Monday, August 14, 2017

TENDAGURU SEHEMU YA TATU



RIWAYA: TENDAGURU
NA: HASSAN O MAMBOSASA
MAHALI: TANZANIA NA MAREKANI



<><><>SEHEMU YA TATU<><><>


"Nasa screenshot yake pamoja na ya gari lake hilo halafu play mwingine" Amri nyingine ilitoka na kijana alifanya kama alivyoagizwa, mkanda wa siku nyingine uliwekwa na mtu akiwa ni yuleyule anayemuona anakuja kupokea wageni uwanjani hapo.

"Piga screenshot kila mkanda wa siku ambazo anafika huyu mtu" Aliweka agizo jingine.

Sunday, August 13, 2017

TENDAGURU SEHEMU YA PILI




RIWAYA: TENDAGURU
NA: HASSAN O MAMBOSASA
MAHALI: TANZANIA NA MAREKANI




<><><>SEHEMU YA PILI<><><>


"Akili kuchekecha tu, hii inaonesha wazi hawa waliuawa ndiyo wakatupwa kwenye maji na si kingine. Haiwezekani wafe hivihivi tu, ninachokihitaji kutoka kwako kuanzia hivi sasa hakikisha kila picha unayoipiga kwenye miili hii zinafikia mezani kwangu"

"Afande" Amri yake iliitikiwa na Askari yule ambaye alikuwa na kamera pia mkononi mwake alisogea na  kuongeza walau picha zingine za upande tofauti kabisa kwenye miili ile.



Saturday, August 12, 2017

TENDAGURU SEHEMU YA KWANZA



RIWAYA: TENDAGURU
NA: HASSAN O MAMBOSASA
MAHALI: TANZANIA NA MAREKANI




<><><>SEHEMU YA KWANZA<><><>


               UWANJA WA NDEGE WA MWALIMU  NYERERE

      Wageni waliyokuwa na asili ya barani Ulaya walionekana wakitoka kwenye mlango maalum, huu ni mtokeo wa wale wote wanaowasili ndani ya uwanja huu. Lilikuwa ni kundi la wazungu waliyovalia mavazi marahisi haswa kwenye macho ya kadamnasi, ilionesha wazi hawa  ni watalii waliyokuwa wapo mapumzikoni na matembezini. Huu  ni mtazamo juu yao lakini hakuna aliyekuwa na uhakika na kile  kilichokuwa kikionekana, ujio wao ndani ya nchi hii ulibaki kuwa  ni habari yao iliyokaa mitimani kwa kila mmoja. kila mmoja alifunika kichwa chake kwa kofia kuhofia haswa jua la jiji  jinsi lilivyokuwa kali. Macho yao  yalistiriwa na miwani ya jua, ilionesha wazi hawakuwa wamezoea mmuliko huu   wa mchana.

Wednesday, August 2, 2017

WITO WA KUZIMU SEHEMU YA MWISHO






WITO WA KUZIMU

NA: HASSAN O MAMBOSASA

MAHALI:TANZANIA


SIMU:+255713776843
      +255762219759

WHATSAPP:+255713776843
         +255762 219759

BLOG: riwayamaridhawa.blogspot.com




SEHEMU YA MWISHO!!
Ndani ya chumba hicho alishuhudia wasichana watatu wakiwa wamekaa wanaongea huku wakicheza karata,alisimama mlangoni hapo akiyathaminisha mazingira ya humo. Kabla hata hajamaliza kuyathaminisha   alifunguliwa pingu zote alizofungwa na kisha alisukumwa ndani kwa nguvu.






______________TIRIRIKA NAYO

    Aligeuka kuwatazama mabinti watatu waliokuwa wamevaa sare kama zake wakiwa wanacheza karata, alibaki akishangaa wasichana hao ambao walimtazama kwa nyodo kila mmoja na kisha waliendelea kucheza karata kama kawaida. Josephine hakuwajali kabisa alienda hadi kwenye eneo ambalo kitanda kimojawapo kilikuwa kitupu kisha akajilaza akiwa anasikilizia maumivu. Alipojilaza tu kwenye kitanda hiko wale wasichna waliweka karata zao chini na kisha wakaenda hadi hapo walipo, bila kuuliza mmojawapo alimvuta mguu kamuangusha chini kisha akampiga teke la ubavu.

Friday, June 23, 2017

HANJAMU YA MSALITI



RIWAYA: HANJAMU YA MSALITI
NA: HASSAN O MAMBOSASA




 SURA YA KWANZA

    Mvumo  wa kutoka mashariki kuelekea magharibi ulirindima, minazi  pamoja na miti mingine mingine iliyopo  ndani ya mandhari hiyo. Ilipepesuka vibaya kwa mkumbo huo, hali hiyo ilidumu ikiwa na karaha kubwa kwa miti ambayo haikuisha kulalama ikitoa mivumo ya aina yake pale matawi au makuti yalipovamiwa. Karaha kwa viumbe hai waliyojichimbia ardhini, ikawa ni   burudani kwa viumbe hai watembeao juu ya mgongo wa ardhi. Mgeuko wa hali ya hewa kutoka ile ya joto  liletwalo na jua hadi kuwa mpulizo,  ndiyo ikawa hivyo kwa upande wao.

Tuesday, March 21, 2017

WITO WA KUZIMU SEHEMU YA ISHIRINI NA TISA


WITO WA KUZIMU

NA: HASSAN O MAMBOSASA

MAHALI:TANZANIA


SIMU:+255713776843
      +255762219759

WHATSAPP:+255713776843
         +255762 219759

BLOG: riwayamaridhawa.blogspot.com




SEHEMU YA ISHIRINI NA TISA!!
Ushahidi ambao ungeweza kumuweka huyo aliyekuwa akimkejeli nyuma ya nondo haukuwepo kabisa ndiyo maana alikuwa akitaabika yeye baada ya kukutwa na vidhibiti vyote vilivyokuwa  ni muhimu san kwa ajili ya kesi hiyo. Hakika alikuwa amepewa kesi ya kuiba Ng'ombe kwa kuwekewa mifupa ndani ya eneo lake, huo ulikuwa ni ushahidi tosha wa tuhuma hiyo ya kuiba Ng'ombe ambayo ilikua ikimkabili hakukuwa na ushahidi mwingine ambao ungeweza kumnusuru.


Monday, March 20, 2017

WITO WA KUZIMU SEHEMU YA ISHIRINI NA NANE



WITO WA KUZIMU

NA: HASSAN O MAMBOSASA

MAHALI:TANZANIA


SIMU:+255713776843
      +255762219759

WHATSAPP:+255713776843
         +255762 219759

BLOG: riwayamaridhawa.blogspot.com





SEHEMU YA ISHIRINI NA SABA!!
Kitendo hicho ilikuwa ni mpango kabambe uliokuwa umesukwa na ukasukika, wote walibaki wakitabasamu kwa kuweza kumtia nguvuni kwani tayari sifa zake walikuwa wameshazisikia kama alikuwa ni mjanja sana. Mwenyeji wake alinyanyuka pale kitini alipokuwa amekaa na alijongea hadi eneo ambalo Norbert alikuwa ameangukia, alimpiga teke la kumsukuma na kupelekea ageuke chali kwani alikuwa yupo kifudifudi.

"Simba hachezewi sharubu hata siku moja, sasa kakuparua na kucha"  ALiongea huku akimtazama mateka wake kwa dharau kuu.



Sunday, March 19, 2017

WITO WA KUZIMU SEHEMU YA ISHIRINI NA SITA

WITO WA KUZIMU

NA: HASSAN O MAMBOSASA

MAHALI:TANZANIA


SIMU:+255713776843
      +255762219759

WHATSAPP:+255713776843
         +255762 219759

BLOG: riwayamaridhawa.blogspot.com





SEHEMU YA ISHIRINI NA SITA!!
Alipotolewa gundi iliyokuwa imeweka mdomoni, bado Kamishna alikuwa amepigwa na bumbuwazi la mwaka.

"Shemeji wewe ndiyo wa kunifanyia hivi kweli?" Happy aliuliza akiwa haamini kabisa

"Haaa! Kamishna hongera kwa kutumia nguvu zako nyingi na kumteka shemeji yako, ninataka utambue kuwa mimi sipo njiani wala nini. Nipo kitandani nimepumzika kesho naendelea na kazi yangu ya kuwatia matumbo ya kuhara" Sauti ya Norbert iliyokuwa imejaa kejeli ilisikika.

Thursday, March 16, 2017

WITO WA KUZIMU SEHEMU YA ISHIRINI NA TANO

WITO WA KUZIMU

NA: HASSAN O MAMBOSASA

MAHALI:TANZANIA


SIMU:+255713776843
      +255762219759

WHATSAPP:+255713776843
         +255762 219759

BLOG: riwayamaridhawa.blogspot.com




SEHEMU YA ISHIRINI NA TANO!!
Kuwafuata wale ambao walikuwa wao mnyororo hatari ilikuwa ni kamari ya kifo lakini alikuwa akijiamini sana, pamoja na hayo alipokuwa kwenye eneo hilo alikumbuka kumshukuru Mungu kwa hatua hiyo aliyokuwa amefikia. Pamoja na kuwa ni mtu ambaye alikuwa  haishi kubadili wasichana bado alikuwa akimkumbuka Mumba kwani imani ilikuwa ipo ndani yake, ndiyo maana alimshukuru ingawa alikuwa akimuasi sana muda mwingine aliokuwa yupo kwenye kazi yake.

  Akiwa yupo kwenye kutoa shukrani hizo kwa aliyemjalia pumzi, simu yake ya mkononi iliita, alipoangalia jina la mpigaji alikuwa ni Kamishna ambaye alikuwa ametoka kumtia homa isiyohitaji  tiba muda mfupi uliopita.


Wednesday, March 15, 2017

WITO WA KUZIMU SEHEMU YA ISHIRINI NA NNE

WITO WA KUZIMU

NA: HASSAN O MAMBOSASA

MAHALI:TANZANIA


SIMU:+255713776843
      +255762219759

WHATSAPP:+255713776843
         +255762 219759

BLOG: riwayamaridhawa.blogspot.com





SEHEMU YA ISHIRINI NA NNE!!

"Kwahiyo unanipa hongo siyo"

"Hapana"


"Natoka mama maana ulishaniambia ila ukumbuke kabisa haya niliyokwambia kwani mwenzenu Khemiri ni marehemu sasa mzigo wake mtaubeba nyinyi" Norbert alingea na kisha alitoa Kirekodi sauti kingine ambacho klikuwa tofauti na kile cha awali, alikisitisha kurekodi na kisha akacheza sehemu ile ambayo alikuwa amerokodi . Sauti ya maongezi yao ndani ya ofisi hiyo yalisikika wazi ambapo Mwanamama huyo alizidi kuchanganyikiwa.

Tuesday, March 14, 2017

WITO WA KUZIMU SEHEMU YA ISHIRINI NA TATU




WITO WA KUZIMU

NA: HASSAN O MAMBOSASA

MAHALI:TANZANIA


SIMU:+255713776843
      +255762219759

WHATSAPP:+255713776843
         +255762 219759

BLOG: riwayamaridhawa.blogspot.com




SEHEMU YA ISHIRINI NA TATU!!
Aliipekua ndani ambako alitoka akiwa na kifa kidogo klichokuwa kikiwa taa ya rangi ya bluu na akamuonesha Norbert ambaye alisikitika tu.


"Huyu ndiye mchawi ndani ya ofisi hii ananasa mawasiliano na pia simu zinazoingia na eneo zinapotoka"  Norbert aliongea na kisha alimpa ishara Moses jun ya cha kufanya kwani walikuwa wametambua wazi kuwa walikuwa wakisilikizwa na msaliti huyo ambaye yupo humo ofisini.


Monday, March 13, 2017

WITO WA KUZIMU SEHEMU YA ISHIRINI NA MBILI




WITO WA KUZIMU

NA: HASSAN O MAMBOSASA

MAHALI:TANZANIA


SIMU:+255713776843
      +255762219759

WHATSAPP:+255713776843
         +255762 219759

BLOG: riwayamaridhawa.blogspot.com






SEHEMU YA ISHIRINI NA MBILI!!
Waandishi wa hxbari hao walibaki midomo wazi baada ndani ya eneo hilo kuingia waziri mbaye alikuwa ni chui na paka na Mheshimiwa Mahujuraja, huyu hakuwa mwingine ila ni Mheshimiwa Barnaba Liwale aliyekuwa waziri wa mambo ya ndani. Yeye alikutana na  maswali ya waandishi wa habari kuhusu ugomvi wao waliokuwa nao ingawa walikuwa ni wanachama wa chama kimoja, maswali hayo yalikuwa ni yenye kuudhi lakini Meshimiwa Liwale aliweka uvumilivu.



Saturday, February 25, 2017

WITO WA KUZIMU SEHEMU YA ISHIRINI NA MOJA


WITO WA KUZIMU

NA: HASSAN O MAMBOSASA

MAHALI:TANZANIA


SIMU:+255713776843
      +255762219759

WHATSAPP:+255713776843
         +255762 219759

BLOG: riwayamaridhawa.blogspot.com



SEHEMU YA ISHIRINI NA MOJA

"Yes! Leo hii tunamfuata hatusubiri  zaidi tukitoka hapa tu jioni hii" Josephine aiongea

"Mfuateni pia msiende kichwakichwa tena inabidi muwe wawili maana yule mtu naye ana akili kama mchawi"  Mheshimiwa aliwambia

"worry out Jack Shaw nipo kazini sasa hivi na tunaenda sasa hivi" Askofu alimtoa hofu

"Yaani tukiipata tu ile paltop yake tutamuachie huyo N001 hayo malaptop yote manne halafu ile tunaiharibu hakuna namna sitaki kwenda Segerea" Mheshimiwa aliongea.

Friday, February 24, 2017

WITO WA KUZIMU SEHEMU YA ISHIRINI



WITO WA KUZIMU

NA: HASSAN O MAMBOSASA

MAHALI:TANZANIA


SIMU:+255713776843
      +255762219759

WHATSAPP:+255713776843
         +255762 219759

BLOG: riwayamaridhawa.blogspot.com




SEHEMU YA ISHIRINI!!
Walikuwa wamecheza mchezo mmoja hatari sana ambao haukufahamika hata na Mhudumu mmoja wa ndani ya nyumba hiyo ya kulala wa geni ya kisasa zaidi, mchezo huo ndiyo maana walifanikiwa kutoka bila hata ya kubakisha maswali kwenye vichwa cha Wahudumu hao juu ya yule MZungu ambaye alikuwa ameingia na Eva mahala hapo. Muda huo hesabu ya haraka iliyokuwa imebaki upande wa maadui ulikuwa umebakia na watu wawili tu ambao ndiyo walikuwa na upinzani mkubwa sana, watu hao nao walikuwa wakihitajika kumalizwa ndani ya muda wowote  kwani mzee wa kazi alikuwa amedhamiria kumaliza kazi yake kabla ya muda aliokuwa amepewa.

Tuesday, February 21, 2017

WITO WA KUZIMU SEHEMU YA KUMI NA TISA

WITO WA KUZIMU

NA: HASSAN O MAMBOSASA

MAHALI:TANZANIA


SIMU:+255713776843
      +255762219759

WHATSAPP:+255713776843
         +255762 219759

BLOG: riwayamaridhawa.blogspot.com



SEHEMU YA KUMI NA TISA
Alipouona tu huo mwili alijikuta akiweka mkono kidevuni mwake na akaanza kukuna kidevu chake kilichokuwa hakina ndevu kutokana na kuzinyoa mara kwa mara, alipoacha kukuna aligeuza macho na kumtazama Askari ambaye alikuwa akikaribiana naye kicheo.

"Rangi hii ya ngozi ni dalili tosha ya kuwa aliuawa kwa sumu, sasa inabidi tuchunguze ili kuhakikisha hilo" Aliongea huku akivaa mipira ya mikono.


Monday, February 20, 2017

WITO WA KUZIMU SEHEMU YA KUMI NA NANE



WITO WA KUZIMU

NA: HASSAN O MAMBOSASA

MAHALI:TANZANIA


SIMU:+255713776843
      +255762219759

WHATSAPP:+255713776843
         +255762 219759

BLOG: riwayamaridhawa.blogspot.com



SEHEMU YA KUMI NA NANE!!
Muda aliokuwa akiendesha gari alipokuwa yupo kwenye barabara ya Mandela alitoa simu yake na kupiga mahali na kisha alizungumza kwa lughz ya kikabila na akakata, walipofika jirani na eneo la Tabata relini aliweka gari kando na watu watatu waliingia kwenye gari hiyo. Wawili kati yao walikaa nyuma katika kile upande na kumuweka Jama kati na mmoja alipanda mbele.



Sunday, February 19, 2017

WITO WA KUZIMU SEHEMU YA KUMI NA SABA



WITO WA KUZIMU

NA: HASSAN O MAMBOSASA

MAHALI:TANZANIA


SIMU:+255713776843
      +255762219759

WHATSAPP:+255713776843
         +255762 219759

BLOG: riwayamaridhawa.blogspot.com





SEHEMU YA KUMI NA SABA
Aliweza kuona nyendo zote ambazo alikuwa amezipitia Khemiri tangu alipotoka bandari  na hadi anafika kwenye nyumba yenye makao yao, eneo hilo alilikariri pamoja na kuchukua kifaa kingine ambacho alikitia faili hilo. Hicho kilikuwa kifaa ambacho kilikuwa kina uwezo kumuongoza hadi ndani ya eneo husika kwa kutumia rekodi iliyokuwa imechukuliwa hapo awali"

"Kazi kwao" Alisema na kisha akakichukua kifaa hicho na kunyanyuka kitini.

Saturday, February 18, 2017

WITO WA KUZIMU SEHEMU YA KUMI NA SITA



WITO WA KUZIMU

NA: HASSAN O MAMBOSASA

MAHALI:TANZANIA


SIMU:+255713776843
      +255762219759

WHATSAPP:+255713776843
         +255762 219759

BLOG: riwayamaridhawa.blogspot.com




SEHEMU YA KUMI NA SITA!!
Alimsogezea Josephine ambaye alishtuka sana akiwa haamini kwani walikuwa amehangaika sana, alimpatia Spider ambaye alijikuta akiinamisha uso wake na huku Tarakilishi hiyo akiiweka pembeni.

"Aaaargh! Norbert hii ni too much sasa, naingia mwenyewe kazini haiwezekani tuhangaike kote aje kufagia akaunti yote" Akosfu Valdermar aliongea

Friday, February 17, 2017

WITO WA KUZIMU SEHEMU YA 15




WITO WA KUZIMU

NA: HASSAN O MAMBOSASA

MAHALI:TANZANIA


SIMU:+255713776843
      +255762219759

WHATSAPP:+255713776843
         +255762 219759

BLOG: riwayamaridhawa.blogspot.com






SEHEMU YA KUMI NA TANO!!
Alikuwa akiendesha maisha hayo hapo kijiji akijifanya  ni mdogo wa babu yake mzaa mama, alikuwa yupo katika kuonekano wa kizee kabisa ambapo ingekuwa ngumu kabisa kwa mtu yeyote ambaye anamfahamu kuweza kumtambua. Huko kijini alikuwa akiishi kwa amani zaidi kuliko hata huko mjini ambapo kulikuwa na kila aina ya raha, alipaona ni mahali sahihi kwake kuweza kutulia kwa siku hizo akiwa huko hadi pale hali itakapokuwa shwari.


Thursday, February 16, 2017

NILE COROCODILE


                                    Nile crocodile





    Crocodile Nile crocodile is found communities in Africa, being the second largest in the world after the majichumvi Mamba. This category prefer to live in lakes, rivers and even dams. This