kukaa kwenye kiti cha changu na mimi nikakaa kwenye usukani.
"tunaelekea wapi sasa, nahitaji nijue sio unaniachia usukani tu bila kusema cjochote" Nilimwambia Nurulayt.
"hapa tupo Nata kwenye njia tatu zinapokutana, fuata barabara inayoenda kusini mashariki hadi katika mji unaoitwa Francistown" Nurulayt aliniambia huku akikinyoosha kiti cha gari miayo ikimtoka mdomoni mwake, niliwasha  gari nikaingiza barabarani na safari ikaendelea kuutafuta mji wa Francis town nikiwa nimewasha taa za gari kwani nuru ya anga ilishaanza kupotea. Baada ya dakika thelathini tangu niingize gari barabarani Nurulayt alikuwa tayari yupo kwenye usingizi mzito sana na kama isingekuwa mkanda wa gari angekuwa kajigeuza ovyo hadi kufikia kuiparamia gia ya gari, siku hii niliendesha gari kwa mwendo wa kasi nikiomba tufike salama kwani sikuwa mwenyeji wa barabara ninayoitumia na alama za barabarani ndiyo kitu pekee kilichonisaidia kuniongoza katika barabara hiyo. Hadi inatimu saa nne ya usiku tayari nilikuwa nimeshafika katika mji wa Francistown uliopo kilomita 185 kutoka Nata nilipotoka, nilipofika hapo ndipo nikamshtua Nurulayt usingizini na nilimtaarifu tumefika tayari.
"ingia hiyo barabara inayoelekea kushoto na uende hadi utapokuta sheli yenye  supermarket" Nurulayt aliniambia maneno hayo alipomaliza alirudi tena kulala.
Niliingiza gari barabarani kwa mara nyingine nikawa naelekea barabara inayoenda kushoto kati ya barabara tatu zilizopo mbele yangu, barabara hizi kwa Tanzania ningezifananisha na makutano ya barabara ya Segera yanayokutanisha barabara tatu zinazoelekea Tanga mjini, Kilimanjaro na Mkoa wa pwani. Eneo la Nata  na hili la Francistown lilifanana kila kitu muundo wa makutano ya barabara zilivyo, niliamua kuwa makini na alama za barabarani kwani hizo ndizo zilikuwa msaada kwangu katika kuniongoza na barabara ya huku ili niweze kufika salama bila hata kupata ajali yoyote. Nilitumia kiasi cha dakika 45 nikawa nimefika katika sheli aliyonielekeza Nurulayt, hapo nilimuamsha tena na nikamtaatifu kuwa nimeshafika. Nurulayt aliamka kisha akatazama mazingira ya hapo kwenye sheli halafu akashuka akaniambia," sogeza gari sehemu ya kuwekea mafuta". Nilisogeza kama alivyoniambia kisha akaongea na na mhudumu wa hapo sheli, alipomaliza alichukua mpira wa kujazia mafuta akatia mafuta hadi mshale wa mafuta katika kioo cha plastiki kilichopo chini ya usukani kikaonesha tenki la gari limejaa. Alifanya malipo kisha akarejea ndani ya gari alipokuwa awali, alipokaa kwenye kiti nilimuangalia usoni nilitarajia aseme lipi juu ya hii safari.
"Mbona unaniangalia hivyo?" Nurulayt aliniuliza.
"nahitaji kujua nini kinachofuata Nuru" Nilimwambia huku nikiwa sijatoa jicho langu usoni mwake.
"ok ok ni hivi, nusu kilomita kutoka hapa kuna mpaka wa Ramekgwebana unaotenganisha Botswana na Zimbabwe. Hivyo inabidi uruke kiti cha nyuma kuna askari wa uhamiaji atakuja kutuvusha hapa kama tulivyovuka kule Trans kalahari border" Nurulayt alinipa maelezo ya mpango unaofuatia. Baada ya dakika kadhaa tangu anipe maelezo hayo  nilimuona askari wa  mmoja aliyebeba mkoba mkubwa mgongoni akija hadi kwenye gari letu usawa wa mlango wa dereva, alipofika niliamua kuruka  kiti nyuma kwani nilijua fika ndiye mtu tunayemsubiri. Yule askari alifungua mlango wa gari akaingia huku akiwa anahema  sana akiwa na mkoba wake  ambao aliupakata mapajani alipokaa kwenye kiti cha gari.
"mambo si mazuri huko" Askari aliongea huku akitutazama kila mmoja.
"vipi huko kuna nini?" Nurulayt aliuliza
"muda mfupi uliopita hapo mpakani walipita watu  wakiwa na  gari yenye mizigo mingi ambayo haikujulikana ni vitu gani, walipekuliwa wakakutwa na na unga na walipotaka kukamatwa wakaanzisha vita ndogo. Wamefanikiwa kukimbia  na gari lao la mizigo kuingia mpaka Zimbabwe kinguvu lakini waliishia msituni wa jirani na mpaka, na hivi ninavyokuambia wanafanya majibizano ya risasi na askari na mpaka mzima umemwagwa askari"  Yule askari alieleza sababu ya mambo kutokuwa mazuri huko mpakani.
"sasa itakuwaje?" Nurulayt aliuliza akionekana kuchanganyikiwa sana na maelezo hayo.
"njia pekee ya kuvuka pale mpakani ni kuvaa sare za kama hizi zangu na viatu" Aliongea yule askari huku akifungua mkoba mkubwa alioingia nao akatupatia sare za askari wa uhamiaji pamoja na viatu vya  kijeshi.
"mkivaa nguo za askari wa uhamiaji mtajulikana ni askari waliongezwa na makao makuu kwenda kupambana na hawa wasafirishaji madawa ya kulevya na mtaruhusiwa kupita. Badilisheni hapahapa" Yule askari alituambia.
"ok hamna shida ila wewe inabidi ushuke tubadilishe nguo kwani mimi ni mwanamke na huyu ni mzazi mwenzangu, hupaswi kuniona nikibadili nguo labda yeye kwakuwa hakuna asichokijua katika mwili wangu" Nurulayt alimuambia yule askari
"mh! OK hamna shida" Yule askari alinitazama kwa jicho la pembeni halafu akatabasamu akaonesha kukubaliana na maneno ya Nurulayt, alishuka  ndani ya gari kwa  haraka  na sisi tukabadilisha kwa haraka halafu tukamuita tulipomaliza kuvaa.
"Hapo safi kabisa yaani mpo kama askari wa uhamiaji, chukueni na hizi  bunduki mzishikilie ili wakituona wajue mnaingia kazini" Yule aliongea baada ya kutuona tukiwa tumevaa magwanda ya askari wa uhamiaji, alifungua ule mkoba tena akatoa bunduki mbili aina ya short gun akatupatia pamoja na mikanda ya risasi. Safari ya kuelekea kwenye mpaka wa Ramekgwebana iluanza na askari yule ndiye aliyekuwa dereva, gari letu lilipoingia barabarani alitoa king'ora cha kubandika akampatia Nurulayt ambaye alikiweka juu ya paa la gari. Mpakani tulifanikiwa kupita bila matatizo na kweli kulikuwa kuna maaskari wengi wakiwa na wana silaha kama hizi tulizokabidhiwa, safari yetu iliendelea na tukawa tumeingia kwenye pori lililopo mwanzaoni mwa nchi ya Zimbabwe. Furaha ilidhihirika machoni mwetu kwa kufanikiwa kukivuka kikwazo kile lakini furaha hii haikudumu kwani dosari kubwa iliingilia furaha hii, tukiwa tupo katikati ya pori usiku majira ya saa sita milio ya risasi ilianza kusikika na vioo vya  gari letu vikaanza  kupasuka.Yule askari ambaye ndiye aliyekuwa dereva wetu alitoa ukelele wa maumivu akiachia usukani wa  gari
 na gari likaingia pembeni ya barabara nusura ligonge mti baada ya  yeye kuwahi kukanyaga breki ya gari.


*Mmmh kunani tena?

*je watafanikiwa kupita salama?


ITAENDELEA!!

DHAHAMA SEHEMU YA KUMI NA TATU




TEMBELEA: www.facebook.com/riwayamaridhawa 



 DHAHAMA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE



SEHEMU YA KUMI NA TATU!!
"Faridaaa!" Shafii aliita jina la mke wake  kwa nguvu huku akijaribu kuinuka kitandani
"Shafii hebu tulia kwanza utasababisha  matatizo mengine tu" Mzee Buruhan alimuambia huku akimzuia asifanye fujo.
"Mama Zayina, Zayina mpo wapi?" Shafii alipiga kelele zaidi na ikabidi daktari aitwe mara moja ili kumtuliza, Mzee Buruhan na Mzee Mahmuf walimshikilia  Shafii hadi daktari alipokuja akamchoma sindano ya usingizi ndiyo ikawa ahueni.
Baada ya Shafii kulala mzee Buruhan na mzee Mahmud  walitoka pamoja na mke wa Hamis wakaenda kuka kwenye madawati ya kusubiria wagonjwa, baada ya muda mke wa Hamis aliondoka kwenda kufuata chakula kwa ajili ya mgonjwa akawaacha wazee hao peke yako.
"Kama nilivyokuambia mzee mwenzangu kuhusu huyu mwanao, awe mkweli ujue tatizo alilonalo ndiyo nitakubali kumsaidia" Mzee Mahmud aliongea.


****


"Mzee mwenzangu tatizo kila kukicha una misemo ambayo imejaa vitendawili vitupu hebu niweke wazi walau kidogo nipate fununu ya jambo linalomsumbua mwanangu" Mzee Buruhan alimlalamikia rafiki yake kutokana na kauli zake zilizo jaa mafumbo.
"mzee mwenzangu hiyo kinyume na utaratibu wa taaluma yangu siwezi kusema hata kama nalitambua tatizo hili, huwa sina tabia ya kukuficha kitu ila kwa hili wacha nikuambie ukweli tu nitakuwa nimekiuka masharti ya utalaamu wangu wa uganga ikiwa nitalisema suala hili pasipo muhusika mwenyewe kufungua kinywa chake na kuliongelea. Utanisamehe kwa hilo" Mzee Mahmud aliongea huku akimshika bega mzee Buruhan ambaye alionekana kuwa njia panda kutokana na matatizo yaliyomkumba mwanae
"mzee mwenzangu hakuna hata njia nyingine ya kunisaidia niweze pata fununu kidogo ya hili suala?" Mzee Buruhan aliuliza huku akiwa ameinamisha uso wake chini akionekana amekata tamaa kabisa ya suala hilo.
"Siku zote mwanamke atakaye mtoto lazima akubali kuvua nguo ya ndani ili alichokificha kionekane na hawezi kupata mtoto ikiwa atakataa kuivua hiyo nguo. Ndiyo hivyo hivyo mwanao akubali alilolificha moyoni mwake lifumbuke la si hivyo hataweza kupata msaada katika hilo, cha kukusaidia akiamka muambie umebaki peke yako ukitaka usipoteze vyote awe muwazi kwangu na kwako. Naenda msalani mara moja mzee mwenzangu" Mzee Mahmud aliongea kisha akajiinua kivivu  kwenye dawati la kusubiri wagonjwa akawa anaelekea chooni, mzee Buruhan alimtazama tu akiwa anatamani sana ajue jambo lililopo ndani ya kichwa chake lakini hakuwa na uwezo wa kufanya hivyo. Mzee Mahmud  aliipopotea katika upeo wa macho yake aliinua kichwa juu akiweka ishara ya kuomba dua halafu akatikisa kichwa kuonesha anasikitishwa, hakuwa na jambo jingine alilomuomba Mungu zaidi ya kumshtakia tu  juu ya balaa lililomkuta mwanae na kumfanya awe na matatizo tu katika mwaka huo ambapo miaka mingine yote aliishi kwa amani na furaha pamoja na familia yake lakini sasa furaha hiyo imetoweka  katika maisha yake. Laiti angelijua kwamba alikuwa anashtaki mtuhumiwa kuwa ameonewa wala asingelifanya hivyo lakini kwakuwa hakujaliwa uwezo wa kulibaini kwani alikuwa ni mwanadamu wa kawaida tu, hakutambua kama jereha la mwanae ni  la kujitakia hivyo halihitaji pole hata kidogo.
   
Mzee Mahmud alipofika kwenye mlango wa msalani baada ya kuondoka pale kwenye dawati alihisi hali isiyokuwa ya kawaida katika mwili wake lakini aliipuzia na kuingia humo msalani, alipoingia ndani alipitiliza sehemu za kujisaidia haja ndogo akawa anaelekea sehemu maalum ya yenye vyoo ndani ambayo hutumiwa na wale wanaohitaji kumaliza haja zao kwa siri tu. Alipofika hilo eneo  alifuata mlango wa moja wa vyoo akashika kitasa ili aufungue lakini alisita baada ya  kusikia upepo mzito ukivuma kwa ghafla ambao ulitaka hata kuupeperusha msuli aliojifunga kiunoni lakini aliuzuia, upepo huo ulipotulia Mzee Mahmud alionekana kukerwa nao kwa kitendo cha kutaka kumuadhiri ambapo aligeuka nyuma akionekana kuwa na hasira za waziwazi juui ya tukio hilo.
"Adabu gani hizo ewe mwanajini wataka kuniadhiri kwa hizo nguvu zako ulizojaliwa?" Mzee Buruhan alilalamika baada ya kumuona yule aliyetaka kumuadhiri kwa kutaka kuupeperusha msuli aliojifunga kiunoni alikuwa yupo mbele yake baada ya kugeuka nyuma, alikutana uso kwa uso na Zalabain akiwa amefumbata mikono kifuani mwake.
"Samahani mzee wangu kwa hilo" Zalabain aliomba radhi.
"sema una shida gani" Mzee Buruhan aliongea huku akiuweka msuli aliojifunga kiunoni vizuri.
"nimekuja kukuambia tu mimi ndiye ninayemtesa Shafii na huwezi kuharibu kazi yangu kwa kujaribu kumsaidia" Zalabain aliongea kwa msisitizo.
"Ndiyo nimeshakutambua tangu unajitokeza pia sipo kwa ajili ya kumsaidia dhalim kama yule bali nipo kwa ajili ya kumsaidia Buruhan ili asiondokewe na nguzo zake zote, kiufupi ni hivi nazuia usimuue yule mziwanda wake asiye na hatia" Mzee Mahmud alimuambia huku akijiamini halafu akameza mate kidogo kisha akaendelea, "Shafii ni haki yake kwa alichokifanya ila Ally hana hatia yoyote na usimuingize katika orodha hiyo, pia ningependa mumponyeshe sikio lske na taya lake ambayo mumjeruhi kutokana na kujaribu kuleta kile kitakachoyafanya majini ya marehemu Hamis yafanye kazi. Ukumbuke pia  yeye anachukia ulilofanyiwa ila mali yako anayoimiliki Shafii ndiyo inamfanya ashindwe kufanya jambo lolote, usihukumu yule asiye na hatia kama ni ufalme utapewa pasipo yeye kupoteza uhai wake".
"unasema nini wewe?" Zalabain alimuuliza Mzee Mahmud
"kama ulivyosikia ewe mwana wa jini, ukumbuke mimi nilikataa kutengeneza uchawi kama uliomtapisha mama yako jana kwasababu najua siyo haki kufanya hivyo, pia niligoma kufanya dawa ya kumuua baba yako ili mama yako awe chini ya mwingine kwasababu najua haikuwa haki. Pia utambue nakuambia usimuue Ally kwasababu najua utakuwa hutendi haki ewe mwanajini kamuuulize ibin Zultash atakueleza, mwisho kabisa nakuambia hivi upotee sasa hivi kuna mtu anaingia humu msalani sasa hivi asije akaniona naongea peke yangu kama kichaa wakati nina akili  zangu timamu" Mzee Buruhan aliongea kisha akageuka nyuma akaingia chooni bila kujali kama Zalabain ameondoka au yupo, baada ya kumaliza haja zake  alitoka hakumkuta Zalabain na akarudi kule alipokuwa yupo awali. Alimkuta mzee Buruhan yupo na Ally wakiongea na iilonekana Ally alikuwa kapona kabisa tatizo la kuvunjika taya na sikio kwani hakuwa mwenye kuweza kuzungumza wala kusikia, lakini hapo alikuwa akizungumza na kusikia vizuri kabisa.
Mzee Mahmud alimuonesha ishara ya kumsalimia Ally kama ilivyokuwa akifanyiwa kwa kutoweza kusikia vizuri lakini.
"Mzee mwenzangu anaongea huyu na kusikia sasa hivi usimsabahi kama vile unamsabahi bubu" Mzee Buruhan alimuambia rafiki yake.
"Yapaswa  tumshukuru Mungu basi mzee wangu maana huu muujiza tosha" Mzee Mahmud aliongea akionekana kufurahishwa na suala hilo.
"Alhamdililah" Ally na baba yake waliitikia kwa pamoja.
Mzee Mahmud alibaki kutabasamu tu kila alipomuangalia Ally kwa kufurahishwa na usikivu alionao Zalabain baada ya kufanya kile alichomuambia, tabasamu lake lilifanya Mzee Buruhan na Ally nao watabasamu  wakijua kafurahishwa na hali ya Ally kutengemaa.
"Ally hebu sogea karibu" Mzee Mahmud alimuambia Ally  huku akimtazama kwa umakini, Ally alimsogelea Mzee Mahmud pasipo kujua ni kipi alichokuwa anataka kufanyiwa kwani alimzoea sana mzee Mahmud na alimchukulia kama baba yake tu. Alipomsogelea Mzee Mahmud aliambiwa achuchumae mbele yake naye akatii amri kama alivyoambiwa, mzee Mahmud alimshika kichwani na akamtamka maneno yasiyoeleweka na kusababisha Ally ashtuke halafu aangalie mazingira ya hapo yalivyo halafu akaenda kukaa kwenye dawati pembeni ya baba yake alipokaa awali.
"Baba hivi hapa tupo kwa ajili gani?" Ally aliuliza tu baada ya kukaa pembeni ya baba yake akionekana kutotambua yupo hapo kwa ajili gani.
"Kha! We Ally maswali gani hayo hutambui kama tupo hapa kumuangalia kaka yako kalazwa tangu jana" Mzee Buruhan alimuambia Ally akionekana kutoelewa kitu alichofanyiwa na  mzee Mahmud hadi akasahau  yupo pale kwa lengo gani wakati alipoingia tu aliulizia hali ya kaka yake.
"Khaa! Kumbe tupo hapa kwa ajili ya kumuangalia firauni huyo, sina muda huo muache afe  maana huyo ni zaidi ya shetani" Ally aliongea maneno ambayo yalizidi kumshangaza sana Mzee Buruhan na akajikuta  akimtazama  mzee Mahmud akionekana kutoelewa kafanya nini, Ally alinyanyuka ili aondoke lakini mzee Mahmud alimuita akamuomba aketi akakaa chini.
"Ally tambua undugu ni kovu na halifutiki usifanye hivyo, najua unaumia kwa kile alichokifanya kaka yako lakini kumbuka ndugu ni ndugu tu" Mzee Mahmud aliongea kwa ustarabu wa hali ya juu akitegemea ataeleweka na Ally lakini haikuwa hivyo.
"Baba zangu mngejua alichokifanya huyo firauni mnayekuja kumuangalua wala msingethubutu kukaa hapa, na sijui hata ni kwasababu gani nilikuwa nikimpenda kwa kipindi chote hicho nahisi aliniroga yule maana miale ya mkufu wake sielewi hata imemifanyaje wakati nilikuwa nikimchukia" Ally aliongea  huku akionesha kumchukia  kaka yake.
"Ally unaongea nini wewe?" Mzee Buruhan aliuliza akionekana kushangaza na maneno anayoyaongea mwanae.
"Mzee mwenzangu kama nilivyokuambia hili tatizo linajulikana ila huyu hatakiwi kulisema na akilisema atakuwa kiziwi kama mwanzo muache huyo Shafii aeleze kila kitu. Unajua..." Mzee Mahmud aliongea maneno yaliyomfanya Mzee Mahmud atulie kimya na alishindwa kumalizia kauli yake baada ya mke wa Hamis kurudi akiwa amebeba chombo cha chakula kwenye mfuko wake.
"Vipi mgonjwa jamani tayari ameshaamka?" Mke wa Hamis aliongea baada tu ya kuwasili na alimuonesha Ally tabasamu kisha akampa mkono akampa mkono ili amsalimie akijua kuwa Ally hawezi kuongea.
Ally hakuupokea mkono wa Mke wa Hamis zaidi ya kusonya kwa nguvu kisha akanyanyuka akasema, "shetani jike mkubwa wewe".
Ally alinyanyuka kwenye dawati la kusubiri wagonjwa akaelekea mahali akimuacha wazee wake na mke wa Hamis wakimshangaa sana, mke wa Hamis alipotaka kumfuata nje Mzee Buruhan alimshika akamzuia.
"Salma mama naomba unisikilize kwa umakini, achana na Ally kwa sasa kaa hapo usubiri muda wa kumuona mgoniwa akizinduka tukamuone" Mzew Buruhan alimuambia Salma mke wa Hamis.
"Lakini Ally kapatwa na nini wazee wangu kwani alikuwa hawezi kuongea na kusikia ila sasa hivi anaongea na kusikia  ila amekuwa kama akili haziko sawa hadi ananisonya mimi" Salma aliongea huku akishangazwa na hali ya Ally yule aliyekuwa anamsikiliza na kumtii na kumuheshimu ameamua kuonesha dharau.
"Hebu mama kuwa muelewa achana na habari za Ally sasa hivi, tufikirie kuhusu mgonjwa tu" Mzee Mahmud aliongea kwa msisitizo huku  akionekana kutopendezwa na maneno ya Salma.
"Sawa baba zangu nimewaelewa" Salma alijibu kwa shingo upande ili tu asiwaudhi  wazee ambao anawaheshimu.


****

 Wakati Ally akifunguliwa na kuanza kumuoneshea dharau upande wa himaya ya Majichungu Zalabain ndiyo alikuwa amerejea muda huo na aliamua kupitia chumbani walipo mama yake na dada yake ili awaone kutokana na upendo alionao kwao, alibisha hodi kwa adabu ingawa alitambua hata akiingia muda huo asingewakuta wakiwa bila stara. Alipokaribishwa aliingia kwa adabu  na akaenda hadi walipokuwa wamekaa kitandani na akawasalimia, halafu naye  akaketi kitandani jirani yao.
"Mwanangu kila nikikutazama namuona baba yako kwa jinsi wote mlivyokuwa na sura zilizofanana, haya niambie unatoka wapi?" Bi Farida aliongea kisha akamuuliza Zalabain.
"Nilikuwa Tanga kwenye  hospitali ya SBN nilienda kuongea na mzee Mahmud" Zalabain alimuambia mama yake.
"Mh! Huyo mzee huko hospitalini anafanya nini?" Bi Farida aliuliza.
"Amekuja kumuangalia mumeo amelazwa" Zalabain alimuambia mama yake.
"Jamadin sina mume kama huyo mimi tena sitaki kumsikia ukimtaja, mume aliyetakiwa kunioa mimi ni Faimu tu na sijui ilitokea nini mpaka nikamkana na nikamsababishia matatizo makubwa sana akahama kijijini akiwaacha jamaa zake. Nampenda Faimu na natamani nimuone hata leo ili nimuombe msamaha maana yeye ndiyo kila kitu kwangu" Bibi Farida aliongea na  mwishowe akalia kutokana na kujutia aliyoyafanya ya hapa zamani, Zalabain ilimbidi amkumbatie mama yake ambembeleze kutokana na upendo alionao kwake.
"Samahani mama kwa kukupa taarifa smbayo hutaki kuisikia,  sipendi uhuzunike nakupenda sana" Zalabain alimuambia mama yake baada ya kunyamaza.
"Nakupenda pia mwanangu" Bi Farida alisema huku akitabasamu kwa mbali, waliendelea kuongea maongezi mengine kwa furaha wakiachana na suala ambalo lilionekana kutomfurahisha kabisa Bi Farida.


****


 Baada ya masaa mawili Shafii aliamka kutoka usingizini akiwa yupo vizuri kiafya kuliko awali, hali yake iliendelea kutengemaa na ilipofika muda wa alasiri aliruhusiwa na daktari na alirudi nyumbani akiwa ameongozana ns wote waliokuja  kumuona hospitali kasoro Ally tu ambaye hakurudi tangu aondoke pale hospitali. Shafii alipelekwa moja kwa moja chumbani kwake na akaachwa apumzike na kisha wazee wake wakakaa sebuleni hadi ilipoingia jioni ndiyo mzee Buruhan na mzee Mahmud waliingia chumbani kwa Shafii wakamkuta akiwa ameamka ameegemea mito kitandani kwake,  Shafii alipoona ujio wa wazee wale alihisi kuna jambo ila alikaa kimya ili apate uhakika wa wasiwasi wake.
"Shafii" Mzee Buruhan alimuita
"Naam Baba" Shafii aliitikia
"unajua kama wewe ndiyo nguzo kuu kati ya nguzo zangu nne zilizobakia?" Mzee Buruhan alimuuliza
"nafahamu hilo baba" Shafii alijibu.
"Hussein hatunaye, Hamid hatunaye, Hassan ni mdogo kwako, Falzal ni mdogo kwako na Ally pia ni mdogo kwako. Wewe pekee ndiyo mkubwa ndiyo kiongozi wao ingawa wote wana maisha yao na hata wanajisomesha wakitaka kujiendeleza kielimu. Nadhani unatambua hilo" Mzee Buruhan alisema.
"Ndiyo baba natambua hilo" Shafii alijibu.
"Sasa basi inapotokea tatizo lenye kuhitaji kuelezewa ili lisizidi zaidi inabidi lielezewe mwanangu ikiwa utakaa kimya haitasaidia chochote" Mzee Buruhan aliongea.
"Baba sijakuelewa unachomaanisha" Shafii aliongea.
"Shafii najua unatambua suala la upotevu wa mke wako na hata mwanao linalokufanya uwe na matatizo kila kukicha, sasa mwanangu ukilificha itakusaidia nini ikiwa unalifahamu chanzo chake. Kumbuka mficha maradhi kifo humuumbua mwanangu, mwanangu ni bora uitoe aibu mbele ya daktari ili utibiwe kuliko kuficha tatizo halafu ufe na ugonjwa. Ongea chanzo cha  haya ni nini?" Mzee Buruhan alimsihi mwanae.
"Baba kusema ukweli sijui wala sitambui suala hili linasababishwa na nini?" Shafii alikataa.
"Shafii vuta kumbukumbu zako vizuri umefanya nini mpaka yote haya yatokee au hutaki  familia yako uione tena ikiwa na upendo" Mzee Buruhan alizidi kumsihi.
"Baba napenda sana familia niione tena ikiwa ina upendo lakini sikukumbuki chochote kilichosababisha haya ninayofanyiwa"  Shafii alikana kabisa juu ya suala hilo.
"Jirani na mashine ya kusaga unga kule Mpirani miaka ishirini na moja iliyopita unakumbuka kilitokea nini pale kwenye  nyumba yako uliyokuwa unaishi  baada ya wewe kuhama tena ilikuwa majira ya saa sita usiku?" Mzee Mahmud aliongea kwa mara ya kwanza na kumfanya Shafii ashtuke kwa jambo alilotajiwa, lilikuwa ni jambo ambalo alishalisahau kabisa katika ubongo wake na sasa alikumbushwa na mzee huyu ambaye ni mganga mtaalam.
"Shafiii unakumbuka nini hiyo siku" Mzee Buruhan naye aliunganisha maelezo ya rafiki yake ingawa hakuyaelewa kabisa, maneno ya mzee  Mahmud  yalimfanya anyamaze ghafla huku akiwa ameinamisha kichwa chake chini.
"Shafii si nakuuliza" Mzes Buruhan aliongea huku akimtikisa bega baada ya kuona yupo kimya, Shafii alikurupuka baada ya  kutikiswa bega kama alikuwa yupo  katika usingizi mzito.
"Ha..hapana  si....sikumbuki chochote" Shafii aliongea kwa kubabaika baada ya kuhisi moja ya jambo baya alilolifanya linakaribia kugundulika.
"Una uhakika?" Mzee Mahmud aliuliza.
"ndiyo baba zangu nina uhakika wa kile ninachokiongea" Shafii alijikaza akajibu kwa kujiamini.
"mzee mwenzangu sisi twende tukanywe kahawa si unaona muda huu na kiubaridi cha kipupwe kimeanza, Shafii kama hujui juu  ya hilo basi inakupasa utambue kuwa maisha ya mkeo  na binti yako yapo kwenye kinywa chako kueleza unachojua na ukikaa kimya jua kinachofuata ni kama kilichowapata wadogo zako ia utambue umebaki peke yako" Mzee  Mahmud huku akiwa tayari amesimama na Mzee Buruhan naye akasimama, wote kwa pamoja walianza kutembea kuelekea ulipo  mlango ili waondoke lakini sauti ya Shafii ikiwaita iliwafanya wasimame na kugeuka wakamtazama.
"Nipo tayari kuwaambia kilichotokea wazee wangu naomba mnisaidie" Shafii aliongea baada ya kuona maji yamemfika shingoni na maneno ya mzee Mahmud ndiyo kabisa yalimfanya akubali. Mzee Mahmud alimtazama Shafii kwa tabasamu hafifu halafu akamuambia, "kesho muda kama huu pale ulipokuwa unaishi kule mpirani ndiyo kutakupa ahueni ya  tatizo lakokwa familia yako"
Mzee Mahmud aliposema maneno hayo alitoka humo ndani bila hata kumuangalia Shafii kwa mara nyingine, Mzee Buruhan naye alifuata akiwa nyuma yake.


****


Maneno ya Ally baada tu ya kupewa mkono na Salma yalimfanya Salma karibia siku nzima akiwa anajifikiria kwani Ally alikuwa amepatwa na nini mpaka awe vile, ilipofika jioni aliamua kutoka na kwenda kumtafuta Ally bila ya kumueleza mtu ili aongee naye tu kwani Ally alikuwa ni mmoja kati ya wanaume aliokuwa anawapenda na kipindi cha nyuma alipokuwa msichana alishajaribu kujivika ujasiri na kumueleza Ally yaliyo moyoni mwake lakini aliishia kukataliwa baada ya Ally kuwa anamuheshimu sana Hamis ambaye alikuwa na mahusiano na Salma kabla hajamuoa. Baada ya mpango ambao ndiyo chanzo cha balaa lote lililowakumba watoto wa  mzee Buruhan, Ally alifungwa akili na akawa anasikiliza wote waliofanya mpango ule bila hata kuwapinga na alifungwa akili baada ya kuujua mpango huo akawa  amekasirishwa nao. Baada ya kufungwa akili ndipo Salma alipompata Ally kutokana na yeye pia ni mmoja kati ya watu walioshiriki huo mpango, alimtumia Ally vyovyote atakavyo baada ya Ally kutopinga kauli yake. Sasa akili ya Ally ilipofunguliwa na Mzee Mahmud na Salma kujibiwa vile alijikuta roho ikimuuma akijua Ally amepatwa na tatizo hivyo  aliamua kumtafuta.  Hakukujua kama Ally wa leo siyo wa jana alichokuwa anakijali yeye ni penzi lake  haramu alilolianzisha kwa Ally hata alipokuwa yupo ndani ya ndoa.
Tamaa za kutamani kingine wakati akiwa tayari ana kingine mkononi ndiyo zilimfanya Salma afanye jambo hilo ambalo lilipelekea afiche siri nzito sana ambayo laiti ingaligundulika mapema basi angekuwa ameleta matatizo makubwa sana kwa Hamis na Ally.
Juhudi za Salma kumtafuta Ally ziliendelea kwa usiku huo akiwa yupo ndani ya gari yake na hatimaye alimkuta akiwa amekaa kwenye matairi yaliyochimbiwa katika uwanja wa mpira  uliopo mkabala na shule ya sekondari ya Usagara, Salma alimfuata hadi hapo akaegesha gari pembeni kisha akashuka akaenda kumkumbatia Ally akitegemea atapokelewa lakini alijikuta akisukumwa hadi akaanguka chini akaumia.
"Kaa mbali na mimi malaya wewe!" Ally alimuambia kwa ukali.
"Lakini Ally mpenzi wangu nimefanyaje?" Salma aliuliza kwa masikitiko makubwa huku akionekana kuumia baada ya kusukumwa.
"Unajifanya hujui siyo tena usiniite mpenzi wako kuanzia hivi sasa, we wa kunifanya mimi mtumwa wa ngono hadi umesababisha nisioe wakati natakiwa kuwa na familia sasa hivi" Ally alifoka.
"Ally nakupenda ndiyo maana nimefanya hivyo hadi nikazaa na wewe" Salma akaongea huku akilia.
"Weee tena ishia hapo hapo" Ally alimkaripia huku akimuongeza teke la mguu Salma.
"Ally nikatae ila ukae ukijua Hamida siyo mtoto wa mume wangu bali ni damu yako, ndiyo maana hata alipozaliwa kaka yako alikutania umefanana naye miguu ila ukweli ile ni damu yako kabisa" Salma aliongea huku akilia, Ally alipuuza maneno ya Salma akaondoka eneo akimuacha akilia ingawa kuna jambo lilikuwa likiisumbua akili baada ya kusikia maneno hayo.




ITAENDELEA!1

Sunday, November 29, 2015

KOSA SEHEMU YA KUMI NA MBILI

RIWAYA: KOSA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA

SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE



 ILIPOISHIA

Tuliendelea na zoezi letu kwa mara ya pili huku nikivua shati langu na Sarina akivua nguo yake ya juu, tulijikuta tukibaki na nguo za ndani pekee na joto lilikuwa kali sana. Kupunguza joto ilinidi niende nikawashe feni la hapo ukumbini, upande ulipo feni ilibidi nimpe mgongo wakati naenda kuliwasha kwani swichi y

DHAHAMA SEHEMU YA KUMI NA MBILI

RIWAYA: DHAHAMA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE


SEHEMU YA KUMI NA MBILI!!
"Asante  kiongozi wetu, mimi hapa
naungana na wazo alilolitoa mkuu wa majeshi la kwenda kuharibu utengenezwaji wa hao wadudu kwani sote tunatambua kwamba Dainun mpya imeibiwa na mpaka ije kupatikana hatujui

Saturday, November 28, 2015

KOSA SEHEMU YA KUMI NA MOJA

 KOSA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA

SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE



 ILIPOISHIA
Sauti ya yule mtu iliniambia, nilikuwa nikimsikiliza kwa umakini huku nikiuendea ule mzigo hadi nikaufikia bila hata kumuangalia Sarina aliyekuwa ananitazama kwa umakini.
"fungua mzigo sasa usiutazame tu" niliambiwa na mimi nikatii nikaufungua mzigo huo ambao uliniacha nikiwa nimepigwa na bumbuwazi kwa kile nilichokiona, hata Sarina naye alipigwa na bumbuwazi kwa alichokiona ndani ya boksi hilo.

DHAHAMA SEHEMU YA KUMI NA MOJA


 DHAHAMA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE



SEHEMU YA KUMI NA MOJA!!
"haina haja ya kuhuzunika mzee mwenzangu bali inabidi uwalaumu wanao na janga hili mzee mwenzangu limeanzwa na wao na sasa mwenzao wanalimaliza" Mzee Mahmud aliongea kisha akanywa kahawa funda moja bila hata kumtilia maanani Mzee Burhan aliyeonekana kutoielewa kauli hiyo.

MFAHAMU PROFESSA GABRIEL RUHUMBIKA


PROFESSA GABRIEL RUHUMBIKA

    Nadhani kwa wale ambao hawakusoma fasihi jina hili litakuwa ni jina geni sana kwenu, ila si mgeni sana ndani ya ulimwengu huu wa fasihi ya kitanzania. Ni mmoja wa wanafasihi maarufu sana ndani ya nchi ya Tanzania na pia mmoja wa wasomi wakubwa sana katika somo la fasihi Afrika na hata duniani kwa ujumla, ameandika kazi nyingi za kifasihi katika lugha ya kiswahili na kingereza.

Friday, November 27, 2015

KOSA SEHEMU YA KUMI

RIWAYA: KOSA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA

SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE



 ILIPOISHIA


Huwaida baada ya kufunguliwa alinifuata kwa kasi huku akiniita mwanaharamu, aliponikaribia alinipiga kibao kikali  halafu akaokota chuma kizito akiwa anahema. Alikinyanyua kila chuma akawa ananielekezea usoni ili anipigae nacho, alikinyanyua kisha akakishusha kwa nguvu. Nilibaki nikifumba macho huku nikisubiri hukumu yangu kwa Huwaida kwa kitendo nilichomfanyia, nilijiona sina thamani tena ya kuendelea kuishi ikiwa yeye anaonesha dhahiri ananichukia na hataki hata kuiona sura yangu kuanzi

DHAHAMA SEHEMU YA KUMI

DHAHAMA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE





SEHEMU YA KUMI!!
Laiti kama wanadamu tungalipewa uwezo wa kuona yaliyojificha katika mioyo ya wenzetu basi Bi

Thursday, November 26, 2015

KOSA SEHEMU YA TISA

 KOSA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA

SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE



 ILIPOISHIA


Nurulayt alizidi kuniambia maelezo ambayo yaliniacha kinywa wazi, Faiz huyu ninayemjua mimi kusikia ni muuaji na jambazi mkubwa.
"Nuru kwahiyo wewe ulikuwa unaishi Afrika ya kusini?" Nlimuuliza Nurulayt ili nipate maelezo yake kiupana zaidi.
"hapana sikuwa naishi Afrika ya kusini ila nilikuwa naenda kumtembelea kaka tu mara chache na hata hiyo siku aliyouawa nilikuwa nilikuwa nimekuja kumsalimia na ndiyo siku hiyo Faiz  akapiga

DHAHAMA SEHEMU YA TISA

 DHAHAMA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE


SEHEMU YA TISA!!
Kilikuwa kimetawaliwa na jazba miongoni mwa watu waliomo humo ndani, kiongozi wa watu

Wednesday, November 25, 2015

KOSA SEHEMU YA NANE

(SASA INAPATIKANA KATIKA ORODHA YA VITABU VYA AMAZON/ NOW AVAILABLE INA THE AMAZON'S BOOK LIST)




 KOSA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA

SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE



 ILIPOISHIA


"hapo upo poa kabisa yaani kama unaenda kunipora tunda vile" Faiz aliongea huku akitia masihara.

DHAHAMA SEHEMU YA NANE

TANGAZO! TANGAZO!

Bado nawathamini wasomaji wangu popoote mlipo, kuonesha kuwathamini kwangu nimeamua kuingiza kitabu cha kielektroniki cha Dhahama katika mtandao wa kimataifa wa Amazon. Wale waliopo mbali na nchi ya Tanzania na wanakihitaji kitabu hiki waweze kukisoma wanaweza kukinunua huko kwa gharama nafuu kabisa iliyoorodheshwa hapo. Kitu cha kufanya ni kuingia amazon.com halafu search Dhahama utakipata hapo, kukisoma ni vizuri ukawa na app ya kufungua ebook kwa wale watumiaji wa smartphone utaipata ndani ya playstore.

NI HAYO TU

Tuesday, November 24, 2015

KOSA SEHEMU YA SABA




 KOSA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA

SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE

DHAHAMA SEHEMU YA SABA

DHAHAMA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGIN

Monday, November 23, 2015

KOSA SEHEMU YA SITA







     KOSA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA

SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE



 ILIPOISHIA


"sentir en casa(jisikie upo nyumbani)" Yule msichana aliniambia huku tukikaa kwenye kochi kwa kupakatana ambapo yeye alikuwa juu mimi chini.
"gracius(asante)" nilimjibu huku nikiwa nimekamata kiuno chake sawia akiwa juu ya mapaja yangu
"delante de Daniella nada imposible sentir en casa querido(mbele ya Daniella hakuna kinachoshindikana jisikia upo nyumbani mpendwa)" Daniella aliniambia kisha akawaambia walinzi wake,"salir(ondoka)".

DHAHAMA SEHEMU YA SITA




 DHAHAMA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGIN



SEHEMU YA SITA!!
Alikiweka kile chombo  mbele ya Shafii kisha akamwaga dawa zake kwenye moto uliomo kwenye chombo hicho, moshi mzito ulitanda humo ndani na mzee Sauti ya radi akawa anaimba nyimbo zisizoeleweka huku akimzunguka Shafii akicheza kama anacheza ngoma ya kikabila. Moshi huo ulipokuja kupungua Mganga akiendelea kucheza alihisi anashikwa kiuno wakati akicheza, moshi ulipoisha alihisi anashikwa makalio kwa kutomaswa. Alipogeula nyuma kumuangalia anayemshika alikutana uso kwa uso na Zalabain akiwa anatabasamu.

Sehemu Ya 4

NDIYO IKAFIKIA HAPA

Meza Ya Uchoraji - Sehemu Ya 3



NDIYO KAFIKIA HATUA HII

Meza Ya Uchoraji - Sehemu Ya 2

BADO MTAALAMU WETU ANAENDELEA NA KAZI YAKE

Meza Ya Uchoraji - Sehemu Ya 1

KUTANA NA PENCIL MASTER MWENYE KIPAJI ADIMU NCHINI TANZANIA



Mwanzo

Sunday, November 22, 2015

KOSA SEHEMU YA TANO

     


              KOSA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA

SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE

DHAHAMA SEHEMU YA TANO

 DHAHAMA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGIN

Saturday, November 21, 2015

KOSA SEHEMU YA NNE




                 
        KOSA

MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA

SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE



 ILIPOISHIA


"haya haraka sana fungeni hiyo diary nimewaambia" Ilisikika sauti  ya mwanamke kutoka mlangoni ikiwapa amri Hassan na Hussein.

DHAHAMA SEHEMU YA NNE




                             DHAHAMA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGIN



SEHEMU YA NNE!!
"Afande tumefanya juhudi za kuuzima huu moto kwa kutumia  kila njia ila imeshindikana hadi maji yanaisha hatukuweza kuuzima na ikatubidi tutumie gesi lakini bado tumeshindwa kuuzima na inasadikika Mkuu wa idara ya sheria makao makuu ya kampuni hizi yupo ndani ya nyumba ya tatu na hajatoka hadi muda huu na hata tulipofika tulikuwa tukisikia kelele za mtu akiomba msaada lakini sasa hazisikiki" Mmoja wa maaskari wa zimamoto aliongea kwa ufupi juu ya tukio hilo la kuungua kwa nyumba hizo, James aliposikia maelezo hayo alipiga kelele huku akiita, "Babaa!". Aliwapita askari wa kikosi cha zimamoto akakimbia kuelekea ulipo moto katika nyumba ya tatu ya kampuni, maaskari wote walianza kumkimbiza ili wamuwahi asiingie ndani ya moto huo kutokana na ukali wake.

DHAHAMA SEHEMU YA TATU

MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE



SEHEMU YA TATU!!
Asp John aliyanakili maelezo ya James kisha akajiandaa kuuliza swali jingine lakini king'ora cha gari la zima moto kilimkatisha na akajikuta akiangalia lilipo gari la zima moto. Wale vijana nao waliliona lile gari la zimamoto likipita pembezoni mwa eneo la tukio kwa tabu kisha likaingia barabarani kisha likaingia barabarani likawa linaelekea Duga Maforoni kwa mwendo wa kasi sana huku milio ya ving'ora vyake ikiwa imetawala njia nzima. Asp John alipoona hali hiyo alihisi kuna jambo na akawa anataka kujua kuna nini kilichotokea, alinyanyua simu ya upepo akaongea kwa muda kisha akatulia akasikiliza upande wa pili na akajikuta amegwaya.
"nyumba za kampuni yenu zilizokuwa zinazinduliwa zote zimeungua kwa moto  wa hitilafu ya umeme" Asp John aliwaambia wale vijana.
"eti nini?" James alisema kwa mshangao.

KOSA SEHEMU YA TATU


   KOSA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA

SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE



 ILIPOISHIA

"dah! Halafu kweli, kwani saa ngapi?" Hassan aliuliza.
"saa kumi kasoro hii tuwahi graundi kama vipi?" Hussein aliongea huku akiiweka shajara kwenye meza,  wote kwa pamoja walichukua vifaa vya mazoezi kisha wakaondoka kuelekea uwanjani. Vijana hawa mpira wa miguu ndiyo ilikuwa burudani yao kuu na waliupenda sana, mapenzi  yao kwenye mpira wa miguu yalijulikana hata kwa baba yao na ndiye aliyewapa moyo wa kuendelea kuonesha kipaji chao kandanda. Mpira wa miguu kwao ilikuwa kama ni mchezo uliwapa umaarufu chuoni kwao na hata mtaa wanapoishi..


Thursday, November 19, 2015

KOSA SEHEMU YA PILI








    KOSA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA

SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE



 ILIPOISHIA
 Walijumuika naye mezani hapo huku wakimtazama sana usoni.
"hivi baba yale ni matukio ya kweli?!" Hussein aliuliza.
"kwa sasa siwezi kuwajibu  mpaka mmalize  kusoma yote" Baba yao aliwajibu.
"ni kisa chenye kuvutia sana" Hassan aliongea akiwa na tabasamu usoni hata kile kilio chake kilichokuwa kinamsumbua sana alikisahau kutokana na kuvutiwa na ukurasa  wa kwanza wa maelezo yaliyomo ndani ya Shajara ya baba yake.
"malizeni kula kwanza ndiyo mengine yatafuata, kama kuongea basi ongeeni mkimaliza kula" Baba yao aliwaambia.

DHAHAMA SEHEMU YA PILI









DHAHAMA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE



 SEHEMU YA PILI!!
"we mwanaharamu wewe simamisha gari nishuke sio kuongeza mwendo" Yule mwanamke alizidi kufoka baada ya kuona mwendo wa gari unazidi kuwa mkali, dereva hakumjibu yule yeye alitoka kwenye usukani akasimama kisha akawaangalia wafanyakazi wa idara nzima akiwa na hofu.
"si mimi ninayeendesha jamani gari linaenda lenyewe hili hebu oneni" Dereva aliongea huku akiwaonesha wafanyakazi wote jinsi usukani ulivyokuwa unajiongoza wenyewe, wafanyakazi wote walipoona hicho kioja walijikuta wakijaribu kutoka nje lakini walishindwa kwani milango haikufunguka na vioo vyote vilijifunga ghafla hata vile vilivyokuwa wazi vyote vilijifunga. Wafanyakazi wote walijaribu kupiga vioo ili wavunje lakini walishindwa kwani vioo vilikuwa vigumu sana, gari nayo ilizidi kuongezeka mwendo hadi ikawa kama ipo kwenye mashindano.