Saturday, January 3, 2015

JINAMIZI

IWAYA :JINAMIZI
MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA
SIMU:+255713776843
+255762219759


WHATSAPP:+255713 776843
ANGALIZO: HII NI RIWAYA YA KUBUNI
ISIYOHUSIANA NA MTU WALA KIKUNDI FULANI,PIA
WAHUSIKA NI WA KUBUNI WASIOHUSIANA NA MTU
YOYOTE.


ANZA SASA.
SEHEMU YA KWANZA
Hekaheka za uchaguzi zilikuwa zimepamba moto
nchini Tanzania,kampeni zenye majigambo zikiwa
zimeshika nafasi yake ndani ya ardhi hii yenye
amani. Vyama tofauti vilikuwa vikihaha huku na
kule ndani ya nchi hii ili viweze kujizolea kura kwa
wananchi, wagombea urais,ubunge na udiwani a

vyama hivyo walijinadi wawezavyo ili kuwashawishi
wananchi wawapigie kura. Hakika zilikuwa ni
kampeni za aina yake zilizoleta upinzani katika
vyama viwili tofauti, kimoja kikiwa ni chama tawala
na kingine kikiwa ni kikuu cha upinzani
nchiniTanzania. Upinzani huu ulipelekea hadi wawe
wanachafuana kupitia vyombo vya habari, huku
wanachama wake wakiwa katika makundi yenye
uhasama mkubwa. Hakika hii ilikuwa ni kipato
tosha kwa wanahabari wenye tamaa ndani ya nchi
hii, wanahabari hawa walidiriki kuandika habari za
uongo zilizoleta uhasama baina ya vyama hivi.
Kampeni ziliendelea kuendeshwa sehemu
mbalimbali za nchi hii huku serikali ikitoa fungu
kwa kila chama ili kiweze kujimudu vyema, kampeni
za vyama vyote zilikuwa za kawaida ila chama
tawala na chama kikuu cha upinzani kampeni
zao zilikuwa zimeimarika zaidi ya vyama vyote.
Chama tawala kilitumia pesa za wanachama wake
matajiri waliojitolea kukifadhili chama kipindi cha
kampeni ,huku wapinzani wao wakuu wakiwa
hawajulikani ni wapi walipopata fedha za nyongeza
za kuweza kufanya kampeni zenye gharama kuliko
uwezo wa chama chao. Utata wa chama hiki
uliwavuta sana waandishi wa kikundi cha
kujitegemea kutoka nchi za Afrika ya mashariki
kuingia kazini, walianza kulifuatilia suala hili kwa
undani sana ili wapate ukweli juu ya chama hiki.
Chama hiki cha wanandishi kinachojulikana kama
WAHANGA kiliundwa na waandishi watano wenye
roho zisizo na hofu na jeuri ya kupuuzia
vitisho , kiliundwa na watu watano kutokana nchi
tano za Afrika ya mashariki amboa ni Norbert Kaila
wa Tanzania,Davis Elius wa Kenya,Joseph Kiiza wa
Uganda,Hilda Alphonce wa Rwanda na Allison Frank
kutoka Burundi. Hawa ndio waliojulikana kama
vichwa ngumu na baadhi ya vigogo, walikuwa
wakitoa jarida lao lenye kuumbua mambo mengi
maovu ndani ya Afrika ya mashariki. Hadi muda
huo wa kampeni walikuwa tayari wameshaingia
nchini Tanzania kwa siri,bwalifanya uchunguzi wa
chini kwa chini huku kampeni zikiwa zinanaendelea.
Uchunguzi wao ukiwa unaendelea
ndio uhasama baina ya vyama hivi ukizidi kushika
hatamu nchini, mauaji ya mgombea ubunge wa
chama kikuu cha upinzani katika jimbo la Kahama
yanatokea katika kampeni za chama hicho wilayani
Kahama mkoani Shinyanga. Mgombea huyu
aliyeitwa Gerald Geofrey alipigwa risasi ya kichwa
akiwa jukwaani akijinadi kwa
wananchi , hali ya sitomfahamu ilitokea baina ya
chama
cha upinzani maarufu kama PTP(people of Tanzania
party) na chama tawala RPP (revolutionist political
party) . PTP walikuwa wakiishutumu RPP ndio
waliohusika na mauaji ya mgombea katika vyombo
vya habari, hali hii ilipelekea RPP watumie muda
wao mwingi kujitetea katika kampeni huku wenzao
wakijinadi kwa
wananchi. Hadi uchaguzi unakaribia tayari RPP
walikuwa wameshapoteza idadi kubwa ya wafuasi
na PTP walikuwa wameshajipatia wafuasi wengi
tofauti na ilivyokuwa awali, RPP walijikuta
wakipigwa kwenye kampeni zao karibu kila mahali.
Hatimaye uchaguzi ukawadia ukawadia na ikawa ni
siku ya mapumziko siku hiyo ya uchaguzi ili
kuwapa fursa wananchi wapige,uchaguzi ulifanyika
katika hali ya utulivu na amani nchi nzima.
*******
Waandishi wa WAHANGA nao walikuwa tayari
wameshafanya uchunguzi na sasa wapo katika
hata za mwisho kabla hawajalilipeleka
jarida lao mtamboni ili liweze kuchapishwa na
hatimaye liingie mitaani, walipolimaliza tayari
uchaguzi ulikwisha fanyika na ilikuwa yanasubiriwa
matokeo ya uchaguzi kwa hamu kubwa ili mshindi
ajulikane. Binti pekee wa WAHANGA Hilda Alphonce
ndiye aliyechukua jukumu la kupeleka nakala za
jarida lao ili liweze kuchapishwa,alipeleka kiwanda
cha EAPL(east africa publishers limited) tawi la Dar
es salaam. Kutoka ofisini kwao hadi zilipo ofisi za
kampuni ya EAPL hakukuwa mbali kwa mwendo wa
miguu ingawa Hilda aliamua kutumia gari la umoja
wao ili
awahu kurudi aweze kuendelea na kazi kama
kawaida,alifanikiwa kufika zilipo ofisi hizo mtaa wa
Libya jirani na kituo cha mafuta kisha akaenda kwa
mtu wao maalum anayewachapishia majarida yao
wakiwa jijini Dar es salaam. Hakuwa na muda wa
kukaa tena maeneo hayo baada ya kukabidhi vitu
muhimu kwa ajili ya uchapishaji, aliondoka ofisini
hapo. Wakati akiwa anatoka nje ya jengo hilo
alipishana na
kijana mwenye suti nyeusi nadhifu akiingia ofisini
humo.
Hakutaka kumtilia shaka yoyote kwa muonekano
alionao, alimuona kama mteja wa kawaida kama
alivyo yeye ktika kampuni hiyo.
******
Kijana aliyepishana na Hilda aliingia moja kwa moja
hadi katika ofisi inayohusika na kupokea nakala za
waandishi , alimkuta mhusika wa upokeaji wa nakala
hizo akiwa ameegemea kiti huku miguu ikiwa
mezani. Aliongea pasipo kuketi katika cha wateja
kilicho jiranj yake, " we Daud huyu malaya kaleta
nini" Daud alijibu bila ya kumtilia maananu
anayezungumza naye, "ni nakala za jarida lao
ambalo linahitajika kuchapishwa". Yule kijana
aliingiza mkono katika mfuko wa koti la suti
yake,alipoutoa ulikuwa na burungutu la pesa
ambalo aliliweka juu ya meza kisha akasema, "hizi
pesa ni zako zote ikiwa utanipatia hizo nakala kabla
hazijafika mitamboni". Daud alikaa sawa kisha
akamtazama yule kijana kwa umakini, alizitazama
na pesa pia kwa macho ya tamaa kisha akasema
"siwezi
kuharibu kazi yangu kisa tamaa". Yule kijana akatia
mkono katika mfuko nyuma wa suruali
yake,alipoutoa ulikuwa umeshika pochi ya kuwekea
hela iliyotuna mithili ya nyoka mwenye hasira.
Aliifungua zipu ya pochi hiyo kwa majivuno kisha
akatoa noti kadhaa na kuzihesabu, aliporidhika nazo
aliziweka juu ya meza huku akisema "maisha yako
unahitaji uyajenge zaidi ya hapa ulipo rafiki,sasa
wewe jifanye mzalendo ukale dona na dagaa". Daud
alizipokea pesa zote kwa pupa kisha akaziweka
halafu
akaziweka katika mkoba wake wa kazi,alipofunga
zipu ya mkoba wake alifungua mtoto wa meza yake
kwa funguo. Alitoa karatasi zote alizokuja nazo
Hilda na kumkabidhi yule kijana akiwa
ametabasamu, "dona na dagaa ni mlo mbaya kwa
masikini ila kwa Tajiri ni chakula bora" Daud
aliongea kwa mzaha na kupelekea wote wacheke.
Waliagana kwa furaha kisha yule kijana akaondoka
ofisini hapo akiwa na nakala hizo za WAHANGA.
Mnamo desemba mwaka huohuo matokeo ya
uchaguzi
huo yalitarajiwa kutangazwa katika ukumbi wa tume
ya taifa ya uchaguzi,tarehe na saa za kutangazwa
kwa matokeo hayo ilitajwa mapema sana. Hatimaye
siku ya siku ikawadia na ukumbi huo ukawa
umejaa wagombea tofauti huku wagombea wa urais
wa kila chama wakawa wamekaa katika viti vilivyo
katika safu moja iliyopo mbele karibia na jukwa
kuu . Ilipotimu saa nne kamili za asubuhi matokeo
hayo yalitangazwa na mwenyekiti wa tume hiyo
mhe Ramadhani Gumbo kwa kutaja asilimia za kura
kwa kila mgombea,hakika ilikuwa ni shangwe kwa
chama cha upinzani PTP huku chama tawala RPP
kikipitwa kwa kura nyingi sana. Vyama vingine
vilivyobakia vilikuwa na upinzani mdogo hivyo
havikuweza kufua dafu kabisa. Mgombea urais
aliyeshinda alipeana mikono na wagombea wote
kwa tabasami kuu,nao wagombea wengine
waliupokea mkono wake kuonesha hawana
kinyongo na wamekubaliana na matokeo hayo.
Mwisho akapeana mkono na mpinzani wake
mkubwa mheshimiwa Dominic Mtalemwa wa RPP,
walipeana mikono wakiwa tabasamu kisha
wakakumbatiana kwa furaha yao ya maigizo.
Wakiwa wamekumbatiana mhe Filbert Ole ambaye
ni mshindi aliongea kwa sauti ya chini, "bado ni
chekechea kwenye siasa usishindane na aliye chuo
kikuu". Maneno hayo ya dharau hayakusikika na
mtu yoyote isipokuwa Mtalemwa mwenyewe
ambaye hakuhisi kama ipo siku atadharauliwa
namna hiyo. Hata hamu ya kukaa eneo haikuwepo
ndani ya nafsi
yake kutokana dharau aliyooneshwa,kwake ilikuwa
ni kuaibishwa ingawa hakuna mtu aliyeiona. Alitoka
hadi nje ya ukumbi katika eneo la maegesho akiwa
na wapambe wake wote,aliingia ndani ya gari
alilokuja kisha akamuamuru dereva aendeshe kurudi
nyumbani kwake.
*******************************************************
Ukimya wa kampuni ya uchapishaji ya EAPL katika
kuchapisha jarida la WAHANGA ulizua hali ya
sintofahamu miongoni mwa waandishi hao wa
kimataifa, kuzungushwa na mtu aliyepokea nakala
zao kuliwashangaza sana kwani haikuwa kawaida
kwa jambo kama hilo kutokea.
"nashauri tuifuatilie nakala yetu" alishauri Norbert
katika kilichowekwa juu ya suala hilo.
"hata mimi naona tufanye hivyo" Davis alimuunga
mkono Norbert
"hapana tusifanye hivyo " Joseph alitoa rai ya
kupingana na mawazo ya Norbeert na Davis kisha
akawaambia "hili suala halijakaa kama
mnavyofikiria nyinyi jamani, kumbukeni tulimchezea
simba sharubu akiwa amesinzia na sasa
amezinduka lakini ametutisha tu pasipo
kutung'ata". Kauli hiyo ilimuacha kila mmoja njia
panda, hali hiyo Joseph aliibaini haraka sana na
ikamlazimu kuwafafanulia "namaanisha hivi kama
jarida lingetoka tungekuwa tumechokonoa mahali
pabaya,bsasa ili kutuonesha mhusika anaweza
kufanikiwa kufanya lolote ndio amezuia kazi yetu".
Wote waliafiki kwa kutikisa kichwa kuashiria
wamekubaliana na hoja ya Joseph.
"jambo ulilolisema Mr Kiiza nakubaliana na wewe
kwa asilimia mia moja na sasa inatubidi tusitishe
kazi ya kuchunguza tukubali kazi yetu imepotea tu"
aliongea Allison kwa mara ya kwanza baada ya
kuwasikiliza wenzake. Akaendelea kuwaambia "cha
msingi ni kuangalia kazi nyingine baada ya hapa,
ila kwa sasa tukubali tumeshindwa kuwazindua
wanachi usingizini".
Baada ya wote kutoa mawazo yao walikaa kimya na
kumtazama Hilda, "hakuna kilichoharibika jamanu
katika suala hilo mimi nahisi tuwaache wasahau
kisha tuwaumbue" Hilda kwa mara ya kwanza
aliongea baada ya kuona anatazamwa na kila
mmoja.
"unamaanisha nini kusema hivyo?" .Alphonce
alimuuliza kwa pupa. Hilda alianza kuifafanua kauli
yake kwa kusema "baada ya kukamilisha uchunguzi
nakala zile nilivutiwa sana nazo,hivyo nilitoa vivuli
vyake kisha picha za ushahidi nikazihamisha
kwenye santuri nikavihifadhi mahali ili ziwe
kumbukumbu kwangu". Wote walitoa
tabasamu na kufufua tumauni jipya mioyoni
mwao
ITAENDELEA!

No comments:

Post a Comment