Monday, December 7, 2015

SHUJAA SEHEMU YA TATU







RIWAYA: SHUJAA

MTUNZI: Hassan O Mambosasa

SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843

SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA HII KWA MARA NYINGINE

ANGALIZO: KAZI YA RIWAYA HII YA KISWAHILI NI KUELIMISHA NA KUENDELEZA KISWAHILI. NDIO MAANA NIMETUMIA KISWAHILI SEHEMU WANAPOZUNGUMZA WAGENI ILI NIENDANE NA JAMII WANAYOSOMA, BAADHI YA MANENO YA KINGEREZA YAMETUMIKA KUAKISI JAMII YA SASA ISIVYOTHAMINI LUGHA YA TAIFA

ILIPOISHIA
Siku iliyofuata Beatrice aliwahi kantini baada ya tu
ya kusikia kengele ya mapumziko, alikaa katika kiti
kilicho mkabala na kiti anachokalia Moses kila siku .
Baada ya muda Moses alifika hapo kantini akiwa
amebeba vitabu mkononi, alienda hadi kwenye kiti
anachokitumia siku na kumkuta Beatrice akiwa
tayari keshawasili eneo hilo. Aliweka vitabu na
kumsabahi
"mambo Bite" ha lafu akavuta kiti na kuketi, Beatrice
alimjibu, "safi tu upo poa?". Alivuta kiti na kuketi
kisha akasema "nipo poa, naona leo umeniwahi" ,
kauli hiyo
ilimfanya Beatrice atabasamu pasipo kusema lolote
huku akimtazama Moses.

ENDELEA NAYO ILI KUPATA UHONDO ULIOMO NDANI
YAKE

SEHEMU YA TATU
Moses aliinuka na kwenda kuagiza kifungua kinywa
kisha akarejea kitini, alimtazama Beatrice na
kumuambia, "mbona leo mtulivu hivyo kuliko
kawaida?". Beatrice akamwambia, "walaa nipo
kawaida siku zote ila sitaki kuongea sana kama kila
siku".

Moses akauliza, "mmmh! kwanini?"

"we unataka nipaliwe kama jana" Beatrice akaongea
kwa sauti yenye mchanganyiko wa deko na
kusababusha Moses acheke. Hakika kiliwazo kingine
kwa Beatrice baada ya kumuona mvulana
anayempenda akicheka, alitokea kupenda karibu kila
kitu cha Moses kasoro huzuni yake.

"na wewe umezidi" Moses aliongea huku akicheka

"na wewe bwana hebu acha hayo, hivi jana ulitaka
kuniambia nini?"

"ohoo! Halafu nilitaka nisahau"

"tell me now(niambie sasa)"
Moses alimuashiria Beatrice angoje kwanza muda
huo alikuwa na anatafuna kitafunwa mdomoni,
alimeza kisha akapika funda moja la chai.
Alipolimeza akasema, "Beatrice najua umejua
umetokea kuwa rafiki yangu mkubwa kwa muda
mfupi tu toka tulipoanza kuwa marafiki", aliposema
hivyo akajiweka vizuri kwenye kiti kisha akaendelea,
"sasa basi nataka unisaidie jambo moja tu kama
utaweza".

"Jambo gani hilo Mose?"

"relax Bite ndio ninakwambia sasa"

"sawa Iam listening you(ninakusikiliza)"

"najua unajua ni kiasi gani nimekuwa nikisumbuliwa
na mdada mwenye kujiita Dream girl, sasa nataka
unisaidie katika kumpata huyu mdada maana
nimechoshwa na tabia yake ya usumbufu"

"sasa hapo how can i help(nitawezaje kusaidia) maana hata huyo mdada
hata mimi simjui"

"I know its hard but try (najua ni ngumu lakini jaribu)ikiwa unanipenda
unanipenda mimi kama rafiki yako"

"mmh! Kusema kweli unanipa majaribu"

"unapenda kuniona nikiwa nina furaha"
"Yeah! Napenda kukuona ukiona ukiwa na furaha"

"please help me(please help me) kama unapenda kuniona nina furaha".

Beatrice allijifikiria kwa muda kisha akasema, "ok I
will try(saa nitajaribu)". Kauli hiyo ikimfanya Moses atabasamu
huku akisema "ukifanikiwa nitakupa zawadi yoyote
uitakayo". Waliendelea kunywa chai hadi muda
wakamaliza kabla ya muda wa mapumziko
haujaisha, waliendelea kuongea mambo mengine ya
kawaida huku Beatrice akiwa ni mwenye furaha
muda wote kama ilivyo kawaida yake. Hatimaye
kengele ya kurudi darasani ikagongwa, wote
walinyanyuka na kuondoka kurudi darasani.
Walitembea hadi sehemu ambayo kila mtu
anatakiwa kuelekea mahali yalipo madarasa yao ,
hapo Beatrice akamwambia Moses, "tuonane muda
wa kutoka kama hutakuwa na nafasi". Moses
alimuonesha ishara ya dole gumba ya kukubaliana
na jambo alilolisema, Moses akiwa na vitabu vyake
mkononi aliamua kuelekea darasani kwao moja kwa
moja. Siku hiyo Moses alijikuta akiwa na hisia za
ghafla juu ya Janet, kila akimfikiria alitamani kuwa
naye karibu zaidi. Akiwa darasani baada ya kipindi
cha kwanza baada ya mapumziko kuisha alijikuta
akimuuliza rafiki yake kipenzi humo darasani kwao,

" Hilary umemuona yule demu niliyekuwa nae
kantini?"

"ndiyo si Beatrice au kuna mwingine?" Hilary alijibu
na kuuliza swali papo hapo.

"unamuonaje?" Moses alimuuliza Hilary.

"aisee yupo poa sana, tena kazama kwako au
hujashtuka?"

"wala hamna kitu kama hicho"

"Mose wa wapi wewe yaani kukaa naye huko kote
bado hujajua"

"hamna hicho kitu wewe punguza fikra zako"

"ok tuache hayo, kwanini umeniuliza hivyo?"

"uongo dhambi ndugu, nahisi kumuhitaji baada ya
necta kuisha?"

"aisee leo umekuwa vipi? maana sio kawaida yako"

"Acha udaku we mwanga, mengine yakaushie tu".
Kauli hiyo ilimfanya Hillary acheke sana huku
akisema, "maajabu ya daunia msongolisti kanasa
leo". Moses naye alijikuta akicheka kwa kauli ya
utani aliyoitoa Hilary.

"haya msongolisti mgoni tupige msuli sasa nahisi
ticha haingii huyu" Moses naye akatumbukiza utani
huku akifungua daftari lake lililopo juu ya meza.
Muda wa kutoka ulipofika Moses na Beatrice
walikutana pale walipoachana awali, siku hiyo
Beatrice alitaka waondoke pamoha na Moses. Moses
akiwa na usafiri wake aliokuja nao alikubali pasipo
kuweka walakini wa aina yoyore, alimfungulia
mlango wa gari na kumruhusu kama malkia wake.

"mmh na wewe bwana kwa mbwembwe" aliongea
Beatrice baada ya kuona Moses amemfungulia
mlango kama kijakazi afanyavyo kwa malkia.

"sasa mgeni akiingia kwenye mali ya mwenyeji
lazima anyenyekewe" Moses alitetea kitendo chake
cha kumfungulia mlango Beatrice. Baada ya Beatrice
kuingia ndani ya gari naye alizunguka upande wa
dereva kisha akamuuliza Beatrice, "nikuache wapi?".
Beatrice akajibu pasipo kumuangalia Moses
"mikocheni kama unaelekea huko". Kauli hiyo
ilimfanya Moses atabasamu baada ya kubaini
wanaelekea sehemu moja, aliwasha gari kisha akaendesha kuelekea getini kisha akatoka na kuingia
barabarani kisha akaliondoa kwa mwendo wa kasi.
Baada ya dakika takribani thelathini walikuwa
wamefika mikocheni katika mtaa wa Warioba
sehemu ambapo kuna barabara iendayo mtaa wa
mazinde, Beatrice aliomba kushushwa
njiani, "kwanini nisikupeleke hadi kwenu?" Moses
aliuliza.

"usijali hapa panatosha tu" Beatrice aliongea akiwa
tayari ameshafungua mlango wa gari baada ya
Moses kusimamisha gari.

"Moses usijali nimefuatwa na gari na dereva yule
pale" Bearice aliongea huku akionesha kwa kidole
upande wa pili wa barabara jirani na waliposimama.
Moses alipotazama pembeni ya barabara aliona gari
aina ya Toyota landcruiser V8 ikiwa imeegeshwa
pembezoni mwa barabara mkabala na alipoegesha
gari lake. Hadi muda huo Beatrice alikuwa tayari
ameshashuka garini na sasa alikuwa akivuka
barabara huku akimpungia mkono Moses, baada ya
Beatrice kuingia katika gari lililomfuata Moses
aliondoa mguu wake kwenye breki kisha akakanyaga mwendo
na kupelekea gari ianze kuondoka taratibu. Allikata
kona kuingia njia iendayo mtaa wa Mazinde ambapo
ndio anaishi, alinyoosha barabara moja kwa moja hiyo moja
mwa umbali mrefu kiasi kisha akakata kushoto
kuingia mtaa wa mazinde halafu akaelekea moja
kwa moja hadi kwenye geti la nyumbani kwao


****

JIJINI KISUMU
NCHINI KENYA
Ndani ya klabu ya hoteli ya Sunset pembezoni mwa
mji huo upande wa magharibi wa nchi hiyo, ndani
ya hoteli hiyo ya nyota tatu kulikuwa na mkutano
mkubwa wa watu wenye maslahi ya aina moja.
Brian, kundi la wazungu wenzake ndio wahudhuriaji
wa mkutano huo wenye. Msemaji wa kikao hicho
alikuwa ni Brian ambaye alifungua kikao hicho kwa
kusema, "habari za jioni ,natumai kila mmoja wetu ni
mzima wa afya na ameitikia wito wa mkutano huu
wa siri wa umoja wetu kwa kujua lengo la mkutano
huu. Pia nadhani ni muda muafaka kwa sisi
tuunyamzishe umoja wa Ulaya ambao umekuwa
kikwazo katika biashara yetu inayotuweka mjini na
inayotuwezesha sisi kuendesha biashara zetu
nyingine, nadhani nyote mnajua kwamba tulimtuma
Tasi akachukue virusi kwa namna yoyote baada ya Professa
kugoma kufanya biashara nami" alinyamaza kwa
muda kisha akanyanyua bilauri ya pombe iliyopo mezani
halafu akapiga funda moja.

"Professa huyu aligoma baada ya kusikia kuwa nina
mpango wa kuvijaribu nchini Tanzania kwenye
makazi yake na ambapo anapatikana mwanae
kipenzi, kutokana na ukaidi sisi tukamwambia
atumie mbinu mbadala ili aweze kutupatia bure
maana mwanzo aligoma kutupatia kwa malipo. Tasu
alifanikiwa kumchoma Professa sindano ya sumu
inayoua taratibu ambayo hadi inamuua hakuwa
ametupatia virusi hao, dawa ya sumu hiyo tulikuwa
tunayo na ikatulazimu tumwambie atapata dawa
kama akileta virusi mikononi mwetu. Yote hayo
bado Professa alikaidi na akaishia kusema ipo
mikononi kwa mtu wake anaemuamini na
hatutowapata, hivyo basi hayo ndio maneno
aliyotuchia yenye ukaidi. Sasa nataka nisikilize
mawazo yenu kila mmoja ili tuweze kupata njia
mbadala" alihitimisha kisha akawatazama
wahudhuriaji wa mkutano huo kila mmoja. Mmoja
wa wazungu alinyoosha mkono na kupelekea Brian
asema , "ndio Obren tunakusikiliza"

"Bosi mi naona tumuache Tasi aendelee na kazi
yake na kama akishindwa tutamuongezea nguvu ili
atuwezeshe kupatikana kwa huyo wa kumuaminiwa
na Professa apatikane haraka iwezekanyo" aliongea
Obren kisha akakaa kwenye kiti chake. Mzungu
mwingine alinyoosha mkono na kupelekea Brian
aseme ,"ndio Campbel tunakusikiliza"

"bosi mimi sikubaliani kabisa na Mr Obren kwa
jambo alilolizungumza, nashauri sis ndio tuingie
kazini na huyo Tasi tumtumie kivingine ila si
kwenye kazi hii" Campel aliongea na kupelekea watu
wote waafiki kwa kutikisa vichwa kuashiria
wamekubaliana na rai ya Campbel. Brian aliinuka
kwenye kiti chake kisha akasema "je kuna mwenye
la ziada juu ya hili? nadhani nyote mmekubalia na
ushauri wa Campbel, sasa kikosi chenu wenyewe
kiingie kazini kuanzia muda huu hamna la ziada".
Brian alihitimisha kisha akainuka kwenye kiti chake
halafu akaondoka.Wote waliobaki walitazamana kila
mmoja huku ukimya ukimya ukiwa umetawala,
Cambel aliuvunja ukimya huo kwa kusema, "jamani
tukutane kambini kwetu kule kwenye mbuga" halafu
akainuka kisha akaondoka eneo hilo.


****


MASAA MAWILI BAADAE
KWENYE MBUGA YA KENYA WILD IMPALA
Mbuga hii iliyo jirani iliyo jirani na ziwa Victoria
kulikuwa na na handaki kubwa sana lililochimbwa
kilomita mbili kutoka ziwani, ndani ya Handaki hilo
kulikuwa na kundi la watu takribani sita wenye asili
ya barani Ulaya. Watu hao walikuwa wameizunguka
meza kubwa ya duara iliyotengenezwa kwa chuma,
meza hiyo ilikuwana urefu uliowafikia kiunoni mwao,
katikati ya meza hiyo kulikuwa na karatasi kubwa
lilioenea karibu meza nzima.

"nafikiri tutumie boti yenye uwezo wa kuzama kama
ilivyo Nyambizi" aliongea Obren ambaye alikuwa ni
mmoja kati ya watu waliokuwa wapo eneo hilo.

"ni njia sana nzuri, sasa tukatokee sehemu gani
iliyokuwa salama" aliongea mzungu mwingine kisha
akauliza swali.

" Calvin mbona rahisi hiyo, tutapita chini kwa chini
hadi katika pori la Rubondo lililopo katika kisiwa cha
Rubondo kisha hapo tutafanya mapumziko ya muda
kisha tutaendelea hadi Kagera" Campbel alijibu swali
hilo huku akielekeza kwenye ramani sehemu
wanazopitia.

"njia nzuri hiyo nadhani ramani itatusaidia kufika"
alisema Calvin

"ndio inasaidia na tukifika huko tutachukuliwa na
helikopta hadi kibaha halafu hapo tutakutana na
Tasi" aliongea Campbel.

"Obren, Calvin, Scott , Jameson na Christian
nadhani tupo pamoja sasa team mambas tuingie.
kazi!" alihitimisha Campbel kisha akanyoosha ngumi
mbele na kupelekea wenzake wote wanyooshe
ngumi na kukutanisha ngumi ya Campbel.

"kazii!" wote waliitikia kwa pamoja kisha wakatoka
kwenda kuchukua vitu vyao vya muhimu



ITAENDELEA!!

Sunday, December 6, 2015

SHUJAA SEHEMU YA PILI





  SHUJAA

MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA



SEHEMU YA PILI
Kujipitisha kwake katika madarasa ya sayansi hakukuzaa matunda yoyote, alijitahidi kumsalimja kwa uchangamfu ili awezs angalau kuzoeana naye. Salamu yake ilijibiwa kawaida na kila akitaka kujiweka karibu naye alishindwa  kutokana na umakini wa kijana huyo kwenye masomo uliomfanya awe hapendi na mabinti. Baada ya jitihada zote kushindikana kushindikana sasa alibuni mbinu mbadala ya kumfikishia ujumbe kijana huyo,  kila siku alikuwa akiwahi shule mapema kabla ya watu wote hawajafika. Muda huo wa asubuhi inayoifukuza alfajiri alikuwa  akiweka kadi mbalimbali za mapenzi katika meza ya kijana huyo, mchezo huu ulimchanganya sana Moses hadi akawa anawauliza wanafunzi wenzake kama anamjua. Kila akijaribu kuwauliza wenzake juu ya jambo hilo aliambulia patupu pasipo kumpata anayemchezea mchezo huo, hali hiyo iliendelea kila siku huku mtumaji akiwa anajiita dream girl.  Hali hiyo ilizidi kuendelea kila siku  anapoingia darasani asubuhi, "be a man(kuwa mwanaume) Mose vitu hivyo havilaziwi damu hata siku moja" mmoja wa wanafunzi alimwambia Moses  baada ya kumuona kila siku akilalamika juu ya tukio la kuletewa kadi na mtu msichana asiyemtambua.  Hali hii ilizidi kuendelea na sasa akawa akikaa kantini muda wa mapumziko analetewa kadi na watu mbambali, kila kadi anayoifungua inatoka kwa yule yule msichana anayejiita dream girl. Hayo yalizidi kumchanganya sana Moses na akawa na shauku ya kumjua huyo

Saturday, December 5, 2015

SHUJAA SEHEMU YA KWANZA





 SHUJAA

MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA

SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP: +255713776843


ANZA SASA
Huzuni ilikuwa imemtawala usoni kijana Moses na
kumfanya aonekane mtu mzima tofauti na
muonekano wake ulivyo, kila akijaribu kuhangaika
kwenda na baba yake katika hospitali tofauti ndani
ya jiji la Dae es salaam juhudi zake zilikuwa
zinagonga mwamba katika kutafuta tabibu awezaye
kumtibu baba yake aliyeugua ghafla pasipo
kujulikana chanzo kuugua huko. "mwanangu najua
unahangaika sana katika kuhakikisha.......ninapona
na ninarudi katika hali ya kawaida ila....." alikatisha
kuongea na kuanza kukohoa mfululizo huku
akimtazama mwanae kwa huruma kisha akaendelea
kusema "sitopona mwanangu ujue najua hujui
chanzo cha kuugua kwangu.." alihema kwa nguvu
huku akimtazama mwanae kwa jicho la huruma sana
kutokana na huzuni iliyomgubika kijana Moses. Baba
Moses akaendelea kusema "nimekuwa nikitumia
muda wa maisha yangu kwa miaka mingi katika
kugundua vitu mbalimbali katika sayansi pasipo
kujua mwisho wa kazi yangu hii , nimekuwa
nikitumiwa na watu matajiri ili niweze kupata fedha
kwa kuitumia kazi yangu vibaya. Sasa haya ndiyo
matokeo ya kazi yangu hii" alisitisha kuzungumza
kisha akamtuma Moses akamletee mkoba wake
anaoutumia kuhifadhi nyaraka zake muhimu.
Hakuwa mwingine bali ni professa Lawrence Gawaza
mwanasayansi wa siku nyingi na bingwa wa
kutengeneza kemikali hatari kwa maisha ya viumbe
hai, sasa yupo kitandani akiwa anaumwa ugonjwa
ulioshindwa kujulikana chanzo chake na matabibu
wa hospitali tofauti alizoenda kufafutiwa tiba. Moses
kijana wa miaka kumi na nane ndio kijana pekee wa
Prof Gawaza,hakuwa na mtu mwingine isipokuwa
mwanae huyo aliyekuwa anampenda sana. Mke
wake kipenzi alifariki siku aliyomzaa Moses, hivyo
hakuwa na mtu wa karibu hapo nyumbani zaidi ya
mwanae huyo.
Moses alimpelekea mkoba baba yake pale kitandani
anapomuuguzia,aliamriwa afungue kwa namba za
siri alizotajiwa na baba yake. Alipofungua alikutana
na makabrasha mengi pqmoja na funguo ndogo
sana, "umeiona hiyo funguo?" Prof Gawaza aliuliza
kwa tabu kutokana na kuzidiwa kwake. "huo pamoja
na hayo makabrasha naomba uwe mtunzaji wake na
usimkabidhi yoyote yule" Prof Gawaza alimwambia
mtoto wake huyo kwa sauti yenye kutoka kwa shida.
Moses naye aliitikia kwa kichwa huku machozi
yakimtoka kutokana na hali ya baba yake ilivyo, "we
ni mwanaume sasa haina haja ya kulia kwani
haisa......idii kitu chochote, kazania masomo yako
halafu....."alishindwa kumalizia kauli hiyo baada ya
kikohozi kumbana. Alikohoa kwa nguvu sana kisha
akaomba maji. Moses alikimbia kutoka chumbani
anapomuuguza baba yake hadi kwenye cha kulia
chakula kwenye jokofu la kupooza maji. Alichukua
bilau moja ndefu akaiweka usawa wa koki ya jokofu,
kisha akafungua koki ya jokofu kuruhusu maji
yaliyopo kwenye chupa kubwa juh ya jokofu hilo
yashuke kwa kasi, Alivyoijaza alirudi kwa kasi hadi
chumbani alipo baba yake, alipofika alimkuta kalalá
mithili ya mtu aliye ndani ya usingizi mzito. "baba
amka unywe maji" alimuita huku akimtingisha
mkono,cha ajabu hakuamka wala kuonesha dalili
zozote za kuamka. Moses alimtingisha baba yake
huyo kwa nguvu lakini hakuamka, aliita kwa sauti
kubwa lakini sauti yake haikuzaa jitihada zozote za
kumuamsha Prof Gawaza katika usingizi wa milele
aliolala. Moses alichanganyikiwa sana na hali
aliyomkuta nayo baba yak baada ya kumletea maji, "
baba! baba! baba! baba! babaaaa!" alipiga kelele
kwa nguvu baada ya kubaini baba yake hakuamka.
"Mose vipi mbona hivyo, kuna nini?" ilisikika sauti
ya mlinziwa nyumba hiyo pale mlangoni kisha
akaonekana mlinzi akivuka kizingiti cha chumba
hiko kwa kasi, kilio cha kwikwi cha Moses ndicho
kilimkaribisha humo chumbani na utulivu wa Prof
Gawaza ambaye alikuwa amelaliwa na Moses kifuani.
Alimnyanyua Moses kisha akaweka mkono katika
upande uliopo moyo katika kifua cha profesa,
hakuridhika akaweka na sikio kabisa kifuani mwa
bosi wake. Alipoinua uso wake ulikuwa umejaa
huzuni sana na alimshika mkono Moses kisha
akaenda naye nje, alipofika akamkalisha kwenye
baraza la nyumba. "yakupasa ujikaze dogo kwani
wewe ni mwanaume, kumbuka wewe ndio msimamizi
wa mali hizi na baba wa baadaye. Dogo jikaze najua
unasikia uchungu" Mlinzi alianza kumpa nasaha
Moses juu ya tatizo lililomfika. Pia akazidi
kumueleza "kumbuka binadamu hatuwezi kuwa
pamoja milele hata siku moja kwani ipo siku
tutatengana, ndio kama hivi mzee kakutoka ingawa
bado tunamuhitaji. Mose kutengana na mtu wako wa
karibu ni mojawapo ya changamoto za maisha na
kipimo cha ukomavu wako, sasa basi inabidi
ujioneshe upo mkomavu kiasi gani kwa kujikaza
katika suala kama hili. Baada ya mlinzi kumpa
Moses maneno ya kumtia moyo aliamua kwenda
kutoa taarifa kwa majirani pamoja na kuwapigia watu
wa karibu na Prof Gawaza.


***************************************

Brown Mcdonald ni mzungu mwenye mtandao
mkubwa dunia unohusiana na uhalifu wa kila aina,
umri wake na utajiri alionao ni vitu viwili tofauti.
Akiwa na vibaraka karibia kila nchi aliowaamini sana
katika biashara zake, hakika hakuna alitakalo
lifanyike katika biashara zake likashindikana. Kijana
huyu ambaye ni mwanajeshi aliyeasi amri katika
kikosi cha Uingereza na mtuhumiwa nambari moja
wa uhalifu barani ulaya aliamua kuja Afrika akiwa na
kundi kubwa la vijana wake baada ya msako wake
kuwa mkali barani Ulaya. Akiwa amevaa sura ya
bandia na alama za vidole mwake aliweza kuficha
muonekano wake pamoja na kupata passport mpya
ya kusafiria kwa njia ya kawaida tu pasipo
kugundulika na wanausalama wa dunia ambao
wanamsaka. Sasa ameingia ukanda wa Afrika ya
mashariki akiwa kama mfanyabiashara mwenye
viwanda vya kusindika katika nchi zote za Afrika ya
mashariki, ndani ya muda mfupi toka aingie katika
ukanda huu amejizolea umaarufu kutokana na ubora
wa bishaa zake. Akiwa anatambulika kama Brian
Stockman aliweza kuwa mfanyabiashara mwenye
ushawishi mkubwa katika soko la kimataifa, viwanda
vyake vilikuwa kama mwamvuli wa kuficha biashara
yake haramu anayoifanya ya kuuza dawa za kulevya
na nyara mbalimbali za serikali. Uongo
alioidanganya dunia ullikuwa umefanikiwa na sasa
alikuwa anajihisi mtu huru katika biashara zake,
aliweza kusafirisha bidhaa haramu pasipo kikwazo
chochote. Akiwa ametimiza mwaka mmoja tu toka
aanze kujulikana na wakazi wa kandahii ya Afrika ya
mashariki, alipata habari ya kugunduliwa kwa hatari
na mwanasayansi wa kitanzania. Taarifa hiyo
ilimvutia sana na akafanya jitihada za kuonanan na
mwanasayansi huyo, aliomba kuonana na
mwanasayansi huyo. Alipokubaliwa alipanga mahali
pa kukutana nae, hilo liliafikiwa na mwanasayansi
huyo.
Baada ya siku mbili walikutana katika mgahawa
uliomo hoteli ya Serena jijini Dar es salaam katika
sehemu iliyojitenga, kila mmoja akiwa na kinywaji
chake na amekaa kwenye kiti kilicho mkabala na
mwenzake. Baada ya kusalimiana Brian(Brown)
alianza kuongea kwa kiswahili kisicho fasaha chenye
maneno ya kingereza "sina mengi za kukuweka hapa
bana Gawaza, nahitaji tufanye bussiness".
"what kind of bussiness(biashata ya aina gani")
aliuliza Gawaza.
"no ipoo ongea na mswahili professa onesha jinsi
gani unatukuza swahili bana" Brian alimuumbua Prof
Gawaza baada kuona anajali sana kingereza kuliko
lugha yake ya taifa.
"ok mr Brian biashara ya aina gani?" prof Gawaza
aliuliza huku akitabasamu.
"i know you are scientist(najua wewe ni
mwanasayansi) na umegundua virus ambao
ninawahitaji kwa ajili ya kasi yangu binafsi" Brian
alieleza kiini cha kukutana.
"virus wale ni hatari sana Mr Brian na bado sijatafuta
dawa yake, huoni kama ni hatari kwako if you
release them(kama utawaachia)" Prof Gawaza
alimwambia Brian huku akipiga funda moja la
mvinyo ulio katika bilauri.
"I don't care about that(sijali kuhusu hilo) Professa
ninachohitaji ni virus na jaribio ndani ya nchi hii"
Brian alisema maneno hayo akiwa na uso wenye
dharau.
"no sipo tayari kwa hilo mr Brian kama unataka
biashara yoyote ya virus nitakupa ila si kujaribu
ndani ya nchi yangu yenye damu yangu...thats all"
Prof Gawaza alinyanyuka kwa hasira na kuondoka
eneo hilo. "we will meet again(tutakutana tena)"
Brian alimwambia kwa sauti kisha akaendelea
kunywa kinywaji chake kwa taratibu. Alipomaliza
alinyanyuka kwenye kiti alichokaa akiwa na hasira
maradufu, "I'll show him (nitamuonesha)" Brian
aliropoka kwa hasira kisha akanyanyuka kuelekea
ulipo mlangi wa kutokea katika mgahawa wa hoteli
hiyo. Alitoka na kuondoka kwa mwendo wa haraka
hadi alipoegesha, aliingia ndani na kuliwasha kisha
akatoweka katika eneo hilo.


**************************************


Maelfu ya watu walihudhuria katika msiba katika
msiba wa Professa Gawaza uliokuwepo nyumbani
kwake maeneo ya mikocheni jijini Dar es salaam,
wengi wakiwa ni ndugu,jamaa na marafiki wa
mwanasayansi huyo maarufu ndani ya jiji la Dar es
salaam. Uwanja wa nyumba hiyo ulifurika watu wa
rika zote wakiwa na mavazi meusi huku wale watu
wa karibu wa marehemu wakiwa wamevalia nguo
nyeusi chini na fulana nyeupe yenye picha ya
marehemu sehemu ya kifuani. Turubai kubwa
lilifungwa nje ya nyumba hiyo pamoja na viti vyenye
rangi moja vilivyokaliwa na wahudhuriaji wa msiba
huo, mtoto pekee wa marehemu ambaye ni Moses
alikuwa kakaa ndani muda wote huku kilio kikiwa
ndiyo kiliwazo chake. Siku iliyofuata mwili wa
marehemu uliagwa katika eneo hilo la nyumbani
kwake kisha msafara wa magari kutoka kwa
wahudhuriaji wa msiba huo uliondoka msibani hapo
kuelekea yalipo makaburi ya kinondoni maeno ya
kinondoni kwa ajili ya kuupeleka mwili wa marehemu
katika nyumba ya milele . Mazishi yalifanyika katika
makburi hayo kisha watu wakatawanyika kuelekewa
makwao na wengine kurudi msibani.
Baada ya siku takribani saba ndugu wote wa
marehemu waliondoka ndani ya nyumba hiyo na
kupelekea Moses mjomba wake ambaye alijitolea
kuishi naye na mlinzi wawe watu pekee waliobaki
katika nyumba hiyo. Maisha bila ya baba yake ndio
yaliyofuata baada ya msiba wake, pesa alizoziacha
baba yake pamoja na msaada wa rafiki mkubwa wa
baba yake aitwae Dk Mbungu ulioweza kumsaidia
katika vitu mbalimbali ndio uliopelekea aweze
kujimudu katika mahitaji yake muhimu ikiwemo
ulipaji wa ada shuleni. Hadi muda huo Moses
alikuwa anasoma kidato cha tano katika shule ya
Neema trust iliyopo mbezi jijjnj Dar es salaam,
aliamua kujiendeleza kielimu kielimu na kutoshika
mambo yoyote yasiyohusiana na elimu ili aweze
kujijenga. Umakini wake katika masomo ulimfanya
awe mwanafunzi bora katika shule yao, hadi muhula
wa kidato unakwisha mnamo mwezi mei mwaka
uliofuata, tayari alikuwa anaongoza shule nzima kwa
kupata alsma za juu kuliko mtu yoyote katika kombi
za sayansi zote. Akiwa likizo alitumia muda wake
mwingi kujisomea na akawa hajishughulishi na
mambo ya anasa, mnamo mwezi wa saba muhula
mpya wa kidato cha sita ukaanza kama ilivyo ratiba
ya nchi nzina ya Tanzania. Ulikuwa muhula wa
masomo ambapo wsnafunzi wengi walizinduka
kutoka kwenye usingizi baada ya kutokuwa makini
katika masomo yao ya kidato cha tano, katika kombi
ya PCB ambayo Moses alikuwa anasoma tayari
umakini wa wanafunzi ulizidi maradufu ingawa
hawakufua dafu mbele ya uwezo wa Moses
aliyezinduka mapema kabla yao.


**************************************

Beatrice Bernard ni binti wa familia yenye uwezo
anayesoma katika shule ya Neema Trust, ni
mojawapo ya wasichana warembo na wenye kuvutia
katika shule hiyo iliyosheheni watoto wa matajiri
kutoka sehemu mbalimbali ndani ya Afrika ya
mashariki. Umbo lake la asili ya asili ndio lilimfanya
avutie kwa kila anayemtazama, mchanganyiko wa
wazazi kutoka makabila tofauti ndio ulimfanya avutie
maradufu. Baba yake mzee Bernard alikuwa ni
muhaya na mama yake akiwa ni mrangi, hakika
alikuwa na umbo tata lililozua maswali na
minong'ono kila apitapo. Yote hayo pamoja na sifa
zote alizozipata na kusumbuliwa na watu kutoka
sehemu mbalimbali, alikuwa ni msichama aliyezama
katika penzi zito la mtu asiyemjali wala kuthamini
upendo wake. Utanashati wa huyo kijana ndio
uliomvutia sana na kufanya awe kiliwazo cha macho
yake, ustarabu na upole wake ndio uliomfanya
apende kuwa nae.maishani mwake. Kijana huyo
hakuwa mwingine ila ni Moses Gawaza kijana
mpenda masomo kuliko anasa kama ilivyo vijana wa
umri wake. Beatrice akiwa anasoma madarasa ya
arts katika kombi ya HKL alijitahido kujenga ukaribu
na kijana wa madarasa ya sayansi bila ya mafanikio,
hii haikumkatisha tamaa Beatrice zaidi ya kupenda
kuwa karibuIRI na Moses kutokana na misimamo
aliyonayo huyo kijana kamaJ mwanaume..

ITAENDELEA!!

Friday, December 4, 2015

DHAHAMA SEHEMU YA MWISHO





     DHAHAMA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE



SEHEMU YA MWISHO!!
 Vijana hao walifaniliwa kuwateka Ally na Jamadin na kuondoka nao ambapo njiani Ally alipigwa kisogoni akazirai akatupwa kando ya reli mita chache kutoka katika mzunguko wa Kwa Minchi majira ya usiku, kupotea kwa Jamadin na Ally nyumbani kwangu ilikuwa ni huzuni sana kwa mke wangu lakini kwangu mimi ilikuwa ni kawaida kwani nilikuwa najua kila kitu. Tulikusanyika nyumbani wanaume wote huku mimi nikionekana kulia sana na nilibembelezwa hadi nikanyamza ndipo tulipoanza kujadiliana kimaigizo nini cha kufanya, baada ya mjadala wanaume wote sita tulikubaliana tuongie mtaani kumtafuta Jamadin na Ally na wake wote wakakaa nyumbani kwangu wakimbembeleza Farida.


****

Thursday, December 3, 2015

KOSA SEHEMU YA MWISHO







HASSAN O MAMBOSASA

SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE



 ILIPOISHIA
Nurulayt aliunyanyua ule mzigo wote kwa kutumia ile mashine ya kubebea mizigo akauingiza ndani ya helikopta kisha akaingia ndani  akakaa sehrmu ya rubani akaniambia, "panda twende".
" unaweza kuendesha helikopta?" Nilimuuliza.
"hebu wacha maswali yako panda bwana wanakuja hao"  Nurulayt aliniambia na muda huo huo tukasnza mtikisiko ambo unatokea ikipita treni, nilipanda kwenye helikopta haraka sana nikiwa nimekaa mlangoni kwa tahadhari. Nurulayt aliwasha helikopta na aliipandisha juu baada ya kuanza kuchanganya huku akiiongoza kuelekea mashariki ili aiache kambi hiyo. Helikopta ilipokuwa juu kabisa wale watu walikuwa wameshafika pale kwenye uwanja  ilipokuwa imeegeshwa, walianza kutupa risasi lakini Nurulayt aliongeza mwendo akawaacha.


MALIZIA MKASA HUU WA KUSISIMUA WENYE KUFUNDISHA


SEHEMU YA MWISHO!!
Baada ya kukivuka kikwazo hicho kwa mara nyingine nilijikuta nikimshukuru Mungu kwa kunifanya niwe mzima hadi muda huo tangu nilipojiweka katika mdomo wa mamba katika kambi ile, siiutarajia kama nitaweza kutoka na kuiba katika kambi ile yenye ulinzi na wapiganaji hodari sana wanaotumia silaha. Nilipomtazama Nurulayt kule mbele nilimuona yupo makini sana kuiongoza helikopta kwa mwendo wa kasi, tulikuwa tumeshaiacha  kambi kwa umbali mkubwa hata ukitumia darubini utaiona kwa mbali sana na hatukuwa na wasiwasi na wale vijana wa Gorilla zaidi ya kusonga mbele.
"GRIIIIIIIII!   GRIIIIIIIIIIIII!  GRIIIIIIIIII! "  Mlio wa  simu ulisikika katika mfuko wa suruali yangu ambao ulinishtua sana kwani nilishasahau kama nilikuwa nimebeba simu kabisa katika tangu mara ya mwisho kuitumia siku ile niliyokutana na Nurulayt tangu tupoteane miaka mitano iliyopita, mlio huo pia ulimshtua Nurulayt na kumfanya atazame nyuma kwa mshangao.
"Abdul umekuja na  simu tena ipo loud, huoni kama ingekuwa ni hatari kwako" Nurulayt aliniambia huku akitazama mbele kwa umakini.
"sikujua kama nina simu kwani nilishasahau kabisa" Nilimwambia huku niitoa ile simu nikaiangalia kwenye kioo na nikakuta mpigaji ni yule yule anayenipa kazi za ajabu tangu nijikute nipo Namibia.
"ipokee basi au kama hutaki izime" Nurulayt aliniambia akionekana kukerwa sana na simu niliyonayo jinsi inavyoita kwa fujo, sikuwa na jinsi kwani nisingeipokea ingekuwa ni hasara yangu na kama ningeipokea ingekuwa ni afadhali kwani sikujua huyu mtu anayejiita F.A.Z anataka kuniambia nini. Niliipokea nikaiweka sikioni bila ya kusema chochote ili nimsikilize yeye.
"Napenda niwapongeze kwa kufanikiwa kuiba almasi niliyowatuma pia naomba nikupongeze kwa kufanikiwa kutolewa hardware zangu mgongoni mwako na huyo malaya wako mkijua sitajua upo wapi  ilihali unayo simu  niliyokupatia mimi mwenyewe yenye Global positioning system yaani GPS, sasa basi hujaweza kunifanya nisijue uliopo Abdul hiyo GPS ya kwenye hiyo simu imeunganidhwa huku nilipo katika kompyuta zangu sasa nitajua ulipo hata uhame bara hili. Kwanza tuachane na hayo kwenye hii simu kuna ramani inayokuelekeza sehemu ya kupeleka mzigo huo sasa mpe huyo malaya alete mzigo unapohitajika, pia kumbukeni helikopta hiyo ina mafuta pungufu sasa  mkijifanya mnazunguka sana jua imekula kwenu na ninahitaji mzigo huo haraka sana" Yule mtu alinipa maelekezo kisha simu ikakatwa, sikuwa na jinsi ikabidi nimuoneshe ramani hiyo Nurulayt na nimuelekeze kila kitu Nurulayt nilichoambiwa. Nurulayt alitii maelezo na safari ya kurudi sehemu iliyooneshwa ndiyo ikaanza kwa mwendo wa kasi ili tuwahi kufika eneo hilo, baada ya saa moja nilihisi helikopta ikianza kushuka taratibu na nilipoangalia chini nikaona alama ya H ya rangi nyeupe ikiwa ipo juu ya ghorofa mojawapo katika mji nadhifu sana ambao sikuujua unaitwaje hadi muda huo.
"Nuru hapa ni wapi?" Nilijikuta nikimuuliza Nurulayt.
"ni Widhoek hapo  au umepasahau kabisa" Nurulayt alinitajia sehemu hiyo ambayo ndiyo mji mkuu wa Namibia tuliouacha hapo awali, sikuweza kuutambua kutokana na muonekano wake  kwa juu kwani ulikuwa ni tofauti sana. Nurulayt aliishusha helikopta hadi ikatua katika alama ile ya H iliyokuwa juu ya ghorofa mojawapo ambalo niliwaona watu wengi walioshika silaha zao wakiwa wapo hapo, Nurulayt alipozima Helikopta tulishuka na kisha tukasimama mbele ya mmoja wa watu tulipwakuta hapo ambaye alitusogelea akaanza kutupekua nguo zetu achukua silaha zetu zote.
"why( kwanini)?" Nilimuuliza yule mtu aliyetupekua
"you are going to meet our Boss,  weapon are not allowed. Follow me (mnaenda kukutana na bosi wetu, silaha haziruhusiwi. Nifuateni)" Yule alituambia kisha akaelekea pembeni ya eneo hilo ambalo kulikuwa na tundu kubwa kama mlango lenye ngazi zinazoingia ndani ya ghorofa hilo, tulimfuata tukiwa tumefuatwa nyuma na vijana wawili wenye silaha nzito sana. Tulishuka ngazi hizo hadi chini kisha tukaufuata ukumbi mwembamba uliotupeleka hadi kwenye mlango wenye kamera kwa juu yenye taa juu yake kama ile ya kule kambini kwa vijana wa gorilla, yule mtu aliyetukagua aliisogelea ile kamera kisha akasema "they are here Boss( wapo hapa Bosi)". Aliposema hivyo alinivuta mkono na kunisogeza karibu na ile kamera  huku akiniambia "your face ( sura yako), niliinua uso  wangu nikaitazama ile kamera huku kengele maalum ikilia na mlango ukafunguka. Tuliingia ndani tukiwa tumeongozana na wale watu na tukatokea katika ofisi pana yenye mandhari ya kuvutia pamoja na milango minne tofauti, mbele yetu  kama mita sita kulikuwa kuna meza yenye mafaili kadhaa pamoja na kiti cha kuzunguka kilichotupa mgongo.
"kaeni kwenye makochi hapo" Sauti ile iiliyokuwa ikinipa kazi nisizozipenda ilitoa  amri ikitokea katika kiti kile cha kuzunguka kilichotupa mgongo, tulikaa katika makochi yaliyopo jirani nasi yakiwa mita sita kutoka pale alipo.
"Abdul, Nurulayt hatimaye tunakutana leo hii" Aliongea yule mtu huku akuzungusha kiti kuangalia tulipo na hapo ndipo nilipoibaini sura yake halisi na nikajikuta nikishtuka sana, Nurulayt naye alishtuka sana kwani alibaini yupo ndani ya himaya  ya hatari.
"FAIZ ni wewe kweli" Niliongea huku nikinyanyuka nikataka kumfuata lakini nulishtushwa na milio ya kukokiwa  bunduki  na  nilipoangalia pembeni nilitazama na bunduki mbili aina ya SPAS-12  kutoka kwa wale  watu tuliyoingia nao, sikuwa na jinsi niliishia kukaa tu palepale huku tayari nikiwa najua kilichonifanya niwe pale.
"kinachowashangaza ni kipi nyinyi? Faiz kuwa hai sio? Mlidhani atakufa kwa hila zenu mlizozifanya nyie wasomali. Abdul yaani uko radhi kujaribu kumuua rafiki yako kipenzi kisa mwanamke ambaye hakupendi mwenye mapenzi na rafiki yako kisa una pesa tu, kakwambia nani pesa inaleta mapenzi mpaka ufanye haya. Ilivyopita miaka kumi ulidhani limeisha sio?" Nilikaripiwa na nikajikuta nikiinama chini baada ya kushindwa kumtazama kutokana na maneno makali aliyokuwa anayatoa hadi machozi yakawa yanamtoka.
"Faiz nisamehe rafiki yangu" Nilijikuta nikiomba msamaha.
"wa kuniomba msamaha ni mimi kwani, muombe Faiz mwenye huruma ya kusamehe ila mimi huwa sisamehi" Yule mtu ambaye nilijua ni Faiz alitoa kauli inayoonesha kukana kama yeye siyo Faiz.
"wewe kama si Faiz ni nani?" Nilimuuliza.
"mimi ni Fauz  Ally Zaid kifupi F.A.Z  au Scorpio pacha wa Faiz Ally Zaid  niliyeikimbia nchi yangu nikiwa na mdogo wangu Khalid na nikazamia Afrika ya kusini kutafuta maisha na nikayapata kama haya niliyokuwa nayo kwa tabu na dhiki nikiwa nina uhakika wa kuja kuipa maisha bora familia yangu lakini wewe ukaivuruga familia hiyo kwa jeuri ya pesa zako ambazo hujui zinatafutwa vipi. Pesa hizo za ulizorithi umeona ni bora uwalipe wale waasi wa Kongo wamteke Fauz halafu wawambie familia yetu walete nusu tani ya almasi  kutoka katika himaya yangu mwenyewe iliyo chini vijana wangu Gorrila boys, unajua matokeo yake ni nini?...........Baba yangu Mzee Ally Zaid aliyekuwa ni mwanajeshi mstaafu akaamua kwenda kujaribu kuiba hiyo almasi akajikuta anauawa kikatili huku nikiwa sijui kama vijana wangu wamemuua bsba yangu mzazi alipokuwa ana harakati za kumkomboa mwanae,   Abdul............Abdul nilijiapiza lazima ulipie kwa kukuonesha hiyo pesa inatafutwaje kama ulivyotembea na wale wanawake  ili kupata dola milioni moja za kimarekani na kuiba hizo almasi ili mfe kama mlivyosababisha baba yangu afe lakini mmepona kwasababu Mungu bado anawahitaji nyinyi mashetani" Aliongea huku machozi yakimtoka  na mwili ikimtetemeka kwa hasira, alipoacha kuongea mlango mmojawapo ukafunguliwa na akaingia mtu aliyetokea kuwa rafiki yangu mkubwa na pia meneja wa makampuni. Khalid Zaid ambaye yule niliyemshuhudia akiwaeleza  waandishi wa habari kuwa nipo masomoni ndiye aliyeingia huku akitoa tabasamu pana sana, nilibaki nikishangaa sana kwani sikutarajia kabisa kama nitakutana naye huku kutokana na kumuamini sana.
"Khalid na wewe pia?" Nilijikuta nikiongea kwa mshangao.
"huyo anaitwa Khalid Ally Zaid na unamfahamu kama kama Khalid Zaid  kwani huwa hatumii jina la kati na Faiz hatumii jina  lake la mwisho, nilimtuma kwa ajili ya kukamilisha kazi hii na ukamuamini bila ya kutambua unamuamini Nyoka" Fauz aliongea huku Khalid akitabasamu.
"huyu ndiye aliyekuwa anakupeleleza na hata siku ile uliyochukua binti ambaye ni mfuasi wangu uliyeamini ni changudoa yeye ndiye aliyeusuka mpango ule mpaka ukanyonya matiti ya yule binti anayeitwa Angel aliyoyapakaa madawa ya kulevya ukalala. Pia huyuhuyu ndiye aliyekupasua mgongoni akakufunga hardware ukiwa hujitambui baada ya kunusishwa Klorofomu ukatupwa kwenye kisiwa katika bahari ya Antlantiki siku nne baadaye na ya tano ukajikuta  umelala ufukweni" Fauz aliongea  tena kunifahamisha juu ya Khalid, muda huohuo mlango mwingine ulifunguliwa na akaingia mtu aliyekuwa anaendeshwa kwenye kiti cha matairi  na msichana ambaye sikuweza kumtambua kabisa. Walifika hadi eneo aliposimama Khalid wakiwa wamevaa kofia zilizoziba nyuso zao kwa sehemu kubwa.
"Abdul umefanya kosa lililozaa maafa mengine bila ya kujijua kwa kutumia jeuri ya pesa zako na wewe ndiyo cha huyu mtu aliyekaa kwenye kiti cha matairi ashindwe kutembea tangu nampata, nadhani huyu hujamtambua ni nani ngoja umuone" Fauz alisema kisha akamfunua kofia yule aliyekaa  kwenye kiti cha matairi.
"Faiz!" Niliropoka baada ya kuiona sura ya Faiz kwa mara nyingine baada ya miaka kumi kupita, Faiz alikuwa ananitazama kwa uso uliojaa na hasira sana huku akiachia tabasamu lisiloashiria furaha katika uso wake.
"unashangaa kuniona nipo hai sio fedhuli mkubwa we?" Faiz aliongea akiwa na hasira sana kisha akamgeukia kaka yake akamuambia, "Kaka ulipokimbia nyumbani ukiwa na mdogo wetu nilikuona huna maana ndiyo maana hata chuo na shuleni nilisema nimezaliwa peke yangu kumbe nina pacha wangu, nimeingia chuo nikapata rafiki nikamuona ana maana kumbe hana maana kwani ametumia watu waniteke na wamenichoma sindano ya sumu ambayo inanifanya niwe katika kiti cha matairi hadi leo hii. Ama kweli umdhaniaye ndiye kumbe siye, huyu baradhuri nilimuona  anafaa kumbe hafai na nikakuona wewe hufai kumbe ndiye unafaa, Fauz huyu mtu namchukia sana" Faiz aliongea huku akitokwa na machozi, mimi mwenyewe machozi yalianza kunitoka kutokana na kujuta sana kutokana na mambo niliyomtendea rafiki yangu tukiwa chuo ingawa machozi hayakuweza kubadilisha ukweli wa jambo hilo liwe halijatokea.
"Faiz nisamehe rafiki yangu nimekosa" Nilimuomba msamaha Faiz  huku nikinyanyuka ili walau nikapige magoti mbele yake anielewe lakini nilishindwa kwenda kutokana na kuwekewa bunduki kwa mara nyingine nilipotaka kwenda. Nilirudi nikakaa chini nikamtazama Nurulayt ambaye alionekana pia kujuta kwa kile alichomfanyia Faiz.
"Abdul tafadhali sana naomba usiniite rafiki yako na ukitaka nikusamehe mlete Huwaida hapa  kwani nilimtumia email nilipokombolewa na anajua juu ya uovu wako na kama huwezi  sitakusamehe, namtaka mpenzi wangu tu kwani sijui umemficha wapi hadi sasa" Faiz aliongea huku uso wake ukiwa umetawaliwa na hasira, nilipisikia hilo suala ikabidi nimtazame Nurulayt kisha nikasema, " Faiz haiwezekani jambo hilo kwani Huwaida niliyempenda na aliyekupenda wewe tayari ni marehemu kwa sasa".
"What! Hapanaaaa" Faiz aliongea kwa uchungu kisha akaanza kulia kwa uchungu huku mishipa ya damu ya kichwa ikiwa imemtoka, nilimuonea huruma saba ingawa chanzo cha yote nilikuwa ni mimi.
"Abdul  kama Huwaida kafa basi mwnao lazima afe kwa namna yoyote" Faiz aliongea kwa uchungu.
"Kifo cha Huwaida ni mimi ndiye mhusika  na si Abdul wala  mtoto wetu Ilham na kama unataka kuniadhibu niadhibu ila kaka yako Fauz lazima pia naye alipe kwa kumuua Sabir kaka yangu aliyekuwa rafiki yake na mshirika na kuhusika kwangu katika kutekwa kwako nilikuwa nalenga Fauz na sio wewe" Nurulayt kwa mara ya kwanza aliingilia kutokana na kusikia suala la kutaka kuuliwa Ilham, maneno hayo yalimfanya Fauz atabasamu.
"Alaa kwahiyo umemfanya kaka yangu awe mtu wa kutembea kwa baiskeli kisa mimi kumuua Sabir na ukadhani yeye ni Fauz, sikulaumu sana  najua umekosea kufananisha kwa jinsi tunavyofanana......Sabir alikuwa ni rafiki yangu sana ila amenigeuka  kwa kuuwa watu wangu pia kutaka kumuua mdogo wangu kwa bomu, hivi ungekuwa wewe mtu kama huyu utamfanyaje?" Fauz aliongea na mwisho akamuuliza swali Nurulayt lililomfanya ashindwe kujibu na pia akajiona  ana hatia sana kwa kufanya kile anachokifanya, Faiz alipoona Nurulayt ameshindwa kujibu swali lake alitoa ishara moja ambayo sikuielewa. Mlinzi mmoja mwenye bunduki alisogea mbele baada ya kutolewa ishara ile kisha akampatia bunduki Faiz, Faiz naye aliishika ile bunduki akaelekeza tulipo kisha akaifyatua ikatoa mlio niliousikia. Kuusikia mlio wa bunduki nilitambua haijanipiga mimi kwani bunduki ikikupiga husikii mlio wowote, nilipomuangalia Nurulayt niliona sindano yenye manyoya kama mshale wa mchezo wa dart ikiwa imemchoma begani mwake. Nurulayt aliutia ule mshale kisha akautupa chini na akabaki akiugulia maumivu, nilipomtazama Faiz nilimuona akitabasamu kisha akanielekezea bunduki mimi akiwa makini sana. Hapo mapigo yalianza kwenda mbio na ikanibidi nifumbe macho tu nikusubiria nitandikwe , mlio wa bunduki niliusikia kwa mara ya pili nikafumbua macho nikamuona Faiz akitabasamu.
"Abdul sioni kosa lako lolote lililobakia kwani umejifunza vya kutosha ila huyo mwanamke ana kosa ndiyo maana nimemuadhibu, kosa lako kubwa ilikuwa ni kutoa pesa katika mpango wa huyu mwanamke hivyo umepata funzo hiyo pesa ya urithi uliyoitoa katika mpango huo inatafutwaje" Faiz aliongea huku akinitazama halafu akamegukia Nurulayt akamuambia "Nuru hiyo ndiyo ulistahiki kwa kuhukumu watu bila kujua kama upo sahihi au haupo, sindano zilizo ndani ya bunduki hii zina sumu ambayo ikiingia kwenye damu huponi na itakuua taratibu kuanzia kiungo  kimoja baada ya kingine hadi unakata roho". Faiz alipomaliza kuongea hivyo nilijikuta nikilia baada ya kusikia Nurulayt kachomwa sindano ya sumu na nikamkumbatia ingawa yeye hakuonesha kuhuzunika hata kidogo. Baada ya kusema maneno hayo Faiz alimgeukia Fauz akamwambia, " hii inawatosha wape vitu vyao", Fauz naye alitii na akamuita kijana wake mmoja akampa mkoba ambao alikuja kunipatia. Niliupokea  mkoba huo nikaufungua   nikakuta hati za mali zangu zote pamoja na kadi zangu za benki, niliufunga mkoba huo kisha nikatulia nikawa nawatazama ndugu wale watatu.
"Niliwaambia waandishi kuwa upo masomoni nadhani sasa muda wa masomo umeisha na umepata funzo sasa upo huru, tupatie kila tulichokupatia" Khalid aliongea huku akitabasamu, nilipoambiwa hivyo nilitoa simu nikamrushia naye akaidaka.
"Abdul natambua kama wewe ni binadamu unakosea kwani hakuna aliyemkamilifu, hivyo nimekusamehe wewe na mwenzako.....Nurulayt naomba unisamehe sana sikuwa na jibsi zaidi ya kufanya hivyo nilivyokufanyia na napenda mtambue mtoto wenu yupo nyumbani kwa Sarina mama yake wa kambo, guards take them to the room" Faiz aliongea
Walinzi walituchukua wakatutoa nje ya chumba hicho wakatupeleka chumba kingine kilicho na nguo tofauti za kike na za kiume, huko tulioga na tukabadilisha nguo kisha tukashuka hadi chini na tukachukua teksi iliyotupeleka hadi nyumbani kwa Nurulayt ambapo tulipanda gari yangu nilipewa tukaanza safari ya kuelekea nyumbani kwa Sarina. Tulifanikiwa  kufika na tukashuka tukaingia ndani ya uzio kisha tukagonga mlango wa mbele tukasubiri kufunguliwa, baada ya dakika kadhaa Sarina alifungua mlango na alinikumbatia kwa furaha baada ya kuniona nimerejea nikiwa mzima. Nurulayt alikaribishwa ndani na hapo tukamsimulia kila kitu hasa juu ya Ilham kuwa ni mwanangu. "Waar is Ilham?( Yuko wapi amelala)" Nurulayt aliuliza akiwa na shauku ya kumuona Ilham
" lê(amelala)" Sarina alimjibu lakini Nurulayt alitaka amuone Ilham tu kwani hakuwa amemuona kwa miaka mitano, ilimbidi Sarina amuelekeze chumba kilipo na Nurulayt akaenda akituacha tukiongea . Aliporejea alikuwa amembeba Ilham ambaye tayari alikuwa ameamka, huku akionekana kuwa ana furaha kwa kumuona mtoto wake kwa mara nyingine.
"Anko umerudi?" Ilham aliongea aliponiona nikiwa nimejea.
"wewe sio anko yule ni baba, umesikia? Haya nenda kamsalimie  baba " Nurulayt alimuambia Ilham
"ok mummy" Ilham alijibu halafu akaja kunikumbatia akiwa na furaha na mimu nikiwa na furaha kwa kumjua mwanangu.
"Sarina...dankie(Sarina......asante) Nurulayt alimshukuru Sarina kwa kumtunzia Ilham, Sarina alitabasamu kuonesha amekubali  shukrani ya Nurulayt.

Nilikaa kwa Sarina kwa siku kadhaa kisha nikaenda hadi Walvis kwa rafiki yangu Jonas nikamchukua hadi nyumbani kwa Sarina, baada ya wiki mbili nilikuwa nipo Tanzania nikiwa na Sarina, Ilham, Nurulayt pamoja na Jonas ambaye nilimpatia nyumba na mtaji kama shukrani kwa msaada wake kwangu nilipokuwa nina shida aliponiokota ufukweni. Miezi miwili iliyofuata nilifunga ndoa na Sarina hapahapa Dar es salaam iliyohudhuriwa na watu mbalimbali na sherehe kubwa ikafanyika katika moja ya hoteli ninazozimiliki, furaha yangu ya kuwa na mwanamke ninayempenda  katika ndoa  ilitimia kuanzia siku hiyo.
Baada ya miezi mitatu tangu nifunge ndoa na Sarina hali ya kuafya ya Nurylayt ilianza kubadilika kwa baadhi ya viungo kushindwa kufanya kazi na  akipolekwa hospitali ilibainika tumechelewa kwani sumu ilishasambaa mwilini kote na hakukuwa na tiba ya kumuokoa, Nurulayt aliugua kitandani kwa muda mrefu sana hadi Sarina anapata ujauzito yeye alikuwa bado ni wa kitandani. Sarina alipojifungua watoto mapacha wa kiume ambao niliwaita Haasan na Hussein yeye bado alikuwa kitandani, baada ya miaka mitatu  tangu aanze kuugua Nurulayt aliaga dunia katika muda wa alasiri na  akatuachia huzuni na majonzi yaliyobaki moyoni mwangu na kunipelekea nitokwe na machozi kipindi naandika mkasa huu ulionikumba. Mungu amlaze pema mama wa mtoto wangu wa kwanza na binti yangu mkubwa kati ya watoto sita niliojaliwa na Muumba, nakumbuka mazishi ya Nurulayt niliteuliwa niingie kaburini kuipokea maiti lakini nilishindwa kutokana na kulia sana hasa nikimkumbuka katika kipindi chote nilichokuwa naye.

****

Walipomaliza ukurasa wa mwisho wa shajara hiyo Hassan na Hussein wote walijikuta wakitokwa na mschozi baada ya kujua mkasa uliomkumba baba yao pamoja na mama yao wa kambo ambaye kamzaa dada yao mkubwa.
"aisee mi Mariam simtaki tena hapa nimepata funzo tosha" Hassan aliongea huku akijifuta machozi.
"kweli pesa haileti mapenzi na pesa ibilisi" Hussein aliongea huku naye akijifuta machozi.
"wanawake wapo wengi nitatafuta mwingine ngoja nimuache jamaa awe naye ili niepuke kufanya kosa kwani alichokifanya baba kimenipa funzo tosha" Hassan aliongea huku akimtazams Hussein.
"kaka hapo umeamua na umefanya busara kubwa sana, tafuta mwingine wazuri wapo wengi sana ndani ya dunia hii. Huwezi jua Mungu amekupangia  nani baada ya Mariam kuchukuliwa na jamaa cha msingi badili direction ya moyo wako tu" Hussein alimshauri Hassan.
"kweli kabisa hii diary imenifunza mengi kabisa, cheki time maana nasikia tumbo linanisokota kwa njaa" Hassan alimwambia Hussein. Hussein alichukua simu yake ya mkononi akaangalia saa na alijikuta akipigwa na mshangao baada ya kuangalia saaa.
"Ebwanaeh! Time imeenda sana saa kumi hii, hebu twende tukale kwanza" Hussein aliongea kisha akasimama akaelekea mlangoni ili aelekee sebuleni, Hassan naye alimfuata kwa nyuma.
Walipofika sebuleni walikutana na wazazi wao wakawasalimia kisha wakataka kwenda kwenye meza ya chakula lakini baba yao aliwaita na akawaambia wakae kwenye kochi.
"Hussein, Hasaan" Mzee Abdul aliita majina yao.
"naam Baba" wote waliitikia kwa pamoja.
"najua mmemaliza kusoma diary yangu wanangu, je Hassan bado unataka kufanya ulichodhamiria?" Mzee Abdul aliuliza
"hapana sitafanya nimejifunza pesa si lolote katika mapenzi" Hassan alijibu.
"vizuri, niliamua kuwaacha mjue maisha yangu nyuma ili mjifunze na nyinyi wanangu. Nafurahi mmejifunza na naomba mfuate hayo mliyojifunza, ukiona umekataliwa jua kuna kizuri unaandaliwa mwanangu sasa utafute anayekupenda ili uje kuwa kama mimi Abdul na mama yenu hapa Sarina" Mzee Abdul aliongea huku Bi Sarina akitabasamu.
"sawa baba tumekuelewa" walijibu kwa pamoja.
"nendeni mkale" Mzee Abdul aliwaruhusu watoto wake, Hassan na Hussein walielekea kwenye meza ya chakula wakiwaacha wazazi wao wakiongea.
"ujue mwanzo sikuliafiki suala la wewe kuwapa watoto ile diary wasome ila sasa naona upo sahihi kabisa Mume wangu" Bi Sarina aliongea kwa sauti ya chini kumuambia mume wake.
"unajua katika suala la kuwafunza watoto inabidi muda mwingine tuwe wawazi kwao ili wajue hasara za jambo hilo mke wangu" Mzee Abdul alimwambia mke wake.
"hakika mume wangu wewe ni baba bora kwa watoto wako" Bi Sarina alimwambia mume wake.
"hata wewe ni mama bora kwa watoto, nakupenda sana" Mzee Abdul aliongea.
"nakupenda pia mume wangu" Bi Sarina aliongea huku akitabasamu.
Tangu siku hiyo Hassan aliachana na habari za kutaka kumdhuru rafiki yake na akawa na urafiki naye.

   MWISHO!!

natumaini umejifunza mengi sana, maoni yako tafadhali kwa mtunzi wa riwaya hii

NDUGU MSOMAJI INABIDI UTAMBUE KUWA LIKE
YAKO NDIYO INIPAYO NGUVU YA KUANDIKA RIWAYA
HII, HIVYO LIKE ILI KAMA UPO PAMOJA NAMI.
COMMENT KAMA UNA USHAURI AU MAONI. USIPIGE SIMU KATIKA NAMBA HIZO HAPO JUU, UJUMBE MFUPI WA MANENO UNATOSHA


DHAHAMA SEHEMU YA KUMI NA SITA





 DHAHAMA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE


SEHEMU YA KUMI NA SITA!!
Mara ya kwanza nilianza kwa Faimu nikawa najipitisha sana kwao ili anuone nikijua nitamnasa tu kama nilivyonasa vijana wa hapo kijijini kumbe Faimu hakuwa kijana wa hivyo, uvumilivu uliponishinda niliamua kumuambia ukweli  lakini pia nilimkosa baada ya kukataliwa na akanitishia kumuambia Hamis.  Mara ya pili niliirudia tabia yangu kwa kumtaka Ally baada ua uzuri wake  kuonekana alipofikia kwenye balehe  lakini pia alinikataa nikajikuta nazidi kumsumbua nikijua nitampata tu kwani ni mtoto yule bado akili haijapevuka zaidi ya kupevuka mwili tu, nilipoona nakataliwa sikuchoka na niliamua kuanzisha mazoea ya kawaida naye.  Siku nilipokuja kuwafuma Farida na Faimu na wote wakakiri kuwa wana uhusiano ndiyo siku niliyoona ya kutumia sababu hiyo kwa njia mbili, kwanza ni kulipa kisasi cha kukataliwa na Faimu na pili ni kumteka Ally kiakili. Nilijua Ally ni bado ana akili za kitoto hivyo nilipanga nimuambie hii habari ili ajue ni jinsi gani nampenda hadi nikaamua kumuambia hiyo habari ili aamini moyo wangu upo kwake, pia nilitaka nimuambie mpenzi wangu juu ya usaliti wa rafiki yao kwao waweze kumfanyia kitu kibaya ili nimcheke na hata amkose Farida.

Wednesday, December 2, 2015

KOSA SEHEMU YA KUMI NA TANO

   RIWAYA: KOSA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA

SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE



 ILIPOISHIA
"ndiyo tunayo moja tuliyoipata kama ngawira" Nurulayt alijibu
"mnatakiwa muwe na ya pili kwani kutungua masniper ishirini sio mchezo hivyo kila mmoja anatakiwa awe na yake" Madam Rhoda alitusisitiza,  kusikia suala hilo wote tuliinama chini kutokana na kutokuwa na namna ya kuipata hiyo silaha.
"hilo msijali nitawasaidia mtimize wajibu wenu, Nuru hebu lete briefscafe mbili zipo chumba ninacholala" Madam Rhoda alimuamuru Nurulayt ambaye alitoka haraka aliposikia amri hiyo kisha akarejea akiwa mikoba miwili ya kufunga kwa namba akampatia Madam Rhoda.




ENDELEA NA MKASA HUU WA KUSISIMUA WENYE KUFUNDIDHA


SEHEMU YA KUMI  NA TANO!!
Nurulayt alimkabidhi mikoba hiyo Madam Rhoda ambaye aliipokea kisha  akaufungua mmojawapo

DHAHAMA SEHEMU YA KUMI NA TANO

RIWAYA: DHAHAMA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE




SEHEMU YA KUMI NA TANO!!
Niliendelea kujipa moyo nikijua ipo siku nitampata na sikutambua kama mawazo yangu ni sawa na kuchemsha mawe nikitegemea yatachemke kutokana na upendo mzito nilionao kwake, sikutambua kama najipa matumaini hayawezekani kutokea hivihivi kama kubadilika kwa majira ya mwaka kutoka kiangazi hadi vuli. Nilichojali ni kupata jibu sikujali itachukua muda gani hadi niwe naye, niliendelea kusumbuka katika kumueleza kila siku lakini niliambulia patupu na nikawa natembea na matumaini ya kumpata tu kichwani mwangu. Matumaini yangu yaliishi katika moyo wangu lakini baadaye yalikufa baada ya muda wa miezi kadhaa tu na nikajikuta nikiumia moyoni, kufa  kwa matumaini yangu kulikuwa ni baada ya kuingia kikwazo katika kumpata Farida...


****


Nakumbuka vizuri kijijini kwetu waliingia wageni ambao walipatiwa eneo ambalo baadaye  walilinunua wakajenga makazi yao ya kudumu, wageni hao walikuwa ni wenye asili ya tofauti na watu walioko kijijini

Tuesday, December 1, 2015

KOSA SEHEMU YA KUMI NA NNE

   KOSA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA

SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE



 ILIPOISHIA

Furaha ilidhihirika machoni mwetu kwa kufanikiwa kukivuka kikwazo kile lakini furaha hii haikudumu kwani dosari kubwa iliingilia furaha hii, tukiwa tupo katikati ya pori usiku majira ya saa sita milio ya risasi ilianza kusikika na vioo vya  gari letu vikaanza  kupasuka.Yule askari ambaye ndiye aliyekuwa dereva wetu alitoa ukelele wa maumivu akiachia usukani wa  gari
 na gari likaingia pembeni ya barabara nusura ligonge mti baada ya  yeye kuwahi kukanyaga breki ya gari.




ENDELEA NA MKASA HUU WENYE KUELIMISHA NA KUSISIMUA




SEHEMU YA KUMI NA NNE!!
Milio ya risasi iliendelea kurindima mithili ya ngoma kwenye sherehe ya kikabila, vioo vya gari letu vilitobolewa na matundu ya risasi ambazo zilikuwa zinatokea upande wa pili wa barabara. Muda huo mimi nilikuwa nimesharuka nje ya gari baada ya kuona kuwa ni hatari ndiyo ipo mbele yetu, Nurulayt naye alikuwa amesharuka nje ya gari kisha akajilaza chini kwenye miti mita kadhaa  kutoka barabarani. Hali ilikuwa ngumu kwa yule askari wa uhamiaji aliyekodiwa na Nurulayt atuvushe mpakani kwani alipojaribu kutoka kupitia mlango wa kushoto ambao alikuwepo Nurulayt kutokana na mlango wa kwake kutokuwa salama kuutumia risasi ilitua mgongoni mwake na kumfanya ageuke nyuma ili aweze kumshambulia aliyemtupia risasi, yule askari alipogeuka aliinua kichwa  ili aone vizuri kwani alikuwa amelala kifudifudi kutokana na risasi iliyompata mgongoni. Nikiwa nimejibanza kwenye mti mnene uliopo mita kadhaa kutoka barabarani, nilimshuhudia yule askari akitobolewa kichwa chake na risasi baada ya kuinua kichwa ili atazame upande anaotokea adui yake. Askari yule hakutoa hata neno la mwisho baada ya risasi hiyo ya masafa marefu  kutoboa kichwa kisha kuendelea na safari hadi kwenye shina mti nililosimama ikapita juu kidogo ya kichwa changu kisha ikaendeleana safari.
"Abdul lala chini haraka utakufa huoni risasi imekukosa hiyo"  Nurulayt aliniambia kwa sauti huku akiweka sawa bunduki aina ya short gun  aliyopewa na yule askari, nililala chini kwa haraka sana na macho nikawa nayaelekeza kwenye gari  letu ambalo bado lilikuwa linanguruma hadi muda huo kutokana na kutozimwa na taa bado zilikuwa zinawaka kuanzia ya ndani hadi za nje. Mlango mbele wa gari letu upande wa kiti cha kushoto cha dereva ulikuwa wazi baada ya yule askari kuufungua akijaribu kutoka nje hivyo ikawa njia  rahisi sana kwa mlengaji  kumuua kwani gari hii mlango mmoja ukiwa wazi basi taa ya ndani inawaka hivyo mtu wa nje anakuona kirahisi. Tukio hili ni tukio jingine linalonifanya nimshukuru Mungu katika maisha yangu kwani nafsi yangu ilinisihi nifungue kioo cha dirisha nililokaa baada tu ya kuvuka mpakani, Nurulayt naye alifanya hivyohivyo na dereva wa gari ambaye ndiye yule askari wa uhamiaji nchini Botswana wala hakufanya hivyo yeye aliendelea kuacha kioo kimepandishwa. Ndiyo maana hata kioo kilipovunjwa ni risasi iliyolengwa na ikampata begani kisha nyingine zikafuata
Tukiwa bado tumelala chini huku bunduki zetu tukiziweka tayari kwa lolote tuliwaona watu wasiopungua kumi wakiwa na bunduki aina ya AK47 karibia wote kasoro mmoa alikuwa ana bunduki aina ya sniper rifle, walikuwa wakitokea katika pori lililopo upande wa pili wa barabara.
"huyu mwenye bunduki ya wadunguaji ndiye aliyempiga dereva wetu risasi ya mgongo na ya kichwa, hivyo tunahitajika kuwamaliza wote ili tuendelee na safari la si  hivyo tutakwamia hapa" Nurulayt aliongea kwa sauti ya chini huku akiweka bunduki yake sawa.
"Hatuhitaji shambulizi la risasi wapo wengi wale tunahitajika tufanye kitu cha ziada" Nilimwambia Nurulayt huku nikiishusha bunduki yake chini kwani alionekana anataka kuitumia.
"come on Abdul kitu kipi hicho zaidi ya risasi kuwamaliza" Nurulayt aliniambia akionekana hajanielewa.
"una visu hapo?" Nilimuuliza
"ndiyo ninavyo hivi hapa" Nurulayt alijibu huku akifungua sare ya askari wa uhamiaji aliyoivaa akatoa visu vinne akanipatia.
"kuwa mtazamaji mama wa mtoto wangu" Nilimuambia huku nikichukua visu, Nurulayt  aliishia kutabasamu tu kisha akanikonyeza halafu akasema, " good luck ingawa sitaweza kukuona ili niwe mtazamaji". Nilitabasamu kisha nikaviweka visu mafichoni halafu nikaanza kujiburuta kama nilivyofundishwa na jeshi la jeshi la kujenga taifa kipindi namaliza kidato cha sita kwa mafunzo miezi mitatu, nilitambaa kwa umbali mrefu kidogo bila hata kujulikana na wale watu waliopo barabarani. Nilipokaribia eneo lenye nyasi ndefu niliokota kipande cha jiwe nikakirusha mbele yangu kiasi cha mita kadhaa huku nikiwatazama wale watu waliopo barabarani. Risasi zilimiminika kuelekwa upande niliorusha jiwe bila hata kuangalia kama kuna adui wanayemlenga, walipoacha kupiga risasi  nilimuona yule mwenye bunduki aina ya Sniper rifle akiwalaumu waliokuwa wanapiga  risasi kisha akawaamrisha waende kuangalia kuna nini. Amri hiyo waliyopewa ilinifanya nitabasamu tu kisha nikachukua majani mengi nikavijivisha mwilini mwangu kuanzia kwenye viatu hadi kwenye kofia ya sare niliyoivaa,  wale watu walikuja sita upande niliokuwepo kwa kasi bila umakini na walikuwa wanapita sehemu niliyopo mimi kwani ni sehemu yenye njia ya kuelekea upande niliorusha jiwe. Walikuwa wakitembea wawili wawili kwa haraka kuwahi eneo lenye majani mengi bila hata kuonekana kama wanafuata tahadhari yoyote, walipofika usawa wangu ndipo walipojuta kuja mbio bila uangalifu kwani wawili wa nyuma niliwazoa mtama na walipoanguka nilikuwa tayari nimesharukia nikawapiga magoti ya kwenye koo kila mmojs wakatulia kama maji mtungini. Wawili wa kati niliwarushia visu vya kwenye shingo kwa haraka walipotaka kugeuka nyuma kuangalia kilichowapata wenzao, nilipomaliza hayo nilijitupa pembeni kwenye vichaka haraka sana na hata wale wawili waliokuwa mbele walipogeuka waliona miili ya wenzao isiyo na uhai ikiwa ipo njiani.
" Oooh! Shit!" Aliongea mmoja kwa sauti huku akihangaika kuchomoa simu ya upepo iliyopo kiunoni mwake bila hata kuangalia usalama wa eneo hilo kutokana na kuchanganyika na vifo vya wenzao vilivyotokea ndani ya muda usiozidi dakika moja, hakutambua kama kufanya hivyo ni uzembe mkubwa katika eneo lisilo na usalama kama hilo. Vichwa vyao tayari vilikuwa vimevurugwa na tukio la kufa wenzao na hapo ndipo nilipopata nafasi ya kufanya shambulizi jingine la kimya kimya na la ghafla, niliachia visu viwili vilivyobakia ambavyo vilitua katika shingo zao nikilenga sehemu ya shingo ambayo ni mwanzo wa koromeo. Walidondoka kama mizigo kutokana shambulizi hilo kisha wakatulia bila hata kuonekana kufurukuta wakati roho zao zikiachana na mwili, hapo ndipo nilipojiuliza kwanini hawa watu wanakufa hivi bila hata kuonesha purukushani zozote kipindi wanaiaga dunia. Maswali yangu niliona hayana mtu wa kunipa  majibu hivyo sikutaka kupoteza muda eneo hilo hata kidogo, nilichukua bunduki nne zenye mikanda nikafunga usalama wa bunduki zote kisha nikazivaa mgongoni  na nilichukua vibebea visasi vilivyojaa kisha nikaanza kusogea upande wa barabarani kwa kujivuta taratibu mithili ya chatu aliyemmeza mnyama ambaye hajamshibisha kisawasawa. Nilipokaribia nililitazama eneo kwa umakini kisha nikachukua bunduki moja aina ya AK47 niliyoichukua kutoka kwa wale watu niliowaua, niliiangalia nikatoa uaalama wake nikaiweka tayari kuanza shambulizi huku nikiwatazama wale watu ambao sasa hivi wamebaki wanne tu. Sikutaka kusubiri tena nilianza kuwalenga kwa mfululizo wawili wakasalimiana na ardhi wakiwa wameshaacha roho za mikononi mwa malaika mtoa roho, waliobaki ni yule mwenye bunduki ya Sniper rifle na wengine wawili wenye AK47 kila mmoja.Walikuwa wamegusana migongo yao huku bunduki zao wakiwa wamezielekeza mithili ya pembe mshabaha, kila mmoja alikuwa akilinda usalama wa wenzake kwa nyuma yake. Walikuwa wakizunguka kula upande  ili wajihami kwani bunduki ile iliyowaua wenzao hawakujua imetokea wapi, walikuwa wakizunguka kuangalia pande tofauti wakionekana wamechanganywa na vifo vya wenzao. Yule mwenye sniper rifle alipoelekea upande aliopo Nurulayt wakati mwenzake akiwa nyuma yake akimlinda nilisikia mlio uliokaribiana na mzinga na wote wawili wakatupwa umbali wa mita moja toka pale waliposimama na damu ilikuwa imeanza kutoka katika vichwa vyao. Mlio huo ulipotoka na wale walipoanguka sikuona dalili za mtu yoyote kuja barabarani ingawa sauti hiyo ilikuwa ni ya bunduki aina ya shortgun, niliamua kutamba hadi nilipomuacha Nurulayt ili kuhakikisha kama ni yeye aliyepiga kwani bunduki kama iliyowapiga wale watu anayo mikononi mwake. Nilimshukuru Mungu nilipomkuta wa mama mtoto wangu salama akiwa amelala kifudifudi akiwa ameelekeza bunduki barabarani, nilimsogelea  Nurulayt karibu na nilipomfikia alishtuka  akanielekezea bunduki usoni kwa haraka sana akiwa amejigeuza akalala chali kwa haraka sana.
"hey ni mimi" Nilimwambia huku nikishtuka kutokana na uso wangu kutazamana na midomo miwili ya bunduki.
"muda mwingine uwe makini unapokuja kwani hiyo mijani uliyoivaa ningekutambua vipi, utakufa wewe mwanaume" Nurulayt aliniambia
"ok nimekuelewa, ile kazi ni ya mkono wako?" Nilimuuliza kuhusu wale watu wawili waliouawa na risasi moja niliyoisikia ikitokea upande aliopo.
"ndiyo, na wale watatu ni kazi ya mkono wako?" Alikiri ndiye aliyepiga ile risasi kisha akaniuliza swali.
"ndiyo, tena nina nyongeza mama" Nilimjibu huku nikiushuaha ule  mzigo wa risasi mgongoni.
"vizuri nadhani wale wengine umewazima" Nurulayt aliongea
"kabisa nimetumia vile visu hata sauti hawajatoa" Nilimpa uhakika wa kumalizika kwa kazi.
"kwa sumu iliyokuwa kwenye vile visu hata maji hawaombi kama vimetua shingoni mwao, twende zetu" Nurulayt huku akijiinua kutoka pale chini alipokuwepo  kisha akaanza kutembea huku akiwa ameinama na amakunja magoti kidogo. Nilimfuata kwa mwendo huo huo aliokuwa anatembea yeye hadi kwenye gari  letu, Nurulayt aliuvuta mwili wa yule askari wa uhamiaji aliyekusaidia kutuvusha hadi nje ya gari kisha akaokota silaha zote za wale watu waliotuvamia akazitia ndani ya gari. Tulilikagua gari letu.kwenye matairi tukakuta ni zima halina tatizo lolote, baada ya kuona tuna uwezo wa  kuendelea na safari hatukuwa na muda wa kusubiri zaidi ya kuingia ndani ya gari na safari ikaendelea kama kawaida ili  tulivuke pori hilo. Hadi tunalipita pori hilo tayari ilikuwa ni saa nane usiku na sasa tulikuwa tumeingia katika mji mdogo ambao sikuujua jina lake unaitwaje, mji ulitawaliwa na ukimya kutokana na wakazi wake kuwa wamepumzika muda huo wa usiku.  Nurulayt naye alizidi kubadili gia za gari akilipita eneo hilo ambalo  hakunitajia  linaitwaje hadi leo hii, alizidi kuwa makini na barabara huku akiwa kimya kabisa na alionekana hakutaka kuongea kabisa. Nilimuacha aendelee kuchezea usukani na mimi nikanyoosha kiti nikajilaza taratibu na usingizi ukachukua nafasi yake, nilikuja kushtuka usingizini baada ya kusikia napigwa kibao . Nilipofumbua macho nilimuona Nutulayt akiniashiria niinuke na mimi nikainuka, nilipotazama pembeni nje niliona giza bado lipo.
"vipi mbona umesimamisha gari hapa?" Nilimuuliza huku nikiangalia njia na nikagundua tupo sehemu yenye miti mingi.
"hebu vua hayo magwanda ya askariwa uhamiaji wa Botswana ni hatari kwetu" Nurulayt aliniambia huku akivua  magwanda yake pamoja na viatu, nami nilivua  magwanda yangu nikavaa nguo za kawaida nilizokuwa nimezivaa hapo awali. Nurulayt naye alivaa nguo zake za mwanzo na safari ikaendelea huku nikiuchapa usingizi kama kawaida. Niliamshwa kwa mara ya pili na Nurulayt tukiwa tupo katika eneo lenye mji mdogo uliochangamka ambao sikuutambua unaitwaje, kwa makadirio ilikuwa ni saa nne asubuhi kutokana na kuangalia upande ambao jua lipo tangu lilipoanza kuchomoza.
"hapa ni wapi?"Nilimuuliza huku nikipiga miayo kutokana na uchovu niliokuwa nao.
"hebu kwanza funga mdomo huo usije ukanimeza bure, hapa ni Runde hebu shuka tukapate stafustahi" Nurulayt aliniongea huku akinifunga mdomo  nilipokuwa napiga miayo, nilishuka kwenye gari na Nurulayt naye alishuka kisha tukaingia kwenye  mgahawa  uliopo pembezoni mwa barabara. Tulipata stafustahi tukarudi kwenye gari tukaendelea na safari kama kawaida, muda huo mimi ndiye niliyekuwa dereva wa gari na ikawa zamu yake Nurulayt kulala. Hadi inatimu saa tisa alasiri tayari nilikuwa nimeshafika katika kijiji ambacho sikukijua kinaitwaje kilichopakana na msitu mkubwa sana, nilipofika hapo nilimuamsha Nurulayt ambaye alishtuka kisha akaanza kutazama mazingira ya eneo tulilopo kisha akanitazama kwa mshangao sana.
"vipi mbona hivyo?" Nilimuliza baada ya kumuona ananishangaa sana.
"Abdul naona sasa tunataka kuuana" Nurulayt aliongea kwa kulalamika.
"kivipi?"Nilimuuliza.
"mwendo gani umeutumia hadi sasa hivi uwe umefika hapa kwenye hichi kijiji jirani na msitu huu wa Chirinda" Nurulayt aliongea akionekana ameshangazwa na mwendo nilioutumua hadi nimefika hapo.
" wa kifo" Nilimjibu
"sikupi uendeshe tena utaniua we mwanaume unafikiri hii formula one" Nurulayt aliongea.
"wewe ulivyokuwa unaendesha kule Kalahari ulikuwa huoni kama utaua mtu, tema unabahati ulilala yaani ungekuwa hujalala ungekufa kwa uoga" Nilimwambia huku nikishuka ndani ya gari, Nurulayt naye alishuka kwenye kisha akaniambia, " funga milango ya gari na unifuate". Nilifunga milango nikamfuata kuelekea katikati ya kijiji ambacho pia sikukitambua kinaitwaje hadi leo hii, Nurulayt aliniongoza hadi katika mlango wa nyumba ambayo inaonekana ni ya siku nyingi ingawa ina kila dalili za kufanyiwa marekebisho. Aligonga mlango  mara moja kisha akatulia kumya, mlango wa nyumba hiyo ulifunguliwa na mwanamke aliyejitanda vitenge vya kizaire ambaye hakuongea chochote zaidi ya kutuashiria tuingie ndani tu ndiye aliyefungua mlango. Sote wawili tuliingia ndani na mwanamke huyo akafunga mlango kwa makomeo kisha akatuuliza, " za safari?".
"Salama lakini sio salama sana" Nurulayt alijibu huku akimfuata yule mwanamke ambaye alikuwa anaingia katika chumba kimojawapo katika nyumba hiyo, nami niliwafuata bila hata kuambiwa niwafuate hadi ndani ya chumba hicho. Mandhari pana ya chumba chenye mitambo mbalimbali ya tarakilishi ndiyo ilionekana ipo ndani ya chumba hicho, upande mmoja kulikuwa kuna kitanda kipana cha kulala.
"jamani karibuni tena" Alituambia tena yule mwanamke.
"tushakaribia nadhani ni muda  muafaka wa kujua tusichokijua Madam Rhoda" Nurulayt alimwambia yule mwanamke kisha akanigeukia mimi akaniambia "Abdul huyu anaitwa Madam Rhoda kama ulivyosikia nikimuita, alikuwa ni msaidizi wa kaka yangu Sabir ambaye aliuliwa na Faiz kama nilivyokueleza hapo awali na ndiyo yeye aliyenipa mwongozo wa kazi hii ya kumtafuta mwanangu kwa kunipatia vifaa vya  kazi vya kusnzia".
Nilitabasamu baada ya kupokea utambupisho huo wa mwanamke aliyetupokea, yule mwanamke naye alitabasamu baada ya mimi kutabasamu.
"Madam huyu ni Abdul baba yake Ilham na nipo naye  kwenye kazi hii" Nurulayt alimpa utambulisho wangu yule mwanamke.
"ok, sasa tuanze kueleweshana" Yule mwanamke aliongea huku akibonyeza vitufe vya tarakilishi ya mapakato iliyopo humo ndani. Kwenye tarakilishi zilikuja picha mbalimbali za kambi ambayo ilionekana ilikuwa ipo katikati ya msitu, kambi hii ilikuwa imezungukwa na minara mbalimbali yenye vibanda kwa juu ambavyo hutumiwa na walinzi wa kambi hiyo.
"jamani hii ndiyo kambi ya kundi la Gorilla katika msitu wa chirinda, ipo kilomita mbili kusini mashariki mwa barabara ipitayo  katikati ya msitu huo, kambi hii ipo ni mali ya Scorpio nadhani Nuru unamfahamu" Yule meanamke alitoa maelezo halafu akamuuliza Nurulayt.
"Scorpio?! Hapana simfahamu" Nurulayt aliongea huku akivuta kumbukumbu katika halmshauri kuu ya mwili wake kama anaweza kumkumbuka lakini halmashauri kuu ambayo ni ubongo ilionesha kutolikumbuka jina hilo, hivyo yeye pia alikataa  kutolikumbuka jina hilo.
"ngoja nikuoneshe picha yake labda unaweza kumkumbuka maana sikuwahi kulijua jina lake halisi zaidi ya hilo la Scorpio" Madam Rhoda aliongea kisha akafungua faili moja lililopo kwenye tarakilishi  yake lililokuwa na picha ambayo sote tuliitambua kwa jina jingine kabisa.
"Faiz!" Nilisema kwa mshangao sana.
"sasa huyu ndiye mmliki wa hilo kundi ingawa kwa sasa hayupo nchi hii na hajulikani wapi alipo, Nurulayt nadhani unamfahamu." Madam Rhoda aliongea.
"muuaji aliyeutoa uhai wa kaka yangu nitamsahsu vipi? Kumbe bado yupo hai wale waasi  wa Kongo tumewalipa hela nyingi wamuue wamemuacha" Nurulayt aliongea kwa uchungu sana.
"haya jamani tuendeleeni na kilichowaleta" Madam Rhoda alisema huku akifungua picha za msitu wa Chirinda  sehemu ya kambi ya Gorilla boys halafu akasema, "kambi hii ina tower zisizopungua ishirini ambazo zina masniper zote sasa ukiingia bila tahadhari umeisha. Kushoto kwake ndani kuna majengo makubwa mawili ya ghorofa yenye makao makuu  ya kambi hiyo, upande wa kusini mwa makao makuu hiyo ndipo kwenye  ghala lenye vito vya thamani na madini mbalimbali waliyowahi kuyateka hawa watu".
ramani hii hapa itawasaidia kupata mwongozo mzuri tena inabidi muwe na bunduki aina sniper rifle kila mmoja kama mnataka muingie bila kugunduliwa kwani wale walinzi wa juu kwenye zile tower mnatakiwa muwaue mkiwa mbali ili wasiwaone wakawatungua, kumbuka wao ni sniper na ndiyo wenye kibarua kikuu cha kuilinda hiyo kambi. Je mna sniper rifle katika silaha zenu?" Madam Rhoda alieleza mwisho akatuuliza juu ya bunduki hiyo kama tunayo.
"ndiyo tunayo moja tuliyoipata kama ngawira" Nurulayt alijibu
"mnatakiwa muwe na ya pili kwani kutungua masniper ishirini sio mchezo hivyo kila mmoja anatakiwa awe na yake" Madam Rhoda alitusisitiza,  kusikia suala hilo wote tuliinama chini kutokana na kutokuwa na namna ya kuipata hiyo silaha.
"hilo msijali nitawasaidia mtimize wajibu wenu, Nuru hebu lete briefscafe mbili zipo chumba ninacholala" Madam Rhoda alimuamuru Nurulayt ambaye alitoka haraka aliposikia amri hiyo kisha akarejea akiwa mikoba miwili ya kufunga kwa namba akampatia Madam Rhoda.


*kesho kutwa nayo siku uhai na afya vinahitajika kulijua KOSA.

DHAHAMA SEHEMU YA KUMI NA NNE

 DHAHAMA


MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA


SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843


SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE



SEHEMU YA KUMI NA NNE!!
"Lakini Ally mpenzi wangu nimefanyaje?" Salma aliuliza kwa masikitiko makubwa huku akionekana kuumia baada ya kusukumwa.
"Unajifanya hujui siyo tena usiniite mpenzi wako kuanzia hivi sasa, we wa kunifanya mimi mtumwa wa ngono hadi umesababisha nisioe wakati natakiwa kuwa na familia sasa hivi" Ally alifoka.
"Ally nakupenda ndiyo maana nimefanya hivyo hadi nikazaa na wewe" Salma akaongea huku akilia.
"Weee tena ishia hapo hapo" Ally alimkaripia huku akimuongeza teke la mguu Salma.
"Ally nikatae ila ukae ukijua Hamida siyo mtoto wa mume wangu bali ni damu yako, ndiyo maana hata alipozaliwa kaka yako alikutania umefanana naye miguu ila ukweli ile ni damu yako kabisa" Salma aliongea huku akilia, Ally alipuuza maneno ya Salma akaondoka eneo akimuacha akilia ingawa kuna jambo lilikuwa likiisumbua akili baada ya kusikia maneno hayo.



****


"  "Ally huyu mtoto kafanana na wewe hiyo miguu balaa ingawa ana sura ya mama yake na baba yake" Shafii aliongea huku akicheka.
"Haaaa! Shemeji nawe waanza kwahiyo waataka sema kafanana na babaye na Ally pamoja nami" Salma alisema huku akimtazama Shafii.
"Ndiyo hivyo ahemeji" Shafii alisema.
"Wewe Chumbio waleta zako sasa huoni kama hiyo miguu ni ya mama yake kabisa, wamefanana tazama kucha hizo uache msifia mdogo wako" Hamis aliongea na kusababisha wati wote wacheke humo ndani.
"Bonoeza usichukie basi masihara ni jadi yetu tangu twacheza michezo ya kitoto, hongera bwana kwa kupata binti mrembo huyo na urembo wake unaonekana tangu akiwa mtoto" Shafiu aliongea huku akimpa mkono wa pongezi rafiki yake kipenzi.
"shukrani Chumbio rafiki wa tangu utotoni" Hamis aliitikia huku akicheka
"sasa Bonoeza hapo inabidi ufuge mbwa na bunduki ununue mapema maana wajanja wataanza kuja kutoa salamu sana kumbe wataka wampate malkia hapa" Shafii alisema na wote waliopo nyumbani kwa Hamisi wakacheka " Maneno aliyoambiwa na Salma ndiyo yalivuta kumbukumbu yakamkumbusha siku hiyo ambayo Hamida alikuwa ndiyo kaletwa nyumbani baada ya kuzaliwa katika hospitali ya Ngamiani, alizidi kukumbuka zaidi na hapo akakumbuka tukio jingine kabisa baada ya kumuona Hamida akiwa na miaka mitano tu tangu azaliwe na siku hiyo alikuwa akibadilishwa nguo na mama yake Salma, siku hiyo alimuona Hamida akiwa ana mwili unaofanana wake sana. Ally alikumbuka zaidi juu ya siku hiyo na akawa anajifikiria kwa umakini haswa ndipo akajikuta anaamini lakini siyo kwa asilimiia zote yale maneno aliyoambiwa na Salma.
"Dah nimefanyishwa dhambi mbaya ya kuzini na mke wa mtu bila kujijua" Alky aliongea huku akikata mitaa na alionekana ni mwenye majuto makuu juu ya jambo hilo ingawa hakutegemea kama atalifanya, alitembea huku uelekeo wake maalum ukiwa haujulikani kwani alikuwa anazurura mitaani tu.
"ni bora nilale nje kuliko kulala kwenye mali haramu niliyokuwa nimekabidhiwa na nikajikuta nimeipokea bila kujijua, ni bora nisifanye kazi niwe masikini kuliko kuitumia hii elimu niliyosomeshwa kwa kutumia fedha haramu zilizosababisha mwanadamu mwenzangu amwage damu kwa manufaa ya wengine. Shahada nimeipata kwa pesa zilizotokana na damu ya mwenzangu kumwagika, nawachukia Shafii, Hamid, Hassan, Hussein, Falzal, Hamisi pamoja  mke wako Salma aliyetoa kitu kichafu ili aangamizwe kiumbe asiye na hatia. Hisan Shelukindo pia mwanaharamu mkubwa wewe umekuwa na maisha mazuri kwa ukatili wenu  huo" Ally aliongea kwa hasira akiwa tayari ameshafika Sahare kwa kutembea tu bila hata mpangilio; alihisi uchovu kwa kutembea siku hiyo nzima na akakaa katika baraza la maduka ambayo yalikuwa ndiyo yamekamilika ujenzi wake lakini bado hayajafunguliwa. Alijiona ni mmoja wa wenye makosa kwa kutumia sehemu ya mali iliyotokana na  njia haramu ingawa hakujijua, alijikuta hata akilengwa na machozi na hatimaye alianza kulia kimya kimya hadi pale alipochoka akainuka kwenye baraza hiyo.
"Bora uwe masikini utaabike kuliko uwe tajiri kwa njia isiyo ya halali bila kujijua, inauma sana" Ally alisema kwa uchungu huku akinyanyuka tena barazani hapo na kuanza kutembea kama ilivyokuwa awali, alitembea akawa anafuata uelekeo wa nyumbani kwa baba yake hadi alipofika akaingia ndani na moja kwa moja akaenda kujitupa sebuleni akalala usingizi mzito bila hata kuwa amekula kitu chochote siku hiyo.

   Asubuhi ya siku iliyofuata aliamka akajisafisha mwili wake akatoka hadi nje, akamuona dereva wa gari za baba yake akiwa yupo barazani akipata kifungua kinywa akamsabahi kisha akawa anaelekea getini.
"Kaka unaelekea wapi nikutoe maana gari zipo hapa" Dereva wa baba yake alimuambia.
"unaweza ukapumzika kaka mkubwa" Ally alimuambia dereva wa gari ya baba yake kisha akatoka nje akawa anaelekea ilipo barabara ya Mombasa, alitembea hadi akipoifikia hiyo barabara akamuita dereva wa pikipiki akaja mara moja.
"Mpirani kaka" Ally alimuambia dereva wa pikipiki ambaye alimchangamkia akamuambia apande tu bila hata kutaja bei, Ally alipanda hiyo pikipiki na safari ikaanza ambapo ilichukua dakika kumi na tano kwa mwendo wa pikipiki akawa ameshafika Mpirani akampa dereva yule pesa yake kisha akaingia mtaani na akatembea hadi mahali ambapo nyumba zipo moja moja na hatimaye akaifikia nyumba kubwa ambayo ipo kama gofu tu ikiwa ipo katikati ya shamba kubwa  ikionekana  kuwa ipo peke yake mbali na makazi ya watu wengine. Nyumba hiyo ilionekana kutolewa milango na baadhi ya madirisha baada ya kukaa siku nyingi bila kutumiwa kama makazi ya watu na eneo zima lenye kuizunguka nyumba hiyo lilikuwa  na majani mengi yaliyoonekana hayaku punguzwa kwa muda mrefu.
Ally aliingia ndani ya nyumba hiyo iliyoezekwa kwa bati  lililochakaa na sakafu ya chini ilionesha kuwa ni ya udongo mwekundu  ambao hutumiwa kukandika kuta za nyumba za udongo, ilikuwa ni nyumba kubwa yenye  vyumba takribani vinne na sebule ambayo ndani ina kuta za udongo zilizowekwa plasta kwa nje. Sebule kubwa ya nyumba hiyo ilikuwa na usafi mkubwa kupitiliza ambao ulimshangaza sana Ally na vyumbani kulikuwa kuna nyuzi nyingi za buibui kiasi kwamba haiwezekani hata kidogo mtu wa kawaida kuingia humo ndani bila hata kusafisha hizo nyuzi za buibui, Ally aliangalia kila chumba akawa anakumbuka matukio tofauti ambayo yalikuwa yakifanyika hasa kipindi ambacho anaishi katika nyumba hiyo ambayo kwa sasa imetekelezwa na mwenyewe.
"Ni historia nisiyoweza kuisahau na ni mazingira yasiyoweza kusahaulikavkwa mtu kama mimi na natamani niyarudie niishi kama nilivyokuwa awali huenda amani ya moyo wangu itarejea kama ilivyokuwa awali" Ally aliongea akiwa amesimama katika mlango wa chumba ambacho ndiyo alikuwa akikitumia kipindi akiishi katika nyumba hiyo.
Akiwa amesimama hapo alisikia sauti ya mtu akipiga uruzi kutoka nje ya nyumba hiyo na ikamlazimu atoke aende kutazama ni nani huyo, alipokuwa akikaribia mlango wa kutokea mlango wa nyumba hiyo alikutana na kijana wa kisomali aliyekuwa akifanana sana na mtu ambaye alikuwa anamjua ila jina lilikuwa limemshamtoka kichwani mwake. Kijana huyo alikuwa amevaa kanzu nyekundu  iliyomka vyema na kofia ya rangi ya kahawia, Ally alipomuona huyo kijana alizidi kuvuta kumbukumbu juu ya alipomuona lakini hakukumbuka chochote.
"habari yako kijana" Ally alimsabahi yule kijana.
"salama tu, shikamoo" Yule kijana aliitikia.
"Marhaba sijui ni nani mwenzangu" Alky aliitikia kisha akamuiliza swali yule kijana.
"naitwa Fahmi ni mjukuu wa mzee mmoja maarufu wa kiarabu anayeitwa  Muburaka" Yule kijana alieleza.
"Mzee Mubaraka huyuhuyu baba yake Faimu waliyehamia kijiji cha Bwagamacho" Ally alisema.
"Ndiyo huyo huyo na mimi ni mtoto wa Faimu" Fahmi alieleza.
"ok ok karibu bwana leo nimekuja kuzuru makazi yetu ya zamani" Ally alieleza.
"Asante sana, mimi huwa ni sehemu yangu ambayo napenda kukaa huwa inanikumbusha mengi sana hii na nikiwa na huzuni basi huwa nakuja kukaa hapa ndiyo maana unapaona pasafi sana hasa upande wa sebule hii" Fahmi alieleza.
"Ok kijana ndiyo maana nilitaka nishangae imekuwaje mpaka pawe  hivi, karibu tukae sote na mimi leo nimependelea sana kukaa humu" Ally alimuambia huku akimpa mkono Fahmi ambaye aliupokea akiwa na tabasamu pana usoni.
"umefanana sana na baba yako hadi mkitabamu mpo hivyohivyo, hakika mungu kawajalia tabasamu pana kijana" Ally alimwambia Fahmy na kusababisha Fahmy atabasamu.
"asante anko, napenda nikuite anko kama hutajali" Fahmi alimuambia  Ally.
"si vibaya waweza kuniita hivyo tu kwani umeonesha heshima kubwa sana kwangu kijana" Ally alisema.
"asante sana nafurahi kuongea na wewe" Fahmi alisema.
"hata mimi pia, vipi baba yako hajambo?" Ally aliongea huku akitabasamu kisha akamuuliza juu ya hali ya baba yake, swali hilo lilimfanya Fahmi aondokwe na uso wa tabasamu usoni mwake ingawa alilazimisha tabasamu hilo lirudi katika uso wake.
"Baba yupo uarabuni kwa sasa na huko ndipo alipojenga maisha yake" Fahmi alijibu huku akilazimisha tabasamu usoni mwake.
"ohoooo! Mpe hongera sana rafiki yangu aliyenijali sana yule" Ally aliongea huku akitabasamu.
Maongezi yao yaliendelea hadi ilipotimu adhuhuri Fahmi akaaga akaondoka na akamuahidi Ally angerejea akiwa na ugeni mkubwa sana kama angekuwepo hapo. Alky alimpa ahadi ya kuwepo eneo kwa siku nzima hivyo angemkuta, hakuutambua ugeni huo ulikuwa ni ugeni gani na laiti angeutambua angetamani hata auone muda huo lakini haikuwezekana. Ally aliendea kukaa hapo hadi ilipofika muda wa alasiri akaja kijana mwingine akiwa na chombo cha chakula akampatia, yule kijana alimuambia chakula hicho kilikuwa kimeagizwa aletewe na Fahmi.  Ally alishukuru sana akakila chakula chote kutokana na njaa  ambayo tayari ilishaanza kushambulia tumbo lake, baada ya kumaliza kula alitoa shukrani kwa ubinadamu aliofanyiwa na yule kijana
aliyetumwa pia akamwambia apeleke shukrani za dhati kwa Fahmi kwa kumjali namna hiyo.
Baada ya kijana yule kuondoka Ally aliendelea kukaa hapo akikumbuka mambo mbalimbali kipindi akiishi  ndani ya nyumba hiyo kabla hajahama, mambo mengine ya furaha na upendo na alivyokuwa akiishi na shemeji yake ambaye alimjali yalimpa tabasamu kila akiyakumbuka ila alipokumbuka wema aliofanyiwa na kaka yake alijikuta anasonya tu kwani hakuupenda hata kidogo huo wema wake na wala hadi muda hakuona umuhimu wake.
"Shetani katumia ushetani kunifanikishia malengo yangu, hadi sasa sioni umuhimu wa mimi kufikia haya malengo ikiwa kuna mwenzangu kateseka kwasababu ya huyo shetani. Kakimbia kwao kwasababu ya huyo shetani. Shetani huyu kanisaidia ili na mimi anitumbukize katika ushetani"Ally aliongea kwa hasira  kisha akanyanyuka akasema, "namchukia maana bila yeye mimi nisingetumiwa kama mtumwa wa ngono na yule malaya aliyekubuhu kwa umalaya tangu yupo kigori. aaargh! Nawachukiaaa!" Ally aliongea kwa hasira kisha akapiga ngumi ukutani na kupelekea sehemu ya plasta iliyowekwa juu ya ukuta wa udongo wa nyumba hiyo uanguke.
Chuki za waziwazi kwa  kaka yake ndiyo zilikuwa zimeutawala moyo wake na hakumpenda kama ilivyokuwa akimpenda hapo awali, hakuona umuhimu wa yeye kumuita kaka wakati kafanya mambo yasiyopendeza kwa mwanadamu yoyote mwenye moyo wa kibinadamu na siyo wa  kama aliokuwa nao kaka yake. Alitokea kuwachukia ndugu zake wote walioshiriki mpango ule hakuona faida ya kuwa na ndugu kama wao katika dunia hii, aliona ni bora angekuwa na undugu na jiwe kuliko kuwa na undugu na hao aliowaheshu kama kaka zake lakini hakuona ustahiki wao wa heshima hiyo aliyowapa.






               SURA YA NANE.
   Majira ya magharibi katika eneo hilo alilokuwepo Ally paliiingia ugeni mwingine ambao haukutia mguu katika eneo hilo kwa miaka kadhaa tangu walipoondoka, ugeni huo ulikuwa ni msafara wa magari mawili ya kifahari yenye thamani kubwa sana nchini Tanzania kwa kipindi chote. Magari hayo yalikatisha katika majani baada ya barabara ya kuingia eneo hilo kuwa imeota majani kila sehemu.  Ally aliposikia mingurumo ya gari hiyo wala hakujishughulisha kwenda kuangalia zaidi ya kutulia vilevile sehemu ya dirishani ya sebule hiyo alipokaa katika eneo ambalo  dirisha limetolewa, aliposikia hatua za mtu akiingia hapo ndani yeye alielekeza machp mlangoni tu na hadi mtu huyo anaingia tayari alikuwa ameshamuona na ni mtu kati ya watu anaowaheshimu akiwa amebeba mikeka inayotengenezwa kwa ukindu maarufu kama majamvi kwa wakazi wa jiji la Tanga
"Ally kumbe huku" Sauti ya mtu huyo ilimsemesha na hapo Ally akainuka akamfuata.
"ndiyo baba nipo huku, shikamoo" Ally alimuamkia baba yake baada tu ya kumjibu swali alilouliza.
"marhaba tumekutafuta sana mchana wa leo ili uje huku maana kuna jambo muhimu sana" Mzee Buruhan alisema.
"sawa baba nipo tayari hakuna kilichoharibika" Ally aliongea huku akimpokea  baba yake majamvi.
"yatandike hapo chini kwa ajili ya wageni watakaokuja maana mzee Mahmud kasema kuna ugeni utafika hapa kwa ajili ya jambo hili tuliloitiwa hapa.
"sawa baba" Ally alitii amri akaanza kuyatandika majamvi chini kama alivyoambiwa na baada ya muda akawa amemaliza.
"vizuri sasa tumsubiri mzee mwenzangu anakuja sasa hivi na nimeambiwa nisiwaruhusu ndugu zako kuingia mpaka yeye afike" Msee Buruhan  aliongea huku akienda kuketi dirishani alipokuwa ameketi Ally awali, Ally naye aliungana naye kwenda kukaa alipokuwa  awali.
Baada ya dakika tano mlio wa pikipiki ulisikika nje ya nyumba hiyo ikija na kisha baada ya dakika moja ikaondoka, muda huo huo mzee Mahmud alionekana akiingia mlangoni akiwa amebeba taa nne kubwa za kuchaji baada ya pikipiki hiyo kuondoka.
"vipi kila kitu tayari?" Mzee Mahmud aliuliza.
"ndiyo kila kitu tayari mzee mwenzangu" Mzee Mahmud alijibu.
"vizuri basi, Ally hujambo mwanangu" Mzee Buruhan alipongeza kisha akamjulia hali Ally.
"Sijambo baba shikamoo" Ally alijibu kisha akamsalimia.
"Marhaba mwanangu vizuri kwa kuwepo hapa, ngoja nianze kazi" Mzee Buruhan aliongea kisha akaanza kutamka maneno yasiyoeleweka akawa anazunguka eneo zima lenye mikeka halafu akafanya hivyo kwenye kila pembe ya ukuta hadi akamaliza sehemu zote na alipomaliza kufanya hivyo aliwasha taa alizokuja nazo akazitundika ukutani kwenye kila kona.
"Sasa hao wanaweza kuingia wakae upande wa kushoto na uwaambie wasiongee mpaka niwaambie mimi, Ally kaa pembeni yangu"  Mzee Mahmud aliongea kisha akakaa chini, mzee Buruhan alitoka nje na baada ya muda akarejea akiwa pamoja na Shafii,Salma, Hamida na Jamal.
Shafii aliongozwa na Jamal hadi eneo wanalotakiwa wakae na alishushwa kwenye kiti akakalishwa kitako, baada ya wote kukaa chini kwenye jamvi waligeuka wakawa wanamtazama mzee Mahmud kujua kinachofuata.
"Bado ugeni mmoja uingie, wageni karibuni" Mzee Mahmud aliongea huku akitazama mlangoni na kupelekea watu wote watazame mlangoni, ugeni ulioingia hapo ulikuwa ni watu  wanaowajua ambapo wengine walishtuka baada ya kuuona ugeni huo ambao haukueleweka umefika hapo kwa usafiri gani kwani walionekana tu wapo mlangoni.
Wa kwanza kuonekana mbele ya macho yao alikuwa ni Zalabain akiwa amevaa joho jeusi  na kofia nyupe ambaye alitambulika kwa Ally na Shafii pamoja na mzee Mahmud, Ally alimtambua Zalabain  kama Fahmi aliyekuwa naye hapo hadi muda wa adhuhuri na hakumfahamu kwa vingine kabisa. Shafii alimtambua huyo mtu kama mbaya wake baada ya kuiona sura yake siku aliyokufa mganga Sauti ya radi na alimkimbia, alipomuona alishtuka sana alitamani hata ardhi ipasuke atumbukie asionekane eneo hilo kwani alishuhudia ukatili wa Zalabain hivyo alimuogopa. Wageni wengine walioingia eneo hilo walikuwa ni Bi Farida na Zayina wakiwa wamevaa nguo za thamani kubwa walizopata wakiwa katika ulimwengu wa majini, Shafii alipowaona alijikuta akijawa na furaha akataka kutamka neno ila ishara ya baba yake ikimkataza kutozungumza ikamfanya atulie.
"Karibu Zalabain mwana Zaif mjukuu wa Zulain mfalme wa himaya ya majini ya  Majichungu, karibu uketi upande ule wa pili ukiwa na wageni wenzako" Mzee Mahmud alisema huku akitabasamu na kusababisha Zalabain atabasamu pia, Zalabain na mama yake pamoja na dada yake walienda kukaa mwingine kabisa pembeni ya upande aliopo Shafii.
"Sasa basi nimewaita hapa ili tuweze kutatua tatizo ambalo lingemsababishia mzee mwenzangu hapa asibakiwe na hata muhomili mmoja ndani ya dunia hii, utatuzi wa tatizo hilo utaanza kuonekana tu ikiwa ukweli wote utakuwa utakuwa hadharani" Mzee Mahmud alisema kisha akamwangalia Shafii akamwambia, "Shafii napenda uanze kuongea ukweli kuanzia unaanza kumpenda Bi Farida na ulivyompata hadi ukamuoa, tafadhali narudia tena tafadhali ukweli ni muhimu katika kila kitu".
Baada ya mzee Mahmud kumaliza kuongea alimpisha Shafii ili aeleze ukweli wake wote, Shafii naye hakuwa na jinsi zaidi ya kueleza ukweli wote juu ya suala hilo ili apate  nafuu ya matatizo yake kwa jinsi anavyoamini na kwa jinsi alivyoambiwa na mzee Mahmud. Shafii alianza kwa kusafisha koo lake kisha akasimulia, "Kwanza napenda nitangulize msamaha kwa hichi nitakachokusimulia ikiwa kitakuwa kimemkwaza yoyote kwani si kizuri, nilikuwa ni mtoto mtiifu sana kwa wazazi wangu kwa kipindi ambacho bado sikuwa nimepevuka kutokana na malezi ya kimaadili aliyonilea baba yangu kwa  kipindi hicho. Ndiyo muda huo huo mke wangu mama Zayina alikuwa angali binti mdogo hata kuvunja ungo bado ingawa alikuwa akitajwa ni mmoja kati ya mabinti wenye uzuri ambao haukuwahi kutokea katika kijiji chetu cha Bwagamacho Baada ya Farida kuanza kupevuka ndipo uzuri huo wa umbo na kila kitu ulianza kuonekana na kipindi hicho na ndiyo wavulana wa rika langu wakaanza kumfuata lakini waliambulia kukataliwa na binti huyo na hata wengine walishtakiwa kwa wazazi wao baada kumtongoza, jambo hilo lilinitisha na kunifanya nishindwe kwenda kumuambia kwa kuhofia ukali wa baba yangu kama akijua. Nilimpenda sana tena sana lakini nilihofia kupigwa sana na baba yangu kama nilivyoshuhudia wenzangu wakifanyiwa hivyo na baba zao baada tu ya mashtaka kuletwa nyumbani juu ya kumtongoza Farida. Baada ya miaka miwili kupita ndipo nilipoanza kupata ujasiri wa kumtongoza ingawa nilikuwa nina uoga kwa mbali, kutongoza kwangu kuligonga mwamba na hata nilipomueleza rafiki yangu kipenzi Hamis ambaye ni kaka yake juu ya suala hilo aliniambia yupo tayari kumsaidia ikiwa tu na yeye nitamsaidia kufanikisha jambo analolitaka.
"Jambo gani wataka nikusaidie  Bonoeza" Nilimuuliza Hamis.kwa kutia jina la utani ambalo hakuwa analipenda kabisa kwa kipindi hicho.
"Shafii waanza sasa nimesema hilo jina silitaki nitaacha kusaidia nikamjaze sumu dada yangu umkose" Hamis alinijia juu baada ya kumtajia hilo jina.
"Hamis nisamehe rafiki yangu niambie shida yako sasa" Nilimuomba radhi na nikawa tayari kuisikiliza hiyo shida yake kwani ndiye rafiki yangu wa shida na raha.
"rafiki yangu hii ni aibu sana hasa kwa vijana wa rika langu na nimeificha ila kwakuwa wewe ni rafiki yangu wa muda mrefu nimeamua nikueleze ili unisaidie na wewe  nikusaidie, kiufupi nampenda sana Salma yule mtoto mzee Rajabu ila mdomo wangu ni mzito kutamka neno hili kwake na ninabaki nikiungua ndani kwa ndani tu" Hamis alinieleza tatizo lake ambalo nilikuwa nipo tayari kumsaidia tu ili nipate moyo wa dada yake  kipenzi, tatizo lake lilikuwa ni dogo tu kwani  hata Salma alikuwa akimpenda vilevile na ishara zote niliziona ila tu wote hawakuwa na ujasiri huo. Nilimsaidia hadi akampata Salma na mimi akaanza harakati za kunisaidia lakini hazikuzaa matunda kabisa kwani msimamo wa Farida bado ulikuwa ni uleule na hata alipomtumia Salma katika suala hilo ilikuwa vilevile na yeye alizidi kunipa moyo kuwa nitampata ingawa nilianza kukata tamaa juu ya suala hilo.  Niliendelea kumbembeleza Farida lakini sikuchoka kwani niliamini yeye alikuwa akinipenda mimi pia na kama angekuwa hanipendi basi angelikuwa amenishitaki siku nyingi nyumbani kwetu juu ya kumsumbua kwangu lakini hakufanya hivyo, hakika sikutambua kama kaanza kukomaa kiakili na jambo kama hilo hakuwa na haja tena kulisema kwani ingeonekana ni akili za kitoto. Niliendelea kujipa moyo nikijua ipo siku nitampata na sikutambua kama mawazo yangu ni sawa na kuchemsha mawe nikitegemea yatachemke kutokana na upendo mzito nilionao kwake, sikutambua kama najipa matumaini hayawezekani kutokea hivihivi kama kubadilika kwa majira ya mwaka kutoka kiangazi hadi vuli. Nilichojali ni kupata jibu sikujali itachukua muda gani hadi niwe naye, niliendelea kusumbuka katika kumueleza kila siku lakini niliambulia patupu na nikawa natembea na matumaini ya kumpata tu kichwani mwangu. Matumaini yangu yaliishi katika moyo wangu lakini baadaye yalikufa baada ya muda wa miezi kadhaa tu na nikajikuta nikiumia moyoni, kufa  kwa matumaini yangu kulikuwa ni baada ya kuingia kikwazo katika kumpata Farida...



*Hatimaye akubali kufunguka

*usikose kujua alichofunguka.