Thursday, December 29, 2016

MJUE PROFESSA PENINA MHANDO MLAMA




MJUE PROFESSA PENINA MHANDO MLAMA


 
Professa Penina Mhando Mlama


      Awamu nyingine ya kipindi chetu cha Msanii wetu  katika  blogu yetu Maridhawa, ni wajibu wetu kukujulisha juu ya watu muhimu kwenye fasihi hii ya lugha ya Kiswahili. Ambao wana mchango mkubwa kisanaa na hadi kitaaluma. Hakika Tanzania ni yenye hazina nyingi katika Sanaa amabazo zimekuwa hazijulikani miongoni mwa Watanzania wenyewe, au hata Wanafasihi wa kizazi hiki
wamekuwa hawawatambui watu hawa ambao ikitajwa historia ya sanaaa ya lugha. Basi katu  huwezi kuwaacha kuwataja, wasomi mbalimbali wa somo hili wamekuwa wakiwaimba mashule pasipo kuwajua  hao ni kina nani. Hivi leo ukimuuliza Mtu fulani aliyesoma  ngazi ya juu ya elimu ya shule ya upili, katu hawezi acha kukutajia majina ingawa si wote wanaowajuia kiundani watu hawa.  Siku ya leo tuna Mama yetu, bibi yetu,wifi yenu, shangazi yenu na wengine ni dada yenu katika kipindi hiki.

    Anaitwa Professa Penina Muhando akiwa na jina la Mlama kama jina  la  mwisho kutokana na  Mwanamke kutumia jina la mume wake daima. Alizaliwa mwaka 1948  huko  Berega mkoani Morogoro nchini Tanzania. Mhando alipata shahada ya  Sanaa  ya ukumbini, shahada ya ualimu na pia shahada ya uzamivu(PHD) katika  lugha na sayansi ya lugha(linguistiki) katika chuo kikuu cha Dar es salaam. Baadaye alipandishwa  kuwa Professa kisha mkuu wa idara ya Sanaa za ukumbini  katika chuo hicho.

     Mhando likuwa ni mmoja wa kundi la  waandishi wa tamthiliya katika kipindi mwishoni miaka ya 1960, ambaye aliibuka kutokana na matokeo ya azimio la Arusha mnamo mwaka 1967. Kipindi ambacho falsafa ya Ujamaa ikawa  ndiyo falsafa inayoongoza nchi, kipindi hicho Sanaa za ukumbini zilikuwa zikikatishwa tamaa sana pale zinapochezwa  tamthiliya za kigeni. Waandishi wa ndani  wakawa wameamriwa kutumia Sanaa zao ili kueneneza falsafa ya ujamaa kwa watu wa Tanzania  kuwaonesha watanzania kuwa hiyo ndiyo njia pekee ya kimaendeleo. Mhando alipatwa na njia panda katika kutumia kingereza au Kiswahili, kutumia  kingereza kingemuwezesha kutumika kazi zake sehemu mbalimbali duniani lakini siyo Tanzania ambapo wengi wao hawatumii lugha hiyo. Kiswahili vilevile kingemuwezesha kutumika nchini tu, mwishowe akaamua kuandika kwa lugha ya Kiswahili.

     Kazi za  awali  za Mhando ni kama  vile
 Haitia (Guilt, 1972),
 Nguzo Mama(1982),
 Lina Ubani(1984) 
Mitumba Ndui(1989)

   Mhando   ni miongoni mwa waandishi waliyokuwa wakiakisi  utaifa wa kiafrika,ni mmoja wa waanzilishi wa harakati za Ukumbi kwa maendeleo (Theatre for development) ambao walitaka watu watumie  tamthiliya ili kuhusisha mambo muhimu katika maisha yao na jamii  yao.
   Mnamo mwaka 2013, aliteuliwa kuwa Mwenyekiti wa baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) na Rais Jakaya Kikwete kwa muda wa miaka mitatu. Hivi sasa bado ni Professa wa chuo kiku cha Dar es salaam, huyu ndiye msaani wetu kwa siku ya leo


            HUYU NDIYE PROFESSA PENINA MHANDO  MLAMA
       (Nakala yetu hii bado ni mbegu)





            TUKUTANE JUMA LIJALO SIKU YA ALHAMISI, MAJIRA KAMA HAYA




No comments:

Post a Comment