Friday, August 18, 2017

TENDAGURU SEHEMU YA TANO






RIWAYA: TENDAGURU
NA: HASSAN O MAMBOSASA
MAHALI: TANZANIA NA MAREKANI





<><><>SEHEMU YA TANO<><><>

Hilo lilikuwa ni zao la kupigana mabusu mbele ya kumbe huyu mwenye miguu mwili asiyejua kuachia nyama yeyote, hapo ndipo wakajiweka huria zaidi hata alipokuja kuketi Mtu mwingine aliye na mwili mkubwa wala hawakujali lolote wao walitulia tu. Hakuna aliyempelekea jicho mtu huyo mwenye asili ya barani ulaya aliyevaa fulana iliyobana pamoja na suruali aina ya jeans


_

Thursday, August 17, 2017

TENDAGURU SEHEMU YA NNE





RIWAYA: TENDAGURU
NA: HASSAN O MAMBOSASA
MAHALI: TANZANIA NA MAREKANI




<><><>SEHEMU YA  NNE<><><>


"Huu ni mwanzo tu nyinyi, tena ninaanza na wewe jioni ya leo" Alisema huku  akiweka alama kwenye jina mojawapo ambalo lipo juu kabisa ya karatasi yake, alipomaliza kuiweka tu hilo jina barua pepe iliiingia kwenye tarakilishi yake na kutoa mlio kutokana na kuiweka proramu maalum ya baruapepe.

"Enheee!" Alijisemea

Monday, August 14, 2017

TENDAGURU SEHEMU YA TATU



RIWAYA: TENDAGURU
NA: HASSAN O MAMBOSASA
MAHALI: TANZANIA NA MAREKANI



<><><>SEHEMU YA TATU<><><>


"Nasa screenshot yake pamoja na ya gari lake hilo halafu play mwingine" Amri nyingine ilitoka na kijana alifanya kama alivyoagizwa, mkanda wa siku nyingine uliwekwa na mtu akiwa ni yuleyule anayemuona anakuja kupokea wageni uwanjani hapo.

"Piga screenshot kila mkanda wa siku ambazo anafika huyu mtu" Aliweka agizo jingine.

Sunday, August 13, 2017

TENDAGURU SEHEMU YA PILI




RIWAYA: TENDAGURU
NA: HASSAN O MAMBOSASA
MAHALI: TANZANIA NA MAREKANI




<><><>SEHEMU YA PILI<><><>


"Akili kuchekecha tu, hii inaonesha wazi hawa waliuawa ndiyo wakatupwa kwenye maji na si kingine. Haiwezekani wafe hivihivi tu, ninachokihitaji kutoka kwako kuanzia hivi sasa hakikisha kila picha unayoipiga kwenye miili hii zinafikia mezani kwangu"

"Afande" Amri yake iliitikiwa na Askari yule ambaye alikuwa na kamera pia mkononi mwake alisogea na  kuongeza walau picha zingine za upande tofauti kabisa kwenye miili ile.



Saturday, August 12, 2017

TENDAGURU SEHEMU YA KWANZA



RIWAYA: TENDAGURU
NA: HASSAN O MAMBOSASA
MAHALI: TANZANIA NA MAREKANI




<><><>SEHEMU YA KWANZA<><><>


               UWANJA WA NDEGE WA MWALIMU  NYERERE

      Wageni waliyokuwa na asili ya barani Ulaya walionekana wakitoka kwenye mlango maalum, huu ni mtokeo wa wale wote wanaowasili ndani ya uwanja huu. Lilikuwa ni kundi la wazungu waliyovalia mavazi marahisi haswa kwenye macho ya kadamnasi, ilionesha wazi hawa  ni watalii waliyokuwa wapo mapumzikoni na matembezini. Huu  ni mtazamo juu yao lakini hakuna aliyekuwa na uhakika na kile  kilichokuwa kikionekana, ujio wao ndani ya nchi hii ulibaki kuwa  ni habari yao iliyokaa mitimani kwa kila mmoja. kila mmoja alifunika kichwa chake kwa kofia kuhofia haswa jua la jiji  jinsi lilivyokuwa kali. Macho yao  yalistiriwa na miwani ya jua, ilionesha wazi hawakuwa wamezoea mmuliko huu   wa mchana.

Wednesday, August 2, 2017

WITO WA KUZIMU SEHEMU YA MWISHO






WITO WA KUZIMU

NA: HASSAN O MAMBOSASA

MAHALI:TANZANIA


SIMU:+255713776843
      +255762219759

WHATSAPP:+255713776843
         +255762 219759

BLOG: riwayamaridhawa.blogspot.com




SEHEMU YA MWISHO!!
Ndani ya chumba hicho alishuhudia wasichana watatu wakiwa wamekaa wanaongea huku wakicheza karata,alisimama mlangoni hapo akiyathaminisha mazingira ya humo. Kabla hata hajamaliza kuyathaminisha   alifunguliwa pingu zote alizofungwa na kisha alisukumwa ndani kwa nguvu.






______________TIRIRIKA NAYO

    Aligeuka kuwatazama mabinti watatu waliokuwa wamevaa sare kama zake wakiwa wanacheza karata, alibaki akishangaa wasichana hao ambao walimtazama kwa nyodo kila mmoja na kisha waliendelea kucheza karata kama kawaida. Josephine hakuwajali kabisa alienda hadi kwenye eneo ambalo kitanda kimojawapo kilikuwa kitupu kisha akajilaza akiwa anasikilizia maumivu. Alipojilaza tu kwenye kitanda hiko wale wasichna waliweka karata zao chini na kisha wakaenda hadi hapo walipo, bila kuuliza mmojawapo alimvuta mguu kamuangusha chini kisha akampiga teke la ubavu.