Monday, November 30, 2015

KOSA SEHEMU YA KUMI NA TATU


TEMBELEA:http://www.facebook.com/riwayamaridhawa




  KOSA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA

SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE



 ILIPOISHIA

Nilienda sehemu yenye silaha nikachagua bastola za aina mbili pamoja na maboksi kadhaa ya risasi, kwa bunduki kubwa nilichukua bunduki aina ya UZI ya nchini Israel ambayo imeundwa na mwanajeshi wa kiyahudi anayeitwa Uziel Gal mwaka 1948. Bunduki hii ni moja  kati ya bunduki hatari duniani yenye uwezo kupiga risasi mfululizo kama ilivyo AK47, MP5 na nyinginezo, nilibeba risasi za kutosha na viwambo vya kuzuia sauti nikaenda kuviweka pale nilipoelekezwa.
"vipi visu hubebi?" Nurulayt aliniulixa huku anipatia visu sita vikubwa, nilivipokea visu hivyo bila ya kusema chochote nikaviweka kwenye gari kisha nikamtazama kama anaweza kuniambia la ziada.
"panda tuondoke" Nurulayt aliniambia nami nikazunguka mbele kwenye mlango wa pembeni ya dereva nikapanda.



ENDELEA NA MKASA HUU WENYE KUELIMISHA NA KUSISIMUA


SEHEMU YA KUMI NA TATU!!

Usukani wa gari hili ulikamatwa na Nurulayt na safari ya kuelekea pori la Chirinda ikaanza mara moja baada ya geti lililokuwa lipo humo ndani kufunguliwa na kifaa maalum, baada ya gari kutoka geti lile lilijifunga tena kama ilivyokuwa awali na tukawa tupo nie ya nyumba hiyo kwa upande mwingine kabisa. Ilikuwa ni majira ya saa tano kasoro za usiku barabara ilikuwa tulivu sana kuliko kawaida, tulikuwa tukipishana na magari machache tu njiani yaliyokuwa yanaitumia barabara kwa muda huo. Tulirudi hadi katikati ya jiji la Widhoek kuifuata barabara ambayp sikuijua inaitwaje hadi muda huo, Nurulayt aliifuata barabara hiyo kuelekea mashariki ya jiji la Widhoek kwa mwendo wa kasi sana. Alikuwa akiweka gia na kutoa gia nyingine huku akicheza na usukani kwa umakini sana na kusababisha gari hii iende mwendo mkali hadi ikawa inatoa mlio kama wa kulalamika kwa kuendeshwa  mwendo huo, gia tano za gari hii zilitumiwa ipasavyo na Nurulayt kama anaendesha gari ya mashindano hali iliyonisababisha nifunge mkanda mwenyewe kwani mwanzo sikuwa nimefunga mkanda. Baada ya muda mfupi tulikuwa tumeingia kwenye eneo la jangwa lisilo na majani wala nyumba za watu, tulipongia katila jagwa hilo ambalo nalijua kwa jina la Kalahari ndiyo mwendo wa gari  ulizidi . Nurulayt hakuonekana kujali sana kwa mwendo aliokuwa anautumia yeye ndiyo alizidi kukanyaga mafuta hadi mshale wa mngurumo  wa gari ukafika sehemu yenye alama nyekundu huku kengele ya hatari ikigonga kwa fujo.
"we mwanamke sikuwezi hata kidogo" Nilimuambia huku nikisikitika kwa mwendo aliokuwa anautumia Nurulayt
"kwanini unasema hivyo?" Nurulayt aliniuliza huku macho yake yakiwa makini kuangalia mbele.
"huu mwendo sijui upo mashindano ya formula 1" Nilimwambia kuhusu mwendo anaoutumia tena niliufananisha mashindano maarufu ya magari ya formula 1 yenye magari yanayooenda kwa kasi sana, maneno yangu yalimfanya Nurulayt atabasamu kisha akasema "we unataka tutembee mwendo wa harusini unafikiri tutafika leo Abdul yaani hapa hatujafika Botswana halafu tunaelekea Zimbabwe".
"Mh! Haya suka twende kazi" Nilimwambia kukatisha mazungumzo yetu kisha nikakaa kimya na sikuongea hadi Nurulayt alipopunguza mwendo akaingia kwenye sheli iliyopo pembezoni mwa barabara.
"vipi mafuta yamepungua?" Nilimuuliza.
"hayajapungua ila yanahitajika yaongezwe" Nurulayt alijibu huku akishuka kwenye gari baada ya gari kuliegesha gari jirani na mashine ya kujazia mafuta, Nurulayt alilipa pesa na gari ikajazwa mafuta hadi tenki lote likajaa kisha akarudi kwenye gari lakini hakukaa kwenye kiti cha dereva bali alikaa kwenye viti vya nyuma na kiti cha dereva kikabaki kitupu kama kilivyo.
"Nuru mbona unakaa huko mbona sikuelewi ?" Nilimuuliza huku nikigeuka nyuma nikamtazama.
"Abdul huelewi nini au mimi kuachia usukani kuja kukaa huku?" Nurulayt aliniuliza.
"ndiyo maana yake hicho ndicho nisichokielewa" Nilimwambia.
"Abdul hapa tupo karibu na West gate na West gate camp katika jangwa hili la Kalahari, mbele kidogo kiasi cha mita 500 kuna mpaka wa Trans Kalahari ambao unatenganisha nchi hii na Botswana na una ulinzi mkali. Sasa basi hatuwezi kuuvuka mpaka huo bila ya kuwa na mtu ambaye ni askari wa pale, nimetoka kwenye kiti cha dereva ili kumpisha askari niliyemkodi kwa ajili ya kutuvusha atuvushe" Nurulayt aliongea kunielewesha juu ya mpango wake ambao nilikuwa siujui kabisa.
"hapo sawa nimekuelewa" Nilimwambia kukubali kuuelewa mpango wake mzima alioupanga, maelezo yake yaliniridhisha na nikatazama mbele.
" sasa sikiliza" Nurulayt aliniambia huku akinivuta bega, niligeuka kumtazama ili  kumsikiliza nini anachotaka kuniambia.
"katika kazi kama hizi usipende kuwa muongeaji na muulizaji wa maswali sana, unatakiwa uwe kimya Abdul ingekuwa mwingine tayari ameshakupiga risasi" Nurulayt aliniambia huku akinitazama kwa umakini usoni, nilimsikiliza maneno yake kisha nikashusha  pumzi halafu nikasema "poa" nikageuka mbele. Baada ya muda takribani dakika kumi kupita mlango wa dereva ulifunguliwa na mtu mwenye mavazi ya kiaskari aliingia ndani ya gari  kisha akatutazama akasema, "samahani kwa kuchelewa".
Askari huyu aliwasha akaliingiza barabarani na safari ikaendelea wote tukiwa kimya bila ya kuongea chochote, baada ya dakika tano tulikuwa tumefika sehemu hiyo ya mpaka ambayo ilkuwa na ukaguzi wa magari yanayotoka na kuingia nchini Namibia. Mpaka huo ulikuwa na njia mbili ambayo moja yanapita magari yanayokwenda nje ya nchi na nyingine yanapita magari yanayoingia ndani ya nchi, tulipokaribia  eneo hilo yule askari aliwela gari kando akatuomba tumsubiri anarejea sasa hivi. Alishuka ndani ya gari akaenda kwenye ofisi zilizopo hapo mpakani, tulibaki tukiwa tunamsubiri na alirejea baada ya dakika takribani tatu kisha akaingia ndani ya gari safari ikaendelea tukawa tunaelekea kwenye mpaka kuvuka. Alipofika eneo la ukaguzi alitoa kadi na makaratasi akawaonesha askari ambao walimruhusu kupita bila hata kumuuliza  lolote, tuliendelea na safari tukivuka bango kubwa linalo  tukaribisha  nchini Botswana. Yule askari aliendesha gari kwa mwendo wa mita takribani 400 kisha akashuka akatuaga akikutakia safari njema, baada ya askari kuondoka Nurulayt alirudi  kwenye usukani kama kawaida na safari ikaendelea kwa mwendo ule ule wa kilevi. Baada ya saa moja tangu tuvuke pale mpakani tulitokea kwenye mji mdogo uliokuwa umechangamka sana, ilikuwa yapata saa saba za usiku na ilitubidi tuegeshe gari kando ya barabara ili tupumzike humo humo ndani ya gari kwa ajili ya usalama wa
vitu vyetu, tulilala usingizi wa mang'amng'am hadi kunakucha tukaendelea na safari yetu. Usukani wa gari kama kawaida ulikamatwa na Nurulayt na mwendo wa gari aliupunguza kwa sababu tulikuwa tumeingia katika makazi ya watu. Tulitembea kwa umbali wa kilomita kadhaa tukawa tumefika sehemu yemmnye barabara mbili ambayo moja inaelekea kushoto na nyingine inaelekea kulia, Nurulayt alipokaribia njia hizo aliweka gari pembeni na jirani na mgahawa aliweka breki ya mkononi huku akiliacha gari likiwa linawaka.
"twende tukanywe chai saa tatu hii" Aliniambia huku akiteremka garini nami nikamfuata bilab kuongea jambo lolote, tuliingia ndani ya mgahawa. Tulipata kifungua kinywa kwa pamoja na tulipomaliza  tulirudi garini na safari ikaendelea huku macho yangu yakiwa dirishani kuangalia mandhari ya nchi hii kwa upande wa sehemu wanazoishi watu wenye hali ya chini. Baina ya zile njia zilizokuwa zimegawanyika sisi tulifuata njia ya upande wa kushoto, tulienda kwa mwendo wa masaa kadhaa tukawa tumefika sehemu yenye mji mdogo uliochangamka sana.
"hapa panaitwa Maun ni sehemu iliyo karibu na hifadhi ya wanyama kwa upande wa kushoto na delta ya mto Okavango kwa upande huo huo" Nurulayt alinielezea  juu ya sehemu iliyokuwa ipo mbele yetu.
"ok" nilimuitikia kwa ufupi tu kisha nikakaa kimya nikimuacha Nurulayt acheze na usukani wa gari, Nurulayt naye hakuwa muongeaji sana  baada ya kunielezea hivyo alikaa kimya akaelekeza umakini  wake barabarani. Haikupita hata nusu saa tangu alivyonieleza hivyo usingizi mzito ulinichukua kutokana na uchovu nilionao uliotokana na kutolala usinfizi wa kutosha, nilikuja kuamka baada ya kusikia napigwa kibao huku jina langu likiitwa.
"Amka wewe tukale jioni hii"Nurulayt aliniambia nilipofumbua macho kumtazama, hapo nilibaini giza llishaanza  kuingia na tulikuwa tunaonana kupitia taa ndogo iliyopo ndani ya gari.
Nilipiga muayo mrefu kisha nikamtazama Nurulayt ambaye alionekana kuchoka sana.
"shuka bwana twende au wewe huhisi njaa?" Nurulayt aliniuliza baada ya kuona namtazama bila ya kushuka kwenye gari.
"hapa ni wapi?" Nilimuuliza bila hata  kujali maneno aliyoniambia.
"bwana hebu shuka huko  mwanaume una maswali kama mwanao, nahisi  kachukua tabia yako" Nurulayt aliongea huku akinisukuma nishuke. Muda huo  yeye alikuwa tayari ameshafungua mlango wa upande wake alikuwa anasubiri mimi tu nishuke, nilifungua mlango nikashuka chini kisha nikaenda hadi upande aliopo Nurulayt ili aniongoze kuelekea hiyo sehemu ya kwenda kula kwakuwa nilikuwa mgeni ndani ya eneo hilo.
"yaani wewe na mwanao mkikaa na mimi nahisi mtaniua maana mna maswali mengi kama polisi" Nurulayt aliendelea kuongea huku akinishika mkono kuelekea ndani ya nyumba moja yenye milango mikubwa ambayo ilikuwa ipo mbele yetu.
"huyo mtoto kachukua tabia zako mimi unanipakazia tu" Nilijitetea kimasihara na kusababisha Nurulayt anisukume begani kimasihara.
"Loh! Lione yaani mwanao nimekaa naye kwa miaka mitano tu lakini alipoanza kuongea kazi nilikuwa nayo ya kujibu maswali tu, na sasa nakutana na baba mtu habari ni hiyohiyo tu yaani kama mnanihoji vile" Nurulayr aliongea akiingia ndani nami nikamfuata, tulikuwa tumeingia kwenye mgahawa mdogo wenye watu wachache jioni hiyo. Nurulayt aliagiza chakula kama ilivyo kawaida yake halafu akaja kuketi meza moja nami, chakula kililetwa na kila mtu akawa anashughulika katika kulijaza tumbo lake. Hatukuongea hadi tulipotoka tularudi ndani ya gari, Nurulayt alienda kukaa kwenye kiti cha changu na mimi nikakaa kwenye usukani.
"tunaelekea wapi sasa, nahitaji nijue sio unaniachia usukani tu bila kusema cjochote" Nilimwambia Nurulayt.
"hapa tupo Nata kwenye njia tatu zinapokutana, fuata barabara inayoenda kusini mashariki hadi katika mji unaoitwa Francistown" Nurulayt aliniambia huku akikinyoosha kiti cha gari miayo ikimtoka mdomoni mwake, niliwasha  gari nikaingiza barabarani na safari ikaendelea kuutafuta mji wa Francis town nikiwa nimewasha taa za gari kwani nuru ya anga ilishaanza kupotea. Baada ya dakika thelathini tangu niingize gari barabarani Nurulayt alikuwa tayari yupo kwenye usingizi mzito sana na kama isingekuwa mkanda wa gari angekuwa kajigeuza ovyo hadi kufikia kuiparamia gia ya gari, siku hii niliendesha gari kwa mwendo wa kasi nikiomba tufike salama kwani sikuwa mwenyeji wa barabara ninayoitumia na alama za barabarani ndiyo kitu pekee kilichonisaidia kuniongoza katika barabara hiyo. Hadi inatimu saa nne ya usiku tayari nilikuwa nimeshafika katika mji wa Francistown uliopo kilomita 185 kutoka Nata nilipotoka, nilipofika hapo ndipo nikamshtua Nurulayt usingizini na nilimtaarifu tumefika tayari.
"ingia hiyo barabara inayoelekea kushoto na uende hadi utapokuta sheli yenye  supermarket" Nurulayt aliniambia maneno hayo alipomaliza alirudi tena kulala.
Niliingiza gari barabarani kwa mara nyingine nikawa naelekea barabara inayoenda kushoto kati ya barabara tatu zilizopo mbele yangu, barabara hizi kwa Tanzania ningezifananisha na makutano ya barabara ya Segera yanayokutanisha barabara tatu zinazoelekea Tanga mjini, Kilimanjaro na Mkoa wa pwani. Eneo la Nata  na hili la Francistown lilifanana kila kitu muundo wa makutano ya barabara zilivyo, niliamua kuwa makini na alama za barabarani kwani hizo ndizo zilikuwa msaada kwangu katika kuniongoza na barabara ya huku ili niweze kufika salama bila hata kupata ajali yoyote. Nilitumia kiasi cha dakika 45 nikawa nimefika katika sheli aliyonielekeza Nurulayt, hapo nilimuamsha tena na nikamtaatifu kuwa nimeshafika. Nurulayt aliamka kisha akatazama mazingira ya hapo kwenye sheli halafu akashuka akaniambia," sogeza gari sehemu ya kuwekea mafuta". Nilisogeza kama alivyoniambia kisha akaongea na na mhudumu wa hapo sheli, alipomaliza alichukua mpira wa kujazia mafuta akatia mafuta hadi mshale wa mafuta katika kioo cha plastiki kilichopo chini ya usukani kikaonesha tenki la gari limejaa. Alifanya malipo kisha akarejea ndani ya gari alipokuwa awali, alipokaa kwenye kiti nilimuangalia usoni nilitarajia aseme lipi juu ya hii safari.
"Mbona unaniangalia hivyo?" Nurulayt aliniuliza.
"nahitaji kujua nini kinachofuata Nuru" Nilimwambia huku nikiwa sijatoa jicho langu usoni mwake.
"ok ok ni hivi, nusu kilomita kutoka hapa kuna mpaka wa Ramekgwebana unaotenganisha Botswana na Zimbabwe. Hivyo inabidi uruke kiti cha nyuma kuna askari wa uhamiaji atakuja kutuvusha hapa kama tulivyovuka kule Trans kalahari border" Nurulayt alinipa maelezo ya mpango unaofuatia. Baada ya dakika kadhaa tangu anipe maelezo hayo  nilimuona askari wa  mmoja aliyebeba mkoba mkubwa mgongoni akija hadi kwenye gari letu usawa wa mlango wa dereva, alipofika niliamua kuruka  kiti nyuma kwani nilijua fika ndiye mtu tunayemsubiri. Yule askari alifungua mlango wa gari akaingia huku akiwa anahema  sana akiwa na mkoba wake  ambao aliupakata mapajani alipokaa kwenye kiti cha gari.
"mambo si mazuri huko" Askari aliongea huku akitutazama kila mmoja.
"vipi huko kuna nini?" Nurulayt aliuliza
"muda mfupi uliopita hapo mpakani walipita watu  wakiwa na  gari yenye mizigo mingi ambayo haikujulikana ni vitu gani, walipekuliwa wakakutwa na na unga na walipotaka kukamatwa wakaanzisha vita ndogo. Wamefanikiwa kukimbia  na gari lao la mizigo kuingia mpaka Zimbabwe kinguvu lakini waliishia msituni wa jirani na mpaka, na hivi ninavyokuambia wanafanya majibizano ya risasi na askari na mpaka mzima umemwagwa askari"  Yule askari alieleza sababu ya mambo kutokuwa mazuri huko mpakani.
"sasa itakuwaje?" Nurulayt aliuliza akionekana kuchanganyikiwa sana na maelezo hayo.
"njia pekee ya kuvuka pale mpakani ni kuvaa sare za kama hizi zangu na viatu" Aliongea yule askari huku akifungua mkoba mkubwa alioingia nao akatupatia sare za askari wa uhamiaji pamoja na viatu vya  kijeshi.
"mkivaa nguo za askari wa uhamiaji mtajulikana ni askari waliongezwa na makao makuu kwenda kupambana na hawa wasafirishaji madawa ya kulevya na mtaruhusiwa kupita. Badilisheni hapahapa" Yule askari alituambia.
"ok hamna shida ila wewe inabidi ushuke tubadilishe nguo kwani mimi ni mwanamke na huyu ni mzazi mwenzangu, hupaswi kuniona nikibadili nguo labda yeye kwakuwa hakuna asichokijua katika mwili wangu" Nurulayt alimuambia yule askari
"mh! OK hamna shida" Yule askari alinitazama kwa jicho la pembeni halafu akatabasamu akaonesha kukubaliana na maneno ya Nurulayt, alishuka  ndani ya gari kwa  haraka  na sisi tukabadilisha kwa haraka halafu tukamuita tulipomaliza kuvaa.
"Hapo safi kabisa yaani mpo kama askari wa uhamiaji, chukueni na hizi  bunduki mzishikilie ili wakituona wajue mnaingia kazini" Yule aliongea baada ya kutuona tukiwa tumevaa magwanda ya askari wa uhamiaji, alifungua ule mkoba tena akatoa bunduki mbili aina ya short gun akatupatia pamoja na mikanda ya risasi. Safari ya kuelekea kwenye mpaka wa Ramekgwebana iluanza na askari yule ndiye aliyekuwa dereva, gari letu lilipoingia barabarani alitoa king'ora cha kubandika akampatia Nurulayt ambaye alikiweka juu ya paa la gari. Mpakani tulifanikiwa kupita bila matatizo na kweli kulikuwa kuna maaskari wengi wakiwa na wana silaha kama hizi tulizokabidhiwa, safari yetu iliendelea na tukawa tumeingia kwenye pori lililopo mwanzaoni mwa nchi ya Zimbabwe. Furaha ilidhihirika machoni mwetu kwa kufanikiwa kukivuka kikwazo kile lakini furaha hii haikudumu kwani dosari kubwa iliingilia furaha hii, tukiwa tupo katikati ya pori usiku majira ya saa sita milio ya risasi ilianza kusikika na vioo vya  gari letu vikaanza  kupasuka.Yule askari ambaye ndiye aliyekuwa dereva wetu alitoa ukelele wa maumivu akiachia usukani wa  gari
 na gari likaingia pembeni ya barabara nusura ligonge mti baada ya  yeye kuwahi kukanyaga breki ya gari.


*Mmmh kunani tena?

*je watafanikiwa kupita salama?


ITAENDELEA!!

DHAHAMA SEHEMU YA KUMI NA TATU




TEMBELEA: www.facebook.com/riwayamaridhawa 



 DHAHAMA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE



SEHEMU YA KUMI NA TATU!!
"Faridaaa!" Shafii aliita jina la mke wake  kwa nguvu huku akijaribu kuinuka kitandani
"Shafii hebu tulia kwanza utasababisha  matatizo mengine tu" Mzee Buruhan alimuambia huku akimzuia asifanye fujo.
"Mama Zayina, Zayina mpo wapi?" Shafii alipiga kelele zaidi na ikabidi daktari aitwe mara moja ili kumtuliza, Mzee Buruhan na Mzee Mahmuf walimshikilia  Shafii hadi daktari alipokuja akamchoma sindano ya usingizi ndiyo ikawa ahueni.
Baada ya Shafii kulala mzee Buruhan na mzee Mahmud  walitoka pamoja na mke wa Hamis wakaenda kuka kwenye madawati ya kusubiria wagonjwa, baada ya muda mke wa Hamis aliondoka kwenda kufuata chakula kwa ajili ya mgonjwa akawaacha wazee hao peke yako.
"Kama nilivyokuambia mzee mwenzangu kuhusu huyu mwanao, awe mkweli ujue tatizo alilonalo ndiyo nitakubali kumsaidia" Mzee Mahmud aliongea.


****


"Mzee mwenzangu tatizo kila kukicha una misemo ambayo imejaa vitendawili vitupu hebu niweke wazi walau kidogo nipate fununu ya jambo linalomsumbua mwanangu" Mzee Buruhan alimlalamikia rafiki yake kutokana na kauli zake zilizo jaa mafumbo.
"mzee mwenzangu hiyo kinyume na utaratibu wa taaluma yangu siwezi kusema hata kama nalitambua tatizo hili, huwa sina tabia ya kukuficha kitu ila kwa hili wacha nikuambie ukweli tu nitakuwa nimekiuka masharti ya utalaamu wangu wa uganga ikiwa nitalisema suala hili pasipo muhusika mwenyewe kufungua kinywa chake na kuliongelea. Utanisamehe kwa hilo" Mzee Mahmud aliongea huku akimshika bega mzee Buruhan ambaye alionekana kuwa njia panda kutokana na matatizo yaliyomkumba mwanae
"mzee mwenzangu hakuna hata njia nyingine ya kunisaidia niweze pata fununu kidogo ya hili suala?" Mzee Buruhan aliuliza huku akiwa ameinamisha uso wake chini akionekana amekata tamaa kabisa ya suala hilo.
"Siku zote mwanamke atakaye mtoto lazima akubali kuvua nguo ya ndani ili alichokificha kionekane na hawezi kupata mtoto ikiwa atakataa kuivua hiyo nguo. Ndiyo hivyo hivyo mwanao akubali alilolificha moyoni mwake lifumbuke la si hivyo hataweza kupata msaada katika hilo, cha kukusaidia akiamka muambie umebaki peke yako ukitaka usipoteze vyote awe muwazi kwangu na kwako. Naenda msalani mara moja mzee mwenzangu" Mzee Mahmud aliongea kisha akajiinua kivivu  kwenye dawati la kusubiri wagonjwa akawa anaelekea chooni, mzee Buruhan alimtazama tu akiwa anatamani sana ajue jambo lililopo ndani ya kichwa chake lakini hakuwa na uwezo wa kufanya hivyo. Mzee Mahmud  aliipopotea katika upeo wa macho yake aliinua kichwa juu akiweka ishara ya kuomba dua halafu akatikisa kichwa kuonesha anasikitishwa, hakuwa na jambo jingine alilomuomba Mungu zaidi ya kumshtakia tu  juu ya balaa lililomkuta mwanae na kumfanya awe na matatizo tu katika mwaka huo ambapo miaka mingine yote aliishi kwa amani na furaha pamoja na familia yake lakini sasa furaha hiyo imetoweka  katika maisha yake. Laiti angelijua kwamba alikuwa anashtaki mtuhumiwa kuwa ameonewa wala asingelifanya hivyo lakini kwakuwa hakujaliwa uwezo wa kulibaini kwani alikuwa ni mwanadamu wa kawaida tu, hakutambua kama jereha la mwanae ni  la kujitakia hivyo halihitaji pole hata kidogo.
   
Mzee Mahmud alipofika kwenye mlango wa msalani baada ya kuondoka pale kwenye dawati alihisi hali isiyokuwa ya kawaida katika mwili wake lakini aliipuzia na kuingia humo msalani, alipoingia ndani alipitiliza sehemu za kujisaidia haja ndogo akawa anaelekea sehemu maalum ya yenye vyoo ndani ambayo hutumiwa na wale wanaohitaji kumaliza haja zao kwa siri tu. Alipofika hilo eneo  alifuata mlango wa moja wa vyoo akashika kitasa ili aufungue lakini alisita baada ya  kusikia upepo mzito ukivuma kwa ghafla ambao ulitaka hata kuupeperusha msuli aliojifunga kiunoni lakini aliuzuia, upepo huo ulipotulia Mzee Mahmud alionekana kukerwa nao kwa kitendo cha kutaka kumuadhiri ambapo aligeuka nyuma akionekana kuwa na hasira za waziwazi juui ya tukio hilo.
"Adabu gani hizo ewe mwanajini wataka kuniadhiri kwa hizo nguvu zako ulizojaliwa?" Mzee Buruhan alilalamika baada ya kumuona yule aliyetaka kumuadhiri kwa kutaka kuupeperusha msuli aliojifunga kiunoni alikuwa yupo mbele yake baada ya kugeuka nyuma, alikutana uso kwa uso na Zalabain akiwa amefumbata mikono kifuani mwake.
"Samahani mzee wangu kwa hilo" Zalabain aliomba radhi.
"sema una shida gani" Mzee Buruhan aliongea huku akiuweka msuli aliojifunga kiunoni vizuri.
"nimekuja kukuambia tu mimi ndiye ninayemtesa Shafii na huwezi kuharibu kazi yangu kwa kujaribu kumsaidia" Zalabain aliongea kwa msisitizo.
"Ndiyo nimeshakutambua tangu unajitokeza pia sipo kwa ajili ya kumsaidia dhalim kama yule bali nipo kwa ajili ya kumsaidia Buruhan ili asiondokewe na nguzo zake zote, kiufupi ni hivi nazuia usimuue yule mziwanda wake asiye na hatia" Mzee Mahmud alimuambia huku akijiamini halafu akameza mate kidogo kisha akaendelea, "Shafii ni haki yake kwa alichokifanya ila Ally hana hatia yoyote na usimuingize katika orodha hiyo, pia ningependa mumponyeshe sikio lske na taya lake ambayo mumjeruhi kutokana na kujaribu kuleta kile kitakachoyafanya majini ya marehemu Hamis yafanye kazi. Ukumbuke pia  yeye anachukia ulilofanyiwa ila mali yako anayoimiliki Shafii ndiyo inamfanya ashindwe kufanya jambo lolote, usihukumu yule asiye na hatia kama ni ufalme utapewa pasipo yeye kupoteza uhai wake".
"unasema nini wewe?" Zalabain alimuuliza Mzee Mahmud
"kama ulivyosikia ewe mwana wa jini, ukumbuke mimi nilikataa kutengeneza uchawi kama uliomtapisha mama yako jana kwasababu najua siyo haki kufanya hivyo, pia niligoma kufanya dawa ya kumuua baba yako ili mama yako awe chini ya mwingine kwasababu najua haikuwa haki. Pia utambue nakuambia usimuue Ally kwasababu najua utakuwa hutendi haki ewe mwanajini kamuuulize ibin Zultash atakueleza, mwisho kabisa nakuambia hivi upotee sasa hivi kuna mtu anaingia humu msalani sasa hivi asije akaniona naongea peke yangu kama kichaa wakati nina akili  zangu timamu" Mzee Buruhan aliongea kisha akageuka nyuma akaingia chooni bila kujali kama Zalabain ameondoka au yupo, baada ya kumaliza haja zake  alitoka hakumkuta Zalabain na akarudi kule alipokuwa yupo awali. Alimkuta mzee Buruhan yupo na Ally wakiongea na iilonekana Ally alikuwa kapona kabisa tatizo la kuvunjika taya na sikio kwani hakuwa mwenye kuweza kuzungumza wala kusikia, lakini hapo alikuwa akizungumza na kusikia vizuri kabisa.
Mzee Mahmud alimuonesha ishara ya kumsalimia Ally kama ilivyokuwa akifanyiwa kwa kutoweza kusikia vizuri lakini.
"Mzee mwenzangu anaongea huyu na kusikia sasa hivi usimsabahi kama vile unamsabahi bubu" Mzee Buruhan alimuambia rafiki yake.
"Yapaswa  tumshukuru Mungu basi mzee wangu maana huu muujiza tosha" Mzee Mahmud aliongea akionekana kufurahishwa na suala hilo.
"Alhamdililah" Ally na baba yake waliitikia kwa pamoja.
Mzee Mahmud alibaki kutabasamu tu kila alipomuangalia Ally kwa kufurahishwa na usikivu alionao Zalabain baada ya kufanya kile alichomuambia, tabasamu lake lilifanya Mzee Buruhan na Ally nao watabasamu  wakijua kafurahishwa na hali ya Ally kutengemaa.
"Ally hebu sogea karibu" Mzee Mahmud alimuambia Ally  huku akimtazama kwa umakini, Ally alimsogelea Mzee Mahmud pasipo kujua ni kipi alichokuwa anataka kufanyiwa kwani alimzoea sana mzee Mahmud na alimchukulia kama baba yake tu. Alipomsogelea Mzee Mahmud aliambiwa achuchumae mbele yake naye akatii amri kama alivyoambiwa, mzee Mahmud alimshika kichwani na akamtamka maneno yasiyoeleweka na kusababisha Ally ashtuke halafu aangalie mazingira ya hapo yalivyo halafu akaenda kukaa kwenye dawati pembeni ya baba yake alipokaa awali.
"Baba hivi hapa tupo kwa ajili gani?" Ally aliuliza tu baada ya kukaa pembeni ya baba yake akionekana kutotambua yupo hapo kwa ajili gani.
"Kha! We Ally maswali gani hayo hutambui kama tupo hapa kumuangalia kaka yako kalazwa tangu jana" Mzee Buruhan alimuambia Ally akionekana kutoelewa kitu alichofanyiwa na  mzee Mahmud hadi akasahau  yupo pale kwa lengo gani wakati alipoingia tu aliulizia hali ya kaka yake.
"Khaa! Kumbe tupo hapa kwa ajili ya kumuangalia firauni huyo, sina muda huo muache afe  maana huyo ni zaidi ya shetani" Ally aliongea maneno ambayo yalizidi kumshangaza sana Mzee Buruhan na akajikuta  akimtazama  mzee Mahmud akionekana kutoelewa kafanya nini, Ally alinyanyuka ili aondoke lakini mzee Mahmud alimuita akamuomba aketi akakaa chini.
"Ally tambua undugu ni kovu na halifutiki usifanye hivyo, najua unaumia kwa kile alichokifanya kaka yako lakini kumbuka ndugu ni ndugu tu" Mzee Mahmud aliongea kwa ustarabu wa hali ya juu akitegemea ataeleweka na Ally lakini haikuwa hivyo.
"Baba zangu mngejua alichokifanya huyo firauni mnayekuja kumuangalua wala msingethubutu kukaa hapa, na sijui hata ni kwasababu gani nilikuwa nikimpenda kwa kipindi chote hicho nahisi aliniroga yule maana miale ya mkufu wake sielewi hata imemifanyaje wakati nilikuwa nikimchukia" Ally aliongea  huku akionesha kumchukia  kaka yake.
"Ally unaongea nini wewe?" Mzee Buruhan aliuliza akionekana kushangaza na maneno anayoyaongea mwanae.
"Mzee mwenzangu kama nilivyokuambia hili tatizo linajulikana ila huyu hatakiwi kulisema na akilisema atakuwa kiziwi kama mwanzo muache huyo Shafii aeleze kila kitu. Unajua..." Mzee Mahmud aliongea maneno yaliyomfanya Mzee Mahmud atulie kimya na alishindwa kumalizia kauli yake baada ya mke wa Hamis kurudi akiwa amebeba chombo cha chakula kwenye mfuko wake.
"Vipi mgonjwa jamani tayari ameshaamka?" Mke wa Hamis aliongea baada tu ya kuwasili na alimuonesha Ally tabasamu kisha akampa mkono akampa mkono ili amsalimie akijua kuwa Ally hawezi kuongea.
Ally hakuupokea mkono wa Mke wa Hamis zaidi ya kusonya kwa nguvu kisha akanyanyuka akasema, "shetani jike mkubwa wewe".
Ally alinyanyuka kwenye dawati la kusubiri wagonjwa akaelekea mahali akimuacha wazee wake na mke wa Hamis wakimshangaa sana, mke wa Hamis alipotaka kumfuata nje Mzee Buruhan alimshika akamzuia.
"Salma mama naomba unisikilize kwa umakini, achana na Ally kwa sasa kaa hapo usubiri muda wa kumuona mgoniwa akizinduka tukamuone" Mzew Buruhan alimuambia Salma mke wa Hamis.
"Lakini Ally kapatwa na nini wazee wangu kwani alikuwa hawezi kuongea na kusikia ila sasa hivi anaongea na kusikia  ila amekuwa kama akili haziko sawa hadi ananisonya mimi" Salma aliongea huku akishangazwa na hali ya Ally yule aliyekuwa anamsikiliza na kumtii na kumuheshimu ameamua kuonesha dharau.
"Hebu mama kuwa muelewa achana na habari za Ally sasa hivi, tufikirie kuhusu mgonjwa tu" Mzee Mahmud aliongea kwa msisitizo huku  akionekana kutopendezwa na maneno ya Salma.
"Sawa baba zangu nimewaelewa" Salma alijibu kwa shingo upande ili tu asiwaudhi  wazee ambao anawaheshimu.


****

 Wakati Ally akifunguliwa na kuanza kumuoneshea dharau upande wa himaya ya Majichungu Zalabain ndiyo alikuwa amerejea muda huo na aliamua kupitia chumbani walipo mama yake na dada yake ili awaone kutokana na upendo alionao kwao, alibisha hodi kwa adabu ingawa alitambua hata akiingia muda huo asingewakuta wakiwa bila stara. Alipokaribishwa aliingia kwa adabu  na akaenda hadi walipokuwa wamekaa kitandani na akawasalimia, halafu naye  akaketi kitandani jirani yao.
"Mwanangu kila nikikutazama namuona baba yako kwa jinsi wote mlivyokuwa na sura zilizofanana, haya niambie unatoka wapi?" Bi Farida aliongea kisha akamuuliza Zalabain.
"Nilikuwa Tanga kwenye  hospitali ya SBN nilienda kuongea na mzee Mahmud" Zalabain alimuambia mama yake.
"Mh! Huyo mzee huko hospitalini anafanya nini?" Bi Farida aliuliza.
"Amekuja kumuangalia mumeo amelazwa" Zalabain alimuambia mama yake.
"Jamadin sina mume kama huyo mimi tena sitaki kumsikia ukimtaja, mume aliyetakiwa kunioa mimi ni Faimu tu na sijui ilitokea nini mpaka nikamkana na nikamsababishia matatizo makubwa sana akahama kijijini akiwaacha jamaa zake. Nampenda Faimu na natamani nimuone hata leo ili nimuombe msamaha maana yeye ndiyo kila kitu kwangu" Bibi Farida aliongea na  mwishowe akalia kutokana na kujutia aliyoyafanya ya hapa zamani, Zalabain ilimbidi amkumbatie mama yake ambembeleze kutokana na upendo alionao kwake.
"Samahani mama kwa kukupa taarifa smbayo hutaki kuisikia,  sipendi uhuzunike nakupenda sana" Zalabain alimuambia mama yake baada ya kunyamaza.
"Nakupenda pia mwanangu" Bi Farida alisema huku akitabasamu kwa mbali, waliendelea kuongea maongezi mengine kwa furaha wakiachana na suala ambalo lilionekana kutomfurahisha kabisa Bi Farida.


****


 Baada ya masaa mawili Shafii aliamka kutoka usingizini akiwa yupo vizuri kiafya kuliko awali, hali yake iliendelea kutengemaa na ilipofika muda wa alasiri aliruhusiwa na daktari na alirudi nyumbani akiwa ameongozana ns wote waliokuja  kumuona hospitali kasoro Ally tu ambaye hakurudi tangu aondoke pale hospitali. Shafii alipelekwa moja kwa moja chumbani kwake na akaachwa apumzike na kisha wazee wake wakakaa sebuleni hadi ilipoingia jioni ndiyo mzee Buruhan na mzee Mahmud waliingia chumbani kwa Shafii wakamkuta akiwa ameamka ameegemea mito kitandani kwake,  Shafii alipoona ujio wa wazee wale alihisi kuna jambo ila alikaa kimya ili apate uhakika wa wasiwasi wake.
"Shafii" Mzee Buruhan alimuita
"Naam Baba" Shafii aliitikia
"unajua kama wewe ndiyo nguzo kuu kati ya nguzo zangu nne zilizobakia?" Mzee Buruhan alimuuliza
"nafahamu hilo baba" Shafii alijibu.
"Hussein hatunaye, Hamid hatunaye, Hassan ni mdogo kwako, Falzal ni mdogo kwako na Ally pia ni mdogo kwako. Wewe pekee ndiyo mkubwa ndiyo kiongozi wao ingawa wote wana maisha yao na hata wanajisomesha wakitaka kujiendeleza kielimu. Nadhani unatambua hilo" Mzee Buruhan alisema.
"Ndiyo baba natambua hilo" Shafii alijibu.
"Sasa basi inapotokea tatizo lenye kuhitaji kuelezewa ili lisizidi zaidi inabidi lielezewe mwanangu ikiwa utakaa kimya haitasaidia chochote" Mzee Buruhan aliongea.
"Baba sijakuelewa unachomaanisha" Shafii aliongea.
"Shafii najua unatambua suala la upotevu wa mke wako na hata mwanao linalokufanya uwe na matatizo kila kukicha, sasa mwanangu ukilificha itakusaidia nini ikiwa unalifahamu chanzo chake. Kumbuka mficha maradhi kifo humuumbua mwanangu, mwanangu ni bora uitoe aibu mbele ya daktari ili utibiwe kuliko kuficha tatizo halafu ufe na ugonjwa. Ongea chanzo cha  haya ni nini?" Mzee Buruhan alimsihi mwanae.
"Baba kusema ukweli sijui wala sitambui suala hili linasababishwa na nini?" Shafii alikataa.
"Shafii vuta kumbukumbu zako vizuri umefanya nini mpaka yote haya yatokee au hutaki  familia yako uione tena ikiwa na upendo" Mzee Buruhan alizidi kumsihi.
"Baba napenda sana familia niione tena ikiwa ina upendo lakini sikukumbuki chochote kilichosababisha haya ninayofanyiwa"  Shafii alikana kabisa juu ya suala hilo.
"Jirani na mashine ya kusaga unga kule Mpirani miaka ishirini na moja iliyopita unakumbuka kilitokea nini pale kwenye  nyumba yako uliyokuwa unaishi  baada ya wewe kuhama tena ilikuwa majira ya saa sita usiku?" Mzee Mahmud aliongea kwa mara ya kwanza na kumfanya Shafii ashtuke kwa jambo alilotajiwa, lilikuwa ni jambo ambalo alishalisahau kabisa katika ubongo wake na sasa alikumbushwa na mzee huyu ambaye ni mganga mtaalam.
"Shafiii unakumbuka nini hiyo siku" Mzee Buruhan naye aliunganisha maelezo ya rafiki yake ingawa hakuyaelewa kabisa, maneno ya mzee  Mahmud  yalimfanya anyamaze ghafla huku akiwa ameinamisha kichwa chake chini.
"Shafii si nakuuliza" Mzes Buruhan aliongea huku akimtikisa bega baada ya kuona yupo kimya, Shafii alikurupuka baada ya  kutikiswa bega kama alikuwa yupo  katika usingizi mzito.
"Ha..hapana  si....sikumbuki chochote" Shafii aliongea kwa kubabaika baada ya kuhisi moja ya jambo baya alilolifanya linakaribia kugundulika.
"Una uhakika?" Mzee Mahmud aliuliza.
"ndiyo baba zangu nina uhakika wa kile ninachokiongea" Shafii alijikaza akajibu kwa kujiamini.
"mzee mwenzangu sisi twende tukanywe kahawa si unaona muda huu na kiubaridi cha kipupwe kimeanza, Shafii kama hujui juu  ya hilo basi inakupasa utambue kuwa maisha ya mkeo  na binti yako yapo kwenye kinywa chako kueleza unachojua na ukikaa kimya jua kinachofuata ni kama kilichowapata wadogo zako ia utambue umebaki peke yako" Mzee  Mahmud huku akiwa tayari amesimama na Mzee Buruhan naye akasimama, wote kwa pamoja walianza kutembea kuelekea ulipo  mlango ili waondoke lakini sauti ya Shafii ikiwaita iliwafanya wasimame na kugeuka wakamtazama.
"Nipo tayari kuwaambia kilichotokea wazee wangu naomba mnisaidie" Shafii aliongea baada ya kuona maji yamemfika shingoni na maneno ya mzee Mahmud ndiyo kabisa yalimfanya akubali. Mzee Mahmud alimtazama Shafii kwa tabasamu hafifu halafu akamuambia, "kesho muda kama huu pale ulipokuwa unaishi kule mpirani ndiyo kutakupa ahueni ya  tatizo lakokwa familia yako"
Mzee Mahmud aliposema maneno hayo alitoka humo ndani bila hata kumuangalia Shafii kwa mara nyingine, Mzee Buruhan naye alifuata akiwa nyuma yake.


****


Maneno ya Ally baada tu ya kupewa mkono na Salma yalimfanya Salma karibia siku nzima akiwa anajifikiria kwani Ally alikuwa amepatwa na nini mpaka awe vile, ilipofika jioni aliamua kutoka na kwenda kumtafuta Ally bila ya kumueleza mtu ili aongee naye tu kwani Ally alikuwa ni mmoja kati ya wanaume aliokuwa anawapenda na kipindi cha nyuma alipokuwa msichana alishajaribu kujivika ujasiri na kumueleza Ally yaliyo moyoni mwake lakini aliishia kukataliwa baada ya Ally kuwa anamuheshimu sana Hamis ambaye alikuwa na mahusiano na Salma kabla hajamuoa. Baada ya mpango ambao ndiyo chanzo cha balaa lote lililowakumba watoto wa  mzee Buruhan, Ally alifungwa akili na akawa anasikiliza wote waliofanya mpango ule bila hata kuwapinga na alifungwa akili baada ya kuujua mpango huo akawa  amekasirishwa nao. Baada ya kufungwa akili ndipo Salma alipompata Ally kutokana na yeye pia ni mmoja kati ya watu walioshiriki huo mpango, alimtumia Ally vyovyote atakavyo baada ya Ally kutopinga kauli yake. Sasa akili ya Ally ilipofunguliwa na Mzee Mahmud na Salma kujibiwa vile alijikuta roho ikimuuma akijua Ally amepatwa na tatizo hivyo  aliamua kumtafuta.  Hakukujua kama Ally wa leo siyo wa jana alichokuwa anakijali yeye ni penzi lake  haramu alilolianzisha kwa Ally hata alipokuwa yupo ndani ya ndoa.
Tamaa za kutamani kingine wakati akiwa tayari ana kingine mkononi ndiyo zilimfanya Salma afanye jambo hilo ambalo lilipelekea afiche siri nzito sana ambayo laiti ingaligundulika mapema basi angekuwa ameleta matatizo makubwa sana kwa Hamis na Ally.
Juhudi za Salma kumtafuta Ally ziliendelea kwa usiku huo akiwa yupo ndani ya gari yake na hatimaye alimkuta akiwa amekaa kwenye matairi yaliyochimbiwa katika uwanja wa mpira  uliopo mkabala na shule ya sekondari ya Usagara, Salma alimfuata hadi hapo akaegesha gari pembeni kisha akashuka akaenda kumkumbatia Ally akitegemea atapokelewa lakini alijikuta akisukumwa hadi akaanguka chini akaumia.
"Kaa mbali na mimi malaya wewe!" Ally alimuambia kwa ukali.
"Lakini Ally mpenzi wangu nimefanyaje?" Salma aliuliza kwa masikitiko makubwa huku akionekana kuumia baada ya kusukumwa.
"Unajifanya hujui siyo tena usiniite mpenzi wako kuanzia hivi sasa, we wa kunifanya mimi mtumwa wa ngono hadi umesababisha nisioe wakati natakiwa kuwa na familia sasa hivi" Ally alifoka.
"Ally nakupenda ndiyo maana nimefanya hivyo hadi nikazaa na wewe" Salma akaongea huku akilia.
"Weee tena ishia hapo hapo" Ally alimkaripia huku akimuongeza teke la mguu Salma.
"Ally nikatae ila ukae ukijua Hamida siyo mtoto wa mume wangu bali ni damu yako, ndiyo maana hata alipozaliwa kaka yako alikutania umefanana naye miguu ila ukweli ile ni damu yako kabisa" Salma aliongea huku akilia, Ally alipuuza maneno ya Salma akaondoka eneo akimuacha akilia ingawa kuna jambo lilikuwa likiisumbua akili baada ya kusikia maneno hayo.




ITAENDELEA!1

Sunday, November 29, 2015

KOSA SEHEMU YA KUMI NA MBILI

RIWAYA: KOSA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA

SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE



 ILIPOISHIA

Tuliendelea na zoezi letu kwa mara ya pili huku nikivua shati langu na Sarina akivua nguo yake ya juu, tulijikuta tukibaki na nguo za ndani pekee na joto lilikuwa kali sana. Kupunguza joto ilinidi niende nikawashe feni la hapo ukumbini, upande ulipo feni ilibidi nimpe mgongo wakati naenda kuliwasha kwani swichi y

DHAHAMA SEHEMU YA KUMI NA MBILI

RIWAYA: DHAHAMA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE


SEHEMU YA KUMI NA MBILI!!
"Asante  kiongozi wetu, mimi hapa
naungana na wazo alilolitoa mkuu wa majeshi la kwenda kuharibu utengenezwaji wa hao wadudu kwani sote tunatambua kwamba Dainun mpya imeibiwa na mpaka ije kupatikana hatujui

Saturday, November 28, 2015

KOSA SEHEMU YA KUMI NA MOJA

 KOSA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA

SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE



 ILIPOISHIA
Sauti ya yule mtu iliniambia, nilikuwa nikimsikiliza kwa umakini huku nikiuendea ule mzigo hadi nikaufikia bila hata kumuangalia Sarina aliyekuwa ananitazama kwa umakini.
"fungua mzigo sasa usiutazame tu" niliambiwa na mimi nikatii nikaufungua mzigo huo ambao uliniacha nikiwa nimepigwa na bumbuwazi kwa kile nilichokiona, hata Sarina naye alipigwa na bumbuwazi kwa alichokiona ndani ya boksi hilo.

DHAHAMA SEHEMU YA KUMI NA MOJA


 DHAHAMA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE



SEHEMU YA KUMI NA MOJA!!
"haina haja ya kuhuzunika mzee mwenzangu bali inabidi uwalaumu wanao na janga hili mzee mwenzangu limeanzwa na wao na sasa mwenzao wanalimaliza" Mzee Mahmud aliongea kisha akanywa kahawa funda moja bila hata kumtilia maanani Mzee Burhan aliyeonekana kutoielewa kauli hiyo.

MFAHAMU PROFESSA GABRIEL RUHUMBIKA


PROFESSA GABRIEL RUHUMBIKA

    Nadhani kwa wale ambao hawakusoma fasihi jina hili litakuwa ni jina geni sana kwenu, ila si mgeni sana ndani ya ulimwengu huu wa fasihi ya kitanzania. Ni mmoja wa wanafasihi maarufu sana ndani ya nchi ya Tanzania na pia mmoja wa wasomi wakubwa sana katika somo la fasihi Afrika na hata duniani kwa ujumla, ameandika kazi nyingi za kifasihi katika lugha ya kiswahili na kingereza.

Friday, November 27, 2015

KOSA SEHEMU YA KUMI

RIWAYA: KOSA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA

SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE



 ILIPOISHIA


Huwaida baada ya kufunguliwa alinifuata kwa kasi huku akiniita mwanaharamu, aliponikaribia alinipiga kibao kikali  halafu akaokota chuma kizito akiwa anahema. Alikinyanyua kila chuma akawa ananielekezea usoni ili anipigae nacho, alikinyanyua kisha akakishusha kwa nguvu. Nilibaki nikifumba macho huku nikisubiri hukumu yangu kwa Huwaida kwa kitendo nilichomfanyia, nilijiona sina thamani tena ya kuendelea kuishi ikiwa yeye anaonesha dhahiri ananichukia na hataki hata kuiona sura yangu kuanzi

DHAHAMA SEHEMU YA KUMI

DHAHAMA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE





SEHEMU YA KUMI!!
Laiti kama wanadamu tungalipewa uwezo wa kuona yaliyojificha katika mioyo ya wenzetu basi Bi

Thursday, November 26, 2015

KOSA SEHEMU YA TISA

 KOSA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA

SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE



 ILIPOISHIA


Nurulayt alizidi kuniambia maelezo ambayo yaliniacha kinywa wazi, Faiz huyu ninayemjua mimi kusikia ni muuaji na jambazi mkubwa.
"Nuru kwahiyo wewe ulikuwa unaishi Afrika ya kusini?" Nlimuuliza Nurulayt ili nipate maelezo yake kiupana zaidi.
"hapana sikuwa naishi Afrika ya kusini ila nilikuwa naenda kumtembelea kaka tu mara chache na hata hiyo siku aliyouawa nilikuwa nilikuwa nimekuja kumsalimia na ndiyo siku hiyo Faiz  akapiga

DHAHAMA SEHEMU YA TISA

 DHAHAMA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE


SEHEMU YA TISA!!
Kilikuwa kimetawaliwa na jazba miongoni mwa watu waliomo humo ndani, kiongozi wa watu

Wednesday, November 25, 2015

KOSA SEHEMU YA NANE

(SASA INAPATIKANA KATIKA ORODHA YA VITABU VYA AMAZON/ NOW AVAILABLE INA THE AMAZON'S BOOK LIST)




 KOSA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA

SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE



 ILIPOISHIA


"hapo upo poa kabisa yaani kama unaenda kunipora tunda vile" Faiz aliongea huku akitia masihara.

DHAHAMA SEHEMU YA NANE

TANGAZO! TANGAZO!

Bado nawathamini wasomaji wangu popoote mlipo, kuonesha kuwathamini kwangu nimeamua kuingiza kitabu cha kielektroniki cha Dhahama katika mtandao wa kimataifa wa Amazon. Wale waliopo mbali na nchi ya Tanzania na wanakihitaji kitabu hiki waweze kukisoma wanaweza kukinunua huko kwa gharama nafuu kabisa iliyoorodheshwa hapo. Kitu cha kufanya ni kuingia amazon.com halafu search Dhahama utakipata hapo, kukisoma ni vizuri ukawa na app ya kufungua ebook kwa wale watumiaji wa smartphone utaipata ndani ya playstore.

NI HAYO TU

Tuesday, November 24, 2015

KOSA SEHEMU YA SABA




 KOSA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA

SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE

DHAHAMA SEHEMU YA SABA

DHAHAMA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGIN

Monday, November 23, 2015

KOSA SEHEMU YA SITA







     KOSA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA

SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE



 ILIPOISHIA


"sentir en casa(jisikie upo nyumbani)" Yule msichana aliniambia huku tukikaa kwenye kochi kwa kupakatana ambapo yeye alikuwa juu mimi chini.
"gracius(asante)" nilimjibu huku nikiwa nimekamata kiuno chake sawia akiwa juu ya mapaja yangu
"delante de Daniella nada imposible sentir en casa querido(mbele ya Daniella hakuna kinachoshindikana jisikia upo nyumbani mpendwa)" Daniella aliniambia kisha akawaambia walinzi wake,"salir(ondoka)".

DHAHAMA SEHEMU YA SITA




 DHAHAMA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGIN



SEHEMU YA SITA!!
Alikiweka kile chombo  mbele ya Shafii kisha akamwaga dawa zake kwenye moto uliomo kwenye chombo hicho, moshi mzito ulitanda humo ndani na mzee Sauti ya radi akawa anaimba nyimbo zisizoeleweka huku akimzunguka Shafii akicheza kama anacheza ngoma ya kikabila. Moshi huo ulipokuja kupungua Mganga akiendelea kucheza alihisi anashikwa kiuno wakati akicheza, moshi ulipoisha alihisi anashikwa makalio kwa kutomaswa. Alipogeula nyuma kumuangalia anayemshika alikutana uso kwa uso na Zalabain akiwa anatabasamu.

Sehemu Ya 4

NDIYO IKAFIKIA HAPA

Meza Ya Uchoraji - Sehemu Ya 3



NDIYO KAFIKIA HATUA HII

Meza Ya Uchoraji - Sehemu Ya 2

BADO MTAALAMU WETU ANAENDELEA NA KAZI YAKE

Meza Ya Uchoraji - Sehemu Ya 1

KUTANA NA PENCIL MASTER MWENYE KIPAJI ADIMU NCHINI TANZANIA



Mwanzo

Sunday, November 22, 2015

KOSA SEHEMU YA TANO

     


              KOSA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA

SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE

DHAHAMA SEHEMU YA TANO

 DHAHAMA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGIN

Saturday, November 21, 2015

KOSA SEHEMU YA NNE




                 
        KOSA

MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA

SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE



 ILIPOISHIA


"haya haraka sana fungeni hiyo diary nimewaambia" Ilisikika sauti  ya mwanamke kutoka mlangoni ikiwapa amri Hassan na Hussein.

DHAHAMA SEHEMU YA NNE




                             DHAHAMA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGIN



SEHEMU YA NNE!!
"Afande tumefanya juhudi za kuuzima huu moto kwa kutumia  kila njia ila imeshindikana hadi maji yanaisha hatukuweza kuuzima na ikatubidi tutumie gesi lakini bado tumeshindwa kuuzima na inasadikika Mkuu wa idara ya sheria makao makuu ya kampuni hizi yupo ndani ya nyumba ya tatu na hajatoka hadi muda huu na hata tulipofika tulikuwa tukisikia kelele za mtu akiomba msaada lakini sasa hazisikiki" Mmoja wa maaskari wa zimamoto aliongea kwa ufupi juu ya tukio hilo la kuungua kwa nyumba hizo, James aliposikia maelezo hayo alipiga kelele huku akiita, "Babaa!". Aliwapita askari wa kikosi cha zimamoto akakimbia kuelekea ulipo moto katika nyumba ya tatu ya kampuni, maaskari wote walianza kumkimbiza ili wamuwahi asiingie ndani ya moto huo kutokana na ukali wake.

DHAHAMA SEHEMU YA TATU

MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE



SEHEMU YA TATU!!
Asp John aliyanakili maelezo ya James kisha akajiandaa kuuliza swali jingine lakini king'ora cha gari la zima moto kilimkatisha na akajikuta akiangalia lilipo gari la zima moto. Wale vijana nao waliliona lile gari la zimamoto likipita pembezoni mwa eneo la tukio kwa tabu kisha likaingia barabarani kisha likaingia barabarani likawa linaelekea Duga Maforoni kwa mwendo wa kasi sana huku milio ya ving'ora vyake ikiwa imetawala njia nzima. Asp John alipoona hali hiyo alihisi kuna jambo na akawa anataka kujua kuna nini kilichotokea, alinyanyua simu ya upepo akaongea kwa muda kisha akatulia akasikiliza upande wa pili na akajikuta amegwaya.
"nyumba za kampuni yenu zilizokuwa zinazinduliwa zote zimeungua kwa moto  wa hitilafu ya umeme" Asp John aliwaambia wale vijana.
"eti nini?" James alisema kwa mshangao.

KOSA SEHEMU YA TATU


   KOSA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA

SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE



 ILIPOISHIA

"dah! Halafu kweli, kwani saa ngapi?" Hassan aliuliza.
"saa kumi kasoro hii tuwahi graundi kama vipi?" Hussein aliongea huku akiiweka shajara kwenye meza,  wote kwa pamoja walichukua vifaa vya mazoezi kisha wakaondoka kuelekea uwanjani. Vijana hawa mpira wa miguu ndiyo ilikuwa burudani yao kuu na waliupenda sana, mapenzi  yao kwenye mpira wa miguu yalijulikana hata kwa baba yao na ndiye aliyewapa moyo wa kuendelea kuonesha kipaji chao kandanda. Mpira wa miguu kwao ilikuwa kama ni mchezo uliwapa umaarufu chuoni kwao na hata mtaa wanapoishi..


Thursday, November 19, 2015

KOSA SEHEMU YA PILI








    KOSA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA

SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE



 ILIPOISHIA
 Walijumuika naye mezani hapo huku wakimtazama sana usoni.
"hivi baba yale ni matukio ya kweli?!" Hussein aliuliza.
"kwa sasa siwezi kuwajibu  mpaka mmalize  kusoma yote" Baba yao aliwajibu.
"ni kisa chenye kuvutia sana" Hassan aliongea akiwa na tabasamu usoni hata kile kilio chake kilichokuwa kinamsumbua sana alikisahau kutokana na kuvutiwa na ukurasa  wa kwanza wa maelezo yaliyomo ndani ya Shajara ya baba yake.
"malizeni kula kwanza ndiyo mengine yatafuata, kama kuongea basi ongeeni mkimaliza kula" Baba yao aliwaambia.

DHAHAMA SEHEMU YA PILI









DHAHAMA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE



 SEHEMU YA PILI!!
"we mwanaharamu wewe simamisha gari nishuke sio kuongeza mwendo" Yule mwanamke alizidi kufoka baada ya kuona mwendo wa gari unazidi kuwa mkali, dereva hakumjibu yule yeye alitoka kwenye usukani akasimama kisha akawaangalia wafanyakazi wa idara nzima akiwa na hofu.
"si mimi ninayeendesha jamani gari linaenda lenyewe hili hebu oneni" Dereva aliongea huku akiwaonesha wafanyakazi wote jinsi usukani ulivyokuwa unajiongoza wenyewe, wafanyakazi wote walipoona hicho kioja walijikuta wakijaribu kutoka nje lakini walishindwa kwani milango haikufunguka na vioo vyote vilijifunga ghafla hata vile vilivyokuwa wazi vyote vilijifunga. Wafanyakazi wote walijaribu kupiga vioo ili wavunje lakini walishindwa kwani vioo vilikuwa vigumu sana, gari nayo ilizidi kuongezeka mwendo hadi ikawa kama ipo kwenye mashindano.