Monday, November 23, 2015

KOSA SEHEMU YA SITA







     KOSA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA

SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE



 ILIPOISHIA


"sentir en casa(jisikie upo nyumbani)" Yule msichana aliniambia huku tukikaa kwenye kochi kwa kupakatana ambapo yeye alikuwa juu mimi chini.
"gracius(asante)" nilimjibu huku nikiwa nimekamata kiuno chake sawia akiwa juu ya mapaja yangu
"delante de Daniella nada imposible sentir en casa querido(mbele ya Daniella hakuna kinachoshindikana jisikia upo nyumbani mpendwa)" Daniella aliniambia kisha akawaambia walinzi wake,"salir(ondoka)".

Walinzi wote walitoka nje baada ya kuinamisha vichwa vyao kuonesha wameridhia amri waliyopewa, tulibaki peke yetu tukiwa huru kuliko ilivyokuwa awali mbele ya walinzi.



ENDELEA NA KKASA HUU WENYE KUELIMISHA NA KUFUNDISHA




SEHEMU YA SITA!!
Nafasi ya kubaki wawili mimi pamoja na Daniella ndiyo ilikuwa wasaa mzuri uliompatia uhuru mwanamke huyu wa kihispaniola mwenye kila kigezo cha kuitwa mrembo na wanaume wote wa dunia hii, mwanamke huyu mwenye ngozi laini yenye weupe wa kizungu wenye kupendeza. Daniella huyu kwa mtazamo na hata kwa kukadiria bado alikuwa binti mdogo tu kama nilivyokadiria umri wake hapo awali, mrembo huyu ni mwenye urembo wa asili ukiwa umeongezwa na urembo wa kisasa. Yaani kuuelezea naweza nikamaliza sifa zote za kusifia na bado nikawa sijautendea haki urembo wake, Daniella pamoja na uzuri wake huo bado hakutaka kukaa na mwanaume wa maisha yake na alitaka awatumie kama nguo au jinsi anavyotaka kunitumia mimi. Tukiwa tumekaa hapo kwenye kochi vurugu ndogondogo za kitandani ndiyo zilianzia na Daniella alionesha kweli kuhitaji liwazo la mwili kuliko kitu kingine kwa muda huo, alifanya kila aina ya  uchokozi katika mwili wangu kwa lengo la kuniweka kwenye ulimwengu usio wa kawaida ambao hutumika kuishi viumbe wawili wa jinsia tofauti. Alionekana alikuwa na uhuru wa kufanya chochote katika himaya yake ndiyo maana alikuwa huru sana kuliko kawaida, nilipotaka nikae vizuri ili tuendelee kutokana na kukaa ndivyo sivyo wakati anaanza vurugu zake niliambulia mkwara mzito akidai nisimakatishe starehe yake. Kwakweli ilinidi nijibu mapigo nikiwa nimekaa ndivyo hapo kwenye kochi na akiwa amenikalia juu huku akishambulia kifua changu baada ya kuvuta shati langu kwa nguvu hadi akakata vifungo vyake. Suruali yangu nayo ilikuwa imevutwa hadi ikawa imeharibiwa zipu na kishikizo cha juu, kiukweli nilikuwa sina cha kufanya nilibaki nikijibu mapigo huku nikiziangalia nguo zangu ambazo nimeingia nazo hapo ndani.  Kila nilipozidi kumfanyia utundu binti huyu ndivyo alivyozidi kufanya vituko kama aliyepandwa na wazimu, nguo zake alizozivaa pia alizichana moja baada ya nyingine nikizidi kumfanyia utundi wangu. Nilipoanza kazi iliyonileta hadi namaliza tayari nilikuwa na alama za meno na kucha mgongo na begani kwangu, Daniella alifanya yote hayo baada ya kuzidiwa na raha ya ulimwengu mwingine wa wawili wawili. Baada ya kumaliza kazi hiyo yeye alibaki akihema mithili ya mkimbia mbio ndefu  huku akinitazama kwa macho malegevu, hakutambua muda huo kama alikuwa kaniparua na kucha wala kuning'ata na meno.
"gracius guapo(asante mzuri)" Alitoa shukrani huku akijiinua kivivu kutokana na shughuli iliyoisha muda mfupi uliopita, aliniinua na mimi kwa kunivuta mkono kisha tukapanda ngazi za kuelekea ghorofani hadi sehemu yenye sebule ndogo pamoja na ukumbi mwembamba mrefu unaotenganisha vyumba vilivyopo jirani na sebule hiyo ndogo. Akiwa anatembea kwa mwendo wa madaha bila hata kuwa na nguo yoyote mwilini kutokana na kuchana nguo zake wakati tunaanza shughuli, aliingia moja kwa moja katika mlango mmojawapo uliopo jirani na ukumbi mwembamba unaotenganisha vyumba. Mimi nikiwa kama kondoo anayekwenda machinjioni bila kujijua niliamua kumfuata tu hadi anaingia kwenye chumba hicho, nilipoingia nikiwa nyuma yake niliona mandhari nzuri ya chumba cha kulala ikiwa na vitu vyote muhimu. Daniella aliniongoza kukipita chumba hicho na tikaingia kwenye mlango wa kioo ulipo pembeni ya chumba hicho ambao nilikuja kuutambua ni bafu la kisasa, huko tulioga kwa pamoja na baada ya  kumaliza tukatoka hadi kwenye chumba tulichokipita huku uchokozi wa kimahaba ukiendelea kama kawaida na Daniella akiwa ameniachia uhuru kuliko ilivyokuwa awali. Shughuli iliyokuwa imeishia mapumziko hapo awali ilianza tena kwa kasi ya ajabu, nikiwa na nguvu baada ya kuumwagia mwili maji na hadi tunamaliza kila mtu alikuwa kachoka na usingizi ndiyo uliochukua nafasi yake kutokana uchovu niliokuwa nao. Sikutambua kinachoendelea hadi pale niliposhtuliwa na kitu chenye ncha kali kikiwa kimegusa shingo yangu, nilipofumbua macho nilikuta panga kali sana likiwa shingoni mwangu. Nilishtuka sana nilipoliona panga hilo tena likiwa limeshikwa na mwanaume mzungu mwenye mwili mkubwa sana alivaa suti nadhifu sana.
"so you slept with my fiancee, you have to die. Son of bitch(kwahiyo umetembea na mchumba wangu, unatakiwa ufe. Mtoto wa mbwa)" Mwanaume huyu aliongea akiwa hana hata chembe ya mzaha usoni mwake na nyuma yake Daniella alikuwepo akiwa tayari amevaa nguo na  alikuwa ameshikiliwa na watu weusi wenye suti nyeusi akiwa anatetemeka.
"You son of bitch I'll cut your throat(wewe mtoto wa mbwa nitakata koromeo lako)" Yule mwanaume huku akinyanyua  panga juu ili atimize azma yake, kiukweli nilikuwa sina la kufanya zaidi ya kufumba macho ili nisishuhudie damu zangu zikiruka.
" mi amor(mpenzi wangu)" Daniella alimuita huyu mwanaume huku akitokwa na machozi
"shut up bitch and close your dustbin otherwise I'll your throat(nyamaza mbwa jike na ufunge pipa lako la taka vinginevyo nitakata koo lako) Yule mwanaume aliongea akimuangalia Daniella huku mkono wake alioshika kisu ukiwa umeshikilia kisu kikiwa usawa wa koo langu. Hakutambua kama alikuwa amefanya kosa kubwa sana kumuangalia Daniella muda ule, akili zangu zikarudi kipindi cha nyuma nilipokuwa najifunza mchezo hatari wa kiyahudi uitwao Krav maga ambao hutumiwa sana na wanajeshi wa israel. Mbinu zote nilizofundishwa na rafiki wa babu yangu ambaye alikuwa mwanajeshi mstaafu wa Israel ndiyo zilinijia kichwani katika muda huo wa hatari mbele ya mwanaume huyu wa shoka. Sikutaka kusubiri ageuke wakati anamuamkaripia Daniella, hapohapo niljivuta pembeni kwa kasi kisha nikaudaka mkono alioshika panga nikaupinda kwa haraka hadi akaacha ukelele na panga likawa limemtoka mkononi. Nilimpiga pigo hafifu la nyuma kisogo akawa ametulia kama maji mtungini, wale wapambe waliomshikilia Daniella walipoona nimeshachafua usalama walikuja kwa kasi lakini waliambulia kipigo kizito kutoka kwangu hadi wakazirai. Nilipowamaliza wote nilitazama Daniella kwa macho makali ingawa aliishia kutabasamu tu huku akianza kupiga makofi nilipoanza kumtazama, milango ya kabati la nguo lililopo humo ndanj lilifunguliwa na mtu mweusi mwenye kimo kirefu alitoka ndani ya kabati akiwa ameshika kamera ndogo na mkoba mdogo.
"Hero You deserve to get our Madam's money for your work(Shujaa unastahili kupata pesa za bosi wetu kwa kazi yako)"  aliongea yule mtu akinipatia mkoba alioushika, Niliupokea ule mkoba kisha nikaufungua na nikabaki nimekodoa macho kwa nilichokiona.
"you suppose to get 200000 us dollars but madam gave you 800000 us dollars for your work(ulitakiwa upate dola 200000 za kimarekani lakini Madam amekupa dola 800000 kwa kwa kazi yako) Aliongea yule mtu huku na kunifanya nijione nipo ndotoni kwa kuweza kukalimisha dola milioni moja kwa kulala na wanawake wawili tu badala ya kulala na wanawake kumi kama nilivyoambiwa. Nilizipokea zile pesa kisha nikapokea nguo mpya za kisasa zilizokuwa ndani ya kabati, muda wote huo Daniella alikuwa anatabasamu baada ya kushuhudia vurugu nililolianzisha pale kitandani kwa wale watu ambao hadi muda huo nilikuwa nimeshatambua kama walikuwa wametumwa waje wanifanyie jaribio hatari.
"everyman who fail this test he suppose to die and not to get money for his work. Congratulation for saving yourself, this is your staff(kila mwanaume anayeshindwa jaribio hili anatakiwa afe na si kupata pesa kwa kazi yake. Hongera kwa kuiokoa nafsi yako, hivi ni vitu vyako) Aliongea yule mwanaume huku akinipa  pesa zangu , funguo ya gari pamoja na simu iliyokuwa. Nilivipokea vitu hivi ambavyo vilikuwa vipo kwenye nguo zangu nilizokuja nazo kisha nikapokea busu zito la Daniella aliyekuwa amesogea karibu yangu muda huo, nilitoka humo chumbani nikiwa nimeshika mkoba mkono mmoja na mkono mwingine ukiwa kiunoni kwa Daniella, yule mwanaume ambaye alinikabidhi mkoba akiwa yupo nyuma yetu akitufuata. Tulienda hadi nje kwenye maegesho kisha nikaingia kwenye gari niliyokuja nayo baada ya kuagana na Daniella, niliondoa gari kwa mwendo wa kasi nikifuata uelekeo wa hotelini nilipochukua chumba. Namshukuru mungu niifika hotelini kisha hadi katika maegesho ya hotelini hapo, niliegesha gari  kisha nikashuka nikiwa na mkoba niliopewa na Daniella. Niliamua kutembea kuelekea ndani lakini nilisita baada ya kusikia sauti ikiita jina langu ikitokea nyuma yangu, nilipogeuka nilimkuta mwanamke aliyevaa shungi la rangi ya kijani na nikabu kwenye uso iliyomfanyia sura yake isionekane hata kidogo. Mwanamke huyu alinikimbilia kisha akanikumbatia akiniacha nimebaki njia panda kutokana na kutomtambua.
 Mwanamke huyu alionesha kunitambua kabisa kutokana na jinsi alivyoanza kunichangamkia
 "Hoe gaan dit(uhali gani)?" alinijulia hali kwa sauti yake nyororo  yenye hadhi ya kumfanya kiziwi aweke umakini ingawa hawezi kusikia kabisa.
" Goed, dankie. wat gaan dit(sijambo, asante. wewe ni nani?)" Nilimwambia hali yangu ilivyo kama alivyoniuliza kisha nikamuuliza yeye ni nani kutokana na kutouona uso yake zaidi ya kuona macho yake yaliyopakwa wanja kwa namna ya kuvutia, nilipomuuliza hivyo alinyanyua nikabu yake akanipa wasaa wa mimi kuiona sura yake halisi iliyonifanya nishtuke sana kwani sikutegemea kumuona hapo na wala sikutarajia kumuona tena.
"Sarina is jy?!(Sarina ni wewe?)" Nilimuuliza kwa mshangao Sarina baada ya kutorajia kumuona hapo katika muda kama huu, nilijikuta nikimkumbatia bila hata kuelewa ujasiri wa kumkumbatia niliutoa wapi. Sarina naye alinipokea nilipomkumbatia na ikawa tumekumbatiana.
" waar was jy(ulikuwa wapi wewe)?" Nilimuuliza kwa mshangao kutokana na kutomuona kwa siku mbili tu ambazo kwangu niliziona ni miezi.
" Ek was in my huis op Thia stad,   in die hotel bly jy ? (nilikuwa nyumbani kwangu katika mji huu, unaishi katika hoteli hii?)" Alinijibu huku uso wake ukiwa umepambwa na tabasamu kisha akaniuliza swali papo hapo.
"ja, kan jy my gas wees? (ndiyo, unaweza kuwa mgeni wangu?)" Nilimjibu kisha nikamuuliza swali lililomfanya ajifikirie huku akipeleka mboni za macho yake pembeni kwa namna inayomfanya azidi kupendeza, halafu akajibu, " seker nie, hoekom nie( hakika, kwanini iwe hapana)". Jibu lake lilinifanya nitabasamu na nikajikuta nimemshika mkono wake kumuongoza hadi ndani. Tulipanda lifti ambayo ilitupeleka hadi ghorofa ambayo ndiyo chumba changu kinapatikana, lifti iliposimama nilimuongoza hadi chumbani kwangu ambapo aliingia bila wasiwasi.
"vyfster kamer, mooi(chumba cha nyota tano, kizuri)" Aliongea alipokuwa anakishangaa chumba changu.
" Jy is welkom om my gas(unakaribishwa mgeni wangu)" Nilimwambia huku nikifanya utiifu wa kumkaribisha ajihisi kama malkia.
"dankie(asante)" Alinishukuru huku akikaa kwenye kochi mojawapo lililopo kwenye chumba hicho.
 "Ek herhaal weer, welkom om my nie-permanente
behuising(narudia tena, karibu kwenye makazi yangu yasiyo ya kudumu)" Nilimkaribisha kwa mara ya pili Sarina huku nikimtazama usoni.
"Dankie, ek voel warm binne omdat ek hierdie rokke(asante, nahisi joto nikiwa nipo ndani hasa nikiwa nimevaa vazi hili)" Sarina aliongea huku akivua juba alilovaa na akabaki na nguo nyingine ndani zilimsitiri sehemu za mwili zake ikiacha wazi sehemu ambazo zingeweza kusitiriwa na juba hilo, alitoa kibanio alichokibana katika nywele zake ndefu kisha akaziachia nywele hizo kwa kutikisa kichwa chake. Niliuona uzuri wake ambao ningeamua kuuelezea hapa nisingeumaliza hata kwa karatasi kumi za maandishi ningekuwa sijautendea haki katika kuuelezea, nilibaki nimetoa macho kama kurunzi ya mlinzi wa makontena ya bandari nikimshangaa. Sarina aligundua kama namuangalia kwakuwa nilibaki nikiwa nimesimama bila hata kusogea na  ikamlazimu  anitazame usoni.
" jy wonder hoekom?(unashangaa nini)" Sarina aliniuliza baada ya kuniona nikiwa namuangalia kama mtu aliyepumbazika ghafla.
"Sarina jy is baie mooi, is die mooiste pêrel(Sarina wewe ni mrembo sana, ni mzuri zaidi ya lulu)" Nilijikuta nikimpa sifa nzuri kutokana na urembo aliokuwa nao Sarina hadi nikamuona ni zaidi ya lulu ipatikanayo baharini kwenye maji yenye kina kirefu, napenda niseme ukweli tu maana uongo dhambi. Nilitokea kumpenda Sarina tangu mara ya kwanza namuona na nilijiapiza laiti ningempata basi yeye ndiye angekuwa mwanamke wa maisha yangu, yaani isingekuwa janga la kuokoa kampuni yangu basi ningekuwa tayari nishatangaza azma yangu kwake ili niweze kumpata.
Nikiwa bado namtazama  nilipompa sifa mrembo huyu ambaye aliishia kutabasamu huku kainamisha macho yake chini, simu iliyopo mfukoni mwangu ilianza kuita kwa fujo hadi Sarina akawa ananitazama baada ya kuusikia simu hiyo
"Abdul ontvang oproepe laat(Abdul simu inaita hebu pokea) Sarina aliniambia kwa maneno ya kiafrikaas ambayo sikuyaelewa kabisa kutokana na kutoijua sana lugha hiyo, niliitoa simu hiyo baada ya Sarina kunipa ishara ya kuipokea simu hiyo na mimi nikaipokea halafu nikaiweka sikioni mwangu kisha nikasema, "hallo".
"hongera kwa kupata mtoto anayekuchangamkia  namna hiyo Abdul, sasa unatakiwa upeleke mzigo wangu nilipokuelekeza halafu ujiandae kwa kazi mpya ya kuifanya" sauti ya mtu anayenipa amri ya kufanya mambo nisiyoyapenda.
"hivi nimekukosea nini wewe mpaka unifanyie hivi, kama pesa uliyonitajia si ungeniachia nikakupatia kwenye akaunti yangu kuliko kunigeuza malaya wa kiume huku ugenini" Nilimlalamikia huyu mtu nisiyemjua ambaye ananipa kazi nisizozitaka.
"nataka uonje uchungu wa kutafuta pesa uliomkuta mwenzako kwa ajili yako" Sauti ile iliniambia.
"kwaajili yangu? kivipi?" Nilimuuliza baada ya kutojua wala kutoelewa kwanini ananiambia hivyo, muda huo nilikuwa nimeshasahau kama Sarina yupo ndani ya chumba changu tena alikuwa akinishangaa ninavyoongea kiswahili ingawa hakutambua wala kuelewa ninachoongea.
"sina muda wa kujibu maswali yako hayo, cha msingi ni kufuata kila ninachokuambia kama unahitaji mali uzikute kama zilivyo. Ukifanya ujanja wowote tu jua utakuwa umejiumiza mwenyewe na utajuta kwa ulichokifanya, peleka hizo pesa kwenye sanduku la posta la Walvis bay na si vinginevyo ndani ya siku kumi nizikute pesa zangu" Sauti ya mtu ambaye anayenipa amri iliongea ikinipa amri nyingine, baada ya kusikia suala la mimi kusababisha mtu apate uchungu wa kutafuta pesa nilibaki kutomuelewa na hata simu ilivyokatika nilikaa chini bila ya kupenda na matatizo yote niliyopitia tangu nilipojikuta nipo ndani ya nchi hii ndiyo yakanijia kichwani mwangu. Mikono niliweka kichwani kwangu kutokana na kuchanganyikiwa na matatizo haya yanayonipata, nilijiona nipo peke yangu na wala sikuwa nafikiria suala la uwepo wa Sarina eneo hilo. Hatua niliyofikia muda huu ilikuwa ni kuelekea kuwa kichaa kwa jinsi nilivyochanganyikiwa na matatizo yanayonikumba, mawazo yangu yote yalikuwa yamehama nje ya chumba hicho ndani ya muda huo.
" wat is die probleem?(nini tatizo?)" Sauti ya Sarina ilinirudisha ndani ya chumba hicho na nikakumbuka uwepo wake kwa muda huo, niliinamisha uso wangu chini hata baada ya kusikia swali lake . Sarina aliamua kunishika kidevu kisha akaniinua juu uso wangu na nikawa natazamana naye, hapo ndipo nikatambua kama Sarina ametoka kwenye kochi alipokuwa ameketi na sasa yupo mbele yangu.
" Vertel my wat is die probleem?(niambie nini tatizo)" Sarina aliniuliza huku akinishika shavuni kwa mikono yake milaini hadi nikajihisi nimesisimka mpaka kwenye nywele zangu, niliinamisha kichwa changu chini nikihofia kuonekana naongea alinacha kama nilivyoonekana na Jonas kwa mara ya kwanza nilipomueleza matatizo yaliyonikuta. Nikiwa nimeinamisha kichwa changu hivyo mkono laini wa Sarina ulichezea nywele zangu za singa ambazo sikuwa nikizitunza, mwili wote ulinisisimka kwa jinsi alivyokuwa anazichezea nywele zangu.
"Sarina  is 'n lang storie te vertel, maar ek het besef ek
het ernstige probleme(Sarina ni hadithi ndefu nikikusimulia ila tambua nina matatizo makubwa)" Nilimuambia Sarina huku nikiangalia juu ya dari kinyonge sana kutokana na matatizo niliyonayo, macho yangu juu ya dari yalivutika ni kitu nilichokiona na nikabaki nikikihakikisha kwa umakini.
"Haa!  Dit dwaas(Haa! Pumbavu huyu)" Nilisema kwa hasira huku nikisimama nikiangalia juu ya dari nikiwa nimekunja sura.

*he! Pumbavu tena ni nani?


TUKUTANE TENA KUMJUA HUYO


No comments:

Post a Comment