Wednesday, December 9, 2015

SHUJAA SEHEMU YA TANO

RIWAYA: SHUJAA

MTUNZI: Hassan O Mambosasa

SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843

SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE

ANGALIZO: UANDISHI WA SEHEMU HII YA TANO UMETUMIA LUGHA KIGENI KWENYE BAADHI YA SEHEMU HASA KATIKA UELEZAJI WA MTAALA WA KEMIA KWA KIDATO CHA SITA KUTOKANA NA UGUMU WA KUFASIRI LUGHA YA SAYANSI

ILIPOISHIA
Alitembea
kwa tahadhari hadi katikati ya miti iliyo jirani na
eneo hilo akiwa na kamera yake ya kipelelezi tofauti
na kamera yake ya kawaida. Ajibanza
hapo hadi aliposhudia ujio wa boti mfano wa
nyambizi iliyofika hadi ukingoni, hadi hapo aliweza
kupiga
picha kila anachokiona kwa msaada wa mwangaza
uliotoka katika taa ya helikopta na taa ya boti. Hadi
watu sita wanashuka kwenye boti ile alikuwa
amewaona na amewapiga picha, boti hiyo pia
alikuwa ameiona na ameipiga picha pia na helikopta
aliipiga vizuri akilenga namba zake zilizopo ubavuni.
Alipomaliza alibaki palepale hadi walipoingia ndani
ya helikopta kuondoka, na ile boti ilipozama chini.
Hapo alirudi kwenye hema kisha akajilaza pembeni
ya msimamizi wake kama ilivyokuwa awali. Hadi
asubuhi inaingia alikuwa macho na jua
lilipochomoza alikusanya vitu vyake kisha
akaondoka porini hapo akiwa na msaidizi aliyepewa

ENDELEA NAYO ILI KUPATA UHONDO ULIOMO NDANI
YAKE

SEHEMU YA TANO
Alifika kisha akakabidhi kila kitu alichokabidhiwa na
ofisi za pori hilo halafu akakodi gari ya kumpeleka
bukoba mjini, uzuri wa hifadhi ya Biharamulo ilikuwa
ina magari ya kukodiwa maalum kwa ajili ya wateja
wao. Norbert alipata gari aina ya landcruiser yenye
mkonga ambayo iliwekwa hapo mahususi kwa
ajili ya kukodiwa, alielewana bei na dereva wa gari
hilo kutoka hapo hadi Bukoba mjini. Baada ya
makubaliano kufikiwa alipanda gari hiyo kisha safari
ikaanza, kwa kuelekea barabara iendayo kaskazini
mwa Biharamulo ili kuisaka Bukoba, ubora wa gari
aliyoikodi kwa masafa marefu ulimfanya awe na
uhakika wa kuwasili Bukoba ndani ya masaa kadhaa.
Pia dereva wa gari naye alijua sana kucheza na
usukani wa gari pamoja na kupangua gia, uhodari
wa dereva huyu ulimfanya Norbert atabasamu na
akijipongeza kwa chaguo lake bora miongoni mwa
madereva wengi aliowakuta jirani na ofisi za hifadhi
ya Biharamulo, walitumia masaa kadhaa wakawa
wameshafika mwanzo wa barabara ya Uganda
inayoeleiea Bukoba mjini. Dereva wa gari hilo alipita
kushoto ili azunguke mzunguko unaounganisha
barabara anatoka na barabara iendayo Bukoba mjini,
aliingia kushoto kuishika barabara hiyo kwa
mwendo wa wastani kisha akaongeza mwendo
baada ya kuingia rasmi katika barabara ya Uganda.
Hakika alimpata dereva aijuaye barabara za mkoa
huo kiundani zaidi kutokana na kuwa mwenyeji wa
mkoa huo. Dereva huyu alinyoosha barabara hiyo ya
Uganda hadi alipofika mwanzo wa barabara ya
Kawawa kisha akangia kushoto kuifuata barabara ya
Kawawa kuelekea mtaa wa Biashara kwenye
barabara ya biashara, aliingia katika barabara ya
Biashara kwa mwendo hadi katika kona ya barabara
iendayo makutano ya barabara ya sokoine ,hapo
alikata kona upande wa kulia kuelekea yalipo
makutano ya barabara hiyo na ya Sokoine. Alipofika
makutano ya barabara za Sokoine na Jamhuri
alinyoosha moja kwa moja kuifuata barabara ya
Jamhuri kwa mwendo wa kasi hadi yalipo makutano
ya Barabara ya Barongo na Jamhuri, hapo
alipunguza mwendo kisha akavuka makutano hayo
kwa mwendo wa wastani halafu akanyoosha moja
kwa moja kuifuata tena barabara ya Jamhuri hadi
zilipo ofisi za CCM hapo aliegesha gari kisha
akateremka akimuacha Norbert ndani ya gari .
Alirudi baada ya dakika kadhaa akiwa na pakiti ya
konyagi akiinywa mdomoni kisha akapanda kwa ajili
ya kuliondoa gari eneo hilo.

"kaka hiyo si pombe na unaendesha gari, hivi si
hatari hiyo?" Norbert alimuuliza

"usijali kaka kuhusu hii kwani bila hii mimi siwezi
kuendeshagari vizuri" Dereva alijibu huku akiweka
gia kuingia barabarani

"ok ni sawa tu tuendelee na safari" Norbert aliongea
kwa mara ya mwisho kisha akakaa kimya kumuacha
dereva aendelee na kazi yake . Dereva aliendelea na
makeke yake ya kuendesha gari huku mkono mmoja
akinywa kipakiti cha konyagi hadi akakimaliza,
alinyoosha barabara ya Jamhuri hadi katika
makutano ya barabara hiyo na barabara ya
Aerodrome.
Alinyoosha barabara hiyo hadi karibu na uwanja wa
ndege wa bukoba kisha akaweka gari pembeni
baada ya kupokea amri kutoka kwa Norbert, Norbert
alishuka hapo kisha akampatia malipo dereva huyo
kama walivyokubaliana. Dereva wa gari aligeuza
kisha akaondoka eneo hilo na Norbert akaelekea katika
ofisi za uwanja wa ndege wa Bukoba kwa miguu.
Baada ya muda mfupi alifika ofisi za uwanja wa
ndege huo kisha akaenda hadi mapokezi. Hapo
mapokezi alimkuta msichana aliyekuwa akiongea na
mgeni, alisubiri hadi alipomaliza kuongea na mgeni
ambaye alionekana ni mteja kisha akamfuata katika
dawati la mapokezi. Alimshika kidevu kwa namna ya
uchokozi.

"we mwanaume wewe naona umetoka kwa mke
mwenzangu" Msichana wa mapokezi alianza
kumtania Norbert pasipo salamu baada ya
kuchezewa kidevu

"aah! bibie mi kijana sasa ulitaka niende wapi"
Nobert aliongea kwa sauti ndogo huku akiwa
ameegemea meza.

"khaa! Yaani umeniacha mimi unaenda kwa bibi
mwingine, muone hutulii kama jogoo" Msichana wa
mapokezi akiongea huku akiwa ameuvuta mdomo
kwa namna ya kudeka.

"bibie usinune basi utasababisha na mimi ninune,
kumbuka ukitabasamu na mimi ndiyo nitatabasamu.
Nilikuwa kikazi zaidi mama" Norbert aliongea ili
kumfanya msichana huyo atabasamu, msichana
huyo alipotabasamu alimwambia "Frida nipe basi
niwahi maana muda ndio huu". Frida aliingiza
mikono chini ya meza ya mapokezi baada ya
kuambiwa hivyo, alitoa tikiti moja ya ndege ya
fastjet kisha akampatia Norbert.

"watu wameshaanza kuingia Nor, hebu wahi" Fridah
alimwambia Norbert

"haya bibie nikirudi jiandae maana nitapeleka posa
kwenu" Norbert aliongea akiwa anaelekea ndani ya
uwanja.

"nyooo lione vile na ukapera umwachie nani" Fridah
alimsindikiza na maneno hayo huku akiwa
amebinua mdomo.

****

 
SHULE YA NEEMA TRUST
"Soil Colloids, the colloidal state refers to a two-
phase system in
which one material in a very finely divided state is
dispersed through second phase.
The examples are:
Solid in liquid - Clay in water (dispersion of clay in
water)
Liquid in gas -Fog or clouds in atmosphere
The clay fraction of the soil contains particles less
than 0.002 mm in size. Particles less than 0.001
mm size possess colloidal properties and are
known as soil colloids. There are ten properties of
soil colloids, anyone can mention them?" Dkt
Jameson alitiririka katika kufundisha katika darasa la
kombi ya PCB kidato cha sita kwa mara ya kwanza toka
alipotambulishwa kwa wanafunzi asubuhi ya siku
hiyo, aliuliza swali na kupelekea darasa zima libaki
na mwanafunzi mmoja tu ndiye aliyenyoosha
mkono.

" your name please(jina lsko tafadhali)" Dkt
Jamesom alimwambia mwanafunzi huyo.

"Moses Gawaza" Mwanafunzi huyo alitaja jina lake.

"ok you can continue(sawa unaweza ukaendelea)
Dkt Jameson alimwambia

"The properties of Soil colloids are size, surface
area, surface charges, absorption cation, absorption
of water,cohesion,adhesion,swelling and shrinkage,
dispersion and floculation, brownian movement and
non permeabilitiy" Moses alitiririka kisha akaketi
kwenye meza yake alipomaliza.

"very good, clap your hands for him(vizuri
sana,mpigieni makofi )" Dkt Jameson aliongea akiwa
na tabasamu pana usoni mwake na kupelekea wanafunzi wote wapige makofi

"Iam hope you know the general properties of Soil
colloids through Mr Gawaza, lets continue in details (natumai
mnajua sifa kuu za Soil colloids kupitia kwa bwana Gawaza tuendelee kiupana).
Size: The most important common property of
inorganic and organic colloids is their extremely
small size. They are too small to be seen with an
ordinary light microscope. Only with an electron
microscope they can be seen. Most are smaller
than 2 micrometers in diameter...." Dkt Jameson
aliendelea kutiririka ili wanafunzi wake wamuelewe.
Hadi kipindi kinaisha tayari muda wa kutoka
shuleni hapo ulikuwa unakaribia, wanafunzi wote
walifurahia sana kipindi cha Dkt Jameson
kilichowafanya waelewe mambo mengi katika somo
la Kemia. Dkt Jameson alimuita Moses baada ya
kumaliza kufundisha kisha akaelekea ofisini, Moses
alitoka kwenda kuelekea ofisini alipoitwa na Dkt
Jameson.

"kaa kwenye kiti Gawaza" DKt Jameson alimwambia
Moses alipoingia ofisini kisha akainuka akiwa
ameshika faili akielekea kwenye makabati ya mafaili
halafu. Aliweka faili kwenye kabati halafu akarejea.

"ndio mwalimu" Moses aliitikia wito.

"unaweza ukaniita kakaJameson kwani mimi ni
kijana kama wewe tu isipokuwa nimekuzidi kielimu
tu" Dkt Jameson alikataa kuitwa kwawadhifa
aliostahiki.

"ndii kaka Jameson" Moses akasema.

"Gawaza najua wewe ni mwanafunzi mwerevu sana
na unajua vitu vingi ambavyo baadhi ya wenzako
hawavijui, sasa kwanini usiwe unawaelekeza
iliwaelewe kama wewe"

"ujue mimi najua kidogo tu na katika hicho kidogo
huwa namfanya mwenzangu atakaye kukijua ili
akijue. Hivyo suala la mimi kuwaelekeza wenzangu
najitahidi ingawa kuna wengine hawataki
kuelekezwa".

"vizuri sana hivi huwa unasoma masomi ya ziada
sehemu? kama unasoma basi hakikisha na wenzako
wanapajua ili wakasome"

"sisomi masomo ya ziada popote ila nilikuwa
ninafundishwa na baba yangu mzazi ambaye kwa
sasa ni marehemu".

"ooh! Pole sana kwa hilo, je baba yako naye alikuwa
mwalimu?"

"hapana hakuwa mwalimu bali alikuwa ni
mwanasayansi maarufu"

"mwanasayansi?! Nawajua wanasayansi wa karibia
bara zima la Africa,jina lake ni nani?"

" Professa Lawrence Gawaza"

"sawa nishamtambua, alikuwa ni mmoja wa
maprofessa wa chuo cha Havard na aliacha kazi
akarejea Tanzania kuendelea na shughuli zake
binafsi. Unaonekana una kipawa kama cha baba
yako, jitahidi utakuwa kama yeye. Ni hayo tu
unawezaa ukarudi darasani".

"sawa kaka asante"

Moses alinyanyuka kwenye halafu akapeana mkono
na Dkt Jameson kisha akaondoka kuelekea darasani.
Muda wa kutoka ulipofika Beatrice alikuja darasani kwa akina Moses
akiwa na bahasha mkononi mwake, alienda hadi
alipo Moses kisha akachukua kiti kilicho jirani
akaketi.

"mambo" alimsabahi Moses

"poa, za masomo" Moses aliitikia salamu akiwa
ametabasamu.

"safi tu, niambie msongolisti wangu" Beatrice
alitumbukiza utani

"nikuambie nini mlimbwende cha zaidi, au nikutolee
mambo ya electric potential sasa hivi" Mosea
alitumbukiza utani na kupelekea Beatrice acheke.

"unataka kunipasua kichwa nini yaani hiyo History ni
janga kwangu" Beatrice alisema huku akimpatia
bahasha Moses halafu akamwambia "ni kadi hii
kesho njoo nyumbani tafadhali ni sherehe yangu ya
kuzaliwa".

"usijali nitakuja maana si jumamosi, tarajia ugeni
wangu Bite"

"sawa leo ninaondoka na gari ya dady maana
amenifuata yupo nje, inabidi nikuage kwa namna
ninayopenda kama hutojali"

"ok niage basi upendevyo Bite".

"waao! simama basi".

Moses alisimama akijua anaagwa kwa namna ya
kawaida tu, akiwa amesimama alishtuka akiwa
amekumbatiwa na Beatrice. Ulaini wa mwili wa
Beatrice na joto lake ulimfanya ajihisi amepigwa
shoti ya ajabu mwilini mwake, Beatrice alimbusu
Moses shavuni kisha akaondoka huku akisema "bye
bye".
Moses alibaki ameduwaa akimtazama Beatrice
aliyekuwa akiondoka, Bratrice alipopotea katika upeo
wa macho yake alibaki akiwa ameduwaa kwa
kilichotokea.

"we boya bisha tena nikuone,changamkia tenda
hiyo" Sauti ya Hillary ilisikika kutoka nyuma yake na
kupelekea akurupuke kwenye mawazo.

"yaani mtoto anajilenga mwenyewe we unashindwa
kumaliza" Hillary aliendelea kumlaumu Moses.

"naona leo umeamua uniaibishe" Moses alimwambia

"nikuaibishe kwa lipi wakati wote wamesepa" Hillary
alimwambia Moses. Moses aliangalia darasa zima
na kukuta darasa lote ni tupu na wao wawili tu ndio
waliobaki.

"daah! Nilijua kuna wanga wananichora" Moses
aliongea huku akichukua begi lake la vitabu.

"wacha uoga wewe ,naona kakupatia barua kabisa"
Hillary alimwambia

"ni kadi tu ya mwaliko"

"poa tusepe kama vipi".

Walitoka humo darasani wakiwa wanaongea mambo
yao mbalimbali, utani kwa marafiki hawa ilikuwa ni
kitu cha kawaida sana.




ITAENDELEA!!

Tuesday, December 8, 2015

SHUJAA SEHEMU YA NNE





RIWAYA: SHUJAA

MTUNZI: Hassan O Mambosasa

SIMU:+255713776843...
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843

SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGI





  ILIPOISHIA

MASAA MAWILI BAADAE
KWENYE MBUGA YA KENYA WILD IMPALA

Mbuga hii iliyo jirani iliyo jirani na ziwa Victoria
kulikuwa na na handaki kubwa sana lililochimbwa
kilomita mbili kutoka ziwani, ndani ya Handaki hilo
kulikuwa na kundi la watu takribani sita wenye asili
ya barani Ulaya. Watu hao walikuwa wameizunguka
meza kubwa ya duara iliyotengenezwa kwa chuma,
meza hiyo ilikuwana urefu uliowafikia kiunoni mwao,
katikati ya meza hiyo kulikuwa na karatasi kubwa
lilioenea karibu meza nzima.

"nafikiri tutumie boti yenye uwezo wa kuzama kama
ilivyo Nyambizi" aliongea Obren ambaye alikuwa ni
mmoja kati ya watu waliokuwa wapo eneo hilo.

"ni njia sana nzuri, sasa tukatokee sehemu gani
iliyokuwa salama" aliongea mzungu mwingine kisha
akauliza swali.

" Calvin mbona rahisi hiyo, tutapita chini kwa chini
hadi katika pori la Rubondo lililopo katika kisiwa cha
Rubondo kisha hapo tutafanya mapumziko ya muda
kisha tutaendelea hadi Kagera" Campbel alijibu swali
hilo huku akielekeza kwenye ramani sehemu
wanazopitia.

"njia nzuri hiyo nadhani ramani itatusaidia kufika"
alisema Calvin

"ndio inasaidia na tukifika huko tutachukuliwa na
helikopta hadi kibaha halafu hapo tutakutana na
Tasi" aliongea Campbel.

"Obren, Calvin, Scott , Jameson na Christian
nadhani tupo pamoja sasa team mambas tuingie.
kazi!" alihitimisha Campbel kisha akanyoosha ngumi
mbele na kupelekea wenzake wote wanyooshe
ngumi na kukutanisha ngumi ya Campbel.

"kazii!" wote waliitikia kwa pamoja kisha wakatoka
kwenda kuchukua vitu vyao vya muhimu







 ENDELEA NAYO ILI KUPATA UHONDO ULIOMO NDANI
YAKE





SEHEMU YA NNE
Baada ya dakika kadhaa wote walirejea wakiwa
wamevaa mabegi ya mgongoni yenye rangi ya kahawia,
wote walielekea kwenye ngazi zilizopo ndani ya
handaki hilo zilizowapeleka mpaka sehemu yenye
bwawa kubwa lililotengenezwa kwa namna ya
kuvutia. Ndani ya bwawa hilo kulikuwa kuna boti ya
kisasa yenye rangi ya kijani ikiwa imeegeshwa
pembezoni mwa bwawa hilo, hadi muda huo tayari
walikuwa wameshafika jirani na boti hiyo ili
kujiandaa kuingia ndani yake. Waliingia kwa pamoja
ndani ya boti hiyo kisha wakaenda kuketi kwenye
viti vilivyomo humo ndani.

"anza safari" Campbel alimwambia nahodha wa boti
hiyo aliyekuwa yupo katika usukani mbele yao.
Nahodha wa boti hiyo alibonyeza kimojawao
miongoni mwa vitufe vingi vilivyopo mbele yake na
kupelekea boti hiyo ijifunike huku umbo lake likiwa
kama yai , alibonyeza tena kitufe kingine kisha
akashikilia usukani wa boti hiyo kwa mikono miwili. Boti
ilizama ndani ya bwawa hilo kuelekea chini kabisa
hadi lilipofika usawa wa bomba kubwa la duara
lenye uwezo wa kupitisha boti hiyo ambayo sasa ipo
katika umbile la nyambizi ya kivita ingawa ina umbo
dogo. Walipita ndani ya bomba hilo hadi kwenye mlango
wa kioo kuashiria ni mwisho wa bomba hilo. Hapo
nahodha alichukua simu ya kijeshi kisha akasema
"Captain B45 hapa. Tupo kwenye mlango, ninahitaji
ufunguliwe tupite". Alipomaliza kuongea alirudisha
simu sehemu yake kisha akashika kwa mkono
mmoja kwa nguvu huku mkono mwingine ukiwa
umeshika chuma kilicho na umbo kama gia ya gari.
Mlango wa kioo uliokuwa mbele yao ulifunguka
kupelekea maji yaingie huku nyuma ya boti hiyo
kukitokea kioo kingine kama cha awali kuzuia maji
yasiingie kwenye handaki, yule nahodha alisukuma
kile chuma kilicho na umbo kama gia ya gari na
kupelekea boti hiyo ianze kwenda kwa mwendo wa
kasi. Akiwa anatumia ramani iliyopo kwenye kioo
kilichopo chini ya usukani pamoja na dira iliyopo
mbele yake, aliweza kukiongoza chombo kuelekea
kusini magharibi mwa eneo walilolopo. Mwendokasi
wa boti hiyo uliwafanya wote waliomo humo ndani
watulie kutokana na kona kali zilizokuwa zikikatwa
na nahodha ili kukwepa miamba iliyomo ziwani.
Nahodha ilimbidi afanye kazi ya ziada katika
kucheza na usukani wa boti hiyo, hadi wanafika
kisiwa cha Rubondo tayari ilikuwa usiku wa manane
hivyo iliwalazimu kuinua boti juu ili wapumzike kwa
muda mfupi kisha waendelee.Waliifungua boti hiyi
ikawa wazi baada ya kuinua juu.

"kwanini tusiende kwenye kingo ya ziwa ile pale
tuka tukapumzike" aliongea Calvin huku akisimama
kwenye kiti chake baada ya kufungua mkanda

"unataka ufanywe kitoweo sio?" aliuliza Nahodha wa
boti hiyo.

"kivipi nahodha?" Calvin naye aliuliza

"hii sio bahari rafiki bali ni ziwa na kuna mamba
pembezoni mwake, sasa ukienda kule unajitafutia
kifo kwani wanakaa pembezoni" Nahodha wa
chombo chao alifafanua

"aaah! nafikiri ni kiumbe kidogo na hakitaweza
kushindana nguvu na mimi" Calvin aliongea kwa
dharau.

"rafiki ukae ukijua mamba wa pale ni wakubwa na
wenye uzito mkubwa sana, sasa suala kushindana
nao nguvu usijidanganye kabisa" Nahodha
alimwambia

"huyo hajui mamba zaidi ya kuwaona kwenye zoo
kawazoea kenge wa majini" Obren aliongea
kimasihara huku akicheka.

"ujue mamba wa humu ziwani wanafika urefu mita
sita na uzito wa tani moja, sasa kama unaweza
kushindana nao nguvu nikupe boti ndogo ya kujaza
na upepo uende" Nahodha alisema.

"aisee hao mamba wa Afrika kama ndio wapo hivyo
basi siendi, tupumzike hapahapa" Calvin kwa upole
huku akirudi kwenye kiti chake baada ya kusimama
kwa muda mrefu.

"sio mamba wa Afrika tu ndio wapo hivyo hata wa
dunia nzima ni wakubwa na uliowaona wewe ni
watoto, ushawahi kusikia ukubwa wa mamba aitwae
Lolong wa Ufilipino?" aliyepo jirani yake alimwambia

"ujue Scott yule mamba waliomkamata Wafilipino
nilijua ni wa uongo" Calvin alimwambia Scott

"sasa ndiyo ujue kuwa yule mamba ni wa ukweli na
haikuwahi kuonekana mamba mkubwa namna ile
kwa mujibu wa watafiti wa mambo ya wanyama"
Campbel naye alimwambia Calvin.

Walipumzika kwa
muda wa nusu saa huku
wakijadiliana mambo mabalimbali, mapumziko
yalipoisha nahodha alibonyeza kitufe na kupelekea
boti ijifunge kama awali kisha akawageukia wakina
Campbel.

"mikanda ni muhimu jamani" aliwaambia kisha
akabonyeza kitufe kingine na kupelekea boti hiyo
ianze kuzama taratibu, alikipeleka mbele kile chuma
kilicho na umbo kama gia ya gari. Boti ilianza
kwenda kwa mwendo mkubwa kama awali na
nahodha wake alizidi kuongeza umakini kuliko awali,
eneo lenye mawe mengi ndani ya ziwa hilo ndio
waliloingia na kupelekea nahodha akate kona kila
mara kuyakwepa mawe hayo. Hadi saa tisa usiku
inaingia tayari walikuwa wameshawasili Kagera
katika hifadhi ya Biharamulo iliyopo pembezoni mwa
ziwa Viktoria, kwa umbali wa mita kadhaa toka
kwenye kingo ya ziwa hilo kulikuwa na helikopta
kubwa ya kisasa aina ya AW139SAR ikiwa
imeegeshwa sehemu tambarare. Boti hiyo iliibuka
juu ya maji pembezoni mwa ziwa kisha ikajifuungua
halafu ikasogea hadi kando kabisa jirani na nchi
kavu, Campbel,Obren,Calvin,Jameson ,Scott na
Christian
ndiyo walioruka hadi nchi kavu kwa ukakamavu
huku nahodha akiwa amebaki ndani ya boti.
Kikosi hiki cha watu sita kilikimbia hadi ilipo
helikopta kisha kikaingia ndani pamoja na mizigo
yao, nahodha wa boti aliishia hapo kama wajibu
wake ulivyomtaka. Aliifunika boti halafu akaizamisha
ndani ya maji kama awali kisha akaondoka eneo
hilo, eneo ambalo boti hiyo iliibuka lilibaki tulivu
kama hakuna jambo lolote lilitokea.

"fungeni mikanda tafadhali" Rubani wa helikopta
aliwaambia vijana wa kazi aliotumwa kuja
kuwachukua ambao nao walitii bila kuweka walakini
wowote. Rubani alikinyanyua chombo chake kama
alivyotakiwa kufanya kisha akakiongoza kuelekea
mahali kilipotakiwa kuelekea, njiani watu wote
walikuwa kimya kusubiri mwisho wa safari ili
washuke. Mnamo alfajiri saa kumi na moja kasoro
helikopta hiyo iliwasili katika uwanja wa mpira
uliopo jirani na shule ya msingi iliyopo maeneo ya
kibaha, pembezoni mwa uwanja huo kulikuwa kuna
gari aina ya AUDI Q8 ikiwa imeegeshwa kwenye
kivuli cha mti wa mwembe. Pembeni ya mwembe
huo kulikuwa na range rover ya rangi ya kijivu.
Helikopta hiyo ilitua katika uwanja huo kisha milango
yake ikafunguliwa baada ya upanga wake kuacha
kuzunguka toka ilipozimwa, vijana sita wa kazi
walishuka wakakutana na Tasi akiwa amesimama
katika uwanja huo akiwasubiri

"karibuni" Tasi aliwaambia huku akiwapa mkono kila
mmoja.

"tushakaribia" Calvin aliongea kwa niaba ya
wenzake. Wote waliondoka hadi yalipoegeshwa
magari yaliyo jirani na uwanja huo kisha wakaingia
kwenye magari hayo, Tasi aliingia kwenye gari aina
ya AUDI Q8 akiwa na Campbel, Obren na Calvin
huku Jameson, Christian na Scott wakiingia kwenye
range rover wakiwa pamoja na dereva aliyekuja na
Tasi.
Msafara wa magari hayo mawili uliondoka uwanjani
hapo baada ya Helikopta iliyotua hapo uwanjani
kuondoka, msafara huu uliingia barabara ya
Morogoro kwa mwendo wa kasi ukielekea katikati ya
jiji.

****

Mnamo saa kumi na moja na nusu alfajiri Moses
alishtuka usingizini kama ilivyo kawaida yake,
aliinuka kitandani halafu akaelekea kwenye mahali
ilipo maliwato ndani ya chumba chake. Huko
alijisafisha vizuri kisha akatoka halafu akafanya
maandalizi kwa ajili ya shule, alipomaliza alitoka
hadi nje kwenye eneo la maegesho ya magari.
Aliingia kwenye gari analotumia kila siku kisha
akaliwasha, aliweka gia taratibu kisha akaachia breki
na kupelekea gari lianze kujongea kuelekea geti ambapo mlinzi tayari alikuwa ameshafungua geti ili
kuruhusu gari, akiwa amesimama pembeni ya geti
kama ilivyo kawaida yake.

"niaje kaka?" Moses alimsabahi mlinzi baada ya
kusimamisha gari alipofika usawa wa getini.

"poa dogo, za asubuhi?" Mlinzi aliitikia salamu huku
akimjulia hali.

"salama tu, hivi anko Kenne katoka saa ngapi
maana nimeona gari moja halipo"

"ametoka mida ya saa kumi alfajiri" Mlinzi alijibu.

"hakukwambia anapoenda"

"ameniambia anaelekea kazini kapata dharura"

"sawa kaka, wacha mi niwahi shule"

"poa dogo".

Moses aliondoa gari kwa mwendo wa kasi akielekea
barabara iendayo mtaa wa Warioba baada ya
kuagana na mlinzi wa nyumbani kwao..


 ****

Saa moja na nusu asubuhi walimu na wanafunzi wote wa shule ya Neema trust
walikuwa wamekusanyika katika eneo maalum la
kukusanyika wanafunzi kila siku asubuhi, haikuwa
kawaida kwa walimu wote kukusanyika hapo ifikapo
muda wa mstarini zaidi ya walimu wa zamu tu. Siku
hiyo shule nzuma ilikuwepo hapo kuashiria kuna
jambo muhimu na mkuu wa shule alikuwepo pia,
ratiba ya kila siku ya mstarini ilianza kisha mkuu wa
shule akasimama kuzunguka na wanafunzi wote.

"habari za asubuhi wanafunzi......natumaini wote
mmeamka salama na mpo na afya njema kama ilivyo
kawaida, dhumuni la kuwaita hapa ni kuwajulisha
juu ya ujio wa mwalimu mpya wa masomo ya Kemia
katika shule mwenye utaalamu wa hali ya juu katika
ufundishaji kutoka nchini Uingereza. Mwalimu huyu
atakuwa pamoja nanyi katika masomo hayo kwa
vidato vya nne, tano na sita kwa muda huu ambao
mwalimu wenu wa Kemia atakuwa likizo baada ya
kupata matatizo ya kifamilia. Napenda nimkaribishe
kwenu Dokta Jameson Share" alihitimisha mkuu wa
shule huku Dkt Jameson akisogea kusalimiana na
wanafunzi.

"habari za asubuhi wanafunzi na vijana wenzangu
kama mimi...........naitwa Dkt Jameson Share
nitakuwa nanyi katika masomo ya kemia katika
kidato vilivyotajwa na mkuu wa shule, hivyo
naombeni ushirikiano wenu kama wanafunzi" Dkt
Jameson alihitimisha na kupeleka shule nzima ipige
makofi.
Wanafunzi wote walitawanyika baada ya taratibu
zingine za hapo mstarini kuisha, waliingia
madarasani moja kwa moja kusubiri vipindi vianze.


 ****

Norbert Kaila ni mwandishi mashuhuri wa habari wa
nchini Tanzania pia ni mpelelezi wa shirika la EASA
(East Africa Security Agency) la Afrika ya mashariki,
kijana huyu alikuwa yupo katika pori la Hifadhi ya
Biharamulo kwa siku tatu zilizopita akifanya utafiti
kama mwandishi wa habari juu ya pori hilo. Kwa
muda wa siku tatu hizo alikuwa anaishi ndani ya
hema akiwa na askari mmoja aliyepewa na ofisi za
wanyama pori zilizo jirani na Hifadhi hiyo. Usiku uliopita
akiwa amelala katika hema lake alishtuliwa na ujio
wa helikopta katika pori hilo, ujio wa helikopta hiyo
ulimpa hamasa ya kutaka kujua ni nini kinaendelea.
Hivyo alitoka katika lake lilipo umbali wa mita
takribani mia tatu toka ilipo helikopta hiyo. Alitembea
kwa tahadhari hadi katikati ya miti iliyo jirani na
eneo hilo akiwa na kamera yake ya kipelelezi tofauti
na kamera yake ya kawaida. Ajibanza
hapo hadi aliposhudia ujio wa boti mfano wa
nyambizi iliyofika hadi ukingoni, hadi hapo aliweza kuoiga
picha kila anachokiona kwa msaada wa mwangaza
uliotoka katika taa ya helikopta na taa ya boti. Hadi
watu sita wanashuka kwenye boti ile alikuwa
amewaona na amewapiga picha, boti hiyo pia
alikuwa ameiona na ameipiga picha pia na helikopta
aliipiga vizuri akilenga namba zake zilizopo ubavuni.
Alipomaliza alibaki palepale hadi walipoingia ndani
ya helikopta kuondoka, na ile boti ilipozama chini.
Hapo alirudi kwenye hema kisha akajilaza pembeni
ya msimamizi wake kama ilivyokuwa awali. Hadi
asubuhi inaingia alikuwa macho na jua
lilipochomoza alikusanya vitu vyake kisha
akaondoka porini hapo akiwa na msaidizi aliyepewa.


 MZEE WA KAZI KAZINI




ITAENDELEA!!

Monday, December 7, 2015

SHUJAA SEHEMU YA TATU







RIWAYA: SHUJAA

MTUNZI: Hassan O Mambosasa

SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843

SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA HII KWA MARA NYINGINE

ANGALIZO: KAZI YA RIWAYA HII YA KISWAHILI NI KUELIMISHA NA KUENDELEZA KISWAHILI. NDIO MAANA NIMETUMIA KISWAHILI SEHEMU WANAPOZUNGUMZA WAGENI ILI NIENDANE NA JAMII WANAYOSOMA, BAADHI YA MANENO YA KINGEREZA YAMETUMIKA KUAKISI JAMII YA SASA ISIVYOTHAMINI LUGHA YA TAIFA

ILIPOISHIA
Siku iliyofuata Beatrice aliwahi kantini baada ya tu
ya kusikia kengele ya mapumziko, alikaa katika kiti
kilicho mkabala na kiti anachokalia Moses kila siku .
Baada ya muda Moses alifika hapo kantini akiwa
amebeba vitabu mkononi, alienda hadi kwenye kiti
anachokitumia siku na kumkuta Beatrice akiwa
tayari keshawasili eneo hilo. Aliweka vitabu na
kumsabahi
"mambo Bite" ha lafu akavuta kiti na kuketi, Beatrice
alimjibu, "safi tu upo poa?". Alivuta kiti na kuketi
kisha akasema "nipo poa, naona leo umeniwahi" ,
kauli hiyo
ilimfanya Beatrice atabasamu pasipo kusema lolote
huku akimtazama Moses.

ENDELEA NAYO ILI KUPATA UHONDO ULIOMO NDANI
YAKE

SEHEMU YA TATU
Moses aliinuka na kwenda kuagiza kifungua kinywa
kisha akarejea kitini, alimtazama Beatrice na
kumuambia, "mbona leo mtulivu hivyo kuliko
kawaida?". Beatrice akamwambia, "walaa nipo
kawaida siku zote ila sitaki kuongea sana kama kila
siku".

Moses akauliza, "mmmh! kwanini?"

"we unataka nipaliwe kama jana" Beatrice akaongea
kwa sauti yenye mchanganyiko wa deko na
kusababusha Moses acheke. Hakika kiliwazo kingine
kwa Beatrice baada ya kumuona mvulana
anayempenda akicheka, alitokea kupenda karibu kila
kitu cha Moses kasoro huzuni yake.

"na wewe umezidi" Moses aliongea huku akicheka

"na wewe bwana hebu acha hayo, hivi jana ulitaka
kuniambia nini?"

"ohoo! Halafu nilitaka nisahau"

"tell me now(niambie sasa)"
Moses alimuashiria Beatrice angoje kwanza muda
huo alikuwa na anatafuna kitafunwa mdomoni,
alimeza kisha akapika funda moja la chai.
Alipolimeza akasema, "Beatrice najua umejua
umetokea kuwa rafiki yangu mkubwa kwa muda
mfupi tu toka tulipoanza kuwa marafiki", aliposema
hivyo akajiweka vizuri kwenye kiti kisha akaendelea,
"sasa basi nataka unisaidie jambo moja tu kama
utaweza".

"Jambo gani hilo Mose?"

"relax Bite ndio ninakwambia sasa"

"sawa Iam listening you(ninakusikiliza)"

"najua unajua ni kiasi gani nimekuwa nikisumbuliwa
na mdada mwenye kujiita Dream girl, sasa nataka
unisaidie katika kumpata huyu mdada maana
nimechoshwa na tabia yake ya usumbufu"

"sasa hapo how can i help(nitawezaje kusaidia) maana hata huyo mdada
hata mimi simjui"

"I know its hard but try (najua ni ngumu lakini jaribu)ikiwa unanipenda
unanipenda mimi kama rafiki yako"

"mmh! Kusema kweli unanipa majaribu"

"unapenda kuniona nikiwa nina furaha"
"Yeah! Napenda kukuona ukiona ukiwa na furaha"

"please help me(please help me) kama unapenda kuniona nina furaha".

Beatrice allijifikiria kwa muda kisha akasema, "ok I
will try(saa nitajaribu)". Kauli hiyo ikimfanya Moses atabasamu
huku akisema "ukifanikiwa nitakupa zawadi yoyote
uitakayo". Waliendelea kunywa chai hadi muda
wakamaliza kabla ya muda wa mapumziko
haujaisha, waliendelea kuongea mambo mengine ya
kawaida huku Beatrice akiwa ni mwenye furaha
muda wote kama ilivyo kawaida yake. Hatimaye
kengele ya kurudi darasani ikagongwa, wote
walinyanyuka na kuondoka kurudi darasani.
Walitembea hadi sehemu ambayo kila mtu
anatakiwa kuelekea mahali yalipo madarasa yao ,
hapo Beatrice akamwambia Moses, "tuonane muda
wa kutoka kama hutakuwa na nafasi". Moses
alimuonesha ishara ya dole gumba ya kukubaliana
na jambo alilolisema, Moses akiwa na vitabu vyake
mkononi aliamua kuelekea darasani kwao moja kwa
moja. Siku hiyo Moses alijikuta akiwa na hisia za
ghafla juu ya Janet, kila akimfikiria alitamani kuwa
naye karibu zaidi. Akiwa darasani baada ya kipindi
cha kwanza baada ya mapumziko kuisha alijikuta
akimuuliza rafiki yake kipenzi humo darasani kwao,

" Hilary umemuona yule demu niliyekuwa nae
kantini?"

"ndiyo si Beatrice au kuna mwingine?" Hilary alijibu
na kuuliza swali papo hapo.

"unamuonaje?" Moses alimuuliza Hilary.

"aisee yupo poa sana, tena kazama kwako au
hujashtuka?"

"wala hamna kitu kama hicho"

"Mose wa wapi wewe yaani kukaa naye huko kote
bado hujajua"

"hamna hicho kitu wewe punguza fikra zako"

"ok tuache hayo, kwanini umeniuliza hivyo?"

"uongo dhambi ndugu, nahisi kumuhitaji baada ya
necta kuisha?"

"aisee leo umekuwa vipi? maana sio kawaida yako"

"Acha udaku we mwanga, mengine yakaushie tu".
Kauli hiyo ilimfanya Hillary acheke sana huku
akisema, "maajabu ya daunia msongolisti kanasa
leo". Moses naye alijikuta akicheka kwa kauli ya
utani aliyoitoa Hilary.

"haya msongolisti mgoni tupige msuli sasa nahisi
ticha haingii huyu" Moses naye akatumbukiza utani
huku akifungua daftari lake lililopo juu ya meza.
Muda wa kutoka ulipofika Moses na Beatrice
walikutana pale walipoachana awali, siku hiyo
Beatrice alitaka waondoke pamoha na Moses. Moses
akiwa na usafiri wake aliokuja nao alikubali pasipo
kuweka walakini wa aina yoyore, alimfungulia
mlango wa gari na kumruhusu kama malkia wake.

"mmh na wewe bwana kwa mbwembwe" aliongea
Beatrice baada ya kuona Moses amemfungulia
mlango kama kijakazi afanyavyo kwa malkia.

"sasa mgeni akiingia kwenye mali ya mwenyeji
lazima anyenyekewe" Moses alitetea kitendo chake
cha kumfungulia mlango Beatrice. Baada ya Beatrice
kuingia ndani ya gari naye alizunguka upande wa
dereva kisha akamuuliza Beatrice, "nikuache wapi?".
Beatrice akajibu pasipo kumuangalia Moses
"mikocheni kama unaelekea huko". Kauli hiyo
ilimfanya Moses atabasamu baada ya kubaini
wanaelekea sehemu moja, aliwasha gari kisha akaendesha kuelekea getini kisha akatoka na kuingia
barabarani kisha akaliondoa kwa mwendo wa kasi.
Baada ya dakika takribani thelathini walikuwa
wamefika mikocheni katika mtaa wa Warioba
sehemu ambapo kuna barabara iendayo mtaa wa
mazinde, Beatrice aliomba kushushwa
njiani, "kwanini nisikupeleke hadi kwenu?" Moses
aliuliza.

"usijali hapa panatosha tu" Beatrice aliongea akiwa
tayari ameshafungua mlango wa gari baada ya
Moses kusimamisha gari.

"Moses usijali nimefuatwa na gari na dereva yule
pale" Bearice aliongea huku akionesha kwa kidole
upande wa pili wa barabara jirani na waliposimama.
Moses alipotazama pembeni ya barabara aliona gari
aina ya Toyota landcruiser V8 ikiwa imeegeshwa
pembezoni mwa barabara mkabala na alipoegesha
gari lake. Hadi muda huo Beatrice alikuwa tayari
ameshashuka garini na sasa alikuwa akivuka
barabara huku akimpungia mkono Moses, baada ya
Beatrice kuingia katika gari lililomfuata Moses
aliondoa mguu wake kwenye breki kisha akakanyaga mwendo
na kupelekea gari ianze kuondoka taratibu. Allikata
kona kuingia njia iendayo mtaa wa Mazinde ambapo
ndio anaishi, alinyoosha barabara moja kwa moja hiyo moja
mwa umbali mrefu kiasi kisha akakata kushoto
kuingia mtaa wa mazinde halafu akaelekea moja
kwa moja hadi kwenye geti la nyumbani kwao


****

JIJINI KISUMU
NCHINI KENYA
Ndani ya klabu ya hoteli ya Sunset pembezoni mwa
mji huo upande wa magharibi wa nchi hiyo, ndani
ya hoteli hiyo ya nyota tatu kulikuwa na mkutano
mkubwa wa watu wenye maslahi ya aina moja.
Brian, kundi la wazungu wenzake ndio wahudhuriaji
wa mkutano huo wenye. Msemaji wa kikao hicho
alikuwa ni Brian ambaye alifungua kikao hicho kwa
kusema, "habari za jioni ,natumai kila mmoja wetu ni
mzima wa afya na ameitikia wito wa mkutano huu
wa siri wa umoja wetu kwa kujua lengo la mkutano
huu. Pia nadhani ni muda muafaka kwa sisi
tuunyamzishe umoja wa Ulaya ambao umekuwa
kikwazo katika biashara yetu inayotuweka mjini na
inayotuwezesha sisi kuendesha biashara zetu
nyingine, nadhani nyote mnajua kwamba tulimtuma
Tasi akachukue virusi kwa namna yoyote baada ya Professa
kugoma kufanya biashara nami" alinyamaza kwa
muda kisha akanyanyua bilauri ya pombe iliyopo mezani
halafu akapiga funda moja.

"Professa huyu aligoma baada ya kusikia kuwa nina
mpango wa kuvijaribu nchini Tanzania kwenye
makazi yake na ambapo anapatikana mwanae
kipenzi, kutokana na ukaidi sisi tukamwambia
atumie mbinu mbadala ili aweze kutupatia bure
maana mwanzo aligoma kutupatia kwa malipo. Tasu
alifanikiwa kumchoma Professa sindano ya sumu
inayoua taratibu ambayo hadi inamuua hakuwa
ametupatia virusi hao, dawa ya sumu hiyo tulikuwa
tunayo na ikatulazimu tumwambie atapata dawa
kama akileta virusi mikononi mwetu. Yote hayo
bado Professa alikaidi na akaishia kusema ipo
mikononi kwa mtu wake anaemuamini na
hatutowapata, hivyo basi hayo ndio maneno
aliyotuchia yenye ukaidi. Sasa nataka nisikilize
mawazo yenu kila mmoja ili tuweze kupata njia
mbadala" alihitimisha kisha akawatazama
wahudhuriaji wa mkutano huo kila mmoja. Mmoja
wa wazungu alinyoosha mkono na kupelekea Brian
asema , "ndio Obren tunakusikiliza"

"Bosi mi naona tumuache Tasi aendelee na kazi
yake na kama akishindwa tutamuongezea nguvu ili
atuwezeshe kupatikana kwa huyo wa kumuaminiwa
na Professa apatikane haraka iwezekanyo" aliongea
Obren kisha akakaa kwenye kiti chake. Mzungu
mwingine alinyoosha mkono na kupelekea Brian
aseme ,"ndio Campbel tunakusikiliza"

"bosi mimi sikubaliani kabisa na Mr Obren kwa
jambo alilolizungumza, nashauri sis ndio tuingie
kazini na huyo Tasi tumtumie kivingine ila si
kwenye kazi hii" Campel aliongea na kupelekea watu
wote waafiki kwa kutikisa vichwa kuashiria
wamekubaliana na rai ya Campbel. Brian aliinuka
kwenye kiti chake kisha akasema "je kuna mwenye
la ziada juu ya hili? nadhani nyote mmekubalia na
ushauri wa Campbel, sasa kikosi chenu wenyewe
kiingie kazini kuanzia muda huu hamna la ziada".
Brian alihitimisha kisha akainuka kwenye kiti chake
halafu akaondoka.Wote waliobaki walitazamana kila
mmoja huku ukimya ukimya ukiwa umetawala,
Cambel aliuvunja ukimya huo kwa kusema, "jamani
tukutane kambini kwetu kule kwenye mbuga" halafu
akainuka kisha akaondoka eneo hilo.


****


MASAA MAWILI BAADAE
KWENYE MBUGA YA KENYA WILD IMPALA
Mbuga hii iliyo jirani iliyo jirani na ziwa Victoria
kulikuwa na na handaki kubwa sana lililochimbwa
kilomita mbili kutoka ziwani, ndani ya Handaki hilo
kulikuwa na kundi la watu takribani sita wenye asili
ya barani Ulaya. Watu hao walikuwa wameizunguka
meza kubwa ya duara iliyotengenezwa kwa chuma,
meza hiyo ilikuwana urefu uliowafikia kiunoni mwao,
katikati ya meza hiyo kulikuwa na karatasi kubwa
lilioenea karibu meza nzima.

"nafikiri tutumie boti yenye uwezo wa kuzama kama
ilivyo Nyambizi" aliongea Obren ambaye alikuwa ni
mmoja kati ya watu waliokuwa wapo eneo hilo.

"ni njia sana nzuri, sasa tukatokee sehemu gani
iliyokuwa salama" aliongea mzungu mwingine kisha
akauliza swali.

" Calvin mbona rahisi hiyo, tutapita chini kwa chini
hadi katika pori la Rubondo lililopo katika kisiwa cha
Rubondo kisha hapo tutafanya mapumziko ya muda
kisha tutaendelea hadi Kagera" Campbel alijibu swali
hilo huku akielekeza kwenye ramani sehemu
wanazopitia.

"njia nzuri hiyo nadhani ramani itatusaidia kufika"
alisema Calvin

"ndio inasaidia na tukifika huko tutachukuliwa na
helikopta hadi kibaha halafu hapo tutakutana na
Tasi" aliongea Campbel.

"Obren, Calvin, Scott , Jameson na Christian
nadhani tupo pamoja sasa team mambas tuingie.
kazi!" alihitimisha Campbel kisha akanyoosha ngumi
mbele na kupelekea wenzake wote wanyooshe
ngumi na kukutanisha ngumi ya Campbel.

"kazii!" wote waliitikia kwa pamoja kisha wakatoka
kwenda kuchukua vitu vyao vya muhimu



ITAENDELEA!!

Sunday, December 6, 2015

SHUJAA SEHEMU YA PILI





  SHUJAA

MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA



SEHEMU YA PILI
Kujipitisha kwake katika madarasa ya sayansi hakukuzaa matunda yoyote, alijitahidi kumsalimja kwa uchangamfu ili awezs angalau kuzoeana naye. Salamu yake ilijibiwa kawaida na kila akitaka kujiweka karibu naye alishindwa  kutokana na umakini wa kijana huyo kwenye masomo uliomfanya awe hapendi na mabinti. Baada ya jitihada zote kushindikana kushindikana sasa alibuni mbinu mbadala ya kumfikishia ujumbe kijana huyo,  kila siku alikuwa akiwahi shule mapema kabla ya watu wote hawajafika. Muda huo wa asubuhi inayoifukuza alfajiri alikuwa  akiweka kadi mbalimbali za mapenzi katika meza ya kijana huyo, mchezo huu ulimchanganya sana Moses hadi akawa anawauliza wanafunzi wenzake kama anamjua. Kila akijaribu kuwauliza wenzake juu ya jambo hilo aliambulia patupu pasipo kumpata anayemchezea mchezo huo, hali hiyo iliendelea kila siku huku mtumaji akiwa anajiita dream girl.  Hali hiyo ilizidi kuendelea kila siku  anapoingia darasani asubuhi, "be a man(kuwa mwanaume) Mose vitu hivyo havilaziwi damu hata siku moja" mmoja wa wanafunzi alimwambia Moses  baada ya kumuona kila siku akilalamika juu ya tukio la kuletewa kadi na mtu msichana asiyemtambua.  Hali hii ilizidi kuendelea na sasa akawa akikaa kantini muda wa mapumziko analetewa kadi na watu mbambali, kila kadi anayoifungua inatoka kwa yule yule msichana anayejiita dream girl. Hayo yalizidi kumchanganya sana Moses na akawa na shauku ya kumjua huyo

Saturday, December 5, 2015

SHUJAA SEHEMU YA KWANZA





 SHUJAA

MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA

SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP: +255713776843


ANZA SASA
Huzuni ilikuwa imemtawala usoni kijana Moses na
kumfanya aonekane mtu mzima tofauti na
muonekano wake ulivyo, kila akijaribu kuhangaika
kwenda na baba yake katika hospitali tofauti ndani
ya jiji la Dae es salaam juhudi zake zilikuwa
zinagonga mwamba katika kutafuta tabibu awezaye
kumtibu baba yake aliyeugua ghafla pasipo
kujulikana chanzo kuugua huko. "mwanangu najua
unahangaika sana katika kuhakikisha.......ninapona
na ninarudi katika hali ya kawaida ila....." alikatisha
kuongea na kuanza kukohoa mfululizo huku
akimtazama mwanae kwa huruma kisha akaendelea
kusema "sitopona mwanangu ujue najua hujui
chanzo cha kuugua kwangu.." alihema kwa nguvu
huku akimtazama mwanae kwa jicho la huruma sana
kutokana na huzuni iliyomgubika kijana Moses. Baba
Moses akaendelea kusema "nimekuwa nikitumia
muda wa maisha yangu kwa miaka mingi katika
kugundua vitu mbalimbali katika sayansi pasipo
kujua mwisho wa kazi yangu hii , nimekuwa
nikitumiwa na watu matajiri ili niweze kupata fedha
kwa kuitumia kazi yangu vibaya. Sasa haya ndiyo
matokeo ya kazi yangu hii" alisitisha kuzungumza
kisha akamtuma Moses akamletee mkoba wake
anaoutumia kuhifadhi nyaraka zake muhimu.
Hakuwa mwingine bali ni professa Lawrence Gawaza
mwanasayansi wa siku nyingi na bingwa wa
kutengeneza kemikali hatari kwa maisha ya viumbe
hai, sasa yupo kitandani akiwa anaumwa ugonjwa
ulioshindwa kujulikana chanzo chake na matabibu
wa hospitali tofauti alizoenda kufafutiwa tiba. Moses
kijana wa miaka kumi na nane ndio kijana pekee wa
Prof Gawaza,hakuwa na mtu mwingine isipokuwa
mwanae huyo aliyekuwa anampenda sana. Mke
wake kipenzi alifariki siku aliyomzaa Moses, hivyo
hakuwa na mtu wa karibu hapo nyumbani zaidi ya
mwanae huyo.
Moses alimpelekea mkoba baba yake pale kitandani
anapomuuguzia,aliamriwa afungue kwa namba za
siri alizotajiwa na baba yake. Alipofungua alikutana
na makabrasha mengi pqmoja na funguo ndogo
sana, "umeiona hiyo funguo?" Prof Gawaza aliuliza
kwa tabu kutokana na kuzidiwa kwake. "huo pamoja
na hayo makabrasha naomba uwe mtunzaji wake na
usimkabidhi yoyote yule" Prof Gawaza alimwambia
mtoto wake huyo kwa sauti yenye kutoka kwa shida.
Moses naye aliitikia kwa kichwa huku machozi
yakimtoka kutokana na hali ya baba yake ilivyo, "we
ni mwanaume sasa haina haja ya kulia kwani
haisa......idii kitu chochote, kazania masomo yako
halafu....."alishindwa kumalizia kauli hiyo baada ya
kikohozi kumbana. Alikohoa kwa nguvu sana kisha
akaomba maji. Moses alikimbia kutoka chumbani
anapomuuguza baba yake hadi kwenye cha kulia
chakula kwenye jokofu la kupooza maji. Alichukua
bilau moja ndefu akaiweka usawa wa koki ya jokofu,
kisha akafungua koki ya jokofu kuruhusu maji
yaliyopo kwenye chupa kubwa juh ya jokofu hilo
yashuke kwa kasi, Alivyoijaza alirudi kwa kasi hadi
chumbani alipo baba yake, alipofika alimkuta kalalá
mithili ya mtu aliye ndani ya usingizi mzito. "baba
amka unywe maji" alimuita huku akimtingisha
mkono,cha ajabu hakuamka wala kuonesha dalili
zozote za kuamka. Moses alimtingisha baba yake
huyo kwa nguvu lakini hakuamka, aliita kwa sauti
kubwa lakini sauti yake haikuzaa jitihada zozote za
kumuamsha Prof Gawaza katika usingizi wa milele
aliolala. Moses alichanganyikiwa sana na hali
aliyomkuta nayo baba yak baada ya kumletea maji, "
baba! baba! baba! baba! babaaaa!" alipiga kelele
kwa nguvu baada ya kubaini baba yake hakuamka.
"Mose vipi mbona hivyo, kuna nini?" ilisikika sauti
ya mlinziwa nyumba hiyo pale mlangoni kisha
akaonekana mlinzi akivuka kizingiti cha chumba
hiko kwa kasi, kilio cha kwikwi cha Moses ndicho
kilimkaribisha humo chumbani na utulivu wa Prof
Gawaza ambaye alikuwa amelaliwa na Moses kifuani.
Alimnyanyua Moses kisha akaweka mkono katika
upande uliopo moyo katika kifua cha profesa,
hakuridhika akaweka na sikio kabisa kifuani mwa
bosi wake. Alipoinua uso wake ulikuwa umejaa
huzuni sana na alimshika mkono Moses kisha
akaenda naye nje, alipofika akamkalisha kwenye
baraza la nyumba. "yakupasa ujikaze dogo kwani
wewe ni mwanaume, kumbuka wewe ndio msimamizi
wa mali hizi na baba wa baadaye. Dogo jikaze najua
unasikia uchungu" Mlinzi alianza kumpa nasaha
Moses juu ya tatizo lililomfika. Pia akazidi
kumueleza "kumbuka binadamu hatuwezi kuwa
pamoja milele hata siku moja kwani ipo siku
tutatengana, ndio kama hivi mzee kakutoka ingawa
bado tunamuhitaji. Mose kutengana na mtu wako wa
karibu ni mojawapo ya changamoto za maisha na
kipimo cha ukomavu wako, sasa basi inabidi
ujioneshe upo mkomavu kiasi gani kwa kujikaza
katika suala kama hili. Baada ya mlinzi kumpa
Moses maneno ya kumtia moyo aliamua kwenda
kutoa taarifa kwa majirani pamoja na kuwapigia watu
wa karibu na Prof Gawaza.


***************************************

Brown Mcdonald ni mzungu mwenye mtandao
mkubwa dunia unohusiana na uhalifu wa kila aina,
umri wake na utajiri alionao ni vitu viwili tofauti.
Akiwa na vibaraka karibia kila nchi aliowaamini sana
katika biashara zake, hakika hakuna alitakalo
lifanyike katika biashara zake likashindikana. Kijana
huyu ambaye ni mwanajeshi aliyeasi amri katika
kikosi cha Uingereza na mtuhumiwa nambari moja
wa uhalifu barani ulaya aliamua kuja Afrika akiwa na
kundi kubwa la vijana wake baada ya msako wake
kuwa mkali barani Ulaya. Akiwa amevaa sura ya
bandia na alama za vidole mwake aliweza kuficha
muonekano wake pamoja na kupata passport mpya
ya kusafiria kwa njia ya kawaida tu pasipo
kugundulika na wanausalama wa dunia ambao
wanamsaka. Sasa ameingia ukanda wa Afrika ya
mashariki akiwa kama mfanyabiashara mwenye
viwanda vya kusindika katika nchi zote za Afrika ya
mashariki, ndani ya muda mfupi toka aingie katika
ukanda huu amejizolea umaarufu kutokana na ubora
wa bishaa zake. Akiwa anatambulika kama Brian
Stockman aliweza kuwa mfanyabiashara mwenye
ushawishi mkubwa katika soko la kimataifa, viwanda
vyake vilikuwa kama mwamvuli wa kuficha biashara
yake haramu anayoifanya ya kuuza dawa za kulevya
na nyara mbalimbali za serikali. Uongo
alioidanganya dunia ullikuwa umefanikiwa na sasa
alikuwa anajihisi mtu huru katika biashara zake,
aliweza kusafirisha bidhaa haramu pasipo kikwazo
chochote. Akiwa ametimiza mwaka mmoja tu toka
aanze kujulikana na wakazi wa kandahii ya Afrika ya
mashariki, alipata habari ya kugunduliwa kwa hatari
na mwanasayansi wa kitanzania. Taarifa hiyo
ilimvutia sana na akafanya jitihada za kuonanan na
mwanasayansi huyo, aliomba kuonana na
mwanasayansi huyo. Alipokubaliwa alipanga mahali
pa kukutana nae, hilo liliafikiwa na mwanasayansi
huyo.
Baada ya siku mbili walikutana katika mgahawa
uliomo hoteli ya Serena jijini Dar es salaam katika
sehemu iliyojitenga, kila mmoja akiwa na kinywaji
chake na amekaa kwenye kiti kilicho mkabala na
mwenzake. Baada ya kusalimiana Brian(Brown)
alianza kuongea kwa kiswahili kisicho fasaha chenye
maneno ya kingereza "sina mengi za kukuweka hapa
bana Gawaza, nahitaji tufanye bussiness".
"what kind of bussiness(biashata ya aina gani")
aliuliza Gawaza.
"no ipoo ongea na mswahili professa onesha jinsi
gani unatukuza swahili bana" Brian alimuumbua Prof
Gawaza baada kuona anajali sana kingereza kuliko
lugha yake ya taifa.
"ok mr Brian biashara ya aina gani?" prof Gawaza
aliuliza huku akitabasamu.
"i know you are scientist(najua wewe ni
mwanasayansi) na umegundua virus ambao
ninawahitaji kwa ajili ya kasi yangu binafsi" Brian
alieleza kiini cha kukutana.
"virus wale ni hatari sana Mr Brian na bado sijatafuta
dawa yake, huoni kama ni hatari kwako if you
release them(kama utawaachia)" Prof Gawaza
alimwambia Brian huku akipiga funda moja la
mvinyo ulio katika bilauri.
"I don't care about that(sijali kuhusu hilo) Professa
ninachohitaji ni virus na jaribio ndani ya nchi hii"
Brian alisema maneno hayo akiwa na uso wenye
dharau.
"no sipo tayari kwa hilo mr Brian kama unataka
biashara yoyote ya virus nitakupa ila si kujaribu
ndani ya nchi yangu yenye damu yangu...thats all"
Prof Gawaza alinyanyuka kwa hasira na kuondoka
eneo hilo. "we will meet again(tutakutana tena)"
Brian alimwambia kwa sauti kisha akaendelea
kunywa kinywaji chake kwa taratibu. Alipomaliza
alinyanyuka kwenye kiti alichokaa akiwa na hasira
maradufu, "I'll show him (nitamuonesha)" Brian
aliropoka kwa hasira kisha akanyanyuka kuelekea
ulipo mlangi wa kutokea katika mgahawa wa hoteli
hiyo. Alitoka na kuondoka kwa mwendo wa haraka
hadi alipoegesha, aliingia ndani na kuliwasha kisha
akatoweka katika eneo hilo.


**************************************


Maelfu ya watu walihudhuria katika msiba katika
msiba wa Professa Gawaza uliokuwepo nyumbani
kwake maeneo ya mikocheni jijini Dar es salaam,
wengi wakiwa ni ndugu,jamaa na marafiki wa
mwanasayansi huyo maarufu ndani ya jiji la Dar es
salaam. Uwanja wa nyumba hiyo ulifurika watu wa
rika zote wakiwa na mavazi meusi huku wale watu
wa karibu wa marehemu wakiwa wamevalia nguo
nyeusi chini na fulana nyeupe yenye picha ya
marehemu sehemu ya kifuani. Turubai kubwa
lilifungwa nje ya nyumba hiyo pamoja na viti vyenye
rangi moja vilivyokaliwa na wahudhuriaji wa msiba
huo, mtoto pekee wa marehemu ambaye ni Moses
alikuwa kakaa ndani muda wote huku kilio kikiwa
ndiyo kiliwazo chake. Siku iliyofuata mwili wa
marehemu uliagwa katika eneo hilo la nyumbani
kwake kisha msafara wa magari kutoka kwa
wahudhuriaji wa msiba huo uliondoka msibani hapo
kuelekea yalipo makaburi ya kinondoni maeno ya
kinondoni kwa ajili ya kuupeleka mwili wa marehemu
katika nyumba ya milele . Mazishi yalifanyika katika
makburi hayo kisha watu wakatawanyika kuelekewa
makwao na wengine kurudi msibani.
Baada ya siku takribani saba ndugu wote wa
marehemu waliondoka ndani ya nyumba hiyo na
kupelekea Moses mjomba wake ambaye alijitolea
kuishi naye na mlinzi wawe watu pekee waliobaki
katika nyumba hiyo. Maisha bila ya baba yake ndio
yaliyofuata baada ya msiba wake, pesa alizoziacha
baba yake pamoja na msaada wa rafiki mkubwa wa
baba yake aitwae Dk Mbungu ulioweza kumsaidia
katika vitu mbalimbali ndio uliopelekea aweze
kujimudu katika mahitaji yake muhimu ikiwemo
ulipaji wa ada shuleni. Hadi muda huo Moses
alikuwa anasoma kidato cha tano katika shule ya
Neema trust iliyopo mbezi jijjnj Dar es salaam,
aliamua kujiendeleza kielimu kielimu na kutoshika
mambo yoyote yasiyohusiana na elimu ili aweze
kujijenga. Umakini wake katika masomo ulimfanya
awe mwanafunzi bora katika shule yao, hadi muhula
wa kidato unakwisha mnamo mwezi mei mwaka
uliofuata, tayari alikuwa anaongoza shule nzima kwa
kupata alsma za juu kuliko mtu yoyote katika kombi
za sayansi zote. Akiwa likizo alitumia muda wake
mwingi kujisomea na akawa hajishughulishi na
mambo ya anasa, mnamo mwezi wa saba muhula
mpya wa kidato cha sita ukaanza kama ilivyo ratiba
ya nchi nzina ya Tanzania. Ulikuwa muhula wa
masomo ambapo wsnafunzi wengi walizinduka
kutoka kwenye usingizi baada ya kutokuwa makini
katika masomo yao ya kidato cha tano, katika kombi
ya PCB ambayo Moses alikuwa anasoma tayari
umakini wa wanafunzi ulizidi maradufu ingawa
hawakufua dafu mbele ya uwezo wa Moses
aliyezinduka mapema kabla yao.


**************************************

Beatrice Bernard ni binti wa familia yenye uwezo
anayesoma katika shule ya Neema Trust, ni
mojawapo ya wasichana warembo na wenye kuvutia
katika shule hiyo iliyosheheni watoto wa matajiri
kutoka sehemu mbalimbali ndani ya Afrika ya
mashariki. Umbo lake la asili ya asili ndio lilimfanya
avutie kwa kila anayemtazama, mchanganyiko wa
wazazi kutoka makabila tofauti ndio ulimfanya avutie
maradufu. Baba yake mzee Bernard alikuwa ni
muhaya na mama yake akiwa ni mrangi, hakika
alikuwa na umbo tata lililozua maswali na
minong'ono kila apitapo. Yote hayo pamoja na sifa
zote alizozipata na kusumbuliwa na watu kutoka
sehemu mbalimbali, alikuwa ni msichama aliyezama
katika penzi zito la mtu asiyemjali wala kuthamini
upendo wake. Utanashati wa huyo kijana ndio
uliomvutia sana na kufanya awe kiliwazo cha macho
yake, ustarabu na upole wake ndio uliomfanya
apende kuwa nae.maishani mwake. Kijana huyo
hakuwa mwingine ila ni Moses Gawaza kijana
mpenda masomo kuliko anasa kama ilivyo vijana wa
umri wake. Beatrice akiwa anasoma madarasa ya
arts katika kombi ya HKL alijitahido kujenga ukaribu
na kijana wa madarasa ya sayansi bila ya mafanikio,
hii haikumkatisha tamaa Beatrice zaidi ya kupenda
kuwa karibuIRI na Moses kutokana na misimamo
aliyonayo huyo kijana kamaJ mwanaume..

ITAENDELEA!!

Friday, December 4, 2015

DHAHAMA SEHEMU YA MWISHO





     DHAHAMA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE



SEHEMU YA MWISHO!!
 Vijana hao walifaniliwa kuwateka Ally na Jamadin na kuondoka nao ambapo njiani Ally alipigwa kisogoni akazirai akatupwa kando ya reli mita chache kutoka katika mzunguko wa Kwa Minchi majira ya usiku, kupotea kwa Jamadin na Ally nyumbani kwangu ilikuwa ni huzuni sana kwa mke wangu lakini kwangu mimi ilikuwa ni kawaida kwani nilikuwa najua kila kitu. Tulikusanyika nyumbani wanaume wote huku mimi nikionekana kulia sana na nilibembelezwa hadi nikanyamza ndipo tulipoanza kujadiliana kimaigizo nini cha kufanya, baada ya mjadala wanaume wote sita tulikubaliana tuongie mtaani kumtafuta Jamadin na Ally na wake wote wakakaa nyumbani kwangu wakimbembeleza Farida.


****

Thursday, December 3, 2015

KOSA SEHEMU YA MWISHO







HASSAN O MAMBOSASA

SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE



 ILIPOISHIA
Nurulayt aliunyanyua ule mzigo wote kwa kutumia ile mashine ya kubebea mizigo akauingiza ndani ya helikopta kisha akaingia ndani  akakaa sehrmu ya rubani akaniambia, "panda twende".
" unaweza kuendesha helikopta?" Nilimuuliza.
"hebu wacha maswali yako panda bwana wanakuja hao"  Nurulayt aliniambia na muda huo huo tukasnza mtikisiko ambo unatokea ikipita treni, nilipanda kwenye helikopta haraka sana nikiwa nimekaa mlangoni kwa tahadhari. Nurulayt aliwasha helikopta na aliipandisha juu baada ya kuanza kuchanganya huku akiiongoza kuelekea mashariki ili aiache kambi hiyo. Helikopta ilipokuwa juu kabisa wale watu walikuwa wameshafika pale kwenye uwanja  ilipokuwa imeegeshwa, walianza kutupa risasi lakini Nurulayt aliongeza mwendo akawaacha.


MALIZIA MKASA HUU WA KUSISIMUA WENYE KUFUNDISHA


SEHEMU YA MWISHO!!
Baada ya kukivuka kikwazo hicho kwa mara nyingine nilijikuta nikimshukuru Mungu kwa kunifanya niwe mzima hadi muda huo tangu nilipojiweka katika mdomo wa mamba katika kambi ile, siiutarajia kama nitaweza kutoka na kuiba katika kambi ile yenye ulinzi na wapiganaji hodari sana wanaotumia silaha. Nilipomtazama Nurulayt kule mbele nilimuona yupo makini sana kuiongoza helikopta kwa mwendo wa kasi, tulikuwa tumeshaiacha  kambi kwa umbali mkubwa hata ukitumia darubini utaiona kwa mbali sana na hatukuwa na wasiwasi na wale vijana wa Gorilla zaidi ya kusonga mbele.
"GRIIIIIIIII!   GRIIIIIIIIIIIII!  GRIIIIIIIIII! "  Mlio wa  simu ulisikika katika mfuko wa suruali yangu ambao ulinishtua sana kwani nilishasahau kama nilikuwa nimebeba simu kabisa katika tangu mara ya mwisho kuitumia siku ile niliyokutana na Nurulayt tangu tupoteane miaka mitano iliyopita, mlio huo pia ulimshtua Nurulayt na kumfanya atazame nyuma kwa mshangao.
"Abdul umekuja na  simu tena ipo loud, huoni kama ingekuwa ni hatari kwako" Nurulayt aliniambia huku akitazama mbele kwa umakini.
"sikujua kama nina simu kwani nilishasahau kabisa" Nilimwambia huku niitoa ile simu nikaiangalia kwenye kioo na nikakuta mpigaji ni yule yule anayenipa kazi za ajabu tangu nijikute nipo Namibia.
"ipokee basi au kama hutaki izime" Nurulayt aliniambia akionekana kukerwa sana na simu niliyonayo jinsi inavyoita kwa fujo, sikuwa na jinsi kwani nisingeipokea ingekuwa ni hasara yangu na kama ningeipokea ingekuwa ni afadhali kwani sikujua huyu mtu anayejiita F.A.Z anataka kuniambia nini. Niliipokea nikaiweka sikioni bila ya kusema chochote ili nimsikilize yeye.
"Napenda niwapongeze kwa kufanikiwa kuiba almasi niliyowatuma pia naomba nikupongeze kwa kufanikiwa kutolewa hardware zangu mgongoni mwako na huyo malaya wako mkijua sitajua upo wapi  ilihali unayo simu  niliyokupatia mimi mwenyewe yenye Global positioning system yaani GPS, sasa basi hujaweza kunifanya nisijue uliopo Abdul hiyo GPS ya kwenye hiyo simu imeunganidhwa huku nilipo katika kompyuta zangu sasa nitajua ulipo hata uhame bara hili. Kwanza tuachane na hayo kwenye hii simu kuna ramani inayokuelekeza sehemu ya kupeleka mzigo huo sasa mpe huyo malaya alete mzigo unapohitajika, pia kumbukeni helikopta hiyo ina mafuta pungufu sasa  mkijifanya mnazunguka sana jua imekula kwenu na ninahitaji mzigo huo haraka sana" Yule mtu alinipa maelekezo kisha simu ikakatwa, sikuwa na jinsi ikabidi nimuoneshe ramani hiyo Nurulayt na nimuelekeze kila kitu Nurulayt nilichoambiwa. Nurulayt alitii maelezo na safari ya kurudi sehemu iliyooneshwa ndiyo ikaanza kwa mwendo wa kasi ili tuwahi kufika eneo hilo, baada ya saa moja nilihisi helikopta ikianza kushuka taratibu na nilipoangalia chini nikaona alama ya H ya rangi nyeupe ikiwa ipo juu ya ghorofa mojawapo katika mji nadhifu sana ambao sikuujua unaitwaje hadi muda huo.
"Nuru hapa ni wapi?" Nilijikuta nikimuuliza Nurulayt.
"ni Widhoek hapo  au umepasahau kabisa" Nurulayt alinitajia sehemu hiyo ambayo ndiyo mji mkuu wa Namibia tuliouacha hapo awali, sikuweza kuutambua kutokana na muonekano wake  kwa juu kwani ulikuwa ni tofauti sana. Nurulayt aliishusha helikopta hadi ikatua katika alama ile ya H iliyokuwa juu ya ghorofa mojawapo ambalo niliwaona watu wengi walioshika silaha zao wakiwa wapo hapo, Nurulayt alipozima Helikopta tulishuka na kisha tukasimama mbele ya mmoja wa watu tulipwakuta hapo ambaye alitusogelea akaanza kutupekua nguo zetu achukua silaha zetu zote.
"why( kwanini)?" Nilimuuliza yule mtu aliyetupekua
"you are going to meet our Boss,  weapon are not allowed. Follow me (mnaenda kukutana na bosi wetu, silaha haziruhusiwi. Nifuateni)" Yule alituambia kisha akaelekea pembeni ya eneo hilo ambalo kulikuwa na tundu kubwa kama mlango lenye ngazi zinazoingia ndani ya ghorofa hilo, tulimfuata tukiwa tumefuatwa nyuma na vijana wawili wenye silaha nzito sana. Tulishuka ngazi hizo hadi chini kisha tukaufuata ukumbi mwembamba uliotupeleka hadi kwenye mlango wenye kamera kwa juu yenye taa juu yake kama ile ya kule kambini kwa vijana wa gorilla, yule mtu aliyetukagua aliisogelea ile kamera kisha akasema "they are here Boss( wapo hapa Bosi)". Aliposema hivyo alinivuta mkono na kunisogeza karibu na ile kamera  huku akiniambia "your face ( sura yako), niliinua uso  wangu nikaitazama ile kamera huku kengele maalum ikilia na mlango ukafunguka. Tuliingia ndani tukiwa tumeongozana na wale watu na tukatokea katika ofisi pana yenye mandhari ya kuvutia pamoja na milango minne tofauti, mbele yetu  kama mita sita kulikuwa kuna meza yenye mafaili kadhaa pamoja na kiti cha kuzunguka kilichotupa mgongo.
"kaeni kwenye makochi hapo" Sauti ile iiliyokuwa ikinipa kazi nisizozipenda ilitoa  amri ikitokea katika kiti kile cha kuzunguka kilichotupa mgongo, tulikaa katika makochi yaliyopo jirani nasi yakiwa mita sita kutoka pale alipo.
"Abdul, Nurulayt hatimaye tunakutana leo hii" Aliongea yule mtu huku akuzungusha kiti kuangalia tulipo na hapo ndipo nilipoibaini sura yake halisi na nikajikuta nikishtuka sana, Nurulayt naye alishtuka sana kwani alibaini yupo ndani ya himaya  ya hatari.
"FAIZ ni wewe kweli" Niliongea huku nikinyanyuka nikataka kumfuata lakini nulishtushwa na milio ya kukokiwa  bunduki  na  nilipoangalia pembeni nilitazama na bunduki mbili aina ya SPAS-12  kutoka kwa wale  watu tuliyoingia nao, sikuwa na jinsi niliishia kukaa tu palepale huku tayari nikiwa najua kilichonifanya niwe pale.
"kinachowashangaza ni kipi nyinyi? Faiz kuwa hai sio? Mlidhani atakufa kwa hila zenu mlizozifanya nyie wasomali. Abdul yaani uko radhi kujaribu kumuua rafiki yako kipenzi kisa mwanamke ambaye hakupendi mwenye mapenzi na rafiki yako kisa una pesa tu, kakwambia nani pesa inaleta mapenzi mpaka ufanye haya. Ilivyopita miaka kumi ulidhani limeisha sio?" Nilikaripiwa na nikajikuta nikiinama chini baada ya kushindwa kumtazama kutokana na maneno makali aliyokuwa anayatoa hadi machozi yakawa yanamtoka.
"Faiz nisamehe rafiki yangu" Nilijikuta nikiomba msamaha.
"wa kuniomba msamaha ni mimi kwani, muombe Faiz mwenye huruma ya kusamehe ila mimi huwa sisamehi" Yule mtu ambaye nilijua ni Faiz alitoa kauli inayoonesha kukana kama yeye siyo Faiz.
"wewe kama si Faiz ni nani?" Nilimuuliza.
"mimi ni Fauz  Ally Zaid kifupi F.A.Z  au Scorpio pacha wa Faiz Ally Zaid  niliyeikimbia nchi yangu nikiwa na mdogo wangu Khalid na nikazamia Afrika ya kusini kutafuta maisha na nikayapata kama haya niliyokuwa nayo kwa tabu na dhiki nikiwa nina uhakika wa kuja kuipa maisha bora familia yangu lakini wewe ukaivuruga familia hiyo kwa jeuri ya pesa zako ambazo hujui zinatafutwa vipi. Pesa hizo za ulizorithi umeona ni bora uwalipe wale waasi wa Kongo wamteke Fauz halafu wawambie familia yetu walete nusu tani ya almasi  kutoka katika himaya yangu mwenyewe iliyo chini vijana wangu Gorrila boys, unajua matokeo yake ni nini?...........Baba yangu Mzee Ally Zaid aliyekuwa ni mwanajeshi mstaafu akaamua kwenda kujaribu kuiba hiyo almasi akajikuta anauawa kikatili huku nikiwa sijui kama vijana wangu wamemuua bsba yangu mzazi alipokuwa ana harakati za kumkomboa mwanae,   Abdul............Abdul nilijiapiza lazima ulipie kwa kukuonesha hiyo pesa inatafutwaje kama ulivyotembea na wale wanawake  ili kupata dola milioni moja za kimarekani na kuiba hizo almasi ili mfe kama mlivyosababisha baba yangu afe lakini mmepona kwasababu Mungu bado anawahitaji nyinyi mashetani" Aliongea huku machozi yakimtoka  na mwili ikimtetemeka kwa hasira, alipoacha kuongea mlango mmojawapo ukafunguliwa na akaingia mtu aliyetokea kuwa rafiki yangu mkubwa na pia meneja wa makampuni. Khalid Zaid ambaye yule niliyemshuhudia akiwaeleza  waandishi wa habari kuwa nipo masomoni ndiye aliyeingia huku akitoa tabasamu pana sana, nilibaki nikishangaa sana kwani sikutarajia kabisa kama nitakutana naye huku kutokana na kumuamini sana.
"Khalid na wewe pia?" Nilijikuta nikiongea kwa mshangao.
"huyo anaitwa Khalid Ally Zaid na unamfahamu kama kama Khalid Zaid  kwani huwa hatumii jina la kati na Faiz hatumii jina  lake la mwisho, nilimtuma kwa ajili ya kukamilisha kazi hii na ukamuamini bila ya kutambua unamuamini Nyoka" Fauz aliongea huku Khalid akitabasamu.
"huyu ndiye aliyekuwa anakupeleleza na hata siku ile uliyochukua binti ambaye ni mfuasi wangu uliyeamini ni changudoa yeye ndiye aliyeusuka mpango ule mpaka ukanyonya matiti ya yule binti anayeitwa Angel aliyoyapakaa madawa ya kulevya ukalala. Pia huyuhuyu ndiye aliyekupasua mgongoni akakufunga hardware ukiwa hujitambui baada ya kunusishwa Klorofomu ukatupwa kwenye kisiwa katika bahari ya Antlantiki siku nne baadaye na ya tano ukajikuta  umelala ufukweni" Fauz aliongea  tena kunifahamisha juu ya Khalid, muda huohuo mlango mwingine ulifunguliwa na akaingia mtu aliyekuwa anaendeshwa kwenye kiti cha matairi  na msichana ambaye sikuweza kumtambua kabisa. Walifika hadi eneo aliposimama Khalid wakiwa wamevaa kofia zilizoziba nyuso zao kwa sehemu kubwa.
"Abdul umefanya kosa lililozaa maafa mengine bila ya kujijua kwa kutumia jeuri ya pesa zako na wewe ndiyo cha huyu mtu aliyekaa kwenye kiti cha matairi ashindwe kutembea tangu nampata, nadhani huyu hujamtambua ni nani ngoja umuone" Fauz alisema kisha akamfunua kofia yule aliyekaa  kwenye kiti cha matairi.
"Faiz!" Niliropoka baada ya kuiona sura ya Faiz kwa mara nyingine baada ya miaka kumi kupita, Faiz alikuwa ananitazama kwa uso uliojaa na hasira sana huku akiachia tabasamu lisiloashiria furaha katika uso wake.
"unashangaa kuniona nipo hai sio fedhuli mkubwa we?" Faiz aliongea akiwa na hasira sana kisha akamgeukia kaka yake akamuambia, "Kaka ulipokimbia nyumbani ukiwa na mdogo wetu nilikuona huna maana ndiyo maana hata chuo na shuleni nilisema nimezaliwa peke yangu kumbe nina pacha wangu, nimeingia chuo nikapata rafiki nikamuona ana maana kumbe hana maana kwani ametumia watu waniteke na wamenichoma sindano ya sumu ambayo inanifanya niwe katika kiti cha matairi hadi leo hii. Ama kweli umdhaniaye ndiye kumbe siye, huyu baradhuri nilimuona  anafaa kumbe hafai na nikakuona wewe hufai kumbe ndiye unafaa, Fauz huyu mtu namchukia sana" Faiz aliongea huku akitokwa na machozi, mimi mwenyewe machozi yalianza kunitoka kutokana na kujuta sana kutokana na mambo niliyomtendea rafiki yangu tukiwa chuo ingawa machozi hayakuweza kubadilisha ukweli wa jambo hilo liwe halijatokea.
"Faiz nisamehe rafiki yangu nimekosa" Nilimuomba msamaha Faiz  huku nikinyanyuka ili walau nikapige magoti mbele yake anielewe lakini nilishindwa kwenda kutokana na kuwekewa bunduki kwa mara nyingine nilipotaka kwenda. Nilirudi nikakaa chini nikamtazama Nurulayt ambaye alionekana pia kujuta kwa kile alichomfanyia Faiz.
"Abdul tafadhali sana naomba usiniite rafiki yako na ukitaka nikusamehe mlete Huwaida hapa  kwani nilimtumia email nilipokombolewa na anajua juu ya uovu wako na kama huwezi  sitakusamehe, namtaka mpenzi wangu tu kwani sijui umemficha wapi hadi sasa" Faiz aliongea huku uso wake ukiwa umetawaliwa na hasira, nilipisikia hilo suala ikabidi nimtazame Nurulayt kisha nikasema, " Faiz haiwezekani jambo hilo kwani Huwaida niliyempenda na aliyekupenda wewe tayari ni marehemu kwa sasa".
"What! Hapanaaaa" Faiz aliongea kwa uchungu kisha akaanza kulia kwa uchungu huku mishipa ya damu ya kichwa ikiwa imemtoka, nilimuonea huruma saba ingawa chanzo cha yote nilikuwa ni mimi.
"Abdul  kama Huwaida kafa basi mwnao lazima afe kwa namna yoyote" Faiz aliongea kwa uchungu.
"Kifo cha Huwaida ni mimi ndiye mhusika  na si Abdul wala  mtoto wetu Ilham na kama unataka kuniadhibu niadhibu ila kaka yako Fauz lazima pia naye alipe kwa kumuua Sabir kaka yangu aliyekuwa rafiki yake na mshirika na kuhusika kwangu katika kutekwa kwako nilikuwa nalenga Fauz na sio wewe" Nurulayt kwa mara ya kwanza aliingilia kutokana na kusikia suala la kutaka kuuliwa Ilham, maneno hayo yalimfanya Fauz atabasamu.
"Alaa kwahiyo umemfanya kaka yangu awe mtu wa kutembea kwa baiskeli kisa mimi kumuua Sabir na ukadhani yeye ni Fauz, sikulaumu sana  najua umekosea kufananisha kwa jinsi tunavyofanana......Sabir alikuwa ni rafiki yangu sana ila amenigeuka  kwa kuuwa watu wangu pia kutaka kumuua mdogo wangu kwa bomu, hivi ungekuwa wewe mtu kama huyu utamfanyaje?" Fauz aliongea na mwisho akamuuliza swali Nurulayt lililomfanya ashindwe kujibu na pia akajiona  ana hatia sana kwa kufanya kile anachokifanya, Faiz alipoona Nurulayt ameshindwa kujibu swali lake alitoa ishara moja ambayo sikuielewa. Mlinzi mmoja mwenye bunduki alisogea mbele baada ya kutolewa ishara ile kisha akampatia bunduki Faiz, Faiz naye aliishika ile bunduki akaelekeza tulipo kisha akaifyatua ikatoa mlio niliousikia. Kuusikia mlio wa bunduki nilitambua haijanipiga mimi kwani bunduki ikikupiga husikii mlio wowote, nilipomuangalia Nurulayt niliona sindano yenye manyoya kama mshale wa mchezo wa dart ikiwa imemchoma begani mwake. Nurulayt aliutia ule mshale kisha akautupa chini na akabaki akiugulia maumivu, nilipomtazama Faiz nilimuona akitabasamu kisha akanielekezea bunduki mimi akiwa makini sana. Hapo mapigo yalianza kwenda mbio na ikanibidi nifumbe macho tu nikusubiria nitandikwe , mlio wa bunduki niliusikia kwa mara ya pili nikafumbua macho nikamuona Faiz akitabasamu.
"Abdul sioni kosa lako lolote lililobakia kwani umejifunza vya kutosha ila huyo mwanamke ana kosa ndiyo maana nimemuadhibu, kosa lako kubwa ilikuwa ni kutoa pesa katika mpango wa huyu mwanamke hivyo umepata funzo hiyo pesa ya urithi uliyoitoa katika mpango huo inatafutwaje" Faiz aliongea huku akinitazama halafu akamegukia Nurulayt akamuambia "Nuru hiyo ndiyo ulistahiki kwa kuhukumu watu bila kujua kama upo sahihi au haupo, sindano zilizo ndani ya bunduki hii zina sumu ambayo ikiingia kwenye damu huponi na itakuua taratibu kuanzia kiungo  kimoja baada ya kingine hadi unakata roho". Faiz alipomaliza kuongea hivyo nilijikuta nikilia baada ya kusikia Nurulayt kachomwa sindano ya sumu na nikamkumbatia ingawa yeye hakuonesha kuhuzunika hata kidogo. Baada ya kusema maneno hayo Faiz alimgeukia Fauz akamwambia, " hii inawatosha wape vitu vyao", Fauz naye alitii na akamuita kijana wake mmoja akampa mkoba ambao alikuja kunipatia. Niliupokea  mkoba huo nikaufungua   nikakuta hati za mali zangu zote pamoja na kadi zangu za benki, niliufunga mkoba huo kisha nikatulia nikawa nawatazama ndugu wale watatu.
"Niliwaambia waandishi kuwa upo masomoni nadhani sasa muda wa masomo umeisha na umepata funzo sasa upo huru, tupatie kila tulichokupatia" Khalid aliongea huku akitabasamu, nilipoambiwa hivyo nilitoa simu nikamrushia naye akaidaka.
"Abdul natambua kama wewe ni binadamu unakosea kwani hakuna aliyemkamilifu, hivyo nimekusamehe wewe na mwenzako.....Nurulayt naomba unisamehe sana sikuwa na jibsi zaidi ya kufanya hivyo nilivyokufanyia na napenda mtambue mtoto wenu yupo nyumbani kwa Sarina mama yake wa kambo, guards take them to the room" Faiz aliongea
Walinzi walituchukua wakatutoa nje ya chumba hicho wakatupeleka chumba kingine kilicho na nguo tofauti za kike na za kiume, huko tulioga na tukabadilisha nguo kisha tukashuka hadi chini na tukachukua teksi iliyotupeleka hadi nyumbani kwa Nurulayt ambapo tulipanda gari yangu nilipewa tukaanza safari ya kuelekea nyumbani kwa Sarina. Tulifanikiwa  kufika na tukashuka tukaingia ndani ya uzio kisha tukagonga mlango wa mbele tukasubiri kufunguliwa, baada ya dakika kadhaa Sarina alifungua mlango na alinikumbatia kwa furaha baada ya kuniona nimerejea nikiwa mzima. Nurulayt alikaribishwa ndani na hapo tukamsimulia kila kitu hasa juu ya Ilham kuwa ni mwanangu. "Waar is Ilham?( Yuko wapi amelala)" Nurulayt aliuliza akiwa na shauku ya kumuona Ilham
" lê(amelala)" Sarina alimjibu lakini Nurulayt alitaka amuone Ilham tu kwani hakuwa amemuona kwa miaka mitano, ilimbidi Sarina amuelekeze chumba kilipo na Nurulayt akaenda akituacha tukiongea . Aliporejea alikuwa amembeba Ilham ambaye tayari alikuwa ameamka, huku akionekana kuwa ana furaha kwa kumuona mtoto wake kwa mara nyingine.
"Anko umerudi?" Ilham aliongea aliponiona nikiwa nimejea.
"wewe sio anko yule ni baba, umesikia? Haya nenda kamsalimie  baba " Nurulayt alimuambia Ilham
"ok mummy" Ilham alijibu halafu akaja kunikumbatia akiwa na furaha na mimu nikiwa na furaha kwa kumjua mwanangu.
"Sarina...dankie(Sarina......asante) Nurulayt alimshukuru Sarina kwa kumtunzia Ilham, Sarina alitabasamu kuonesha amekubali  shukrani ya Nurulayt.

Nilikaa kwa Sarina kwa siku kadhaa kisha nikaenda hadi Walvis kwa rafiki yangu Jonas nikamchukua hadi nyumbani kwa Sarina, baada ya wiki mbili nilikuwa nipo Tanzania nikiwa na Sarina, Ilham, Nurulayt pamoja na Jonas ambaye nilimpatia nyumba na mtaji kama shukrani kwa msaada wake kwangu nilipokuwa nina shida aliponiokota ufukweni. Miezi miwili iliyofuata nilifunga ndoa na Sarina hapahapa Dar es salaam iliyohudhuriwa na watu mbalimbali na sherehe kubwa ikafanyika katika moja ya hoteli ninazozimiliki, furaha yangu ya kuwa na mwanamke ninayempenda  katika ndoa  ilitimia kuanzia siku hiyo.
Baada ya miezi mitatu tangu nifunge ndoa na Sarina hali ya kuafya ya Nurylayt ilianza kubadilika kwa baadhi ya viungo kushindwa kufanya kazi na  akipolekwa hospitali ilibainika tumechelewa kwani sumu ilishasambaa mwilini kote na hakukuwa na tiba ya kumuokoa, Nurulayt aliugua kitandani kwa muda mrefu sana hadi Sarina anapata ujauzito yeye alikuwa bado ni wa kitandani. Sarina alipojifungua watoto mapacha wa kiume ambao niliwaita Haasan na Hussein yeye bado alikuwa kitandani, baada ya miaka mitatu  tangu aanze kuugua Nurulayt aliaga dunia katika muda wa alasiri na  akatuachia huzuni na majonzi yaliyobaki moyoni mwangu na kunipelekea nitokwe na machozi kipindi naandika mkasa huu ulionikumba. Mungu amlaze pema mama wa mtoto wangu wa kwanza na binti yangu mkubwa kati ya watoto sita niliojaliwa na Muumba, nakumbuka mazishi ya Nurulayt niliteuliwa niingie kaburini kuipokea maiti lakini nilishindwa kutokana na kulia sana hasa nikimkumbuka katika kipindi chote nilichokuwa naye.

****

Walipomaliza ukurasa wa mwisho wa shajara hiyo Hassan na Hussein wote walijikuta wakitokwa na mschozi baada ya kujua mkasa uliomkumba baba yao pamoja na mama yao wa kambo ambaye kamzaa dada yao mkubwa.
"aisee mi Mariam simtaki tena hapa nimepata funzo tosha" Hassan aliongea huku akijifuta machozi.
"kweli pesa haileti mapenzi na pesa ibilisi" Hussein aliongea huku naye akijifuta machozi.
"wanawake wapo wengi nitatafuta mwingine ngoja nimuache jamaa awe naye ili niepuke kufanya kosa kwani alichokifanya baba kimenipa funzo tosha" Hassan aliongea huku akimtazams Hussein.
"kaka hapo umeamua na umefanya busara kubwa sana, tafuta mwingine wazuri wapo wengi sana ndani ya dunia hii. Huwezi jua Mungu amekupangia  nani baada ya Mariam kuchukuliwa na jamaa cha msingi badili direction ya moyo wako tu" Hussein alimshauri Hassan.
"kweli kabisa hii diary imenifunza mengi kabisa, cheki time maana nasikia tumbo linanisokota kwa njaa" Hassan alimwambia Hussein. Hussein alichukua simu yake ya mkononi akaangalia saa na alijikuta akipigwa na mshangao baada ya kuangalia saaa.
"Ebwanaeh! Time imeenda sana saa kumi hii, hebu twende tukale kwanza" Hussein aliongea kisha akasimama akaelekea mlangoni ili aelekee sebuleni, Hassan naye alimfuata kwa nyuma.
Walipofika sebuleni walikutana na wazazi wao wakawasalimia kisha wakataka kwenda kwenye meza ya chakula lakini baba yao aliwaita na akawaambia wakae kwenye kochi.
"Hussein, Hasaan" Mzee Abdul aliita majina yao.
"naam Baba" wote waliitikia kwa pamoja.
"najua mmemaliza kusoma diary yangu wanangu, je Hassan bado unataka kufanya ulichodhamiria?" Mzee Abdul aliuliza
"hapana sitafanya nimejifunza pesa si lolote katika mapenzi" Hassan alijibu.
"vizuri, niliamua kuwaacha mjue maisha yangu nyuma ili mjifunze na nyinyi wanangu. Nafurahi mmejifunza na naomba mfuate hayo mliyojifunza, ukiona umekataliwa jua kuna kizuri unaandaliwa mwanangu sasa utafute anayekupenda ili uje kuwa kama mimi Abdul na mama yenu hapa Sarina" Mzee Abdul aliongea huku Bi Sarina akitabasamu.
"sawa baba tumekuelewa" walijibu kwa pamoja.
"nendeni mkale" Mzee Abdul aliwaruhusu watoto wake, Hassan na Hussein walielekea kwenye meza ya chakula wakiwaacha wazazi wao wakiongea.
"ujue mwanzo sikuliafiki suala la wewe kuwapa watoto ile diary wasome ila sasa naona upo sahihi kabisa Mume wangu" Bi Sarina aliongea kwa sauti ya chini kumuambia mume wake.
"unajua katika suala la kuwafunza watoto inabidi muda mwingine tuwe wawazi kwao ili wajue hasara za jambo hilo mke wangu" Mzee Abdul alimwambia mke wake.
"hakika mume wangu wewe ni baba bora kwa watoto wako" Bi Sarina alimwambia mume wake.
"hata wewe ni mama bora kwa watoto, nakupenda sana" Mzee Abdul aliongea.
"nakupenda pia mume wangu" Bi Sarina aliongea huku akitabasamu.
Tangu siku hiyo Hassan aliachana na habari za kutaka kumdhuru rafiki yake na akawa na urafiki naye.

   MWISHO!!

natumaini umejifunza mengi sana, maoni yako tafadhali kwa mtunzi wa riwaya hii

NDUGU MSOMAJI INABIDI UTAMBUE KUWA LIKE
YAKO NDIYO INIPAYO NGUVU YA KUANDIKA RIWAYA
HII, HIVYO LIKE ILI KAMA UPO PAMOJA NAMI.
COMMENT KAMA UNA USHAURI AU MAONI. USIPIGE SIMU KATIKA NAMBA HIZO HAPO JUU, UJUMBE MFUPI WA MANENO UNATOSHA


DHAHAMA SEHEMU YA KUMI NA SITA





 DHAHAMA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE


SEHEMU YA KUMI NA SITA!!
Mara ya kwanza nilianza kwa Faimu nikawa najipitisha sana kwao ili anuone nikijua nitamnasa tu kama nilivyonasa vijana wa hapo kijijini kumbe Faimu hakuwa kijana wa hivyo, uvumilivu uliponishinda niliamua kumuambia ukweli  lakini pia nilimkosa baada ya kukataliwa na akanitishia kumuambia Hamis.  Mara ya pili niliirudia tabia yangu kwa kumtaka Ally baada ua uzuri wake  kuonekana alipofikia kwenye balehe  lakini pia alinikataa nikajikuta nazidi kumsumbua nikijua nitampata tu kwani ni mtoto yule bado akili haijapevuka zaidi ya kupevuka mwili tu, nilipoona nakataliwa sikuchoka na niliamua kuanzisha mazoea ya kawaida naye.  Siku nilipokuja kuwafuma Farida na Faimu na wote wakakiri kuwa wana uhusiano ndiyo siku niliyoona ya kutumia sababu hiyo kwa njia mbili, kwanza ni kulipa kisasi cha kukataliwa na Faimu na pili ni kumteka Ally kiakili. Nilijua Ally ni bado ana akili za kitoto hivyo nilipanga nimuambie hii habari ili ajue ni jinsi gani nampenda hadi nikaamua kumuambia hiyo habari ili aamini moyo wangu upo kwake, pia nilitaka nimuambie mpenzi wangu juu ya usaliti wa rafiki yao kwao waweze kumfanyia kitu kibaya ili nimcheke na hata amkose Farida.

Wednesday, December 2, 2015

KOSA SEHEMU YA KUMI NA TANO

   RIWAYA: KOSA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA

SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE



 ILIPOISHIA
"ndiyo tunayo moja tuliyoipata kama ngawira" Nurulayt alijibu
"mnatakiwa muwe na ya pili kwani kutungua masniper ishirini sio mchezo hivyo kila mmoja anatakiwa awe na yake" Madam Rhoda alitusisitiza,  kusikia suala hilo wote tuliinama chini kutokana na kutokuwa na namna ya kuipata hiyo silaha.
"hilo msijali nitawasaidia mtimize wajibu wenu, Nuru hebu lete briefscafe mbili zipo chumba ninacholala" Madam Rhoda alimuamuru Nurulayt ambaye alitoka haraka aliposikia amri hiyo kisha akarejea akiwa mikoba miwili ya kufunga kwa namba akampatia Madam Rhoda.




ENDELEA NA MKASA HUU WA KUSISIMUA WENYE KUFUNDIDHA


SEHEMU YA KUMI  NA TANO!!
Nurulayt alimkabidhi mikoba hiyo Madam Rhoda ambaye aliipokea kisha  akaufungua mmojawapo

DHAHAMA SEHEMU YA KUMI NA TANO

RIWAYA: DHAHAMA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE




SEHEMU YA KUMI NA TANO!!
Niliendelea kujipa moyo nikijua ipo siku nitampata na sikutambua kama mawazo yangu ni sawa na kuchemsha mawe nikitegemea yatachemke kutokana na upendo mzito nilionao kwake, sikutambua kama najipa matumaini hayawezekani kutokea hivihivi kama kubadilika kwa majira ya mwaka kutoka kiangazi hadi vuli. Nilichojali ni kupata jibu sikujali itachukua muda gani hadi niwe naye, niliendelea kusumbuka katika kumueleza kila siku lakini niliambulia patupu na nikawa natembea na matumaini ya kumpata tu kichwani mwangu. Matumaini yangu yaliishi katika moyo wangu lakini baadaye yalikufa baada ya muda wa miezi kadhaa tu na nikajikuta nikiumia moyoni, kufa  kwa matumaini yangu kulikuwa ni baada ya kuingia kikwazo katika kumpata Farida...


****


Nakumbuka vizuri kijijini kwetu waliingia wageni ambao walipatiwa eneo ambalo baadaye  walilinunua wakajenga makazi yao ya kudumu, wageni hao walikuwa ni wenye asili ya tofauti na watu walioko kijijini

Tuesday, December 1, 2015

KOSA SEHEMU YA KUMI NA NNE

   KOSA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA

SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE



 ILIPOISHIA

Furaha ilidhihirika machoni mwetu kwa kufanikiwa kukivuka kikwazo kile lakini furaha hii haikudumu kwani dosari kubwa iliingilia furaha hii, tukiwa tupo katikati ya pori usiku majira ya saa sita milio ya risasi ilianza kusikika na vioo vya  gari letu vikaanza  kupasuka.Yule askari ambaye ndiye aliyekuwa dereva wetu alitoa ukelele wa maumivu akiachia usukani wa  gari
 na gari likaingia pembeni ya barabara nusura ligonge mti baada ya  yeye kuwahi kukanyaga breki ya gari.




ENDELEA NA MKASA HUU WENYE KUELIMISHA NA KUSISIMUA




SEHEMU YA KUMI NA NNE!!
Milio ya risasi iliendelea kurindima mithili ya ngoma kwenye sherehe ya kikabila, vioo vya gari letu vilitobolewa na matundu ya risasi ambazo zilikuwa zinatokea upande wa pili wa barabara. Muda huo mimi nilikuwa nimesharuka nje ya gari baada ya kuona kuwa ni hatari ndiyo ipo mbele yetu, Nurulayt naye alikuwa amesharuka nje ya gari kisha akajilaza chini kwenye miti mita kadhaa  kutoka barabarani. Hali ilikuwa ngumu kwa yule askari wa uhamiaji aliyekodiwa na Nurulayt atuvushe mpakani kwani alipojaribu kutoka kupitia mlango wa kushoto ambao alikuwepo Nurulayt kutokana na mlango wa kwake kutokuwa salama kuutumia risasi ilitua mgongoni mwake na kumfanya ageuke nyuma ili aweze kumshambulia aliyemtupia risasi, yule askari alipogeuka aliinua kichwa  ili aone vizuri kwani alikuwa amelala kifudifudi kutokana na risasi iliyompata mgongoni. Nikiwa nimejibanza kwenye mti mnene uliopo mita kadhaa kutoka barabarani, nilimshuhudia yule askari akitobolewa kichwa chake na risasi baada ya kuinua kichwa ili atazame upande anaotokea adui yake. Askari yule hakutoa hata neno la mwisho baada ya risasi hiyo ya masafa marefu  kutoboa kichwa kisha kuendelea na safari hadi kwenye shina mti nililosimama ikapita juu kidogo ya kichwa changu kisha ikaendeleana safari.
"Abdul lala chini haraka utakufa huoni risasi imekukosa hiyo"  Nurulayt aliniambia kwa sauti huku akiweka sawa bunduki aina ya short gun  aliyopewa na yule askari, nililala chini kwa haraka sana na macho nikawa nayaelekeza kwenye gari  letu ambalo bado lilikuwa linanguruma hadi muda huo kutokana na kutozimwa na taa bado zilikuwa zinawaka kuanzia ya ndani hadi za nje. Mlango mbele wa gari letu upande wa kiti cha kushoto cha dereva ulikuwa wazi baada ya yule askari kuufungua akijaribu kutoka nje hivyo ikawa njia  rahisi sana kwa mlengaji  kumuua kwani gari hii mlango mmoja ukiwa wazi basi taa ya ndani inawaka hivyo mtu wa nje anakuona kirahisi. Tukio hili ni tukio jingine linalonifanya nimshukuru Mungu katika maisha yangu kwani nafsi yangu ilinisihi nifungue kioo cha dirisha nililokaa baada tu ya kuvuka mpakani, Nurulayt naye alifanya hivyohivyo na dereva wa gari ambaye ndiye yule askari wa uhamiaji nchini Botswana wala hakufanya hivyo yeye aliendelea kuacha kioo kimepandishwa. Ndiyo maana hata kioo kilipovunjwa ni risasi iliyolengwa na ikampata begani kisha nyingine zikafuata
Tukiwa bado tumelala chini huku bunduki zetu tukiziweka tayari kwa lolote tuliwaona watu wasiopungua kumi wakiwa na bunduki aina ya AK47 karibia wote kasoro mmoa alikuwa ana bunduki aina ya sniper rifle, walikuwa wakitokea katika pori lililopo upande wa pili wa barabara.
"huyu mwenye bunduki ya wadunguaji ndiye aliyempiga dereva wetu risasi ya mgongo na ya kichwa, hivyo tunahitajika kuwamaliza wote ili tuendelee na safari la si  hivyo tutakwamia hapa" Nurulayt aliongea kwa sauti ya chini huku akiweka bunduki yake sawa.
"Hatuhitaji shambulizi la risasi wapo wengi wale tunahitajika tufanye kitu cha ziada" Nilimwambia Nurulayt huku nikiishusha bunduki yake chini kwani alionekana anataka kuitumia.
"come on Abdul kitu kipi hicho zaidi ya risasi kuwamaliza" Nurulayt aliniambia akionekana hajanielewa.
"una visu hapo?" Nilimuuliza
"ndiyo ninavyo hivi hapa" Nurulayt alijibu huku akifungua sare ya askari wa uhamiaji aliyoivaa akatoa visu vinne akanipatia.
"kuwa mtazamaji mama wa mtoto wangu" Nilimuambia huku nikichukua visu, Nurulayt  aliishia kutabasamu tu kisha akanikonyeza halafu akasema, " good luck ingawa sitaweza kukuona ili niwe mtazamaji". Nilitabasamu kisha nikaviweka visu mafichoni halafu nikaanza kujiburuta kama nilivyofundishwa na jeshi la jeshi la kujenga taifa kipindi namaliza kidato cha sita kwa mafunzo miezi mitatu, nilitambaa kwa umbali mrefu kidogo bila hata kujulikana na wale watu waliopo barabarani. Nilipokaribia eneo lenye nyasi ndefu niliokota kipande cha jiwe nikakirusha mbele yangu kiasi cha mita kadhaa huku nikiwatazama wale watu waliopo barabarani. Risasi zilimiminika kuelekwa upande niliorusha jiwe bila hata kuangalia kama kuna adui wanayemlenga, walipoacha kupiga risasi  nilimuona yule mwenye bunduki aina ya Sniper rifle akiwalaumu waliokuwa wanapiga  risasi kisha akawaamrisha waende kuangalia kuna nini. Amri hiyo waliyopewa ilinifanya nitabasamu tu kisha nikachukua majani mengi nikavijivisha mwilini mwangu kuanzia kwenye viatu hadi kwenye kofia ya sare niliyoivaa,  wale watu walikuja sita upande niliokuwepo kwa kasi bila umakini na walikuwa wanapita sehemu niliyopo mimi kwani ni sehemu yenye njia ya kuelekea upande niliorusha jiwe. Walikuwa wakitembea wawili wawili kwa haraka kuwahi eneo lenye majani mengi bila hata kuonekana kama wanafuata tahadhari yoyote, walipofika usawa wangu ndipo walipojuta kuja mbio bila uangalifu kwani wawili wa nyuma niliwazoa mtama na walipoanguka nilikuwa tayari nimesharukia nikawapiga magoti ya kwenye koo kila mmojs wakatulia kama maji mtungini. Wawili wa kati niliwarushia visu vya kwenye shingo kwa haraka walipotaka kugeuka nyuma kuangalia kilichowapata wenzao, nilipomaliza hayo nilijitupa pembeni kwenye vichaka haraka sana na hata wale wawili waliokuwa mbele walipogeuka waliona miili ya wenzao isiyo na uhai ikiwa ipo njiani.
" Oooh! Shit!" Aliongea mmoja kwa sauti huku akihangaika kuchomoa simu ya upepo iliyopo kiunoni mwake bila hata kuangalia usalama wa eneo hilo kutokana na kuchanganyika na vifo vya wenzao vilivyotokea ndani ya muda usiozidi dakika moja, hakutambua kama kufanya hivyo ni uzembe mkubwa katika eneo lisilo na usalama kama hilo. Vichwa vyao tayari vilikuwa vimevurugwa na tukio la kufa wenzao na hapo ndipo nilipopata nafasi ya kufanya shambulizi jingine la kimya kimya na la ghafla, niliachia visu viwili vilivyobakia ambavyo vilitua katika shingo zao nikilenga sehemu ya shingo ambayo ni mwanzo wa koromeo. Walidondoka kama mizigo kutokana shambulizi hilo kisha wakatulia bila hata kuonekana kufurukuta wakati roho zao zikiachana na mwili, hapo ndipo nilipojiuliza kwanini hawa watu wanakufa hivi bila hata kuonesha purukushani zozote kipindi wanaiaga dunia. Maswali yangu niliona hayana mtu wa kunipa  majibu hivyo sikutaka kupoteza muda eneo hilo hata kidogo, nilichukua bunduki nne zenye mikanda nikafunga usalama wa bunduki zote kisha nikazivaa mgongoni  na nilichukua vibebea visasi vilivyojaa kisha nikaanza kusogea upande wa barabarani kwa kujivuta taratibu mithili ya chatu aliyemmeza mnyama ambaye hajamshibisha kisawasawa. Nilipokaribia nililitazama eneo kwa umakini kisha nikachukua bunduki moja aina ya AK47 niliyoichukua kutoka kwa wale watu niliowaua, niliiangalia nikatoa uaalama wake nikaiweka tayari kuanza shambulizi huku nikiwatazama wale watu ambao sasa hivi wamebaki wanne tu. Sikutaka kusubiri tena nilianza kuwalenga kwa mfululizo wawili wakasalimiana na ardhi wakiwa wameshaacha roho za mikononi mwa malaika mtoa roho, waliobaki ni yule mwenye bunduki ya Sniper rifle na wengine wawili wenye AK47 kila mmoja.Walikuwa wamegusana migongo yao huku bunduki zao wakiwa wamezielekeza mithili ya pembe mshabaha, kila mmoja alikuwa akilinda usalama wa wenzake kwa nyuma yake. Walikuwa wakizunguka kula upande  ili wajihami kwani bunduki ile iliyowaua wenzao hawakujua imetokea wapi, walikuwa wakizunguka kuangalia pande tofauti wakionekana wamechanganywa na vifo vya wenzao. Yule mwenye sniper rifle alipoelekea upande aliopo Nurulayt wakati mwenzake akiwa nyuma yake akimlinda nilisikia mlio uliokaribiana na mzinga na wote wawili wakatupwa umbali wa mita moja toka pale waliposimama na damu ilikuwa imeanza kutoka katika vichwa vyao. Mlio huo ulipotoka na wale walipoanguka sikuona dalili za mtu yoyote kuja barabarani ingawa sauti hiyo ilikuwa ni ya bunduki aina ya shortgun, niliamua kutamba hadi nilipomuacha Nurulayt ili kuhakikisha kama ni yeye aliyepiga kwani bunduki kama iliyowapiga wale watu anayo mikononi mwake. Nilimshukuru Mungu nilipomkuta wa mama mtoto wangu salama akiwa amelala kifudifudi akiwa ameelekeza bunduki barabarani, nilimsogelea  Nurulayt karibu na nilipomfikia alishtuka  akanielekezea bunduki usoni kwa haraka sana akiwa amejigeuza akalala chali kwa haraka sana.
"hey ni mimi" Nilimwambia huku nikishtuka kutokana na uso wangu kutazamana na midomo miwili ya bunduki.
"muda mwingine uwe makini unapokuja kwani hiyo mijani uliyoivaa ningekutambua vipi, utakufa wewe mwanaume" Nurulayt aliniambia
"ok nimekuelewa, ile kazi ni ya mkono wako?" Nilimuuliza kuhusu wale watu wawili waliouawa na risasi moja niliyoisikia ikitokea upande aliopo.
"ndiyo, na wale watatu ni kazi ya mkono wako?" Alikiri ndiye aliyepiga ile risasi kisha akaniuliza swali.
"ndiyo, tena nina nyongeza mama" Nilimjibu huku nikiushuaha ule  mzigo wa risasi mgongoni.
"vizuri nadhani wale wengine umewazima" Nurulayt aliongea
"kabisa nimetumia vile visu hata sauti hawajatoa" Nilimpa uhakika wa kumalizika kwa kazi.
"kwa sumu iliyokuwa kwenye vile visu hata maji hawaombi kama vimetua shingoni mwao, twende zetu" Nurulayt huku akijiinua kutoka pale chini alipokuwepo  kisha akaanza kutembea huku akiwa ameinama na amakunja magoti kidogo. Nilimfuata kwa mwendo huo huo aliokuwa anatembea yeye hadi kwenye gari  letu, Nurulayt aliuvuta mwili wa yule askari wa uhamiaji aliyekusaidia kutuvusha hadi nje ya gari kisha akaokota silaha zote za wale watu waliotuvamia akazitia ndani ya gari. Tulilikagua gari letu.kwenye matairi tukakuta ni zima halina tatizo lolote, baada ya kuona tuna uwezo wa  kuendelea na safari hatukuwa na muda wa kusubiri zaidi ya kuingia ndani ya gari na safari ikaendelea kama kawaida ili  tulivuke pori hilo. Hadi tunalipita pori hilo tayari ilikuwa ni saa nane usiku na sasa tulikuwa tumeingia katika mji mdogo ambao sikuujua jina lake unaitwaje, mji ulitawaliwa na ukimya kutokana na wakazi wake kuwa wamepumzika muda huo wa usiku.  Nurulayt naye alizidi kubadili gia za gari akilipita eneo hilo ambalo  hakunitajia  linaitwaje hadi leo hii, alizidi kuwa makini na barabara huku akiwa kimya kabisa na alionekana hakutaka kuongea kabisa. Nilimuacha aendelee kuchezea usukani na mimi nikanyoosha kiti nikajilaza taratibu na usingizi ukachukua nafasi yake, nilikuja kushtuka usingizini baada ya kusikia napigwa kibao . Nilipofumbua macho nilimuona Nutulayt akiniashiria niinuke na mimi nikainuka, nilipotazama pembeni nje niliona giza bado lipo.
"vipi mbona umesimamisha gari hapa?" Nilimuuliza huku nikiangalia njia na nikagundua tupo sehemu yenye miti mingi.
"hebu vua hayo magwanda ya askariwa uhamiaji wa Botswana ni hatari kwetu" Nurulayt aliniambia huku akivua  magwanda yake pamoja na viatu, nami nilivua  magwanda yangu nikavaa nguo za kawaida nilizokuwa nimezivaa hapo awali. Nurulayt naye alivaa nguo zake za mwanzo na safari ikaendelea huku nikiuchapa usingizi kama kawaida. Niliamshwa kwa mara ya pili na Nurulayt tukiwa tupo katika eneo lenye mji mdogo uliochangamka ambao sikuutambua unaitwaje, kwa makadirio ilikuwa ni saa nne asubuhi kutokana na kuangalia upande ambao jua lipo tangu lilipoanza kuchomoza.
"hapa ni wapi?"Nilimuuliza huku nikipiga miayo kutokana na uchovu niliokuwa nao.
"hebu kwanza funga mdomo huo usije ukanimeza bure, hapa ni Runde hebu shuka tukapate stafustahi" Nurulayt aliniongea huku akinifunga mdomo  nilipokuwa napiga miayo, nilishuka kwenye gari na Nurulayt naye alishuka kisha tukaingia kwenye  mgahawa  uliopo pembezoni mwa barabara. Tulipata stafustahi tukarudi kwenye gari tukaendelea na safari kama kawaida, muda huo mimi ndiye niliyekuwa dereva wa gari na ikawa zamu yake Nurulayt kulala. Hadi inatimu saa tisa alasiri tayari nilikuwa nimeshafika katika kijiji ambacho sikukijua kinaitwaje kilichopakana na msitu mkubwa sana, nilipofika hapo nilimuamsha Nurulayt ambaye alishtuka kisha akaanza kutazama mazingira ya eneo tulilopo kisha akanitazama kwa mshangao sana.
"vipi mbona hivyo?" Nilimuliza baada ya kumuona ananishangaa sana.
"Abdul naona sasa tunataka kuuana" Nurulayt aliongea kwa kulalamika.
"kivipi?"Nilimuuliza.
"mwendo gani umeutumia hadi sasa hivi uwe umefika hapa kwenye hichi kijiji jirani na msitu huu wa Chirinda" Nurulayt aliongea akionekana ameshangazwa na mwendo nilioutumua hadi nimefika hapo.
" wa kifo" Nilimjibu
"sikupi uendeshe tena utaniua we mwanaume unafikiri hii formula one" Nurulayt aliongea.
"wewe ulivyokuwa unaendesha kule Kalahari ulikuwa huoni kama utaua mtu, tema unabahati ulilala yaani ungekuwa hujalala ungekufa kwa uoga" Nilimwambia huku nikishuka ndani ya gari, Nurulayt naye alishuka kwenye kisha akaniambia, " funga milango ya gari na unifuate". Nilifunga milango nikamfuata kuelekea katikati ya kijiji ambacho pia sikukitambua kinaitwaje hadi leo hii, Nurulayt aliniongoza hadi katika mlango wa nyumba ambayo inaonekana ni ya siku nyingi ingawa ina kila dalili za kufanyiwa marekebisho. Aligonga mlango  mara moja kisha akatulia kumya, mlango wa nyumba hiyo ulifunguliwa na mwanamke aliyejitanda vitenge vya kizaire ambaye hakuongea chochote zaidi ya kutuashiria tuingie ndani tu ndiye aliyefungua mlango. Sote wawili tuliingia ndani na mwanamke huyo akafunga mlango kwa makomeo kisha akatuuliza, " za safari?".
"Salama lakini sio salama sana" Nurulayt alijibu huku akimfuata yule mwanamke ambaye alikuwa anaingia katika chumba kimojawapo katika nyumba hiyo, nami niliwafuata bila hata kuambiwa niwafuate hadi ndani ya chumba hicho. Mandhari pana ya chumba chenye mitambo mbalimbali ya tarakilishi ndiyo ilionekana ipo ndani ya chumba hicho, upande mmoja kulikuwa kuna kitanda kipana cha kulala.
"jamani karibuni tena" Alituambia tena yule mwanamke.
"tushakaribia nadhani ni muda  muafaka wa kujua tusichokijua Madam Rhoda" Nurulayt alimwambia yule mwanamke kisha akanigeukia mimi akaniambia "Abdul huyu anaitwa Madam Rhoda kama ulivyosikia nikimuita, alikuwa ni msaidizi wa kaka yangu Sabir ambaye aliuliwa na Faiz kama nilivyokueleza hapo awali na ndiyo yeye aliyenipa mwongozo wa kazi hii ya kumtafuta mwanangu kwa kunipatia vifaa vya  kazi vya kusnzia".
Nilitabasamu baada ya kupokea utambupisho huo wa mwanamke aliyetupokea, yule mwanamke naye alitabasamu baada ya mimi kutabasamu.
"Madam huyu ni Abdul baba yake Ilham na nipo naye  kwenye kazi hii" Nurulayt alimpa utambulisho wangu yule mwanamke.
"ok, sasa tuanze kueleweshana" Yule mwanamke aliongea huku akibonyeza vitufe vya tarakilishi ya mapakato iliyopo humo ndani. Kwenye tarakilishi zilikuja picha mbalimbali za kambi ambayo ilionekana ilikuwa ipo katikati ya msitu, kambi hii ilikuwa imezungukwa na minara mbalimbali yenye vibanda kwa juu ambavyo hutumiwa na walinzi wa kambi hiyo.
"jamani hii ndiyo kambi ya kundi la Gorilla katika msitu wa chirinda, ipo kilomita mbili kusini mashariki mwa barabara ipitayo  katikati ya msitu huo, kambi hii ipo ni mali ya Scorpio nadhani Nuru unamfahamu" Yule meanamke alitoa maelezo halafu akamuuliza Nurulayt.
"Scorpio?! Hapana simfahamu" Nurulayt aliongea huku akivuta kumbukumbu katika halmshauri kuu ya mwili wake kama anaweza kumkumbuka lakini halmashauri kuu ambayo ni ubongo ilionesha kutolikumbuka jina hilo, hivyo yeye pia alikataa  kutolikumbuka jina hilo.
"ngoja nikuoneshe picha yake labda unaweza kumkumbuka maana sikuwahi kulijua jina lake halisi zaidi ya hilo la Scorpio" Madam Rhoda aliongea kisha akafungua faili moja lililopo kwenye tarakilishi  yake lililokuwa na picha ambayo sote tuliitambua kwa jina jingine kabisa.
"Faiz!" Nilisema kwa mshangao sana.
"sasa huyu ndiye mmliki wa hilo kundi ingawa kwa sasa hayupo nchi hii na hajulikani wapi alipo, Nurulayt nadhani unamfahamu." Madam Rhoda aliongea.
"muuaji aliyeutoa uhai wa kaka yangu nitamsahsu vipi? Kumbe bado yupo hai wale waasi  wa Kongo tumewalipa hela nyingi wamuue wamemuacha" Nurulayt aliongea kwa uchungu sana.
"haya jamani tuendeleeni na kilichowaleta" Madam Rhoda alisema huku akifungua picha za msitu wa Chirinda  sehemu ya kambi ya Gorilla boys halafu akasema, "kambi hii ina tower zisizopungua ishirini ambazo zina masniper zote sasa ukiingia bila tahadhari umeisha. Kushoto kwake ndani kuna majengo makubwa mawili ya ghorofa yenye makao makuu  ya kambi hiyo, upande wa kusini mwa makao makuu hiyo ndipo kwenye  ghala lenye vito vya thamani na madini mbalimbali waliyowahi kuyateka hawa watu".
ramani hii hapa itawasaidia kupata mwongozo mzuri tena inabidi muwe na bunduki aina sniper rifle kila mmoja kama mnataka muingie bila kugunduliwa kwani wale walinzi wa juu kwenye zile tower mnatakiwa muwaue mkiwa mbali ili wasiwaone wakawatungua, kumbuka wao ni sniper na ndiyo wenye kibarua kikuu cha kuilinda hiyo kambi. Je mna sniper rifle katika silaha zenu?" Madam Rhoda alieleza mwisho akatuuliza juu ya bunduki hiyo kama tunayo.
"ndiyo tunayo moja tuliyoipata kama ngawira" Nurulayt alijibu
"mnatakiwa muwe na ya pili kwani kutungua masniper ishirini sio mchezo hivyo kila mmoja anatakiwa awe na yake" Madam Rhoda alitusisitiza,  kusikia suala hilo wote tuliinama chini kutokana na kutokuwa na namna ya kuipata hiyo silaha.
"hilo msijali nitawasaidia mtimize wajibu wenu, Nuru hebu lete briefscafe mbili zipo chumba ninacholala" Madam Rhoda alimuamuru Nurulayt ambaye alitoka haraka aliposikia amri hiyo kisha akarejea akiwa mikoba miwili ya kufunga kwa namba akampatia Madam Rhoda.


*kesho kutwa nayo siku uhai na afya vinahitajika kulijua KOSA.