Friday, June 23, 2017

HANJAMU YA MSALITI



RIWAYA: HANJAMU YA MSALITI
NA: HASSAN O MAMBOSASA




 SURA YA KWANZA

    Mvumo  wa kutoka mashariki kuelekea magharibi ulirindima, minazi  pamoja na miti mingine mingine iliyopo  ndani ya mandhari hiyo. Ilipepesuka vibaya kwa mkumbo huo, hali hiyo ilidumu ikiwa na karaha kubwa kwa miti ambayo haikuisha kulalama ikitoa mivumo ya aina yake pale matawi au makuti yalipovamiwa. Karaha kwa viumbe hai waliyojichimbia ardhini, ikawa ni   burudani kwa viumbe hai watembeao juu ya mgongo wa ardhi. Mgeuko wa hali ya hewa kutoka ile ya joto  liletwalo na jua hadi kuwa mpulizo,  ndiyo ikawa hivyo kwa upande wao.