Saturday, January 3, 2015

KOSA


   RIWAYA: KOSA
MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA
SIMU:+255713776843
+255762219759

WHATSAPP:+255713776843
SHUKRANI ZOTE ANASTAHIKI MWENYEZIMUNGU
MUUMBA WA DUNIA NA VILIVYOMO KWA KUNIPATIA
AFYA NJEMA ILIYONIWEZESHA KUANDIKA RIWAYA
HII KWA MARA NYINGINE

ANZA SASA KUUFUATILIA MKASA HUU

SEHEMU YA KWANZA!!
   Sauti ya kulalamika ilisikika ikitoka ndani ya chumba kimojawapo cha nyumba ya kifahari iliyopo katikati jiji la Tanga, ni ndani ya mtaa ambao una makazi ya watu wenye nazo katika jiji hili katika maeneo ya Raskazone. Kijana mmoja mwenye asili ya kisomali aitwae  Hassan alikuwa akilalamika mbele ya pacha wake anayeitwa Hussein, machozi yenye kutiririka mithili ya chemchem ya  maji ndiyo yalikuwa yamefunika mboni za macho yake hadi akawa anaona ukungu katika macho yake. Hussein alikuwa ana kazi ya kumbembeleza pacha yake huyo aliyelia akilitaja jina la msichana, kilio chake kilikuwa ni uchungu tosha kwa pacha wake aliyekuwa anambembeleza. Neno mapenzi ndiyo lilitawala kinywa cha Hassan muda wote aliokuwa analia, kupende ndiyo kulimliza kijana huyo. Muda wote mapacha hawa ambao wanapendana kwa dhati wakiwa wanabembelezana, hawakutambua kama waliacha wazi mlango wa chumba chao wanacholala zaidi ya mmoja kulia tu na mwingine akiweka mawazo yake katika kumbembeleza mwenzake.

JINAMIZI

IWAYA :JINAMIZI
MTUNZI: HASSAN O MAMBOSASA
SIMU:+255713776843
+255762219759


WHATSAPP:+255713 776843
ANGALIZO: HII NI RIWAYA YA KUBUNI
ISIYOHUSIANA NA MTU WALA KIKUNDI FULANI,PIA
WAHUSIKA NI WA KUBUNI WASIOHUSIANA NA MTU
YOYOTE.


ANZA SASA.
SEHEMU YA KWANZA
Hekaheka za uchaguzi zilikuwa zimepamba moto
nchini Tanzania,kampeni zenye majigambo zikiwa
zimeshika nafasi yake ndani ya ardhi hii yenye
amani. Vyama tofauti vilikuwa vikihaha huku na
kule ndani ya nchi hii ili viweze kujizolea kura kwa
wananchi, wagombea urais,ubunge na udiwani a