Sunday, November 22, 2015

KOSA SEHEMU YA TANO

     


              KOSA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA

SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE



 ILIPOISHIA
"ok mam(sawa mama)" Mlinzi aliitikia kwa utiifu kisha akatoka nje akatuacha tukiwa wawili katika sebule hiyo na hakuwa na kufanya zaidi ya kutii amri aliyopewa na bosi iliyo na matusi mazito juu yake. Huyu mwanamke ambaye nilimtambua kama Jasmin alianza mambo yake papo hapo na mimi ikanibidi nitimize wajibu ulionileta hapo kwa mbinu zote ninazozijua, baada ya masaa matatu nilikuwa nimemaliza nusu ya kazi yangu iliyonileta ambayo niliifanya kwa msukumo tu. Kitendo cha kufanya mapenzi na mwanamke nisiyemjua kwangu niliona ni kazi ya kujidhalilisha ingawa tayari nimefanya na sasa ninahitajika nifanye kwa mara nyingine, mtaka cha uvunguni siku zote lazima ainame na huwezi ukachukua cha uvunguni ukiwa umesimama. Pia mtaka waridi sharti avumilie miiba, namaanisha ukitaka jambo lolote zuri kwa njia ya mkato lazima ukubaliane na hali ya kulipata hilo jambo. Binafsi nilikuwa nataka dola milioni moja ili niokoe kampuni yangu kwa muda wa siku kumi hivyo lazima nikubaliane na njia rahisi ya kuipata na masharti yake.




ENDELEA NA MKASA HUU WENYE KUELIMISHA NA KUFUNDISHA




SEHEMU YA TANO!!
Baada ys kuimaliza nusu ya starehe kwa Jasmin Peterson na nusu ya kazi ya kulazimishwa na mtu nisiyemjua, tulienda katika bafu la kisasa lililopo ndani ya nyumba hiyo ya kifahari. Jambo lingine nisilolitaka ndiyo nilikuwa nalifanya nikiwa ndani ya himaya ya mwanamke huyu mwenye ulinzi kama kiongozi wa nchi, kuoga na mwanamke nisiyempenda wala kumjua ndiyo jambo nisilolitaka lakini ikanibidi nifanye hivyo kwani sikuwa na jinsi. Jasmin mwenyewe alionekana kulifurahia tendo la kuoga na mimi mithili ya mwanamke anayeoga mpenzi wake, majina kadhaa ya kimapenzi aliniita wakati akiusugua mgongo wangu kwa namna ya kuvutia ambayo kwangu sikuiona kama inavutia. Maneno yake ya kimahaba aliyokuwa akiniita humo bafuni humo yalikuwa ni wimbo unaokera ndani ya masikio yangu, ilinibidi tu nijilazimishe tu kutabasamu kila aliponiita jina la kimahaba lakini moyoni nilitamani hata nimpige vichwa vya pua kwa jinsi maneno yake yalivyokuwa yakinikera. Humo bafuni ndipo nilipobaini kwamba usichokipenda hutapenda chochote juu yake, yaani ukiwa humpendi mtu basi hata jambo lolote litakalofanywa na huyo usiompenda utaliona ni karaha hata kama likiwa la kupendeza kwa wengine. Jasmin kwa muonekane ni mwanamke wa kuvutia na mwenye umbo kama msichana ingawa kavuka umri wa kuitwa msichana sasa anaelekea kuitwa mtu mzima, ngozi laini umbo  pamoja na sura ya kitoto aliyokuwa nayo bado ilikuwa haikuwa sababu tosha ya kunifanya nifirahie kufanya tendo ambalo wenzangu wa imani tofauti na dini yangu wanaita kuvunja amri ya sita. Maneno haya ninayoyaongea kwa kijana ambaye hana akili timamu anaweza kuniona sipo timamu huku akiiona kama ni bahati kufanikiwa kufaraguana na mwanamke mwenye pesa kama Jasmin,  lakini kwangu haikuwa bahati hata kidogo na niliona ni sawa kuwa mtumwa wa ngono kwasababu ya pesa ambayo dola milioni moja  ningempatia huyu mtu anayenifanya niwe mtumwa wa ngono kwa ajili ya pesa ambazo ningempatia papo hapo kama ningekuwa na kadi yangu ya benki. Nilikuwa mvumilivu wa kero za kutazama mwili mtupu wa Jasmin tukiwa bafuni akiwa anafanya kila kituko cha kutaka kunitamanisha mimi,  tulipomaliza tulienda chumbani kwake na akanifanyia kila jambo analohitaji kufanyiwa mwanaume na mke wake. Chakula kililetwa baada ya sote wawili kuhisi njaa ikishambulia matumbo yetu, tulikula chakula kitamu na kizuri ambacho kwangu hakikuonekana kama kitamu kutokana na vituko vya Jasmin akinifanya kama mume wake. Ilikuwa ni karaha sana kwangu kutokana na kutopendezwa na mambo aliyokuwa ananifanyia  hapo mezani, joho la uvumilivu ndiyo niliuvika  mtima wangu ili kusitiri hasira isije ikaniletea matatizo ndani ya himaya ya huyu mwanamke mwenye kila jeuri ya pesa. Tulipomaliza kula vyombo vilikuja kutolewa na vijakazi wake wa kike wenye vazi maalum ambao ndiyo mwanzo walileta chakula kwa kitoroli maalum chenye kusukumwa mithili ya kitanda cha hospitali. Maisha ya kifalme ndiyo aliyokuwa anaishi Jasmin  katika nyumba yake hiyo ya kifahari na alikuwa ana uwezo wa kumfanya  mtu chochote ikiwa tu atamuudhi, muda huo pia ndiyo nilijua kuwa Jasmin si mwanamke mwenye roho ya kawaida yaani ni mwanamke mwenye roho ya chui au simba. Niliyajua haya baada ya kujikaza kisabuni nikamuuliza sababu ya wafanyakazi wake kuwa watiifu namna ile.
"lazima wawe watiifu  kwani wakileta ujinga nakata vichwa vyao au kumwaga ubongo wao kwa risasi, hebu angalia pale ukutani" Jasmin aliongea kwa kiswahili fasaha kilichonishangaza sana yaani kama mtu aliyekaa Tanzania kwa muda mrefu huku akinionesha kidole ukutani halafu akabonyeza kitufe kilichopo kitandani mwake. Nilipoangalia ukutani niliona ukuta ukiwa umejigawa katika chumba chake na ndani yake kukiwa na silaha za aina mbalimbali za kivita, hapo ndipo karaha za Jasmin niliziona ni raha na nilimeza mate kwa kihoro hadi nikahisi kama yananikaba kutokana na uoga niliokuwa kila nikimtazama  Jasmin aliyekuwa akiongea nilimuona  kama akisimulia visa kale. Yaani hata kuuliza swali jingine niliogopa kwa kuhofia angeniona mpelelezi kisha aninyofoe kichwa.
"kila mfanyakazi wangu anatambua kama sipendi mzaha ndiyo maana yule hanithi pale sebuleni nilimpokaripia alitoka nje anajua ningenyofoa koromeo lake kama angeendelea kukaa" Jasmin alizidi kuongea na kunifanya nizidi kuwa kihoro ndani ya moyo wangu, alifunga ile sehemu aliyoifungua kisha akanisogelea halafu akaniambia "nahitaji tena kuondoa baridi iliyovamia ndani ya mwili wangu".  Alipoongea maneno hayo akianza kunibusu busu la kifaransa lililochukua dakika kadhaa, mimi  nilianza kazi yangu iliyonileta kwa mara ya pili tena safari hii nikija na nguvu mpya baada ya kuona nipo kwenye eneo la hatari sana na sikuhitajika nimkwaze mwanamke huyu. Nilipomaliza wajibu wangu tayari nilikuwa nimechoka na Jasmin naye alikuwa amechoka na usingizi ndiyo ulichukua nafasi yake ndani ya muda huo baada ya kufanya kazi hii nzito tena kwa nguvu za ziada. Ilikuwa ni usiku ambao sikuutambua ni saa ngapi tulipomaliza purukushani za kubadilishana tusichonacho kwa kila mmoja, asubuhi na mapema niliamka baada ya kushtushwa na mlio wa kukokiwa kwa bunduki na nilipofumbua macho nilikutana na bomba mbili za bunduki zikiwa zinanitazama. Nilifikicha vizuri kisha nikafungua macho tena na nikaona vile vile ninaangaliana uso kwa uso na bunduki ya bomba mbili yenye kitako kimoja tu na isiyo na sehemu ya kuning'iniza kibeba risasi maarufu kama magazine, Jasmin ndiye aliyekuwa ameishika bunduki hiyo akiwa na uso usio na mzaha hata kidogo akinitazama machoni. Nilijikuta nikishindwa hata kupepesa jicho kwa uoga na nilikuwa nimekodoa macho mbele huku nikihema kama kifaru mwenye hasira, uoga ulikuwa upo ndani ya nafsi yangu kwa muda huo lakini nilijikuta nikishindwa hata kutetemeka ndani ya eneo hilo kwa kuoneshewa bunduki yenye bomba mbili wakati sikuwahi hata kuoneshewa bastola usoni mwangu. Jasmin kwa kumtazama usoni hakuwa akitania hata kidogo yaani alionekana kumaanisha kile alichodhamiria, nilipoangalia kidole chake cha shahada kilikuwa kwenye kifyatulio kikiminywa taratibu.
'PUU!' Sauti ya mto nilioulalia ndiyo  ulinifanya nihisi nimelengwa na risasi na nilipoangalia sehemu ya mto huo nilikuta imepasuliwa kitu ambacho si risasi ya moto, muda huo Jasmin alikuwa akicheka kwa nguvu kisha akaniangukia kifuani mwangu huku akiniambia, "nimependezwa na ujasiri wako, ingekuwa mwingine angezimia kwa kutishiwa bunduki yenye risasi za mpira". Wakati anaongea maneno hayo bado sikuwa na amani ingawa ni kweli nilitambua  risasi iliyopiga mto ilikuwa ni ya mpira kutokana na kutokuwa na dalili ya risasi ya moto kupiga mto huo, risasi ambazo hutumiwa na polisi katika kutawanya watu wanaoandamana ndiyo niliyotishiwa hapa na huyu mwanamke anayeona ni sehemu ya utani wa kawaida.
"nimependa ujasiri ulionao na nimetokea kukupenda hivyo nitakulipa mara mbili ya kazi yako" Jasmin aliongea akiwa yupo kifuani mwangu akichezea sehemu ya bustani iliyopo katika kifua changu.

****


"Hussein hebu acha kusinzia unanipa tabu yaani unaniegemea kama umeegemea mto" Hassam aliongea huku akimsukuma Hussein aliyekuwa amemuegemea baada ya kuzidiwa na usingizi, Hussein alishtuka huku akipifa miayo inayoashiria kazidiwa na usingizi na alihitaji kulala na si vinginevyo.
"sasa hivi saa ngapi" Hussein aliuliza huku macho yake yakiwa yanarembua kama mlevi aliyezidiwa na kilevi.
" hebu ngoja niangalie....heh! kumbe saa sita kasoro hii" Hassan aliongea baada ya kuangalia saa ya kwenye simu yake ya mkononi.
" tulale tu maana bi mkubwa ukichekewa kuamka kwake ni kesi" Hussein aliongea huku akiifunga shajara kisha akanyanyuka akaenda kwenda kitanda kingine kilichopo jirani. Usingizi ndiyo ulichukua nafasi kwa kila mmoja kwa muda huo baada ya kugundua kuwa walikuwa wamepitiliza muda wa kulala.
Asubuhi na mapema wote waliamka kwa pamoja na wakaelekea uwanjani kwa ajili ya kufanya mszoezi ya viungo wakiwa pamoja na wenzao wa mtaa wanaoishi, saa mbili asubuhi walirejea nyumbani  baada ya mazoezi kuisha. Walienda kusafisha miili yao kisha wakaelekea mezani kupata kifungua kunywa kilichokuwa tayari kimeandaliwa na msaidizi wa kazi nyumbani kwao, walipomaliza kupata kifungua kinywa walielekea moja kwa moja chumbani kwao kwa ajili ya kuisoma shajara kama kawaida yao.
"dah! Ujue kuna wanawake dunia hii wana roho za shetani, si ulimsoma Jasmin jana alivyokuwa  anafanya" Hassan aliongea huku akiichukua shajara baada ya kuingia chumbani mwao.
"kama ni mimi haja zote hapohapo bunduki si mchezo wewe hata kama ya mpira isiyoua" Hussein aliongea huku akiketi kitandani kujiandaa kusoma shajara hiyo.
"aisee bunduki ni habari nyingine kabisa halafu mdingi si nilisikia aliwahi kucheza krav maga akiwa mdogo, kwanini asimkalishe huyo mwanamke" Hassan aliongea huku akicheka.
"wewe bunduki si ngumi  useme utaijua kuipangua, hebu fungua tuendelee kusoma muda unaenda" Hussein aliongea na Hassan akafungua kitabu ili waendelee kusoma.

****

Moyo wangu ulipata amani baada ya Jasmin kuonesha dhahiri hakuwa na nia ya kuniua, asubuhi hiyo tulioga kwa pamoja kama ilivyokuwa jana kisha nikavaa nguo zangu nilizoingia nazo hapo awali na Jasmin akavaa nguo yake mojawapo ya gharama iliyopo kwenye kabati la nguo humo chumbani. Jasmin akinipatia bahasha iliyotuna ambayo niliifungua kuihakikidha na nikakuta nimepewa malipo kama aliyoniahidi hapo awali na akanipatia funguo ya gari huku akiniambia, "kwa ajili yako kwa kunifikisha ninapopataka". Niliupokea huo ufunguo kisha nikampokea yeye aliyejileta kwa lengo la kupokea kumbatio kutoka kwangu, busu zito alinipatia kisha akanitoa hadi nje kwenye gari aina ya buggati yenye rangi nyekundu.
"nadhani ufunguo unao" Aliniambia huku akirmlegeza macho yake, niliutoa ule ufunguo alionipatia kisha nikaminya kitufe cha rimoti na gari nayo ikatoa mlio kuashiria mlango upo wazi. Niliingia ndani nikiwa siamini kama nimekabidhiwa gari yenye bei sana kama hiyo kwa kulala na mwanamke kwa usiku mmoja tu pamoja dola laki mbili, niliiwasha gari nayo ikatii amri kisha nikaitia gia halafu nikaiondoa taratibu huku Jasmin akinioneshea ishara ya busu. Nilipotoka ndani ya geti la nyumba hiyo nilifuata barabara ambayo nilipita jana wakati nakuja na teksi hadi hotelini kisha nikaiegesha kwenye maegesho  ya hoteli nikaingia ndani hadi chumbani kwangu, nilijitupa kitandani kwangu nikiwa nayafikiria ya siku iliyopita ambayo yalikuwa yanapita kama mkanda wa sinema katika kichwa changu. Tukio la kuwekewa bunduki usoni mwangu pamoja na tukio la kuona zana za kivita ndiyo matukio yaliyokuwa yakipita ndani ya kichwa changu kuliko matukio yote ya siku iliyopita. Ukweli sikutarajia kama nitakutana na mwanamke mwenye roho ya paka kama Jasmin mwenye matani ya ajabu kama jambazi, nilipotoka  salama kwenye himaya yake nilibaki nikimshukuru Mungu kwa mara nyingine kuliko ninavyopaswa kumshukuru nikiiona siku mpya nilipolala baada ya kuzini na nikaamka salama. Mawazo hayo yalianza kuniletea usingizi wa mapema ambao haukudumu baada ya simu niliyokabidhiawa kuanza kuita kwa fujo, niliipokea simu hiyo kisha nikatulia kimya kusikiliza maelezo ya huyu anayepiga.
"Abdulhafidh hongera kwa kumaliza wajibu wako umebakisha siku tisa kasoro na unatakiwa ukamilishe dola laki tisa zilizobakia. Sasa huna muda wa kupumzika inabidi uende mtaa wa Diaz nyumba namba 10 kwa mwanamke anayeitwa Daniella raia wa kihispania asiyejua kingereza kiswahili wala kiafrikaas, anajua kihispaniola tu sasa utajijua mwenyewe utaongea naye vipi ila tambua anakusubiri..Pia nilipokuambia ni wanawake wanaokaa mtaa ya wa watu wenye nszo sikumaanisha wanakaa mtaa mmoja nilimaanisha mitaa, una masaa 206  yakukamilisha kazi hii ambayo ni sawa ya siku nane na nusu. Kazi ianze kama unataka kunusuru kampuni yako" Sauti ileile inayonipa amri ndiyo ilisikika ikiniambia tena nikafanye mapenzi kama nagawa  dawa kwa wagonjwa, sikuwa na jinsi zaidi ya kukubali kukubali kufanya kazi hiyo. Niliondoka chumbani kwangu kwa haraka hadi nilipoiacha gari niliyokabidhiwa na Jasmin kisha niliiwasha na nikaondoka kwa mwendo wa kasi hotelini hapo nikielekea mtaa wa Diaz kama nilivyoelekezwa na nilikuwa nikitumia ramani ndogo iliyopo ndani ya gari iliyounganishwa na GPS kuniongoza. GPS ambayo kirefu chake ni GLOBAL POSITIONING SYSTEM  ni kifaa kinachoonesha mahali ambapo kifaa kingine kilichonganishwa  nacho kilipo au kuonesha ramani ya sehemu kwa kutumia mwezi usio wa asili(artifiacial satelite) katika kutafuta mitaa, GPS iliyopo kwenye gari hii niliitumia kutafuta mtaa wa Diaz na pia kunielekeza kwa kufuata barabara ninayoiona kupitia ramani iliyopo kwenye kioo cha kifaa kilichopo ndani ya gari.   Baada ya dakika kumi na tano nilifanikiwa kufika hadi kwenye geti la  nyumba niliyoekekezwa, mlinzi wa gapo getini alipoliona gari langu hapo alikuja hadi usawa wa kioo cha dereva kisha akanitazama halafu akasema, "welcome sir (karibu mzee)". Alikuwa ni mlinzi mwenye mwili mnene na uliojengeka kimazoezi ambaye alionekana kuutambua ugeni wangu eneo hilo, geti lilifunguliwa nikaingiza gari ndani ya uzio wa nyumba hiyo. Nililifikisha kwenye maegesho kisha nikashuka baada ya kufunguliwa mlango na  mlinzi kwa heshima, niliangaza kila sehemu ya nyumba hiyo niliposhuka tu na macho yangu yakatua kwa msichana wa takribani miaka ishirini na tisa au thelathini akiwa amesimama mbele ya walinzi wawili wenye miili mikubwa sana.
"eres bienvenido guapo(unakaribishwa mzuri) " Msichana huyo alikaribisha kwa lugha ya kihispaniola akiwa na tabasamu mwanana kisha akasogelea hadi nilipo halafu akanikumbatia.
"gracius querido(asante mpendwa)" Nilimjibu kutokana na kuifahamu lugha ya kihispaniola kupitia biashara zangu nilizokuwa nikifanya nchi mbalimbali duniani ikiwemo zinazotumia lugha hiyo.
" ¡Vámonos dentro(twende ndani)" Msichana ambaye  ana kila sifa ya urembo aliniambia huku akiwa amejilaza kifuani kwangu mbele ya walinzi wake, tulielekea kwenye mlango wa nyumba ya kifahari unafanana na mlango wa kasri la kifalme ambao tayari ulikuwa umefunguliwa na walinzi waliopo mlangoni. Tuliingia ndani ya nyumba hiyo ambayo ni ya kifahari kuzidi hata ya Jasmin, ulinzi uliopo humo ndani ulikuwa mkubwa sana kuliko hata wa rais wa nchi hiyo. Vijana wenye mitutu ya bunduki walikuwa wametapakaa kila kona kuhakikisha usalama wa humo  unakuwepo, Muda huo yule msichana alikuwa habanduki katika kifua changu na mkono wake kazungusha sehemu ya chini ya ubavu wangu wa kushoto. Walinzi wote waliinamisha vichwa vyao kila tulipopita kuonesha utiifu wao kwa huyu msichana ambaye alionekana ni bosi wao.
"sentir en casa(jisikie upo nyumbani)" Yule msichana aliniambia huku tukikaa kwenye kochi kwa kupakatana ambapo yeye alikuwa juu mimi chini.
"gracius(asante)" nilimjibu huku nikiwa nimekamata kiuno chake sawia akiwa juu ya mapaja yangu
"delante de Daniella nada imposible sentir en casa querido(mbele ya Daniella hakuna kinachoshindikana jisikia upo nyumbani mpendwa)" Daniella aliniambia kisha akawaambia walinzi wake,"salir(ondoka)".
Walinzi wote walitoka nje baada ya kuinamisha vichwa vyao kuonesha wameridhia amri waliyopewa, tulibaki peke yetu tukiwa huru kuliko ilivyokuwa awali mbele ya walinzi.




*ASIYEIPENDA KAZI KAZINI, JE ATAFANYA KAZI?

*ABDULHAFIDH MBELE YA MWANAMKE MWENYE HIMAYA KUBWA ZAIDI JE ATATOKA?

*JE ATAFANIKIWA KUOKOA MAKAMPUNI YAKE?



No comments:

Post a Comment